Jumatatu, 5 Mei 2014

TOBA YA KWELI KATIKA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU


(Matendo 2:38) “Petro akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”
Biblia inasema katika (Matendo 2) kwamba mahubiri ya Petro yaliwagusa kwa undani watu na hata kuwasababisha watubu dhambi zao. Walichomwa mioyo yao na kumwambia Petro na mitume wengine, “Tutendeje ndugu zetu? Petro akawaambia tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kisto mpate ondoleo la dhambi zenu nayinyi mtapokea kipawa cha Roho Mtaakatifu” (Matendo 2:38). Mahubiri ya Petro yanatuonyesha wazi kuwa imani katika injili nzuri ya maji na ya Roho ni ya muhimu sana katika kumpokea Roho Mtakatifu na pia inatuonyesha jinsi toba la kweli lilivyo. Tunapaswa kutambua kuwa tunaweza kumpokea Roho Mtakatifu sambamba na ondoleo la dhambi kwa kuyaangalia maandiko matakatifu kwa karibu na kwa kuamini katika injili nzuri ya maji na ya Roho.
Jambo la kwanza tunalotakiwa kuwa nalo ili kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ni imani katika toba la kibiblia. Hata hivyo, tunatakiwa kuwa makini ili tusije tukalielewa toba hili kuwa ni majuto. Toba maana yake ni imani katika Yesu Kristo. Tunaweza kuona katika Biblia kuwa watu walijuta kwa kumsulubisha Bwana. Walijuta kumuuliza Petro kwamba wafanye nini na walizikiri dhambi zao hata kabla ya Petro kuwaambia watubu. Tunaweza kuona kuwa toba ambalo Petro alilizungumzia halikuwa kuzijutia dhambi wala kuzikiri, bali ilikuwa ni kumpokea Yesu Kristo katika moyo wa kila mtu kama Mwokozi na kuwa na imani katika injili nzuri ambayo Yesu ametupatia. Na hii ndiyo asili nzuri ya toba.
Upendo wa Yesu Kristo ulikuja kwetu kabla hayajakuwepo majuto-binafsi kwa dhambi za mioyo yetu. Hii inamaanisha kuwa Yesu alizichukua dhambi zetu pale alipobatizwa katika Mto Yordani, alikufa Msalabani, na kisha akafufuka toka kwa wafu. Kwa njia hii, alizisafisha hatia na dhambi zetu zote.
Toba la kweli maana yake ni kuamini katika ukweli huu. Je, unafikiri kuwa dhambi zetu zimesafishwa moja kwa moja kwa kule kujuta na kuomba msamaha? Ukweli ni kuwa hili sio toba la kweli. Toba la kweli maana yake ni kupokea ondoleo la dhambi zetu kwa kuamini katika injili nzuri ya ubatizo wa Yesu na damu yake. Biblia inasema kuwa tunasamehewa dhambi zetu kwa toba. Vivyo hivyo, inatupasa kuiamini injili ya ubatizo wa Yesu na damu yake ili tuweze kupokea ondoleo kamili la dhambi zetu.
Petro alitoa huduma ya ubatizo “katika jina la Yesu Kristo” kwa wale waliomwamini Yesu. Yesu alibatizwa ili aweze kuzichukua dhambi za wanadamu wote. Ubatizo na kifo chake juu ya Msalaba ulikuwa ni ukamilifu wa injili nzuri inayowawezesha waamini kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu (Mathayo 3:15-17). Mwanadamu anaweza kutakaswa kwa kuamini katika ubatizo wa Yesu na damu yake pale Msalabani. Kwa kifupi, wale waliopokea ondoleo la dhambi kwa kuamini katika injili wamempokea Roho Mtakatifu.
Je, sala zitaweza kuleta uwepo wa Roho Mtakatifu ndani?
Watu hawatoweza kupokea msamaha wa dhambi na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao hata ikiwa watafanya maombi ya dhati kutaka uwajilie. Ili tuweze kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu, ni muhimu kuamini injili njema iliyokamilishwa kwa ubatizo wa Yesu na damu yake pale msalabani. Roho Mtakatifu wa Mungu hutunukiwa kwa wale walio kuwa na dhambi amabao wametakaswa moja kwa moja.
Imani katika injili ni kumkubali Yesu kama mwokozi wa kweli. Matendo 2:38 inasema, “tubuni mbatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”Mtume Petro alisema kwamba uwepo wa Roho Mtakatifu hutolewa kwa wale walio samehewa dhambi zao kwa njia ya imani katika toba ya kweli. Msamaha wa dhambi na kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ni pacha.
Biblia inasema“Tubuni mkabatizwe kilammoja kwa jina lake Yesu Kristo mpate ondoleo la dhambi zenu nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwa ahadi hii ni kwaajili yenu na kwa watoto wenu kwa watu wote walio mbali na kwa wote watakao itwa na Bwana Mungu wetu wa mbinguni” (Matendo 2:38-39).
Mtu aweza kupokea Roho Mtakatifu kwa sharti kwamba moyo wake umetakaswa, usio na dhambi. Hivyo imetupasa kuamini injili ambayo Yesu Kristo ametupatia. Lazima tutakaswe baada ya kupokea msamaha wa dhambi kwa kuamini injili njema inayosema dhambi zetu zote ulimwenguni zilitakaswa pale Yesu Kristo alipobatizwa. Ndipo hapo tutakapoweza kupokea Roho Mtakatifu. Ni mapenzi ya Mungu kwa Roho Mtakatifu kuweka makazi ndani ya wanadamu “maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kutakaswa kwenu” (1 Wathesalonike 4:3).
Msamaha wa kweli hutolewa si kwa njia na juhudi za watu kujitoa muhanga au kuwa wema, bali kwa kuamini injili ambayo Mungu Utatu Mtakatifu aliyoitimiza kupitia Yohana mbatizaji. Mungu Utatu Mkatifu huwatunukia uwepo wa Roho Mtakatifu kwa wale wote waliokwisha samehewa dhambi zao kwa kuamini injili njema. Umati wa watu ulichomwa mioyo pale ulipo yasikia Petro aliyoyanena siku ile ya pentekoste. Walipaza sauti na kuuliza “Tutendeje ndugu zetu?”  (Matendo 2:37). Hii hudhihirisha kwamba tayari wamekwisha badilishwa kifikra zao na sasa wanamwamini Yesu Kristo kuwa ni mwokozi na Bwana wao. Na pia wamekwisha okolewa kutokana na dhambi zao kwa kuamini toba ya kweli aliyo ihubiri Petro. Msamaha wa dhambi ulikwisha tolewa kwa wanadamu wote kwa kutegemea imani zao katika injili njema ya ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Dhumuni la ubatizo wa Yesu ni kumwezesha yeye abebe dhambi za ulimwengu. Kwa kuamini hili ndilo sharti moja wapo muhimu la kupokea Roho Mtakatifu. Mungu ametupatia uwepo wa Roho Mtakatifu kwa wale wanao iamini injili ya kweli iliyo na msingi wa ubatizo wa Yesu Kristo. “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini na tazama mbinguni zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama huwa akija juu yake” (Mathayo 3:16). Kuja kwa Roho Mtakatifu katika siku ile ya pentekoste kuna uhusiano wa pekee na imani ya mitume katika injili njema: ubatizo wa Yesu, damu yake msalabani na ufufuko.
Katika Matendo inasema kwamba watu waliobatizwa katika jina la Yesu walimpokea Roho Mtakatifu moja kwa moja katika muda huo huo. Yatupasa kuamini kwamba kupokea Roho Mtakatifu ni karama ya pekee toka kwa Mungu. Ili tuweze kupokea karama hii, inatupasa kwamba dhambi zetu zote zisafishwe kwa kupitia imani katika ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani.
Kulingana na Matendo, wale wote walio sikia mahubili ya Petro ambapo alishuhudia akisema, “Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”  (Matenda 2:40).  Walitii maonyo yake na kubatizwa. Kile tunachojifunza tokakatika biblia ni kwamba, mitume katika siku hizo za kanisa la mwanzo walimpokea Roho Mtakatifu kwa msingi wa imani zao katika ubatizo wa Yesu Kristo na damu yake msalabani. Hili ndilo sharti muhimu la kuweza kumpokea Roho Mtakatifu. Imani katika ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani ni jambo lisilo wekwa kando ikiwa mtu atahitaji msamaha wa dhambi.
Imani ituongozayo katika kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia ya toba ya kweli.
Hebu tuangalie katika Mtendo 3:19,“tubuni basi mrejee, ili dhambi zenu zifutwe zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.” Tutawezaje basi kuelezea nini maana ya toba? Hebu na tufikirie upya tena.
Katika biblia, toba maana yake ni kuirudia imani ya ukombozi. Katika nyakati hizo watu walishika tabia kama walivyo penda nafsini mwao na kuviabudu vitu vilivyo umbwa na Mungu. Lakini baada ya kugundua kwamba Yesu Kristo alikwisha kuwaokoa toka dhambini kwa maji na kwa damu yake, ndipo wakaanza kubadilika. Hii ndiyo toba ya kibiblia. Toba ya kweli ni kuirudia injili njema ya maji na Roho.
Ni ipi toba iliyo ya kweli inayo hitajika katika kumpokea Roho Mtakatifu? Ni katika kuamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani “zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.”Ikiwa watu watakuwa na imani hii, basi watasamehewa dhambi zao na kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa kuwa Yesu amewatakasa wenye dhambi wote duniani kwa njia ya ubatizo wake na damu yake msalabani, imetupasa basi kuamini hili ili tuweze kupokea ukombozi na uwepo wa Roho Mtakatifu.
Ili tuweze kumwamini Yesu na kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu, inahitajika dhambi zote zitwikwe juu ya Yesu kwa imani ya ubatizo wake na kifo chake msalabani. Yatupasa kuamini kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu zote na kufa msalabani ili ahukumiwe kwa ajili ya dhambi hizo. Hii ndiyo imani sahihi na toba ya kweli, amabayo inayotuwezesha kuwa na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu.
Roho Mtakatifu huja juu ya wale wote walio kwisha samehewa dhambi zao zote. Kwanini Mungu ametoa Roho Mtakatifu kama karama kwa wale wote walio kwisha pokea ukombozi? Kwasababu Roho Mtakatifu, akiwa mtakatifu, anahitaji kuweka makazi ndani yao na kuwachapa mhuri kuwa wana wa Mungu.
Roho Mtakatifu ni Mungu. Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja. Ni nafsi tatu lakini ni Mungu mmoja kwa wale wote wenye kuamwamini Yesu. Baba alikuwa na mpango wa kutuokoa sisi tokana na dhambi zetu, na hivyo Mwana Yesu alikuja ulimwenguni akabatizwa na Yohana ili kuzichukua dhambi za ulimwengu, alikufa msalabani, alifufuka toka kuzimu siku ya tatu na kupalizwa mbinguni. Roho Mtakatifu hutuongoza katika kuiamini injili njema kwa kushuhudia juu ya ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Mungu huwaweka mihuri wale wote walio kwisha kuokolewa kwa kupitia Roho Mtakatifu. Mungu huwatunukia Roho Mtakatifu wale wote wanao amini injili inayo sema kuwa, Yesu alizichukua dhambi za ulimwengu. Mungu huwapa Roho Mtakatifu kama ahadi na kama mhuri kuashiria kuwa ni watoto wake. Roho Mtakatifu ni uthibitisho wa mwisho katika wokovu wa dhambi kwa wale wenye kuamini injili njema.
Wale wote walio na Roho Mtakatifu ni watoto wa Bwana. Wale walio na uwepo wa Roho Mtakatifu wakati wote hupata nguvu upya kila wakati. Huwa na imani madhubuti katika maneno ya Mungu juu ya ubatizo waYesu na damu yake pale msalabani. Ni wenye furaha ya kweli. Wale wote wenye kutubu
kwa njia iliyo sahihi hawatakuwa na dhambi tena mioyoni mwao na hivyo watakuwa na uwepo wa Roho Mtakatifu.

Biblia inasema kwamba, ipo toba iletayo msamaha wa dhambi. Je, umekwisha fanya toba ya aina hiyo? Ukitubu na kuifuata imani ya kweli, nawe pia utaweza kupokea injili njema. Nakusihi utubu dhambi zako na umpokee Roho Mtakatifu. Je, uko tayari kutubu na kuamini injili njema ambayo itakuongoza katika kumpokea Roho Mtakatifu?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni