Tunaweza kuona katika (kutoka
25:8-9) Nao wanifanyie patakatifu; ili
nipate kukaa kati yao. Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo
vyake vyote, ndivyo mtakavyo vifanya.” (waebrania
3:6) “bali
Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba yake ni sisi, kama
tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho.” kwamba Mungu alimwita Musa na akammwambia
kupajenga mahali pa kuabudia ambapo Mungu ataishi. Mahali ambapo Mungu anaishi
au kushinda hapo panaitwa madhabahu. Katika malango na katika mapaa ya
madhabahu hii kulikuwa na fumbo lililokuwa limefichika, yaani fumbo la Yesu Kristo.
Katika kifungu hiki ambacho Mungu aliwaamuru watu wa Israeli kuijenga madhabahu
hii, basi ninaamini kuwa Mungu anatueleza sisi kuijenga madhabahu hii katika
mioyo yetu ili kwamba aweze kuishi ndani yetu.
Nini ambacho tunapaswa kukifanya ikiwa tunahitaji Mungu akae ndani yetu?
Kwanza kabisa, kwa kweli ni lazima tufahamu jinsi ambavyo Mungu alivyozisafisha
dhambi zetu zote kwa kupitia Neno la Injili ya maji na Roho. Na ni lazima
tuamini katika ukweli huo. Ili kufanya hivyo, kwanza ni lazima tuziangalie
nafsi zetu kimsingi. Tangu kuzaliwa kwetu hatukuwa na chaguo jingine lolote
bali kuzaliwa kama wenye dhambi. Inawezekanaje basi kwa Roho wa Mungu mtakatifu
kukaa katika mioyo ya watu kama sisi? Ili Roho wa Mungu aweze kukaa katika
mioyo ya wenye dhambi ni lazima basi hawa
wenye dhambi wawe na imani inayoamini katika Injili ya kweli. Kwa maneno
mengine, Roho mtakatifu anakaa ndani yetu pale tu tunapokuwa tumezioshelea
mbali dhambi zetu kwa kufahamu na kuamini katika Injili ya maji na Roho. Kule
kusema kuwa Roho mtakatifu anaweza kukaa katika mioyo kumwezesha kwa kuamini
katika ukweli wa milele wa maji na Roho.
Madhabahu ambapo Mungu anapenda kukaa
Hata hivyo, watu wengi ambao bado hawajapokea ondoleo la
dhambi hawafahamu ukweli huu. Unafikiri
ni kwa nini Mungu alimwamuru Musa kulijenga Hema takatifu la kukutania? Alimwamuru
Musa kwa sababu alitaka kukaa katika mioyo yetu. Tatizo ni kuwa watu wengi
kutokana na kutojua kwao juu ya ukweli huu (Injili ya maji na Roho), wanatuimia
kiasi kikubwa cha fedha kujenga majengo ya makanisa makubwa na ya kushangaza na
wanadanganyika kuamini kuwa haya ndiyo mahekalu ambapo Mungu anaishi.
Watu wa jinsi hiyo wapo tayari kutoa fedha yote walioweza
kuipata katika kipindi chote cha maisha yao kwa Mungu, kwa sababu wanafikiria
kimakosa kuwa makanisa yao yanaweza kufanyika
ni mahekalu ya Mungu mtakatifu ikiwa kama watayajenga majengo ya
kifahari na makubwa. Lakini je, ni kweli kuwa Mungu atapendezwa ikiwa tutajenga
makanisa makubwa ya kupendeza na kisha tukampatia Mungu?. Je, ni kweli kuwa
Mungu atakubaliki ikiwa utafanya jambo kama hili? Je, kanisa hili litafanyika kuwa madhabahu
ambayo inakaliwa na Mungu? Hivyo si kweli kabisa. Haya ni matokeo ya imani
isiyofahamu ukweli wa Injili ya maji na Roho na walioangukia katika uongo mkuu.
Madhabahu ambayo Mungu anataka kuishi si jengo kubwa la
kanisa bali ni moyo wako ambao umeoshwa dhambi zako. Mungu anapenda kukaa ndani
ya mioyo ya wenye haki ambao wamepokea ondoleo la dhambi na waliofanyika
watakatifu. Ili kulifanya hili liwezekane tunatakiwa kutoa sala zetu za toba ili
tuweze kutakaswa? Hapana, kwa kweli siyo hivyo. Hata hivyo, kuna watu wengi
wakristo wa siku hizi wanafikiri na kuamini namna hii.
Ili kulijenga Hema takatifu la kukutania kwa kupitia Musa,
Mungu aliwaamuru wana wa Israeli kumtolea sadaka. Kama ilivyoandikwa katika (kutoka 25:3-7). Baada ya kuzipokea sadaka hizi
kupitia Musa alijenga madhabahu ya Mungu kwa vifaa hivi kwa kupitia wafanyakazi
ambao waliipokea hekima toka kwa Mungu. Kama ambavyo Mungu alimwamuru Musa
kulijenga Hema takatifu la kukutania katika Agano la kale, basi katika Agano
jipya, Mungu anatutaka sisi pia kujenga madhabahu katika mioyo yetu ili aweze
kuishi ndani yetu. Vifaa vya imani ambavyo kwa hivyo tunaweza kuvitumia katika
kuijenga madhabahu hii ni Neno la Injili ya maji na Roho. Kwa vifaa vya Injili
hii ya maji na Roho ni lazima tuzioshelee mbali dhambi zetu zote na kusafishwa.
Kwa kutueleza sisi kujenga madhabahu yake Mungu anatueleza sisi kuweka wazi
moyo wako na kisha kuamini katika Injili ya maji na Roho.
Jambo hili sasa linazusha swali jingine juu ya aina ya
imani ambayo tunapaswa kuwa nayo ili Mungu aweze kuishi katika mioyo ya wenye
dhambi. Jibu ni rahisi na la wazi. Kwa kuwa Mungu mtakatifu aweze kuishi katika
mioyo ya wenye dhambi, ni lazima kwanza wenye dhambi hawa wafahamu kile ambacho
Injili ya maji na roho inawaeleza, na kisha ni lazima waamini katika ukweli
huo. Ndipo mioyo yao inapoweza kusafishwa na kupokea ondoleo la dhambi, na
ndipo hapo tu Mungu Mtakatifu anapoweza hatimaye kuishi katika mioyo ya watu wa
jinsi hiyo ambao wamepokea ondoleo la dhambi wanapokuwa wameuachilia mbali
ugumu wao na wakamini katika Injili ya
maji na roho, ambayo ni majaliwa ya Mungu, basi Mungu anaweza kuja na kukaa
katika mioyo yao.
Hii ndiyo sababu 1wakorintho 3: 16-17 inasema, “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la
Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu akiliharibu hekalu
la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu,
ambalo ndilo ninyi.” Mungu ni mtakatifu na asiye na dhmbi. Kwa hiyo, anaeza
tu kuja katika mioyo yetu wakati inapokuwa imesafishwa vizuri kwa Neno la Injili
ya maji na Roho. Biblia inasema kwa wazi kuwa ni wale tu waliopokea ondoleo la
dhambi ndiyo wanaweza kupokea karama ya Roho Mtakatifu (Matendo ya mitume 2:38)
"Injili ya maji na Roho" inapatikana katika blog hii
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni