Jumatatu, 30 Juni 2014

YOHANA MBATIZAJI HAKUSHINDWA


(Mathayo 11:1-14)
“Ikawa Yesu alipokwisha kuwaagiza wanafunzi wake kumi na wawili, alitoka huko kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao. Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza, ‘Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?’ Yesu akajibu akawaambia, ‘Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami.’ Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, ‘Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme. Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii. Huyo ndiye aliyeandikiwa haya,
‘Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njiayako mbele yako.’ Amin, nawaambieni, hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye. Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka. Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana. Na ikiwa mnataka kukubali, yeye ndiye Eliya atakayekuja.”
Tunapaswa Kuifahamu Huduma ya Yohana Mbatizaji
Ni huduma gani hasa ambayo Yohana Mbatizaji aliitimiza kabla ya Yesu? Wakristo wengi leo hii hawamfahamu vizuri Yohana Mbatizaji, hivyo wanatakiwa kupata mtazamo mpya kuhusu Yohana Mbatizaji ili waweze kumfahamu na kuikubali huduma yake kikamilifu. Sisi sote tunapaswa kuwa na ufahamu sahihi na kuukubali uhusiano kati ya huduma ya Yesu na ile yaYohana Mbatizaji. Kwa kuufahamu uhusiano huu kikamilifu, basi unapaswa kwanza kulipokea ondoleo la dhambi kwa imani.
Katika kifungu cha leo cha Maandiko, Yesu aliwaambia wanafunzi wa Yohana Mbatizaji, “Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.
Kwa kweli vipofu waliokutana na Yesu walifunguliwa macho yao, viwete waliweza kusimama na kutembea, waliokuwa wamepagawa na mapepo waliwekwa huru, na injili ilihubiriwa kwa maskini wa roho.
Tunachopaswa kukitambua hapa ni kwamba huduma ya Yesu ilihusisha kazi ya kuwafungua macho vipofu. Kwa maneno mengine, katika wakati huu, Bwana ametupatia injili ya maji na Roho, ambayo ni injili ya kweli inayowafungua macho wenye dhambi ambao bado wanatembea katika giza. Kabla ya kukutana na Yesu Kristo, kila mtu alikuwa na dhambi katika moyo wake na alikuwa ni kipofu wa kiroho mbele ya Mungu. Sisi pia, tulikuwa hatuufahamu uhalisia wa injili ya maji na Roho, wala hatukutambua kuwa Yesu ni nani, pia sisi sote tulikuwa hatuzifahamu dhambi zetu na matokeo mabaya ambayo yangejiri kwa sababu ya dhambi hizo. Pia hatukuwa na upendo kwa Neno la kweli la injili ya maji na Roho, ambalo ni Kweli ya wokovu ambayo Yesu ametupatia.
Hata hivyo, watu wengi sasa wameisikia Neno lenye nguvu la injili ya maji na Roho, na kwa kule kuiweka imani yao katika Neno la injili, basi macho yao ya kiroho yamefunguliwa na wameuvumbua Ukweli unaowawezesha kuokolewa toka katika dhambi zao zote. Wale wanaoifahamu na kuiamini injili hii ya kweli sasa wameuvumbua Ukweli wa ondoleo la dhambi ambao walikuwa hawaufahamu hapo kwanza: Macho yao ya kiimani yamefunguliwa, na sasa wanaifanya kazi ya Mungu. Kama ilivyo katika macho yetu ya kimwili ambapo tunaona kila kitu katika ulimwengu huu, sasa tunaweza kuona ulimwengu wa kiroho kwa wazi hasa baada ya macho yetu ya kiroho kufunguliwa kwa kupitia imani yetu katika injili ya maji na Roho. Hivi ndivyo mtu anavyoweza kuufikia ufahamu kwamba huduma ya Yesu inahusu hasa huduma ya injili ya maji na Roho.
Kwa sababu ya dhambi zetu, wewe na mimi tulikuwa ni vipofu na viwete wa kiroho, na kwamba hatukuweza kuiona huduma ya Mungu wala kuifanya kazi yake. Kwa maneno mengine, sisi pia tulikuwa ni wenye dhambi ambao tulikuwa tumefungwa ili kwenda kuzimu. Hata hivyo, Yesu Kristo alikja hapa duniani, alibatizwa na Yohana Mbatizaji, akaimwaga damu yake Msalabani, na kwa sababu hiyo akazitimiza kazi ambazo ziliondolea mbali dhambi zote za ulimwengu. Kwa hiyo, yeyote atakayeamini katika Ukweli huu ataona bayana kuwa dhambi zake zote zimeoshelewa mbali kikamilifu. Kwa kweli Yesu Kristo amezisafishilia mbali dhambi zetu zote kwa kuja hapa duniani, kwa kubatizwa na Yohana Mbatizaji, na kwa kuimwaga damu yake Msalabani.
Hata sasa, kazi hizo za Mungu, zinaendelea kujifunua vizuri katika mioyo ya wale wote wanaoamini katika injili ya maji na Roho. Bwana wetu ameyafunua macho ya waamini wake kiroho, na ametufanya sisi tuliokuwa viwete kiroho, kuinuka na kusimama kwa miguu yetu kwa kupitia nguvu ya injili ya maji na Roho.
Hapa tunahitaji kutambua kuwa ikiwa tutajaribu kuifanya kazi ya Mungu pasipo kuwa na imani katika injili ya maji na Roho,  basi ni hakika kuwa hakutakuwa na faida yoyote kwa miili yetu wala kwa roho zetu. Wale ambao bado hawajapokea ondoleo la dhambi zao wanafikiri wakati wote, “Ninapaswa kuishi maisha mema. Ninapaswa kuwa mwema kwa kila mtu.” Lakini hakuna hata mmoja ambaye anaweza kulifanya hili, yaani kutenda mema na kuishi maisha mema.
Kabla hatujaifahamu injili ya maji na Roho, tulikuwa na dhambi katika mioyo yetu na kwa sababu hiyo sisi sote tulikuwa na dhambi katika mioyo yetu na kwa sababu hiyo tulikuwa ni wenye dhambi, na hivyo hatukuweza kuifahamu kazi ya Mungu ya haki ilivyo na wala hatukuweza kuitenda. Hata hivyo, kwa kuwa Bwana wetu alizipokea dhambi zetu zote mara moja na kwa wote kwa kupitia ubatizo wake, na kwa sababu alizisafishilia mbali kwa damu yake aliyoimwaga Msalabani hali akiwa amejitwika dhambi za ulimwengu, basi hapo tuliweza kuokolewa toka katika dhambi zetu zote.
Sasa tunaweza kuishi kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu kwa sababu Yesu Kristo ametuokoa toka katika dhambi kwa nguvu ya injili ya maji na Roho. Sasa tunaweza kumwezesha yeyote yule kuionja radha ya nguvu ya injili  hii ya kweli na kisha kuokolewa.
Yesu Kristo ametuwezesha kuokolewa toka katika dhambi na laana zetu zote kwa kuleta maisha mapya kwako wewe na mimi ambao tulikuwa ni viwete kwa kupitia Ukweli wa wokovu. Alichosema Yesu hapa ni kuwa, “wenye ukoma wanatakaswa na viziwi wanasikia; wafu wanafufuliwa,” kimetimizwa katika mioyo yetu yote inayoamini katika injili ya maji na Roho.
Tulipokuwa tungali wenye dhambi, pia tulikuwa ni wakoma wa kiroho. Wakati huo mioyo yetu ilikuwa na dhambi, na hatukuweza kusafishwa toka katika dhambi zetu zote hadi pale tulipoiweka imani yetu katika injili ya kweli ya maji na Roho.
Pia Bwana wetu alisema kuwa viziwi watasikia. Tulipokuwa wenye dhambi, hatukuweza kulifahamu Neno la Mungu hata pale tuliposikia. Lakini sasa, kwa kuwa tumefunikwa na nguvu ya injili ya maji na Roho kwa kuiweka imani yetu juu yake, tunaweza kulifahamu Neno la Mungu, na kufahamu maana yake ya kweli, na kisha kuliamini hilo Neno kwa mioyo yetu yote.
Kila mtu ulimwenguni pote anaishi katika njaa na kiu ya kiroho. Watu wanateseka kutokana na upofu wa ulemavu wa kiroho. Lakini Bwana bado anawapatia nafasi ya kuponywa mara moja kwa kuturuhusu kuwahubiria injili ya maji na Roho. Ni lazima tuwaonee huruma. Tunahitaji kukumbuka kuwa wakati tulipokuwa hatuifahamu injili hii ya wokovu, ambayo ni injili ya maji na Roho, hatukuwa na ukamilifu, na kwamba hatukuweza kufanya lolote zaidi ya kuishi hali tukiwa na dhambi zetu zote katika mioyo yetu. Hatupaswi kuisahau neema yake yenye huruma ambayo imewageuza wenye dhambi kuwa wenye haki.
Kwa hiyo, kile ambacho Bwana wetu alikizungumza kwa wanafunzi wa Yohana Mbatizaji kuhusu maajabu ambayo alikuwa anayatenda alikuwa na lengo kuwafanya wafahamu kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mwokozi wa kweli na Masihi atakayekuja. Baadhi wanaweza kusema kuwa wakati Yohana Mbatizaji alipofungwa, alijaribiwa hadi akawa na mashaka ikiwa Yesu alikuwa ni Masihi atakayekuja, na kwamba hii ndio sababu aliwatuma wanafunzi wake kwenda kwa Yesu. Lakini hii si kweli.
Yohana Mbatizaji alikuwa ni nani? Alikuwa ni mkuu kati ya wote waliozaliwa na wanawake. Alikuwa ni mkuu kuliko mtumishi mwingine yeyote wa Mungu. Kwa maneno mengine, sio kwamba Yohana alikuwa hamwamini Yesu kiasi kuwa akatuma wanafunzi wake kwenda kumuuliza, “Wewe ndiye yule ajaye?” Bali alichokuwa anakifanya ni kuwaelimisha wanafunzi wake ili waweze kufahamu hasa kuwa Yesu ni nani.
Yohana Mbatizaji alikwishaamini na kufahamu kuwa Yesu ni Mwokozi na Mwana wa Mungu; zaidi ya yote, alikuwa amekwishasikia ushuhuda wa Mungu Baba wakati alipombatiza Yesu Kristo katika Mto Yordani (Mathayo 3:17), na pia yeye mwenyewe alikuwa ni shahidi aliyekuwa akimshuhudia Yesu. Yohana Mbatizaji aliwatuma wanafunzi wake kwa Yesu kwa kuwa wanafunzi wake walikuwa hawamfahamu Yesu kikamilifu, na alitaka kuwafundisha kuwa Yesu Kristo ndiye Mwokozi atakayekuja.
 Kwa kweli baada ya Yohana Mbatizaji kufahamu kuwa Yesu Kristo alikuwa ni Masihi atakayekuja, alijaribu kuiondoa huduma yake na kuwapeleka wanafunzi wake kwa Bwana. Ili kumfunua Yesu kwa taifa  la Isareli, Yoahan Mbatizaji alisema kuwa, “Yeye[Yesu] hana budi kuzidi, bali mimi kupungua” (Yohana 3:30).Kwa mfano, Andrea, ndugu wa Simoni Petro, alikuwa ni mwanafunzi wa Yohana, lakini alimfuta Bwana mara baada ya kumsikia Yohana akimshuhudia Yesu (Yohana 1:40).
Hata hivyo, ubishi unaotolewa juu ya Yohana Mbatizaji unaeleza mambo mengi yasiyo na maana hata pale ambapo hawamfahamu Yohana Mbatizaji vizuri, huku wakidai, “Yohana Mbatizaji alikuwa ameshindwa. Aliangukia  katika majaribu na akashindwa kumwamini Yesu. Imani yake ilivurugika baada ya kufungwa.” Lakini ndugu zangu waamini, hampaswi kuiwekea mashaka imani ya Yohana Mbatizaji.
Yohana Mbatizaji na Yesu walikuwa na majukumu yao ambayo walipaswa kuyatimiza pamoja kwa majaliwa ya Mungu Baba. Na majukumu haya yalikuwa ni kubatiza na kubatizwa, huduma ambazo zilikuwa na lengo la kuitimiza haki ya Mungu. Hii ndio sababu Yesu na Yohana Mbatizaji kila mmoja aliishuhudia huduma ya mwenzake.
Mathayo 11:7-9 inasema,  “Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme. Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.”Hapa Yesu alisema, “Kwa nini mlikwenda nyikani? Kumwona nabii? Ikiwa ni hivyo, mpo sahihi. Ninawaambia kuwa Yohana Mbatizaji ni mba mkuu zaidi ya nabii.” Kisha Yesu alimwelezea
Yohana Mbatizaji kwa kunukuu Malaki 3:1 katika Maandiko. Mathayo 11:10 ni kifungu kinachonukuu Malaki 3:1. Katika kifungu hiki, Yesu alisema, “Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi natuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, atakayeingeneza njia yako mbele yako.”Kwa maneno mengine, kwa kunukuu kifungu kilichoandikwa katika Malaki 3:1, Yesu alishuhudia kuwa Yohana  Mbatizaji alikuwa ni mtumishi halisi wa Mungu ambaye ndiye aliyetumwa kumtangulia Yesu Mwenyewe. Mtumishi wa Mungu aliyeandikwa katika Malaki 3:1 ni nani? Si mwingine bali ni Yohana Mbatizaji. Malaki 4:5-6 pia inaonyesha kuwa mtumishi anayetajwa katika Malaki 3:1—“Namtuma mjumbe wangu”—ina maanisha ni Yohana Mbatizaji. Katika Mathayo 11:11, Yesu alisema, “Amin, nawaambieni, hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.”
Kwa nini Bwana alituambia hili? Kwa nini alisema kuwa Yohana Mbatizaji alikuwa ni mkuu kuliko wote waliozaliwa na wanawake? Hapa Yesu anatueleza kuwa Yohana  Mbatizaji alikuwa ni mtumishi halisi wa Mungu aliyekuwa ametabiriwa katika Agano la Kale, na kwamba yeye ni mwakilishi wa wanadamu. Kifungu hiki kinaendelea kwa kueleza sentensi ngumu: “Walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” Waalimu wengi wa uongo wanamhukumu Yohana Mbatizaji kuwa mtu aliyeshindwa kwa kuangalia kifungu hiki. Wanadai “Kwa sababu Yohana alikuwa na mashaka kuhusu Yesu’ kuwa ni Masihi, na kwa sababu hiyo alitathminiwa na Bwana kuwa ni mtu wa mwisho.” Madai haya ni upuuzi mtupu. Ila, kile anachokisema hapa Yesu ni kwamba ingawa Yohana Mbatizaji alikuwa ni mwakilishi wa wanadamu, kwa upande wa kiroho, alikuwa ni mtu wa chini ambaye hakuweza kufananishwa na wale waliokuwa wamefanyika watoto wa Mungu. Kwa maneno mengine, pamoja na kuwa Yohana Mbatizaji alikuwa ni mwakilishi wa wanadamu wote katika mwili, basi yeye hakuweza kufananishwa na walele waliozaliwa tena upya.
Kwa kweli Yohana alikuwa ni mkuu katika mtazamo wa kibinadamu. Yeye alilelewa kama Mnadhiri, na aliishi maisha ya kitawa akiwa nyikani akila nzige na asali ya mwitu. Kutokana na mtazamo wa haki wa kibinadamu, ni kweli kuwa Yohana alikuwa ni mkuu. Lakini hii haki ya kibinadamu haina maana yoyote hasa pale inapolinganishwa na haki ya Mungu ambayo inaweza kutolewa kwa yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kwa imani. Kwa sababu ya wale waliofanyika kuwa watu wa Ufalme wa Mbinguni kwa kuamini katika injili ya maji na Roho wameipokea haki ya Mungu, basi hao ni wakuu kuliko mtu yeyote anayeitegemea haki yake binafsi. Mtu anaweza kuwa mwakilishi wa wanadamu katika ulimwengu huu katika mwili, lakini yeye ni mdogo kuliko wale waliofanyika watu wa Mungu kwa kuamini katika injili ya maji na Roho.
Hivyo basi, wakati Yesu aliposema, “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni wapatikana kwa nguvu, na wenye nguvu wauteka,”alisema hiyo kwa sababu Yohana Mbatizaji alikuwa amembatiza mara moja na hivyo kuzipitisha dhambi za ulimwengu kwenda kwa Yesu. Kwa hiyo, Yohanan Mbatizaji alikuwa ni Kuhani Mkuu wa wisho na nabii wa mwisho wa Agano la kale, na huduma yake iliisha pale alipombatiza Yesu na akamshuhudia. Kwa maneno mengine, Yesu anatueleza kuwa kila kitu cha Agano la Kale kiliisha kwa kuonekana kwake na kwa kuonekana kwa Yohana Mbatizaji, na kwa huduma ya Yohana Mbatizaji ya kumbatiza Yesu. Kwa lugha nyingine, tangu wakati ambapo Yohana Mbatizaji na Yesu walikuja hapa ulimwenguni, hapo ndipo haki yote ya Mungu ilitimizwa. Kipindi cha Agano Jipya kilifunguliwa wakati Yesu alipokuja hapa duniani na kubatizwa na Yohana Mbatizaji.
 Kipindi hiki cha Agano Jipya ni kipindi cha nguvu ya injili, ni wakati ambapo yeyote anayeamini katika injili ya maji na Roho anaweza kupokea ondoleo la dhambi na kufanyika mwana wa Mungu. Kadri Agano la Kale lilivyodumu hadi siku za Yohana Mbatizaji, wakati Yesu alipokuja hapa duniani, wakati alipozichukua dhambi za mwanadamu kwa ubatizo wake, akaimwaga damu yake, na kuzitoweshea mbali dhambi zetu zote, basi tangu hapo malango ya Mbinguni yamefunguliwa kwa wote wanaoamini katika Ukweli huu.
Wakati Yesu alipozichukua dhambi zote za kila mmoja katika ulimwengu huu kwa kubatizwa, basi hapo ndipo kipindi cha Agano Jipya kilipoanza. Neno lote la unabii la Agano la Kale lilitimizwa kwa kupitia Yohana Mbatizaji na kwa kupitia Yesu Kristo.
Yesu Kristo alizipokea dhambi zote za wanadamu mara moja na kwa wote kwa kubatizwa na Yohana Mbatizaji, kisha akaimwaga damu yake Msalabani, na kwa sababu hiyo amezitoweshea mbali dhambi zote za ulimwengu. Hii ndio sababu Bwana wetu alisema tangu siku za YohanaMbatizaji hata sasa Ufalme wa Mbinguni wapatikana kwa nguvu.
Yeyote anayeamini katika Ukweli huu anaweza kuingia Mbinguni kwa imani kwa kuwa Yesu alizipokea dhambi za ulimwengu kwa kuupokea ubatizo toka kwa Yohana Mbatizaji. Kwa lugha tofauti, Yesu aliweza kuzichukua dhambi zote za wanadamu mara moja na kwa wote kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuwa amezipitisha dhambi zote za mwanadamu kwenda kwa Yesu. Yohana Mbatizaji aliweza kulitimiza jukumu la kuzipitisha dhambi za ulimwengu kwenda kwa Yesu akiwa kama Kuhani Mkuu wa mwisho wa Agano laKale na hii ni kwa sababu Yohana Mbatizaji alikuwa amezaliwa toka katika ukoo wa Haruni Kuhani Mkuu.
Kule kusema kila mtu anayeamini katika Ukweli huu anaweza kuingia Mbinguni kwa imani ni kutokana na ukweli kuwa Yohana Mbatizaji alikuwa amezipitisha dhambi zote za ulimwengu kwenda kwa Yesu kwa kumbatiza, na pia ni kwa sababu Yesu alizichukua dhambi za ulimwengu na ndio maana kipindi cha wokovu kwa mwanadamu kimetufikia. Kwa tukio hili la kihistoria, kipindi cha Agano la Kale kiliisha, na kipindi cha Agano Jipya kilianza.
Yesu aliitimiza huduma yake kama Mwokozi wetu mkamilifu kwa kuzichukua dhambi zetu zote za mwanadamu kwa ubatizo wake, na kwa kuimwaga damu yake, na kwa kufufuka tena toka kwa wafu. Hivyo basi, wakati mpya umefika kwa wale wote wanaoamini katika ubatizo ambao Yohana Mbatizaji aliutoa kwa Yesu, ambapo Ufalme wa Mbinguni unapatikana kwa nguvu.
Ukweli ni kuwa Ufalme wa Mbinguni hauwezi kuchukuliwa kwa nguvu ya kimwili. Sasa, maana ya kiroho ya kifungu hiki ni ipi? Maana yake ni hii: Yesu anatueleza juu ya fumbo la Mbinguni, kwamba mtu yeyote anaweza kuingia Mbinguni kwa kuamini katika injili hii kwa sababu Yesu alizipokea dhambi zote za ulimwengu wakati Yohana Mbatizaji alipombatiza Yeye, na kwa sababu ya kusulubiwa na kuimwaga damu yake na kufufuka tena toka kwa wafu.

Bwana wetu alisema, “Manabii wote na torati walitabiri hadi wakati wa Yohana.”Kwa maneno mengine, unabii wa Agano la Kale ulidumu hadi wakati wa Yohana Mbatizaji. Na kwa kweli ni sahihi kusema kipindi cha Agano la Kale kilidumu hadi kuzaliwa kwa Yesu. Lakini unabii wa Agano la Kale ulitimizwa kiroho wakati Yohana Mbatizaji alipombatiza Yesu.

Jumamosi, 31 Mei 2014

INJILI YA MAJI NA ROHO

MAANA YA UBATIZO
Ubatizo maana yake kusafishwa, kuzikwa, (kuzamishwa) na maana ya kiroho kutwikwa dhambi kwa kuwekea mikono, kama ilivyofanywa katika Agano la kale, (Walawi 4:29, 16:21).
Wakati wana wa Israeli walipotoa sadaka ya upatanisho katika nyakati za Agano la Kale, isingekuwa njia sahihi kumchinja mnyama wa sadaka pasipo kwanza kuwekewa mikono juu ya kichwa chake kwa kutwikwa dhambi juu yake kwa niaba yao na ilikuwa ni kuonyesha jinsi ya ubatizo wa Yesu utakao kuja katika Agano Jipya. Hivyo inakuwa ni kosa na kuvunja sheria ya Mungu kuamini msalaba wa Yesu pekee bila kuamini pia ubatizo wake.
Katika Agano Jipya, ubatizo wa Yesu na Yohana Mbatizaji ulikuwa ni kusafisha dhambi za ulimwengu. “ubatizo wa Yesu” una maana ya kuchukua dhambi zote za wanadamu, kutakaswa kwa dhambi zote za ulimwengu.
Yesu alibatizwa na Yohana Mbatizaji, mwakilishi wa wanadamu na kuhani mkuu katika uzao wa Haruni, na kubebeshwa dhambi zote za ulimwengu juu yake. Hili ni dhumuni kuu la ubatizo.
Maana ya kiroho neno “ubatizo” ni “kutwika, kuzikwa” Hivyo “ubatizo wa Yesu” maana yake dhambi zote alitwikwa Yesu na kuhukumiwa badala yetu. Ili kuokoa wanadamu, Yesu alizibeba dhambi zetu zote kwa ubatizo wake na kufa kwa dhambi hizo.
Yote haya, kifo chake na pia kifo chako na changu wenye dhambi wote ulimenguni na ufufuko wake ni ufufuo wa watu wote. Kujitoa kwake sadaka ni wokovu wa wenye dhambi na ubatizo ni ushuhuda Halisi katika kutusafisha dhambi zetu zote sisi walimwengu. Hivyo, Mtume Paulo alisema “Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamira safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. (1Petro 3:21)
Sisi kama waumini wa Kristo yatupasa kujifunza maana halisi ya ubatizo, maana katika huo tunapata wokovu. Maji hayana la kufanya katika wokovu, bali ni ishara ya nje ya kile ulichokiamini ndani yako.
Rejea maandiko haya katika Biblia “Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderea. Mtu wa elimu akafika Efeso; alikuwa hodari katika maandiko. Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; Na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu. Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukuwa kwao, wakamweleza njia ya bwana kwa usahihi zaidi. (Matendo 18:24-26)
Apolo aliyajua maandiko na alijua ubatizo wa Yohana tu, ambao haukuwezesha waumini kupokea Roho Mtakatifu, hata Prisila na Akila walipomsikia walimchukua na kumfundisha njia ya bwana kwa usahihi zaidi. Hata leo hii kuna watu wengi hawajui maana ya ubatizo kwa ujumla wake. Kwanini Apolo alifundishwa njia ya bwana kwa usahihi zaidi? Jibu la swali hili tutalipata katika aina nyingine ya ubatizo wa Yesu.
Watu wengi ulimwenguni hawafahamu ni kwanini Yesu alikuja katika ulimwengu na kubatizwa na Yohana Mbatizaji. Hivyo hebu tuzungumzie sababu za ubatizo wa Yesu na juu ya Yohana Mbatizaji aliyembatiza Yesu.
Kwanza, yatupasa kuwaza juu ya nini kilichomfanya Yohana Mbatizaji abatize watu katika mto Yordani. Inaelezwa katika( Mathayo 3:1-12) kwamba Yohana Mbatizaji alibatiza watu ili kuwalejesha kwa Mungu toka katika dhambi kwa kutubu kwao.
Kimsingi umuhimu wa ubatizo uliofanywa na Yohana Mbatizaji ulikuwa kwaajili ya toba ambayo iliwarudisha Waisrael kwa Yesu ambaye angekuja baadaye. Toba maana yake kugeuka toka maisha ya dhambi na kumwani Masiya ili kusamehewa dhambi zote.
Jambo la kwanza Yesu alilolifanya katika huduma yake ya wazi ilikuwa ni kubatizwa na Yohana Mbatizaji. Dhambi zote za ulimwengu zilitwikwa juu yake kwa njia hii.
Hivyo ubatizo wa Yesu ulikuwa ndiyo mwanzo wa wokovu wa Mungu kwa wanadamu pamoja pia na tendo la haki kwa Yesu kuweza kutakasa dhambi zote za ulimwengu juu yake kwa njia ya ubatizo.
Yesu alikuja ulimwenguni na kubatizwa na Yohana Mbatizaji, injili ya ufalme wa Mbinguni ndipo ilipoanza. Mbingu zilifunuka kwa ubatizo wake kama ilivyoelezwa katika Mathayo 3:15 ilikuwa sawa sawa kabisa na sadaka ya upatanisho iliyoelezwa katika (Walawi 1:1-5, 4:27-31) nyakati za Agano la kale.
Moja ya mafundisho potofu katika nyakati hizi za imani ya kikiristo ni kwamba, utaweza kuokolewa unapomkiri Yesu kuwa mwokozi kwa kuwa bwana ni pendo. Biblia inasema “Yeyote aliitaye jina la Bwana ataokolewa” (Matendo 2:21, Warumi10:13) ambapo pia inasema “Si kila mtu aniitaye Bwana Bwana ataingia ufalme wa mbinguni, bali wale wote watendao mapenzi ya Baba yangu wa Mbinguni”(Mathayo 7:21).
Kwanini tujifunze ubatizo kwa undani, hebu soma kifungu hichi” Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko, akawauliza je? Mlimpokea Roho Mtakatifu Mlipoamini? Wakamjibu, La hata kusikia kwamba kuna roho Mtakatifu hatukusikia. Akawauliza mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, kwa ubatizo wa Yohana. Paulo akisema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu.” (Matendo 19:1-4)
“Je ulipokea Roho Mtakatifu pale ulipoamini?” hata waKristo swali hili hawalifahamu. Mtume Paulo aliwauliza waamini wa Yesu kama walipokea Roho Mtakatifu pale walipoamini kwa mara ya kwanza na akafafanua jinsi waamini wanavyoweza kumpokea Roho Mtakatifu. Katika fungu hili la maneno kwa kupata ushuhuda wa nguvu ya ubatizo wa Yesu, Paulo aliamsha imani zao tena. Apollo alipokuwa Korintho, baada ya Paulo kupita Asia ndogo, na kufika Efeso, na kuwakuta wanafunzi wa Yesu, aliwaambia, “Je mlipokea Roho Mtakatifu mara mlipoamini?” Usharika wa korintho haukuelwa lolote juu ya ukweli huu, kuwa wanapokea Roho Mtakatifu wakimwamini Yesu.
*      Wangelijua na kuamini ubatizo ambao Yesu alipokea
Kusikia kuwa walikuwa wamebatizwa kupitia ubatizo wa Yohana pekee, Paulo alifafanua juu ya mahusiano ya ubatizo wa Yesu na ule wa Roho Mtakaifu. Ndipo wakaelewa maana ya ubatizo wa Yesu walioupokea. Kuna tofauti kubwa sana kati ya kumwamini yeye huku tukijua maana ya ubatizo ambao Yesu alipokea kutoka kwa Yohana, na kumwamini yeye bila kujua maana ya mahusiano ya ubatizo wa Yesu na ule wa Roho Mtakaifu. Ndipo wakaelewa maana ya ubatizo wa Yesu walioupokea.
Sasa je, ni ubatizo gani Yohana aliutoa kwa watu? Yohana aliwaambia watu kutubu, kuikimbia dhambi na kumrudia Mungu. Ubatizo ambao Yohana aliutoa ulikuwa ni ubatizo wa kutubu ambao uliwafanya watu watubu. Lakini ubatizo ambao Yesu alipokea kutoka kwa Yohana katika Mathayo 3:13-17 ulipokewa ili kuitimiza haki ya Mungu, na ndio maana tunasema ulikuwa tofauti na wa Yohana.
Ubatizo ambao Yesu aliupokea kutoka kwa Yohana ulikuwa wa kuondoa dhambi za wanadamu.
Imani yao ilikuwa tofauti kabisa na imani ya Paulo, kwani ubatizo walioupokea haukuwa wa kujua picha halisi ya ukweli huu.
Sasa ubatizo huu ni kuikamilisha haki ya Mungu unamaanisha nini? Una maana kwamba kwa
kubatizwa, Yesu alichukua dhambi za wanadamu kuanzia dhambi ya Adamu mpaka Mwanadamu yule wa mwisho.

Mathayo 3:15-16 Inasema “Yesu akajibu akasema, na iwe hivyo, kwa kuwa imetupasa kuitimiza haki yote, ndipo akamruhusu.”Haki ya Mungu inaweza kupatikana katika ubatizo ambao Yesu alipokea ndani ya imani inayoikubali damu ya msalabani kwa hiyo wale ambao mioyo yao imesamehewa dhambi kwa kuamini ubatizo huo na damu yake msalabani ni lazima wapokee ubatizo wa maji kwa imani. Kwa nini? Kwa sababu kwa imani ya ubatizo wake, dhambi zote zimeondoshwa kikamilifu, ndio maana Paulo alieleza ubatizo wa Yesu kwa wale ambao hawakupokea Roho Mtakatifu.
Watu wengi wamekuwa wakijaribu kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia wanazozifahamu wao kama kurudia rudia maneno na nyinginezo, lakini hizo si njia sahihi katika wokovu.
Yatupasa kuwa na uelewa sahihi katika neno la ubatizo, ukisoma (Matendo 18:24-26, na Matendo 19: 1-4) utaona ya kwamba Apolo alipita Efeso akahubiri ubatizo, na uelewa wake ulikuwa katika ubatizo wa Yohana tu. Na Paulo alipita eneo hilo hilo la Efeso baada ya Apolo kuondoka na kuwafundisha ubatizo kwa usahihi zaidi ambapo walipokea Roho Mtakatifu. Hivyo katika ubatizo tunapokea Roho Mtakatifu.
Damu ya Yesu msalabani ni matokeo ya ubatizo na si kumwaga damu msalabani ndiko kuliko mwezesha Yesu kubeba dhambi zetu. Alibeba dhambi zetu pale alipo batizwa na ndipo alipokwenda msalabani akiwa tayari amekwisha beba dhambi hizo zote za ulimwengu hatimaye kufa ili kuleta upatanisho wa dhambi za ulimwengu.
Hivyo msalaba ni matokeo ya ubatizo aliopokea Yesu, kwa kuwa Yesu alikwisha beba dhambi zetu kwa njia ya ubatizo wake, kumwaga damu msalabani ndiko hitimisho la kuelekea upatanisho wa dhambi zetu zote.

Unapomtwika Yesu dhambi zako katika ubatizo unakuwa umesamehewa makosa yako yote, ndipo Roho Mtakatifu anapata nafasi ya kukaa ndani yako. Tunaweza kuzaliwa upya kiroho kwa kuamini ubatizo na damu ya Yesu.

Jumatatu, 5 Mei 2014

TOBA YA KWELI KATIKA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU


(Matendo 2:38) “Petro akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”
Biblia inasema katika (Matendo 2) kwamba mahubiri ya Petro yaliwagusa kwa undani watu na hata kuwasababisha watubu dhambi zao. Walichomwa mioyo yao na kumwambia Petro na mitume wengine, “Tutendeje ndugu zetu? Petro akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kisto mpate ondoleo la dhambi zenu nayinyi mtapokea kipawa cha Roho Mtaakatifu” (Matendo 2:38). Mahubiri ya Petro yanatuonyesha wazi kuwa imani katika injili nzuri ya maji na ya Roho ni ya muhimu sana katika kumpokea Roho Mtakatifu na pia inatuonyesha jinsi toba la kweli lilivyo. Tunapaswa kutambua kuwa tunaweza kumpokea Roho Mtakatifu sambamba na ondoleo la dhambi kwa kuyaangalia maandiko matakatifu kwa karibu na kwa kuamini katika injili nzuri ya maji na ya Roho.
Jambo la kwanza tunalotakiwa kuwa nalo ili kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ni imani katika toba la kibiblia. Hata hivyo, tunatakiwa kuwa makini ili tusije tukalielewa toba hili kuwa ni majuto. Toba maana yake ni imani katika Yesu Kristo. Tunaweza kuona katika Biblia kuwa watu walijuta kwa kumsulubisha Bwana. Walijuta kumuuliza Petro kwamba wafanye nini na walizikiri dhambi zao hata kabla ya Petro kuwaambia watubu. Tunaweza kuona kuwa toba ambalo Petro alilizungumzia halikuwa kuzijutia dhambi wala kuzikiri, bali ilikuwa ni kumpokea Yesu Kristo katika moyo wa kila mtu kama Mwokozi na kuwa na imani katika injili nzuri ambayo Yesu ametupatia. Na hii ndiyo asili nzuri ya toba.
Upendo wa Yesu Kristo ulikuja kwetu kabla hayajakuwepo majuto-binafsi kwa dhambi za mioyo yetu. Hii inamaanisha kuwa Yesu alizichukua dhambi zetu pale alipobatizwa katika Mto Yordani, alikufa Msalabani, na kisha akafufuka toka kwa wafu. Kwa njia hii, alizisafisha hatia na dhambi zetu zote.
Toba la kweli maana yake ni kuamini katika ukweli huu. Je, unafikiri kuwa dhambi zetu zimesafishwa moja kwa moja kwa kule kujuta na kuomba msamaha? Ukweli ni kuwa hili sio toba la kweli. Toba la kweli maana yake ni kupokea ondoleo la dhambi zetu kwa kuamini katika injili nzuri ya ubatizo wa Yesu na damu yake. Biblia inasema kuwa tunasamehewa dhambi zetu kwa toba. Vivyo hivyo, inatupasa kuiamini injili ya ubatizo wa Yesu na damu yake ili tuweze kupokea ondoleo kamili la dhambi zetu.
Petro alitoa huduma ya ubatizo “katika jina la Yesu Kristo” kwa wale waliomwamini Yesu. Yesu alibatizwa ili aweze kuzichukua dhambi za wanadamu wote. Ubatizo na kifo chake juu ya Msalaba ulikuwa ni ukamilifu wa injili nzuri inayowawezesha waamini kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu (Mathayo 3:15-17). Mwanadamu anaweza kutakaswa kwa kuamini katika ubatizo wa Yesu na damu yake pale Msalabani. Kwa kifupi, wale waliopokea ondoleo la dhambi kwa kuamini katika injili wamempokea Roho Mtakatifu.
Je, sala zitaweza kuleta uwepo wa Roho Mtakatifu ndani?
Watu hawatoweza kupokea msamaha wa dhambi na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao hata ikiwa watafanya maombi ya dhati kutaka uwajilie. Ili tuweze kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu, ni muhimu kuamini injili njema iliyokamilishwa kwa ubatizo wa Yesu na damu yake pale msalabani. Roho Mtakatifu wa Mungu hutunukiwa kwa wale walio kuwa na dhambi amabao wametakaswa moja kwa moja.
Imani katika injili ni kumkubali Yesu kama mwokozi wa kweli. Matendo 2:38 inasema, “tubuni mbatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”Mtume Petro alisema kwamba uwepo wa Roho Mtakatifu hutolewa kwa wale walio samehewa dhambi zao kwa njia ya imani katika toba ya kweli. Msamaha wa dhambi na kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ni pacha.
Biblia inasema“Tubuni mkabatizwe kilammoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwa ahadi hii ni kwaajili yenu na kwa watoto wenu kwa watu wote walio mbali na kwa wote watakao itwa na Bwana Mungu wetu wa mbinguni” (Matendo 2:38-39).
Mtu aweza kupokea Roho Mtakatifu kwa sharti kwamba moyo wake umetakaswa, usio na dhambi. Hivyo imetupasa kuamini injili ambayo Yesu Kristo ametupatia. Lazima tutakaswe baada ya kupokea msamaha wa dhambi kwa kuamini injili njema inayosema dhambi zetu zote ulimwenguni zilitakaswa pale Yesu Kristo alipobatizwa. Ndipo hapo tutakapoweza kupokea Roho Mtakatifu. Ni mapenzi ya Mungu kwa Roho Mtakatifu kuweka makazi ndani ya wanadamu “maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kutakaswa kwenu” (1 Wathesalonike 4:3).
Msamaha wa kweli hutolewa si kwa njia na juhudi za watu kujitoa muhanga au kuwa wema, bali kwa kuamini injili ambayo Mungu Utatu Mtakatifu aliyoitimiza kupitia Yohana mbatizaji. Mungu Utatu Mkatifu huwatunukia uwepo wa Roho Mtakatifu kwa wale wote waliokwisha samehewa dhambi zao kwa kuamini injili njema. Umati wa watu ulichomwa mioyo pale ulipo yasikia Petro aliyoyanena siku ile ya pentekoste. Walipaza sauti na kuuliza “Tutendeje ndugu zetu?”  (Matendo 2:37). Hii hudhihirisha kwamba tayari wamekwisha badilishwa kifikra zao na sasa wanamwamini Yesu Kristo kuwa ni mwokozi na Bwana wao. Na pia wamekwisha okolewa kutokana na dhambi zao kwa kuamini toba ya kweli aliyo ihubiri Petro. Msamaha wa dhambi ulikwisha tolewa kwa wanadamu wote kwa kutegemea imani zao katika injili njema ya ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Dhumuni la ubatizo wa Yesu ni kumwezesha yeye abebe dhambi za ulimwengu. Kwa kuamini hili ndilo sharti moja wapo muhimu la kupokea Roho Mtakatifu. Mungu ametupatia uwepo wa Roho Mtakatifu kwa wale wanao iamini injili ya kweli iliyo na msingi wa ubatizo wa Yesu Kristo. “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini na tazama mbinguni zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama huwa akija juu yake” (Mathayo 3:16). Kuja kwa Roho Mtakatifu katika siku ile ya pentekoste kuna uhusiano wa pekee na imani ya mitume katika injili njema: ubatizo wa Yesu, damu yake msalabani na ufufuko.
Katika Matendo inasema kwamba watu waliobatizwa katika jina la Yesu walimpokea Roho Mtakatifu moja kwa moja katika muda huo huo. Yatupasa kuamini kwamba kupokea Roho Mtakatifu ni karama ya pekee toka kwa Mungu. Ili tuweze kupokea karama hii, inatupasa kwamba dhambi zetu zote zisafishwe kwa kupitia imani katika ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani.
Kulingana na Matendo, wale wote walio sikia mahubili ya Petro ambapo alishuhudia akisema, “Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”  (Matenda 2:40).  Walitii maonyo yake na kubatizwa. Kile tunachojifunza tokakatika biblia ni kwamba, mitume katika siku hizo za kanisa la mwanzo walimpokea Roho Mtakatifu kwa msingi wa imani zao katika ubatizo wa Yesu Kristo na damu yake msalabani. Hili ndilo sharti muhimu la kuweza kumpokea Roho Mtakatifu. Imani katika ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani ni jambo lisilo wekwa kando ikiwa mtu atahitaji msamaha wa dhambi.
Imani ituongozayo katika kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia ya toba ya kweli.
Hebu tuangalie katika Mtendo 3:19,“tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.” Tutawezaje basi kuelezea nini maana ya toba? Hebu na tufikirie upya tena.
Katika biblia, toba maana yake ni kuirudia imani ya ukombozi. Katika nyakati hizo watu walishika tabia kama walivyo penda nafsini mwao na kuviabudu vitu vilivyo umbwa na Mungu. Lakini baada ya kugundua kwamba Yesu Kristo alikwisha kuwaokoa toka dhambini kwa maji na kwa damu yake, ndipo wakaanza kubadilika. Hii ndiyo toba ya kibiblia. Toba ya kweli ni kuirudia injili njema ya maji na Roho.
Ni ipi toba iliyo ya kweli inayo hitajika katika kumpokea Roho Mtakatifu? Ni katika kuamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani “zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.”Ikiwa watu watakuwa na imani hii, basi watasamehewa dhambi zao na kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa kuwa Yesu amewatakasa wenye dhambi wote duniani kwa njia ya ubatizo wake na damu yake msalabani, imetupasa basi kuamini hili ili tuweze kupokea ukombozi na uwepo wa Roho Mtakatifu.
Ili tuweze kumwamini Yesu na kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu, inahitajika dhambi zote zitwikwe juu ya Yesu kwa imani ya ubatizo wake na kifo chake msalabani. Yatupasa kuamini kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu zote na kufa msalabani ili ahukumiwe kwa ajili ya dhambi hizo. Hii ndiyo imani sahihi na toba ya kweli, amabayo inayotuwezesha kuwa na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu.
Roho Mtakatifu huja juu ya wale wote walio kwisha samehewa dhambi zao zote. Kwanini Mungu ametoa Roho Mtakatifu kama karama kwa wale wote walio kwisha pokea ukombozi? Kwasababu Roho Mtakatifu, akiwa mtakatifu, anahitaji kuweka makazi ndani yao na kuwachapa mhuri kuwa wana wa Mungu.
Roho Mtakatifu ni Mungu. Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja. Ni nafsi tatu lakini ni Mungu mmoja kwa wale wote wenye kuamwamini Yesu. Baba alikuwa na mpango wa kutuokoa sisi tokana na dhambi zetu, na hivyo Mwana Yesu alikuja ulimwenguni akabatizwa na Yohana ili kuzichukua dhambi za ulimwengu, alikufa msalabani, alifufuka toka kuzimu siku ya tatu na kupalizwa mbinguni. Roho Mtakatifu hutuongoza katika kuiamini injili njema kwa kushuhudia juu ya ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Mungu huwaweka mihuri wale wote walio kwisha kuokolewa kwa kupitia Roho Mtakatifu. Mungu huwatunukia Roho Mtakatifu wale wote wanao amini injili inayo sema kuwa, Yesu alizichukua dhambi za ulimwengu. Mungu huwapa Roho Mtakatifu kama ahadi na kama mhuri kuashiria kuwa ni watoto wake. Roho Mtakatifu ni uthibitisho wa mwisho katika wokovu wa dhambi kwa wale wenye kuamini injili njema.
Wale wote walio na Roho Mtakatifu ni watoto wa Bwana. Wale walio na uwepo wa Roho Mtakatifu wakati wote hupata nguvu upya kila wakati. Huwa na imani madhubuti katika maneno ya Mungu juu ya ubatizo waYesu na damu yake pale msalabani. Ni wenye furaha ya kweli. Wale wote wenye kutubu
kwa njia iliyo sahihi hawatakuwa na dhambi tena mioyoni mwao na hivyo watakuwa na uwepo wa Roho Mtakatifu.

Biblia inasema kwamba, ipo toba iletayo msamaha wa dhambi. Je, umekwisha fanya toba ya aina hiyo? Ukitubu na kuifuata imani ya kweli, nawe pia utaweza kupokea injili njema. Nakusihi utubu dhambi zako na umpokee Roho Mtakatifu. Je, uko tayari kutubu na kuamini injili njema ambayo itakuongoza katika kumpokea Roho Mtakatifu?

Jumatano, 30 Aprili 2014

SHERIA ALIZOTUPATIA MUNGU


Mungu aliweka sheria ulimwenguni kwa sababu zifuatazo;
1. aliwapa wenye dhambi sheria na amri ili waokolewe kwa dhambi zao “ kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria” (Warumi 3:20)
2. Sheria ya pili ni sheria ya imani iokoayo wenye dhambi. “Sheria ya Roho wa uzima” ( Warumi 8:2) inayotoa njia ya wokovu kupitia imani katika Yesu Kristo mwokozi wetu (Warumi 5:1-2).Yesu alishuka ulimwenguni kutimiza hii sheria. Yesu aliweka Sheria ya wokovu ili kuokoa wale wote wenye dhambi ulimwenguni.
Kwa asili kulikuwa na sheria mbili zilizotolewa na Mungu: sheria ya dhambi na mauti na ile sheria ya roho wa uzima. Sheria ya Roho wa uzima ilimwokoa Paulo toka katika sheria ya dhambi na mauti. Hii ilimaanisha kuwa kwa kuamini katika ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani, ambavyo vilichukulia mbali dhambi zake zote, Paulo auliungana na Yesu na kisha akaokolewa toka katika dhambi zake zote. Sisi sote ni lazima tuwe na imani inayotuunganisha na ubatizo wa bwana na kifo chake msalabani. Soma fungu hili; Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo. Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.( wakolosai:2:11-12)
Mungu aliweka sheria ya imani kwa wale tu wenye kuamini wokovu utokanao kwa maji na roho.  Yeye atakaeokolewa na kuwa mwana wa Mungu yampasa kwanza kuamini sheria hii ya imani ambayo Mungu ameitoa. Ndiyo pekee njia ya kuokoka. Kwa haya, ameruhusu njia ya kwenda Mbinguni kwa wale wenye kuamini kuzaliwa kiroho katika kweli tokana na sheria hii.
Vipo vipengele 613 vya sheria ya Mungu vinavyohusu maisha yetu ya kila siku. Lakini iliyo kuu kati ya hii ni amri kumi ambazo yatupasa kuzifuata mbele ya Mungu. Kupitia amri zilizo andikwa na Mungu tutaweza kutambua ni kwa kiasi gani tumeacha utii kwake. (Warumi 3:19-20).
Sababu ya Mungu kutupatia amri zake ilikuwa ni kutufanya tugundue na kuziona dhambi zetu, kamwe hatutoweza kuzishika amri zote, hivyo yatupasa kunyenyekea kwa kukubali ukweli kwamba sisi ni wenye dhambi na Mungu anajua kwamba kamwe hatutoweza kuishi kwa kufuata sheria yake. Hivyo alishuka ulimwenguni kama mwanadamu, alibatizwa na kuhukumiwa msalabani. Kujaribu kuishi kwa kufuata sheria ya Mungu ni dhambi ya kiburi. Hatupaswi kufanya hivyo.
Ku wapi,basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La ! bali kwa sheria ya imani. Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria ( Warumi 3:27-28) Pia soma katika (Warumi 4:1-8)

Kuna sehumu imeandikwa imani bila matendo imekufa lakini soma kwa umakini utaona ya kuwa si matendo ya sheria bali matendo ya imani ndiyo yanayo hitajika. Je mwenye Roho Mtakatifu anaweza kutenda dhambi makusudi kwa sababu tu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria? Hapana, maana mtu huyu amempokea Roho Mtakatifu na matunda ya Roho.

Ijumaa, 18 Aprili 2014

AMINI ILI ROHO MTAKATIFU AKAE NDANI YAKO


(Mathayo 25:1-12)
“Ndipo ufalme wa Mbinguni utakapofanana na wanawali waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana harusi. Watano wao walikuwa wapumbavu na watano wenye busara. Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao na wasitwae na mafuta pamoja nao, bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. Hata bwana harusi alipokawia wote wakasinzia wakalala usingizi. Lakini usiku wa manane pakawa na kelele, haya bwana arusi tokeni mwende kumlaki. Mara wakaondoka wanawali wale wote wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara tupatieni mafutayenu kidogo maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu wakisema hayatatutosha sisi naninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie. Na hao walipokuwa wakienda kununua mafuta bwana harusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana Bwana tufungulie Akajibu akasema, Amin nawaambia siwajui ninyi. Basi kesheni kwa sababu hamwijui siku wala saa.”
Ni watu gani walio mfano wa wanawali walio na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao?
Katika kifungu kilichopita hapo juu tumeona wanawali watano wenye busara na wapumbavu, wanawali wapumbavu waliwaomba wale wenye busara kuwagawia kiasi cha mafuta ya taa lakini wenye busara  wakawajibu wale wapumbavu “hayatatutosha sisi na ninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie”.Hivyo wakati wale walio wapumbavu wakienda nje kununua mafuta hayo, wale wenye busara walikuwa nayo katika taa zao na kuingia katika sherehe za harusi. Sasa basi ni kwanamna gani tunaweza kuyatayarisha mafuta kwa ajili ya Bwana? Kitu pekee tunachoweza kufanya ni kuusubiri msamaha wake wa dhambi katika mioyo yetu.
Katikakati ya watu tunaweza kupata aina mbili za imani. Moja ni imani ya injili ya msamaha wa dhambi. Hii ndiyo inayopelekea kumpokea Roho Mtakatifu. Nyingine ni ile ya kuwa mwaminifu wa kanuni za dini bila kujali mtu kusamehewa au kutosamehewa dhambi.
Kwa wale wote walio waaminifu kwa kanuni za dini, injili hubaki kuwa mzigo kwao kuichukulia. Kama walivyo wanawali wapumbavu waliokwenda nje kununua mafuta pale bwana harusi alipo ingia, wale wote wanaohama toka nyumba moja ya kuabudu kwenda nyingine kwa matumaini ya kumpookea Roho Mtakatifu ndani yao, hawamdanganyi yeyote bali nafsi zao. Watu wa aina hii ni wenye kiburi ambao kwa kweli ndiyo wanao hitaji kuwa na imani ya injili njema katika mioyo yao kabla ya siku ya hukumu. Watuhawa hutamani kuwa na Roho Mtakatifu kwa kumuonyesha Mungu ukereketwa wao.
Tuone ushuhuda wa shemasi mmoja aliyefanya juhudi kubwa katika kumpokea Roho Mtakatifu. Ushuhuda huu kwa hakika utatusaidia sana. “Nilifanya kila niwezalo ili kumpokea Roho Mtakatifu. Nilidhani kwamba, ikiwa nitajitolea nafsi yangu kwa imani yangu kwa uaminifu nitaweza kumpokea Roho Mtakatifu na matokeo yake nilijikuta kuhama kanisa moja hadi jingine, nyumba moja ya sala kwenda nyingine. Watu katika moja wapo ya nyumba hizi za sala walikuwa wakipiga kinanda cha umeme ikiwa ni sehemu ya ibada.Mchungaji aliyekuwa akiongoza mkutano huu aliwaita wale wote waliohitaji kumpokea Roho Mtakatifu moja baada ya mwingine na walipo wekewa mkono wa mchungaji katika mapaji ya nyuso zao, kila mtu baada ya tendo hilo alianza kunena kwa lugha. Mchungaji aliruka huku na kule akishikilia kipaza sauti nakupaza sauti “pokea moto, moto, moto!” na kuweka mkono wake juu vichwa vya watu na kusababisha baadhi yao kupagawa na kuanguka. Mwanzoni nilikuwa na wasiwasi ikiwa tendo hili linamaana ya kumpokea Roho Mtakatifu lakini tayari nilikuwa nimeathirika na mikutano ya aina hii. Licha ya haya yote kamwe sikuweza kupokea Roho Mtakatifu.
Baada ya tukio hili niliamua kwenda milimani nakujaribu kulia na kuomba usiku kucha nikiwa nimeegemea mti. Wakati mwingine nilijaribu kufanya maombi ndani ya pango lakini yote haikusaidia. Baada ya yote haya nilijaribu kufanya maombi usiku kucha kwa siku arobaini lakini kamwe sikuweza kumpokea Roho Mtakatifu. Semina hii ilikuwa ikifanyika kwa juma mara moja na kufululiza majuma saba.
Katika semina hii kulikuwa na mafundisho kuhusu upendo wa Mungu, msalaba na ufufuko wa Yesu, tendo la kuwekewa mikono, tunda la roho na kukua kiroho. Katika muda huo wakati ratiba ya semina ilipokuwa ikikaribia kuisha, mnenaji mkuu katika semina hiyo aliniwekea mikono juu ya kichwa changu na kuanza kuniombea ili niweze kumpokea Roho Mtakatifu huku nikimfuatisha maneno yake kama alivyonielekeza. Nilitulia na kunyanyua viganja vya mikono yangu na kuelekeza juu na kuanza kupiga kelele “la-la-la-la!” kwa kurudia rudia. Mara ghafla nilipokuwa nikipiga kelele “la-la-la-la!” nilianza kunena moja kwa moja lugha ya ajabu. Watu wengi walinipongeza baada ya hapo katika kumpokea Roho Mtakatifu. Lakini nilipokuwa mwenyewe nyumbani nilihofu. Hivyo nikaanza kujitolea kufanya kazi katika semina hiyo. Nilidhani kwamba ilinipasa kujitolea kwa kazi kama hii mapema sana. Hivyo nilisafiri nchi nzima katika kutoa huduma na nilipo wawekea mikono wagonjwa, magonjwa yao yalionekana kupona ingawa baadhi yaliwarudia baadaye.  Na baadaye nikapata maono na nikagundua yakuwa naweza pia kutoa unabii. Chakushangaza unabii wangu mara nyingi ulikuwa wakweli.
Tokea hapo nilialikwa sehemu za kila aina na kulakiwa kwa shangwe. Lakini bado nilikuwa na hofu ndani yangu ndipo nikasikia sauti ikisema “usitange tange toka sehemu moja kwenda nyingine namna hii badala yake nenda ukawasaidie jamaa zako nyumbani katika kupokea wokovu.” Hata hivyo sikuelewa maana halisi ya wokovu. Nilichokuwa nakielewa nikile wengi walichokuwa wakisema kwamba, ikiwa nitaacha kuzitumia karama za Roho Mtakatifu basi atanipokonya. Kwa upande mwingine nilihofu kutumia uwezo wangu lakini sikuweza kujizuia hilo.
Siku moja nilisikia kuwa yupo mwanamke fulani ambaye ni wa dini ya Shama aliyehitaji kumwamini Yesu, hivyo mimi pamoja na rafiki yangu tulikwenda kumtembelea. Hatukumfahamisha juu ya ujio wetu kabla. Lakini mwanamke huyo alikuwa akitusubiria mlangoni nakuanza kutuambia “nilishajua kwamba mnakuja” mara ghafla alianza kutunyunyizia maji na kusema “hakuna tofauti kati ya ushama wa mashariki na ushama wa magharibi”. Alituita sisi kuwa ni “washama wa Yesu” na kutunyoshea kidole akisema “huyu ndugu ni muoga lakini huyu si muoga” Kile ambacho mwanamke huyu alichokua akisema kiligeuka kuwa kama pigo katika kichwa. Nikaanza kuwaza kwamba yote niliyokuwa nikiyatenda hayakuwa tofauti nayale ambayo dini ya shama wakitenda. Hakuna nilichokuwa nimekwisha tenda ili kumleta Roho Mtakatifu ndani yangu kwa sababu bado nilikwa na dhambi moyoni.”
Tokana na ushuhuda huu tunajifunza kwamba, swala la kumpokea Roho Mtakatifu lipo nje ya uwezo wetu. Kwasababu imani ya aina hii haihusiani na injili ya Mungu kwani wale wote wanaoishi katika aina hii ya udini ndiyo wasio kuwa na mafuta katika taa zao.
Taa katika biblia inamaana ya kanisa, na mafuta maana yake Roho Mtakatifu. Biblia inakusudia kwamba wale wote wanao hudhuria kanisani, iwe ni kanisa la Mungu au si la Mungu pasipo kumpokea Roho Mtakatifu, bado ni wapumbavu.
Wapumbavu wote hupandisha mori siku hata siku. Watu hawa hupandisha hisia zao kali na kujitolea kimwili mbele ya Mungu. Ikiwa tungelisema kuwa hisia zetu ziwe za kiwango cha sentimita 20 na hivyo kufanya kila siku 1 kupandisha sentimita 1, basi ingelichukua siku 20 kuweza kufikia kiwango cha juu katika hisia zetu zote. Hisia zao katika imani hupata nguvu mpya kwa kila maombi ya asubuhi, maombi ya usiku kucha, maombi ya kufunga na mikutano ya uamsho na pia katika maisha ya kila siku. Huathirikana tabia hii ya kudumu katika kuenenda kwa hisia.
Hisia zao hupanda katika jina la Yesu. Huudhuria kanisani ili kupandisha hisia zao, lakini mioyo yao bado imechanganyikiwa huku wakitafuta sababu nyingine. Sababu ya hili ni kwamba imani yao imetokana na kile kinachotokana na mwonekano wa nje kimwili na hivyo kuhitaji shinikizo la mara kwa mara ili kusukuma hisia zao ili moto wa hisia usizimike ndani yao. Hata hivyo bado hawato weza kumpokea Roho Mtakatifu kwa aina hii ya imani. Kwa kupandisha hisia hizo kamwe hakutoweza kuwafanya kumpokea Roho Mtakatifu.
Sote imetupasa kuwa tayari na imani sahihi ili kuweza kumpokea Roho Mtakatifu katika uwepo kamili wa Mungu. Na ndipo pekee tutakapo kuwa na haki ya kumpokea Roho Mtakatifu. Ni kwanamna gani basi tunaweza kuwa na imani ambayo inatupa haki ya kuwa na Roho Mtakatifu? Ukweli upo katika injili njema ambayo ilikamilishwa kwa ubatizo wa Yesu Yordani na kumwaga damu yake Msalabani.
Mungu alituita kuwa sisi ni kama “wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu” (Isaya 1:4). Lazima tulikubali hili. Kwa asili wanadamu wamezaliwa wakiwa wanadhambi aina 12 (Marko 7:21-23). Wanadamu hawawezi kujizuia kutotenda dhambi tokea wanapozaliwa hadi kufa. Katika Yohana 1:6-7 imeandikwa, “palitokea mtu ametumwa kutoka kwa Mungu jina lake Yohana. Hivyo alikuja kwa ushuhuda ili aishuhudie ile nuru wote wapate kuamini kwa yeye”.Yohana Mbatizaji alimbatiza Yesu na kumtwika dhambi zote za ulimwegu akisema “tazaama mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya dunia” (Yohana 1:29).
Tuliokolewa kwa dhambi zote na kuushukuru ubatizo wa Yesu Kristo. Kama Yohana asingeli mbatiza Yesu Kristo nakutotangaza kwamba alikuwa ndiye mwana kondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu, basi tusingeliweza kumjua Yesu kwamba ndiye aliye beba dhambi zetu zote kuelekea msalabani. Tusingeliweza kuifahamu njia ya kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa hiyo basi tunamshukuru Yohana kwa ushuhuda kwani sasa tunaelewa yakwamba Yesu ndiye aliye beba dhambi zetu zote na hivyo tunaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa imani hiyo.
Kwa imani hii basi tumekuwa wanaharusi tuliotayarishwa kamili kumpokea Yesu Kristo, Bwana harusi. Sisi ni wanawali tulio mwamini Yesu na tumejitayarisha kamili kumpokea Roho Mtakatifu.
Je, unaamini injili ya maji na Roho kwa moyo wako wote? Je, unaanini kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu kwa ubatizo wake kwa Yohana? Biblia inasema “basi imani, chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo” (Warumi 10:17). Nilazima tuamini yakwamba Yesu alibatizwa na Yohana na kufa msalabani ilituweze kumpokea Roho Mtakatifu. Yatupasa kuelawa kwamba kumpokea Roho Mtakatifu kutawezekana ikiwa tutaamini kwamba Yesu alikuja ulimwenguni akiwa kama mwanadamu na kubatizwa na Yohana hivyo alikufa msalabani na kufufuka.
Hata leo hii yapo makundi mawili ya wanaoamini kama ilivyo kwa wanawali kumi katika ile habari ya hapo mwanzo. Sasa basi wewe nawe uko upande upi? Yakupasa ujue ile njia ya kweli ambayo utaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa hakika. Ni kwa imani gani utaweza kumpokea Roho Mtakatifu? Je utaweza kumpokea Roho Mtaktifu kwa kupitia shauku itokanayo na ukereketwa utokanao na dini kama Shama?
Je utaweza kweli kumpokea Roho Mtakatifu katika hali ya kupoteza fahamu? Je utaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini ushabiki wa kidini? Biblia inasema kwamba Yesu alipobatizwa kwa kuzamishwa na kuibuka toka kwenye maji Roho wa Mungu alitua kama hua juu yake. Alibatizwa ili kubeba dhambi zetu zote na hivyo kuweka bayana kwamba atakwenda kusulubiwa ili kulipia mshahara wa makosa yetu yote.
Yesu alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi za ulimwengu na hivyo kwenda msalabani ili tuweze kuokolewa na kupokea kipawa cha Roho Mtaktifu. Jambo hili ni kweli. Yesu alibatizwa na Yohana, akahukumiwa kwa dhambi zetu zote msalabani na kufufuka. Lazima tuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani ili tupate msamaha wa dhambi zetu zote.
Tunaweza kuona toka ubatizo wa Yesu (Mathayo 3:13-15) kwamba, Roho Mtaktifu huja kwa amani kama ashukavyo huwa kwa wale waliotakaswa kwa kuamini ubatizo wa Yesu. Ili kumpokea Roho Mtakatifu ni muhimu kuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani. Roho Mtakatifu huja juu ya mtu katika hali ya utulivu na amani kama vile hua pale mtu huyo anapo amini msamaha wa dhambi. Wale ambao tayari wamekwisha mpokea RohoMtakatifu yawapasa kuelewa kwamba hili limewezekana kutokana na msamaha wa dhambi
kwa imani. Roho Mtakatifu hutua juu ya wale wote wanao amini msamaha wa dhambi kwa mioyo yao yote.
Yesu Kristo alikuja kwa mkate na divai ya uzima wa milele (Mathayo 26:26-28, Yohana 6:53-56) Yesu alipoibuka toka majini baada ya kubatizwa, palitokea sauti mbinguni ikisema “Huyu ni mwanangu mpendwa wangu ninaye pendezwa naye” (Mathayo 3:17).
Nirahisi kuamini katika Mungu kwa Utatu. Mungu ni Baba wa Yesu na Yesu ni Mwana wa Mungu. Roho Mtakatifu pia ni Mungu. Utatu huu ni Mungu mmoja kwetu. Yakupasa kujua kwamba, kamwe hautoweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini msalaba pekee au kujaribu kujitakasa binafsi kwa matendo ya haki. Utaweza kumpokea Roho Mtakatifu pale unapoamini ubatizo wa Yesu na hivyo kumtwika dhambi zote juu yake, na kuamini kusulubiwa kwake ili kutupatanisha kwa dhambi zetu zote.
Hakika hivi ndivyo ilivyo rahasi na wazi ju ukweli huu! Si vigumu kupokea msamaha wa dhambi na Roho Mtakatifu. Mungu huzungumza nasi kwa namna iliyo rahisi. Kiwango cha akili ya mtu wa kawaida ni kati ya 110 na 120 (yaani IQ - intelligence quotient). Injili yaMungu ni rahisi kumtosheleza mtu wa kawaida kuielewa. Hata kwa watoto wa umri kati ya miaka 4 na 5 injili hii njema kamwe haijawa ngumu kueleweka kwao.
Lakini Mungu anapo zungumza nasi juu ya kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani kwa njia iliyo rahisi zaidi, je, tusingeliweza kweli kumwelewa? Mungu husamehe dhambi zetu zote na kutupa Roho Mtakatifu kama zawadi kwa wale wote waaminio injili hii.

Mungu anatuambia kwamba hatutoweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kupitia tendo la kuwekewa mikono au sala ya toba. Roho Mtakatifu haji kwa namna ambavyo tutakapo funga au kujitolea au hata kuomba usiku kucha milimani. Ni aina gani basi ya imani itakayo sababisha kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu? Ni imani ya ukweli wa kwamba Yesu alikuja hapa ulimwenguni alibatizwa ili kubeba dhambi zetu zote, akafa msalabani na alifufuka.

Jumatano, 16 Aprili 2014

UPATANISHO WA DHAMBI KATIKA AGANO LA KALE NA JIPYA


Na mtu awaye yote katika watu wa nchi akifanya dhambi pasipo kukusudia, kwa kufanya neno lolote katika hayo ambayo BWANA alizuiria yasifanywe, naye akapata hatia, akijulishwa hiyo dhambi yake kwa ajiri ya dhambi yake aliyoifanya, ndipo atakapoleta mbuzi mke mkamilifu, awe matoleo yake kwajiri ya dhambi yake aliyoifanya. Naye ataweka mkono wake kichwani mwake hiyo sadaka ya dhambi, na kumchinja sadaka ya dhambi mahali hapo pa sadaka ya kuteketezwa. Kasha kuhani atatwaa katika hiyo damu yake kwa kidole chake, na kuitia katika pembe za madhabahu ya kuteketeza na damu yake yote ataimwaga  chini ya madhabahu (Walawi 4:27-30)
Mwenye dhambi anapotaka kupatanishwa na dhambi alizotenda kwa kila siku ilimpasa kuleta mnyama asiye na doa mbele ya hema takatifu. Ndipo ilimpasa kumwekea mikono juu ya sadaka hiyo ya mnyama  ili kumtwika dhambi zake zote, kumchinja koo na kutoa damu kwa kuhani ili iweze kuletwa mbele ya Mungu. Kitakachofuata ni kumalizia hatua iliyobaki ili ikamilishe msamaha wa wenye dhambi.
Pasipo sheria na amri za Mungu, watu wasingeweza kujua ikiwa kwamba wana dhambi au la. Tunapojichunguza wenyewe kupitia sheria na amri za Mungu tunagundua kwamba tuna dhambi. Dhambi zetu hazikuhukumiwa kwa viwango vyetu, bali ni kwa sheria na amri za Mungu.
Katika Agano la kale, dhambi zilitwikwa juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi kwa kuwekewa mikono. Na baadaye mwenye dhambi hakuwa tena na dhambi ndipo sadaka hiyo ilipopaswa kuchinjwa na kufa badala ya mwenye dhambi. Mpangilio huo wa utoaji wa sadaka ya dhambi ni kivuli cha hukumu na upendo wa Mungu.
“Kisha atayaondoa mafuta yake yote kama vile mafuta yanayoondolewa katika hizo za amani; kisha kuhani atayateketeza juu ya madhabahu iwe harufu ya kupendeza kwa bwana”  (Walawi 4: 31) mafuta katika biblia yana maana ya Roho Mtakatifu. Hivyo, ili tuweze kupatanishwa kwa dhambi zetu zote yatupasa pia kuchukulia ndani ya moyo wetu upatanisho wa dhambi zetu kwa namna ya Mungu aliyo iweka.
Mungu aliwaeleza wana wa Israel kwamba sadaka ya dhambi katika Agano la kale ilipaswa iwe ni mwana kondoo, au mbuzi au ndama dume. Sadaka hiyo ilichaguliwa kwa uwangalifu mkubwa. Sababu ya sadaka kuwa safi ni kwamba ilipaswa kuonyesha Yesu Kristo ambaye angezaliwa kwa uwezo wa Roho mtakatifu na kuwa sadaka ya dhambi kwa wanadamu wote.
Watu wa Agano la kale walizitwika dhambi zao kwa kuweka mikono juu ya mnyama asiye na doa, kuhani alihudumia kwa sadaka hiyo ili kulipizia dhambi. Hii ndiyo namna ambayo Israel walipatanishwa kwa dhambi.

kifungu kingine kinacho zungumzia mambo hayo ni (Walawi16:21). Hivyo tafakari kwa kina na utaona kwamba bila kuwekea mikono juu ya sadaka husika, damu haitakua na maana yoyote katika kuondoa dhambi. Iliwapasa Israel kuamini katika mambo yote ya sadaka ya dhambi.
SABABU GANI YESU ALIBATIZWA YORDANI?
Hebu sasa natuangalie tukio lile Wakati kuhani mkuu wa mbingu alipokutana na kuhani mkuu wa mwisho wa wanadamu. Hapa tunaweza kuona haki ya Mungu kupitia ubatizo ulio leta upatanisho wa dhambi zote za ulimwengu.
Yohana Mbatizaji aliye mbatiza yesu alikuwa mkuu kati ya wote waliozaliwa na mwanamke. Yesu alimshuhudia Yohana Mbatizaji katika (Mathayo 11:11) “amini nawaambieni, hajaondokea mtu katika uwazao wa mwanamke aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji”. Namna ile dhambi za watu zilivyoweza kufutwa wakati kuhani mkuu Haruni alipoweka mikono juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi katika siku ile ya upatanisho, ndivyo hivyo katika Agano jipya dhambi zote za ulimwengu zilivyoweza kufutwa pia pale Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji.
Injiri ya kuzaliwa upya mara ya pili ni injiri iliyokamilisha ondoleo la dhambi zetu zote za zamani, za sasa na zijazo mbeleni. Hivyo injiri ya ukombozi kupitia ubatizo wa Yesu ilikuwa ni injiri ya Mungu iliyopangiliwa ili kutimiza haki yote, ambayo iliokoa wote duniani. Yesu alibatizwa kwa jinsi iliyostahili ili kupatanisha dhambi za ulimwengu.
Nini maana ya’ haki yote’? (Yohana 3: 13-15) Maana yake ni Mungu kusafisha dhambi zote za ulimwengu kwa njia inayostahili. Yesu alibatizwa ili kutakasa dhambi zote za wanadamu “ kwa maana haki ya Mungu anadhihirishwa ndani yake toka imani hadi imani”(Warumi 1:17). Haki ya Mungu imedhihirishwa katika uwamuzi wa kumtuma mwana wake Yesu hapa duniani ili kutakasa dhambi za ulimwengu kupitia ubatizo wake kwa Yohana Mbatizaji na kwa kifo chake msalabani.
Katika Agano jipya, haki ya Mungu imeelezwa kupitia ubatizo wa Yesu na damu yake. Tunakuwa wenye haki kwasababu Yesu Alibeba dhambi zetu zote katika mto Yordani. Tunapoukubali wokovu huu wa Mungu ndani ya mioyo yetu haki ya Mungu inatimizwa kwa uhakika.
Kila kitu katika Agano la kale kina mwenzake katika Agano jipya kwa Agano la kale “tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake imekusanya” (Isaya 34:16)
Kutimia kwa unabii wa wokovu katika Agano la kale kulihitimishwa kwa njia ya ubatizo wa Yesu katika Agano jipya. Hivyo unabii wa Agano la kale hatimaye ulipata mwenzake katika Agano jipya. Vile watu wa Israel walivyopatanishwa kwa dhambi zao mara moja kwa mwaka katika Agano la kale, ndivyo ilivyo sasa dhambi za watu wote ulimwenguni zilivyo twikwa Yesu na kufutiliwa mbali milele katika Agano jipya.
Ikiwa hukubali na kuamini hili moyoni mwako juu ya huu ukweli wa ubatizo wa Yesu na kifo chake pale msalabani kamwe hautoweza kutakaswa dhambi zako hata kama wewe unaishi maisha ya utakatifu kwa kiwango kikubwa. Yesu alikufa msalabani kwasababu alibeba dhambi zako zote kwa ubatizo wake.
(Warumi 8:3-4) maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwasababu ya mwili, Mungu kwa kumtuma mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio na dhambi aliihukumu dhambi katika mwili, ili maagizo ya tirati yatimizwe ndani yetu sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili bali mambo ya roho.
Kwakuwa sisi ni wanadamu tusioweza kamwe kufuata sheria na amri za Mungu kutokana na udhaifu wa miili yetu, Yesu alibeba dhambi zetu zote juu yake. Huu ni ukweli wa ubatizo wake. Ubatizo wa yesu ulitabili kifo chake pale msalabani. Hii ni hekima Halisi ya injiri ya Mungu.
Ikiwa umekuwa ukiamini kifo cha Yesu pekee, sasa nakusihi ugeuke na ukubali kwa moyo wako wote injiri ya wokovu kupitia ubatizo wa Yesu. 

Jumamosi, 12 Aprili 2014

MWANADAMU HUTENDA DHAMBI KATIKA MAISHA YAKE YOTE


Katika 1Yohana1:10 inasema  “tukisema kwamba hatukutenda dhambi twamfanya yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.Hapajatokea yeyote ambaye hajatenda dhambi mbele ya Mungu. Hata biblia inasema “bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani ambaye afanyaye mema asifanye dhambi(Mhubiri 7:20).Watu wote hutenda dhambi mbele ya Mungu.
Ikiwa mtu yeyote atasema kwamba hajatenda dhambi basi ni muongo. Watu hutenda dhambi maishani mwao pote hadi saa ya mwishoni kabla ya kufa, na hii ndiyo maana Yesu alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi hizo zote. Ikiwa hatujawahi kutenda dhambi basi tusingelihitaji kumwamini Mungu kuwa ni mwokozi. Bwana anasema “neno langu si neno lako” kwa wale wenye fikra wakidhani kuwa hawajatenda dhambi.
Ikiwa mtu hana imani katika injili njema ya maji na Roho basi anastahili kuangamia. Ikiwa mtu mwenye haki au mwenye dhambi atasema kwamba hajatenda dhambi mbele za Mungu, basi huyo hatastahili kuiamini injili njema.
Bwana amempa kila mmoja zawadi nzuri ya injili njema. Tulikiri dhambi zetu zote nakutubu ilikupokea msamaha kwa injili njema. Tunaweza kuirudia injili hii ambayo Mungu aliyo tupatia kama msamaha wa dhambi zetu na kuiamini ili kuweza kuwa na usharika wa Roho Mtakatifu. Maana ya kweli ya usharika wa Roho mtakatifu ipo katika injili ya maji na Roho, na pia kwa wale tu walio na injili hii ndiyo watakao weza kuwa na ushirika na Mungu.
Wanadamu walikuwa mbali na Mungu kwa sababu ya dhambi walizorithi kwa Adamu na Hawa. Lakini leo hii sisi tuliokuwa tumerithi mbegu ya uovu tunaweza kutarajia kuwa na usharika na Mungu kwa mara nyingine tena. Ili kuweza kufanikisha hayo yote ni lazima tuwe na imani ya injili ya maji na Roho toka kwa Yesu Kristo, na hivyo kuwa na msamaha wa dhambi ambazo zilituweka mbali na Mungu.
Wale wote wenyekuamini injili njema ndiyo watakao okolewa kutokana na dhambi zote, na hapo basi Mungu atawajaza Roho Mtakatifu. Wenye haki wataweza kuwa na ushirika na Mungu kwa kuwa wamempokea Roho Mtakatifu. Kwa wale wote waliowekwa mbali na Mungu kutokana na dhambi zao lazima wairudie injilinjema ya maji na Roho na kuiamini na hapo ndipo watakapoweza kuanza kuwa na ushirika na Mungu.
Kuwa na Roho Mtakatifu ndani huja kutokana na imani katika injili njema. Lazima tujue kwamba kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu huja pale tunapoamini injili ya maji na Roho tu. Kuiamini injili njema ndiko kunako jenga njia mpya kumuelekea Mungu. Bwana amevunja ukuta wa kati ulio kuwa ukitutenganisha naye kwa sababu ya dhambi zote mbili, yaani dhambi tuzitendazo maishani na ile dhambi ya asili, na hivyo tutaruhusiwa kuwa na ushirika na Mungu kwa kupitia imani yetu katika injili njema ya maji na Roho.
Yatupasa kuanzisha upya ushirika na Roho Mtakatifu kwa mara nyingine tena. Usharika wa kweli na Roho Mtakatifu hufanikishwa kwa kupita kuelewa injili ya maji na Roho na kutii kwa imani. Ushirika wa Roho Mtakatifu huja pale tunapokuwa na imani ya kweli na msamaha wa dhambi ambao unatokana na injili njema. Wale wote ambao wahajapokea msamaha wa dhambi kamwe hatoweza kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu.

Kwa maneno mengine hakuna yeyote atakaye weza kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu pasipo kuiamini injili ya maji na Roho. Ikiwa bado ni vigumu kwako kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu basi ni lazima kwanza ukubali kwamba bado hajaamini injili ya maji na Roho na hivyo dhambi zako hazijasafishwa. Je, unatamani kuwa na uhusiano na Roho Mtakatifu? Sasa basi amini injili iliyokamilishwa kwa ubatizo wa Yesu na damu yake. Ndipo hapo tu utaweza kusamehewa dhambi zako zote na thawabu yako itakuwa ni kumpokea Roho Mtakatifu ndani ya moyo wako. Injili hii njema kwa hakika ndiyo inayotuletea ushirika na Roho Mtakatifu.