Jumapili, 30 Machi 2014

MANABII WA UONGO


(Yuda 1:11) inasema, “Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya kora.” Ipi sasa ndio njia ya Kaini? Kaini alienda mbali na njia ya Mungu, na Mungu akamwadhibu. Wale waliotekwa na shetani wanafanya kazi ili kupata pesa. Kifungu kinaendelea kusema, “wameikimbilia tamaa katika kosa la Balaam kwa kutafuta faida” Wachungaji waliotekwa na shetani wanahubiri sana ili kupata pesa, wamefungwa na shetani, wanatenda kazi za manabii wa wa uwongo. Manabii hawa wa uwongo hufurahia kupata pesa nyingi zinazotolewa kama sadaka makanisani. Wanatumia nguvu kubwa kuhubiri pale wanapoona waumini wao wanamwaga pesa nyingi makanisani kama sadaka. Na pale waumini wanatoa pesa kidogo, manabii wa uwongo hata hawathubutu kuwabariki. Hivi ndivyo ilivyo kuwa waliomezwa na shetani wanatoa huduma makanisani ili hatimaye wapate pesa.
Ukitoa pesa nyingi, wanakupa hata madaraka makubwa kanisani kama mtumishi ama mzee wa kanisa. Lakini kama wewe sio mtoaji, hawawezi kamwe kukupa hata cheo kanisani. Hawa ambao kifungu hiki cha maneno kinawazungumzia ni wale wapenda pesa tu. Hawa walikuwa akina nani? Biblia inawataaja akina Balaam, Nabii wa Agano la Kale, aliyewaingiza watu wa Israeli katika biashara ya kuwauza ili kupata pesa. Watu kama Balaam wanafanya kazi kwa nguvu za shetani, hao ndio wanaofanya huduma kujichumia pesa. Fungu hilo la maneno hatimaye linatuambia kuwa watu wanaingia kuwa “mateka wa Kora” Watu hawa waliunda vyama vyao na kusimama kinyume na makanisa ya Mungu. Watu wanaopenda pesa wataishia kuwa watu wa kusimama kinyume na Mungu.
(Yuda 1:12) Inasema, “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamupamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawinguyasiyo na maji, yachukuliwayona upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa.” Wale wanaowatazama watu kwa mtazamo wa pesa, ni wataalamu wa kudanganya wengine na kuwaibia waumini wao pesa. Kwa kuwa watumishi wa shetani ni aina ya watumishi wenye njaa ya kujishibisha, wanajijali wao wenyewe, hawafikiri juu ya Roho za wengine. Hata kama watu wanamwamini Yesu, wengi wao wanatawaliwa na hawana amani ndani yao, wana hofu juu ya dhambi zao, na wanaendeshwa na ujinga wa hofu zao. Watumishi wa shetani wanapanda mbegu ya uongo kwa kudanganya wakifuata nguvu ya shetani. Na kila mara wakiongea habari za neno la Mungu, wanachanganya na uongo hata hawana aibu. Kwa hiyo Biblia inawaelezea wao kama “mawimbi yenye nguvu ya baharini, yanayobubujika aibu yao” (Yuda 1:13).
Wakati wa siku za mwisho ukifika, mapepo yataongeza nguvu ya kupotosha watu. Na hivyo hata watumishi watazidisha nguvu. Katika nyakati za mwisho, kabla ya Yesu hajarudi, shetani atafanya kazi kubwa hata ndani ya makanisa katika ulimwengu huu. Mapepo yatapamba moto, unabii utazidi sana. Jambo la muhimu sana hapa ni kwa wale ambao bado hawajazaliwa kwa upya hata kama wanamwamini Yesu, hata kama waiamini Injili ya Maji na Roho iliyotolewa na Bwana, na kupokea ondoleo la dhambi na karama za roho Mtakatifu. Na kwa kuwa na Roho Mtakatifu, ni sharti wawe na uzima wa milele. Lakini wale watumishi wa Mungu waliotekwa na shetani, hutafuta baraka za mwili tu, nguvu ya uponyaji, kuongea kwa ndimi, na kutenda miujiza kama misingi ya matakwa yao na malengo. Ndiyo sababu watu hawa huweka kipaumbele kwa yale shetani anayowaagiza. Katika dunia ya leo, mtu akianza kuongea kwa ndimi katika nyumba zao za ibada, watu wanaomzunguka mtu huyu humsifu na hata kumpigia makofi. Na wale wasioweza kuongea kwa ndimi huwekwa katika chumba kimoja na kufundishwa namna ya kunena kwa lugha ama kuongea kwa ndimi, wakirudia rudia “Lul-lu-lujah, Lul-lu-lujah,
Haleluya.” Wanapojaribu kurudiarudia maneno haya kwa haraka, inafikia hatua wanaongea maneno yasiyoeleweka, maneno ya ajabu ajabu, kama vile umeweka kanda mbovu kwenye redio (Katika kuongea haraka, maneno yanakwama katika ulimi). Inapofikia asilimia 80 ya watu wamepoteza namna ya kuongea vizuri, kwa ndimi zao kukwamisha maneno, ni nani kati yao ataweza kutamka maneno kwa ukamili? Ni kwa sababu wafuasi hao wamewekewa mikono na watu wenye pepo, nao pia hupandwa na roho hiyo. Pepo hufanya makao na kukaa mioyoni mwao. Ni kwa sababu wamejaa pepo, ndiyo maana wanaongea kwa kuongozwa na pepo. Msidanyike na kazi za mapepo, lakini iaminini kuwa Injili ya kweli ya Roho Mtakatifu mioyoni na kati ya wale wanaoamini Injili ya Maji na Roho iliyoandikwa katika Biblia. Hata sasa, kazi potofu za mapepo zinaendelea kati ya wale wanofuata imani za Kikarismatiki.
Lakini Mkitubu Siku Hiyo
(Mathayo 7:22-23) inasema, “Wengi wataniambia siku ile, Bwana Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza? Ndipo nitaawambia dhahiri, sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu ninyi mtendao maovu.” Watu wengi wanaamini kwamba kujifanya nabii kwa jina la Bwana, kutoa pepo, kutenda miujiza, kwa jina la Bwana, ni kazi za Mungu na Roho Mtakatifu, Kuna wakristo katika dunia ya leo wanaodai kutoa pepo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, Manabii wanapoonekana kutenda miujiza, wanasema kwa kujiamini, hiyo ni kazi ya Roho Mtakatifu. Lakini neno linasema, mambo hayo sio kazi ya Roho Mtakatifu. Neno linasema kuwa nguvu hiyo ya kuondoa mapepo, ishara, maajabu na miujiza mbalimbali ni kazi za shetani. Licha ya hayo, watu bado wanaamini kuwa hizo ni kazi za Roho Mtakatifu. Kazi za shetani zilikuja kwa ajili ya wale waliuoandaliwa maangamizi, na watu wale ambao wanafanya ishara na miujiza kamwe hawawezi kuokolewa. Kwa hiyo Biblia inatuonya kuwa “Wapendwa, msiziamini kila roho, bali zijaribuni kuona kama zinatoka kwa Mungu, kwa sababu, manabii wa uongo wamekwenda duniani.” (1 Yohana 4:1).

Alhamisi, 27 Machi 2014

UBATIZO KATIKA WOKOVU

                                        

 Tunapaswa kuzaliwa upya kupitia imani zetu, kukombolewa kutoka dhambini mwetu na kufanywa wenye haki. Na ndivyo pekee tunaweza kuingia katika ufalme wa milele Mbinguni Biblia inasema,“Amin, amin nakuambia, mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu” (Yohana 3:5) “Kuzaliwa upya kwa maji na Roho” ni njia pekee ya kuingia katika ufalme wa Mungu wa milele.
  Nini basi maana ya “kwa maji” na kwa “Roho” ambamo kunaruhusu kuzaliwa upya. “Maji” katika Biblia inamaanisha “ubatizo wa Yesu”
  Kwa nini Yesu aliye Mungu, alibatizwa na Yohana Mbatizaji? Je, ilikuwa ni kuonyesha unyenyekevu wake? Je, ilikuwa ni kutangaza kwamba yeye ni Masiha? La, hasha! Haikuwa hivyo.
  Wakati Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji kwa njia ya “kuwekewa mikono juu ya kichwa chake” (Walawi 16:21) ilikuwa ni “kitendo kiadilifu cha mtu mmoja” (Warumi 5:18) kinachotwalisha mbali dhambi za mwanadamu.
  Katika Agano la Kale, Mungu aliwapa Waisraeli sheria ya neema ya ukombozi. Hivi ndivyo ilivyo kuwa ile siku ya Upatanisho ambapo dhambi zote za Israeli katika mwaka huo zingelipiwa kwa maungamo kupitia Kuhani Mkuu Haruni, kwa kuwekea mikono yake kwenye kichwa cha mnyama wa kafara.
    Palikuwa na maneno ya ufunuo yaliyotabiriwa kuhusu sadaka ya ondoleo la dhambi milele. Ilionyesha ukweli kwamba dhambi za wanadamu zingetwaliwa kwa mara moja na Yesu aliye kuja katika mwili wa mwanadamu kutokana na mapenzi ya Mungu Baba. Na alibatizwa na Yohana Mbatizaji ambaye alikuwa ni wa uzawa wa Haruni na kuwa alikuwa mwakilishi wa wanadamu wote.
  Wakati Yesu alipotaka kubatizwa alimwambia Yohana “Kubali hivi sasa kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote” (Mathayo 3:15). Hapa neno“ndivyo itupasavyo” ina maana ya “kwa kuwekewa mikono”ni kwa nia ya kubebeshwa dhambi za ulimwengu kwa Yesu ili haki yote iweze kutimizwa kwetu sisi sote. Neno“haki” kwa Kigiriki “dikaiosune” lina maana ya “hali ya kustahiki”au “kuwa na stahili katika tabia au matendo katika kufanyizwa kuwa mwenye haki au kufaa”

Yesu alihimiza haki zote kwa niaba ya watu wote kwa kupitia ubatizo katika namna ya haki na stahili zote. Hivyo kwa kuchukua dhambi za watu wote kupitia ubatizo wake, siku iliyofuata baada ya ubatizo huo, Yohana Mbatizaji alishuhudia kwa kusema “Tazama Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!” (Yohana 1:29)
Kwa dhambi zote za wanadamu juu ya mabega yake, Yesu alitembea kuelekea msalabani. Kwa niaba alichukua hukumu ya dhambi alizo zibeba mwenyewe kupitia ubatizo wake. Alikufa msalabani hali akisema “Imekwisha” (Yohana 19:30). Kwake yeye mwenyewe alizibeba dhambi zetu sote na kupokea hukumu iliyo kamili kwa niaba yetu.
Maji, yakiwa na maana ya Ubatizo wa Yesu, ni Mfano wa mambo haya ya Wokovu.
  Hivyo, pasipo “kuwa na imani juu ya ubatizo wa Yesu” hatutookolewa. Na ndiyo maana Mtume Paulo alitamka kwamba “mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi” (1 Petro 3:21)
Siku hizi watu wengi wenye kumwamini Yesu hawauamini ubatizo wake wa “maji” bali huamini kifo chake tu, katika msalaba. Je, imani hii yaweza kweli kuokoa wenye dhambi? Je,itawezekana kweli kukombolewa kutoka kwenye dhambi zetu zote kwa kuamini Damu ya Yesu tu? Je, itaweza kutuletea wokovu wetu? Hasha! Hatutaweza kupata ukombozi wa Mungu kwa imani juu ya kifo cha Yesu msalabani pekee.
Wakati wana wa Israeli walipotoa sadaka ya upatanisho katika nyakati za Agano la Kale, isingekuwa njia sahihi kumchinja mnyama wa sadaka pasipo kwanza kuwekewa mikono juu ya kichwa chake kwa kutwikwa dhambi juu yake kwa niaba yao. Hivyo inakuwa ni kosa na kuvunja sheria ya Mungu kuamini msalaba wa Yesu pekee bila kuamini pia ubatizo wake.
Hivyo, Mtume Paulo alisema “Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamira safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. (1Petro 3:21) Kama ilivyo kwa wale walio acha kuamini “maji” makuu (mafuriko) nyakati za Nuhu waliangamizwa, ndivyo ilivyo kwa wale ambao hawata amini “maji” yaani “ubatizo wa Yesu” hakika wataangamia!
 Imani iliyo kamili ituongozayo kuelekea wakovu ulio wa kweli ni ile iliyo juu ya “aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo” (1Yohana 5:6) Yatubidi kuamini yote mawili, ubatizo na msalaba wa Yesu Kristo. Mtume Yohana alinena juu ya imani iliyo sahihi ni kuamini “ushuhuda wa Roho, maji na damu” (1Yohana 5:9)
  Kinachojenga na kubainisha imani iliyo ya kweli ni kuamini kwamba, “Yesu ni Mungu Halisi na alikuja katika mwili wa mwanadamu kwa uweza wa Roho kwa njia ya Mwanamwali Mariam na kubeba dhambi zetu zote kwa kubatizwa katika mto Yordan na Yohana Mbatizaji aliye kuhani mwakilishi wa wanadamu. Yesu alikwenda msalabani akiwa amezibeba dhambi zote za ulimwengu, na kupata hukumu isiyostahili kwake kwa ajili yetu” Hivyo basi, Injili haitoweza kukamilika pasipo “ubatizo wa Yesu” yaani “maji” Haijalishi ni kwa namna ipi iliyo sahihi una mwamini Yesu, pasipo kuamini jambo hili hautoweza kuingia katika wokovu wa milele. 

VIPAWA VYA ROHO MTAKATIFU


Tukiangalia Biblia tunaweza kuona vipawa vya Roho mtakatifu vinatajwa sehemu tofauti tofauti. Vipawa hivi vinawakilishwa na warumi 12:6-8, 1 wakorintho 12:8-10 na waefeso 4:11. lakini leo hebu tuangalie vipawa tisa vilivyotajwa katika 1wakorintho 12.
1) Kipawa cha Neno la ufahamu. Huu ni ufahamu wa siri ya Injili ya maji na Roho iliyofichika kulingana na uvuvio wa Mungu, katika maandiko ya Biblia yenye nguvu ya Roho mtakatifu. Uwezo wa kueleza na kueneza Injili hii ya maji na Roho hii kipawa cha Neno la ufahamu.
2) Kipawa cha Neno la Busara. Kipawa cha neno la busara haina maana ya busara ya kibinadamu kama vile akili na utambuzi. Kipawa hiki cha kile cha kutatua matatizo mbalimbali yaletwayo na wanadamu katika kueleza neno la Biblia kwa imani.
3) Kipawa cha Imani. Kipawa cha Imani ni ile hali ya kuonyesha imani ya matendo katika Neno. Kipawa hiki hutolewa pale tunapolisikia neno la Mungu na tunapoliamini neno hili kwa imani thabiti. Roho mtakatifu anafanya kazi ili imani yetu ikue ndani ya mioyo yenu. Kwa kipawa hiki, Mungu anatuwezesha kuziokoa Roho za watu kutoka katika dhambi zao.
4) Kipawa cha Uponyaji: Badala ya kujaribu kuponya magonjwa ya mwilini, mitume lazima watambue kuwa Mungu anawataka watambue mapenzi ya Mungu kupitia madhaifu yao ya mwilini. Anataka wajue ukuu wa Mungu kupitia magonjwa walio nayo, yeye anaangalia uponyaji wa kiroho zaidi kwanza kuliko yale ya kimwili. Mungu anatushauri kuwaombea wagonjwa (James 5:14-15) na sala hizi ni zile ambazo kila mtakatifu anaweza kusema.
5) Kipawa cha kutenda miujiza. Hii ni ile nguvu ya imani inayoamini na kufuata neno la Mungu miujiza inalenga imani inayoamini neno la Mungu linalotengua sheria ya asili ya Imani ambazo zinafahamika Imani hiyo ya mitume inajenga nguvu katika imani zetu na kutuwezesha kuzaa matunda zaidi. Mungu anawafanya mitume watende kwa imani.
6) Kipawa cha Unabii. Hii ni kuamini neno la Mungu na kulieneza kwa niaba yake. Tangu Agano la kale hata jipya Mungu ametufunulia mapenzi yake na mipango. Hivyo manabii wa kweli ndio wanaoweza kuthibitisha usahihi au makosa ya wengine katika maandiko ya neno la Mungu. Kwa hiyo wale wasioeneza neno la Mungu lililoandikwa katika maandiko kwa imani za manabii wa uwongo. Unabii sahihi ni kueneza neno la Mungu kwa imani. Kwa kuwahubiria watu neno la Mungu mitume na watumishi wa Mungu ni lazima wawawezeshe kumwabudu Mungu, kufariji na kuhimizana. Yesu kristo ametoa pamoja na mwili wake, kanisa, kipawa cha imani inayoamini neno la watumishi wa Mungu.
7) Kipawa cha kupambanua Roho. Kupambanua Roho ni kipawa au uwezo wa kutambua kama watu wamepokea ondoleo la dhambi au tu wamesikia kinachosemwa. Kwetu sisi tunaoishi nyakati hizi za mwisho, kama hatuna kipawa hiki, tunadanganywa na shetani (1 Timotheo 4:1) na kipawa hiki, tunaweza kuwatambua wale wanaotafuta na kufuata vipawa vya Roho mtakatifu, na kuweza kutofautisha kati ya aliyezaliwa upya na yule ambae hajapokea ondoleo la dhambi na Roho mtakatifu.
8) Kipawa cha kunena kwa lugha. Inaposemwa kuwa mitume wanaongea kuwa lugha ina maana wanaongea ukweli juu ya ufalme wa mbinguni. Mitume wanapomwomba Mungu,, ni rahisi sana kwao kunena kwa lugha, ambayo inaeleweka na Mungu pekee. Licha ya kujaribu kunena, ni sharti tuweke mkazo katika kuelewa Neno la Biblia. Ni lazima tutambue kuwa ni bora kuongea maneno matano tunayoyaelewa na kuwafunza wengine kuliko kunena maneno elfu kumi (1 Wakorintho 14:19).

9) Kipawa cha kutafsiri ndimi. Huu ni uwezo wa kufundisha mapenzi ya Mungu ili kila mmoja aelewe kuwa kutafsiri neno lililotoka kwa Mungu kipawa hiki cha kutafsiri lugha kilitolewa na kanisa la kwanza kwa lengo la kueneza Injili, na sasa kinaweza kuonekana katika huduma ya kutafsiri na kufafanua mafundisho ya Injili. Kama mtu akiweza kuongea kwa lugha za kienyeji, hawezi kuhitaji mtafsiri, ila yule anayeweza kuongea lugha nyingi za duniani anahitaji mtu wa kutafsiri.

JINSI YA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU


Moja, wale wanaopenda kupokea Roho mtakatifu ni lazima waamini Injili ya maji na Roho na kupokea ondoleo la dhambi.
Pili, wanahitaji kuwa na imani thabiti juu ya ukweli kuwa, Mungu anatoa Roho mtakatifu kwa wale tu waliopokea ondoleo la dhambi, hata sasa kuanzia enzi za mitume (matendo 2:38).
Tatu, mioyo yao lazima igeuke mbali na dhambi ya kutoamini neno la Biblia na kutokuwa na imani.
Nne, kupokea Roho mtakatifu, Roho zao zinahitaji kufundishwa neno kikamilifu. Wanapaswa kusikiliza kwa uangalifu neno lililobarikiwa la kuzaliwa upya kwa maji na Roho, na wakihitaji zaidi, watapaswa kushirikiana katika vikundi vya Injili pamoja na watumishi wa Mungu na kupokea Roho mtakatifu. Roho mtakatifu atawafanya waliamini Neno la Mungu mioyoni mwao, kuzaliwa upya na kumpokea. Lakini kama wakijaribu kumpokea Roho mtakatifu bila ridhaa yao, ila bila ridhaa kwa kutoa sala za toba na kujaribu kuishi maisha ya utakatifu,
au pia wakimwigiza Roho mtakatifu wakijaribu kumpokea kwa kujinyima, kufunga, au sala za milimani, hapo wataishi kuanguka katika kuchanganyikiwa.
Tunapaswa kukumbuka kwamba Roho wa Mungu haji kwa sababu watu wanataka kumpokea wenyewe, bali huja kwa wale walio tayari kumpokea. Roho mtakatifu haji kwa wale wanaashinda milimani wakiomba, kushiriki mikutano ya karismatiki au wanaotaka vipawa tu, kama unafikiria ulipokea kitu fulani kama karama ya Roho mtakatifu katika mikutano hiyo, au kwa imani yako, basi hapo kuna jambo unapaswa kulitafakari kwanza. Na hii ni kama kuna dhambi au hakuna moyoni mwako. Unapaswa kutambua kuwa ulichokipokea si kutoka kwa Roho mtakatifu bali shetani, na ni lazima ukiondoe. Ni lazima tutambue ni wapi na kwa nini Roho mtakatifu anatenda kazi. Kuna jambo ambalo hatupaswi kulisahau katika kutafuta kupokea Roho mtakatifu. Hii ni kuamini ubatizo wa Yesu (mathayo 3:15) na damu yake msalabani. Roho mtakatifu anajitegemea, ila huja kwa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu kristo na damu yake msalabani na ondoleo la dhambi zao. Roho mtakatifu huja na kutenda kazi ndani ya maisha ya wale wanaoiamini Injili ya maji na Roho kama wokovu wao wa kweli.

Jumatano, 26 Machi 2014

MUNGU ROHO MTAKATIFU


Mungu Roho Mtakatifu sio nguvu tu bali pia anazo tabia
Roho Mtakatifu ni nafsi ya tatu katika utatu. Imani ya Mitume inaweka mkazo katika Roho Mtakatifu, inasema “namwamini Roho Mtakatifu” ni muhimu sana kwa Mitume kujua hakika huyu Roho Mtakatifu na kazi zake ni zipi. Na pia tunapaswa kujua vipawa vya Roho Mtakatifu, ambavyo vitafafanuliwa mbele kidogo ya sura hii. Tunapokiri kumwamini Roho Mtakatifu, kabla hatujatafakari nguvu za ajabu alizo nazo, ni lazima tuzingatie ukweli kuwa tunapokea Roho Mtakatifu pale tunapomwamini Mungu Baba na kazi za Mwanae. WaKristo wengi wana tabia ya kudhani wanaweza kupokea Roho Mtakatifu muda wowote na mara nyingi wanavyoweza. Lakini hili ni kosa kubwa. Lazima tutambue kuwa Roho Mtakatifu sio malaika, ila ni Mungu anayestahili sifa na kuabudiwa. Tunaweza kupokea Roho Mtakatifu tukimwamini Mungu Baba na kazi za Mwanae.
*      Mungu Roho Mtakatifu hufanya nini?
Nini hasa Roho Mtakatifu hufanya? Kwanza Roho Mtakatifu hushiriki katika huduma inayoogozwa na Mungu Baba na Mwana. Roho Mtakatifu alishiriki katika kazi za uumbaji zilizoanzishwa na Mungu Baba. Si hayo tu, pia alishiriki katika kazi za uumbaji zilizoanzishwa na Mungu Baba. Si hayo tu, pia alishiriki katika kazi za ukombozi zilizokamilishwa na Mungu Mwana kwa kuleta ushuhuda. Hii inajionyesha katika huduma ya ukombozi iliyokamilishwa na Yesu na kukamilishwa kwa kila mtume.
*      Tunawezaje kupokea ubatizo wa Roho Mtakatifu?
Ili kuelewa ubatizo na Roho Mtakatifu, kwamba tunapaswa kuelewa kwa nini Yesu alibatizwa na Yohana na kufa msalabani. Katika (warumi 3:23) tunasoma “wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” kila Mwanadamu amezaliwa akiwa na dhambi na hawezi ila kutenda dhambi mbele za Mungu, na kulingana na (warumi 6:23), inayotuambia kuwa “mshahara wa dhambi ni mauti” kila Mwanadamu hawezi kujiepusha na hukumu ya kifo kama mshahara wake wa dhambi. Lakini Mungu Baba anayewapenda wanadamu, ameandaa njia ambayo kwayo, tunaweza pata ondoleo la dhambi, kuhukumiwa kwazo na kuokolewa kutoka dhambini, yote haya kupitia Yesu, Mungu Baba alimtuma Mwanaye mpendwa, Yesu na akaimimina adhabu juu ya Yesu kupitia ubatizo na kusulubiwa msalabani. Badala yetu Yesu akachukua dhambi na kudhihakiwa hadi kufa na Mungu Baba. Licha ya kuwa Yesu alikuwa na haki alikufa na kushinda mauti. Alifufuka na alitoka kuzimu. Ni kwa jinsi gani sasa utimilifu wa ondoleo la dhambi unaunganishwa na wanadamu? Kwa kuamini kazi zake, maana yake ni sisi kupokea ondoleo la dhambi. Yesu aliyebeba dhambi za wanadamu kwa kubatizwa na Yohana katika mto Yordani alipokea adhabu zote pale msalabani ili kutupa ondoleo la dhambi. Tukiamini kuwa Yesu alibatizwa na Yohana na kuugulia kifo kama kujitoa kwa ajili ya dhambi zetu basi hapo tunapata haki ya Mungu, ya kuwa watoto wake, na kupata nafasi ya uzima wa milele (wagalatia 3:27) inasema “kama wengi wenu walivyobatizwa katika Kristo, wamekuwa waKristo.” (Yohana 3:16) inasema, kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe wa pekee ili kila amwaminie asipotee, bali awe na uzima wa milele” mstari huu, tunastahilishwa mara tu tunapoamini kuwa dhambi zetu zimepitishwa kwa Yesu kwa ubatizo aliopokea kwa Yohana na kuamini adhabu ya msalabani. Neno ubatizo linabeba maana nyingi mojawapo ni kutakasa dhambi, na ya pili ni kuunganisha. Ni lazima tutambue kuwa, kubatizwa na Roho Mtakatifu ni kujua na kuamini namna gani Yesu ameondoa matatizo ya maovu ya wakosaji ni kuwa ni kwa imani tunapokea ubatizo wa Roho mtakatifu. Kuwa Roho Mtakatifu amekuja mioyoni mwetu, kukaa ndani yetu na kutunganisha, ina maana tumeamini ubatizo wa Yesu. Huduma hii ya Roho Mtakatifu imeelezwa vizuri katika (Mathayo 3:13-17). Yesu alisema kuwa sababu ya kubatizwa kwake na Yohana ilikuwa kutimiza haki ya Mungu kwa mbinu ya ubatizo wake aliopokea kutoka kwa Yohana. Hivyo kupokea Roho Mtakatifu, ni sharti kwanza tuamini kwamba Yesu alichukua dhambi za wanadamu kwa kubatizwa na Yohana. Hivyo ndivyo tunavyoweza kuunganishwa na Roho Mtakatifu, hata Biblia pia inasema kuwa tunampokea Roho Mtakatifu kwa kuamini neema ya ondoleo na dhambi, kwamba Yesu alisulubiwa na kuimwaga damu yake kwa sababu alizikubali dhambi zote za wanadamu kupitia ubatizo wake. Roho Mtakatifu anakaa ndani ya mioyo yetu na wale waliotakaswa dhambi zao kwa ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani. Hii inaonekana katika mazungumzo kati ya Yesu na Nikodemu. Nikodemu alienda kumwona Yesu, Yesu akamwambia wale waliozaliwa upya wanaweza kuuona ufalme wa Mungu. Kuzaliwa upya maana yake, Roho iliyokufa inahuishwa na kufanywa mpya, na kupata nafasi katika ufalme wa mbinguni. Kusikia ukweli juu ya kuzaliwa upya, Nikodemu hakuelewa maana yake, ndipo akamwuliza Yesu, hayo yanawezekanaje.
Yesu akajibu  “Amini Amini nakuambia, Usipozaliwa kwa maji na kwa Roho huwezi kuingia Ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:5) kwa kuamini tu huduma ya Yesu kuwa ndiyo iliyoondoa dhambi zote za dunia na hata mizizi ya dhambi, ndipo tunaweza kuzaliwa upya na kazi hiyo ya ajabu ilitimia Yesu alipobatizwa na kufa msalabani tukiamini, Roho Mtakatifu atakaa ndani yetu. Hakuna juhudi, kazi wala mafanikio, uwezo au tabia ya mtu inayoweza kukufanikisha katika hili. Tunahitaji imani ile inayoamini ukweli kuwa ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani ndivyo vinavyotakasa dhambi za wanadamu. Tunahitaji kuzingatia yale Yesu aliyoendelea kusema katika mazungumzo yake na Nikodemu. Yesu alisisitiza umuhimu kuwa ni sharti tuzaliwe upya kwa maji na Roho. Huduma ya Roho Mtakatifu inayohuisha Roho zetu, kwa ubatizo wa Roho Mtakatifu sio tu ni badiliko la kuanzia ndani ya moyo wa mtu, bali pia ni huduma kubwa inayotendeka. Kwa sababu ya hili, huduma yenyewe haiwezi kuonekana kupitia sababu zetu au ufahamu wetu. Tunaloweza kujua ni kupokea ubatizo wa Roho Mtakatifu pamoja na ondolea la dhambi tulilopokea ndani ya mioyo yetu tulipoamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani. Tunatambua kuwa tumekuwa watoto wa Mungu tunapopokea Roho Mtakatifu kama zawadi (Warumi 8:15).
*      Roho Mtakatifu ni nani?
Roho Mtakatifu ni nafsi ya tatu ya Uungu. Imani ya Utatu ndio msingi mkubwa wa imani. Ukweli wote unaweza kufahamika na kueleweka kwa kuamini Injili ya Maji na Roho. Kwa nini? Sababu ni kama zifuatazo.
·         Kwa sababu wenye dhambi ni viumbe wa Mungu, ukweli juu ya utatu hauwezi kujulikana hadi mtu anapopata ondoleo la dhambi kwa kuiamini Injili ya maji na Roho.
·         Kwa sababu ya makosa yetu, mioyo ya wanadamu imetiwa giza na dhambi. Kama vile kioo kisivyoweza kuona kikiwa kimepakwa tope, macho ya mioyo ya wenye dhambi hayawezi kuona yale Mungu wa utatu aliyotenda.
·         Bila nuru ya Roho Mtakatifu, hatuwezi kamwe kujua yaliyo ndani ya Mungu. Kama ilivyo Roho Mtakatifu alivyo shahidi kuwa Neno la Mungu ni kweli (Yohana 16:13), Roho Mtakatifu anatuwezesha sisi kujua ukweli juu ya maji na Roho, kwa kuwa yeye mwenyewe ni Mungu mwenye nafsi kamili na ufahamu, nia na hisia. Anakaa ndani ya wale wanaoamini Neno la Mungu na kulifanyia kazi. Ni sharti tumwabudu yeye, tumwamini na kumtii.

*      Ni zipi kazi kuu za Roho Mtakatifu?
Roho Mtakatifu anafanya kazi ya kutunza Roho za Mitume waliosamehewa dhambi kwa kuamini Injili ya maji na Roho. Roho Mtakatifu anafanya kazi kulingana na imani zetu katika maandiko matakatifu.
·         Anabeba ukweli kuwa Neno la Mungu ni kweli. Roho Mtakatifu anatoa garantii kwa wale walioliamini Neno la ubatizo wa Yesu na msalabani. Yeye anayeihakiki imani yake kuwa ni hakika ni Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu anafanya kazi kati ya wale wanaoliamini Neno. Roho Mtakatifu anahakiki imani ya wale wanaoimini Injili ya maji na Roho. Anatoa garantii, kwa maneno mengine, wale wanaoamini kuwa Yesu alikuja duniani ili kuitakasa dunia na dhambi kwa njia ya ubatizo na damu yake msalabani.
·         Roho Mtakatifu yupo na mwenye haki, na anawafanya waishuhudie injili ya maji na Roho kwa wenye dhambi. Katika Yohana 16:8-9 alisema “akija atauhukumu ulimwengu kwa haki na dhambi kwa sababu hawajamwamini Roho Mtakatifu anaihakiki injili ya maji na Roho katika mioyo ya wenye haki (Yohana 14:26). Anachukua ushuhuda wa yale ambayo Mungu amefanya anatuwezesha kujua kuwa Yesu alikuja duniani, na kuchukua dhambi zetu kwa kubatizwa, kufa msalabani, na anatuwezesha sisi kuyaamini hayo yote.
·         Anafanya tumwamini Mungu, na kuliitia jina lake. Roho Mtakatifu anawafanya wenye haki kuomba. Warumi 8:15 inasema,  “Kwa kuwa hamkupokea tena roho ya utumwa iletayo hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana. Ambayo kwa hiyo twalia Abba, yaani ‘Baba’”.  Roho Mtakatifu anawawezesha Mitume kumwita Mungu na kumwamini yeye kama “Abba, Baba”.
·         Roho Mtakatifu anatuwezesha kuzifanyia kazi karama alizotupatia. Anatuwezesha kufanya kazi za haki za Mungu kwa uwezo wake 1Wakorintho 15:10 inasema, “kwa neema ya Mungu, nipo kama nilivyo, na neema yake kwangu si bure, nalijitaabisha sana kuliko hao wote, lakini bado si mimi, ila ni neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.”
·         Roho Mtakatifu anatuongoza mpaka tuingie Mbinguni, Roho Mtakatifu anawawezesha wenye haki kuitunza imani yao mpaka wafike ufalme wa Mungu, na hubaki nao kama mwalimu wao.

*      Kumpokea Roho Mtakatifu ni hatua ya tofauti kwa Mkristo?

Licha ya kuwa Yesu hatoi Roho Mtakatifu kwa wenye dhambi, bado kuna wengi wasio tayari kubadili misimamo yao. Wakati wale wasiojua injili ya maji na Roho wanapopata kiu ya kupokea Roho Mtakatifu, hupokea pepo na kudai na Yesu amewajia na hapo huishia kushikwa na mapepo na nguvu za giza, hivyo, watu wasijaribu kupokea Roho Mtakatifu kwa nguvu zao wenyewe. Ni hatari sana kwa mtu ambaye hajapokea ondoleo la dhambi kuomba apate Roho Mtakatifu. Ni sharti tutambue kuwa, ni upuuzi kuomba jambo lisilowezekana. Biblia inasema, mamlaka ya wale waliopokea ondoleo la dhambi ni kubwa (Yohana 20:23). Yesu alisema  “kama ukisamehe dhambi ya yeyote utasamehewa, ila usiposamehe, hutasamehewa” mamlaka hii wanapewa wale tu, waliopokea ondoleo la dhambi, na kupokea Roho Mtakatifu. Mamlaka kubwa, na majukumu pia ni makubwa. Yesu alimwambia petro, “nimekupa funguo za mbinguni”, hii ni mamlaka waliyopewa wale waliopokea ondoleo la dhambi kwa njia ya Injili ya maji na Roho. Mamlaka ya wale waliopokea ondoleo la dhambi na Roho Mtakatifu mioyoni mwao kwa kuamini injili ya maji na Roho ni ya ajabu sana. Wanayo mamlaka ya kuongoza watu kwenda mbinguni na hata kutupwa kuzimu. Kwa hiyo Mitume hawaenezi Injili ya ondoleo la dhambi kwa wakosaji na kuwaacha jinsi walivyo, hapo itakuwa makosa yapo kwao kwa kuwaacha wakipotea mamlaka ya kusamehe dhambi za watu kutolewa wa Mitume.

UTATU MTAKATIFU


Kuna nafsi tatu za utatu mtakatifu, kwa maneno mengine Mungu ni yule yule.
Tuangalie maandiko yanasema nini kuhusu utatu mtakatifu
*      Agano la kale.
Ø  Kwanza kabisa, katika Agano la kale tunaona kuwa Mungu ni moja: Sikiliza ewe Israel, Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja”(Kumbukumbu la Torati 6:4).
Ø  Agano la kale pia linaeleza kuhusu nafsi mbalimbali (utatu mtakatifu) “Kisha Mungu akasema, ‘tufanye mtu kwa mafano wetu, kwa sura yetu” (Mwanzo 1:26) “Haya na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.” (Mwanzo 11:7). Vifungu hivi vinadhihirisha kuwa Mungu yupo katika nafsi nyingi.
*      Agano jipya.
Ø  Nafsi tatu (utatu mtakatifu) unajifunua katika ubatizo wa Yesu Kristo ambao ndio mwanzo wa huduma zake.  “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini, na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake, na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayepenzwa naye” (Mathayo 3:16-17).  Kifungu hicho hapo juu kinaeleza utatu mtakatifu uliofunuliwa katika ubatizo wa Yesu uliofanywa na Yohana Mbatizaji. Katika kifungu hiki tunajua ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu, ambaye Roho Mtakatifu anafanya kazi pamoja nae. Ambaye kwa Mungu ni mwanae mpendwa aliye pendezwa nae. Kupitia ishara hii, utatu mtakatifu wa Mungu unajifunua. Yesu aliweza kukamilisha haki yote ya Mungu kwa sababu alichukua dhambi za mwanadamu kupitia ubatizo alioupata kupitia kwa Yohana mbatizaji. Kwa sababu ya ubatizo ilimpasa Yesu kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na hii ndio “haki ya Mungu”  ambayo baba aliikamilisha kupitia mwanae Yesu. Kwamba Yesu alibeba dhambi zetu kupitia tendo kuu la ubatizo na hiyo ndiyo haki ya Mungu, na ukweli huu umethibitishwa na Baba na Roho mtakatifu. Hivyo Baba, Mwana Roho mtakatifu wamejifunua katika nafsi tofauti, lakini Mungu ni yule yule.
Ø  (Mathayo 28:19) “ basi, enendeni mkawafanye, mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho mtakatifu”. Pia inadhihirisha kwamba Baba, Mwana na Roho mtakatifu kila mmoja ni nafsi inayojitegemea, lakini kwa wakati huo huo wote ni wa moja kwani ni Mungu yule yule mmoja. Tunapomwamini Mungu, twamwamini Mungu mmoja aliyeunganishwa na nafsi tatu. Mungu Baba, Mwana na Roho mtakatifu kama Imani ya Kikristo inavyokiri ni Mungu aliyepo tofauti kabisa na Miungu wengine. Dini zingine zinaamini kuwa Yesu ni nafsi moja kati ya manabii wengi, lakini hii sio sahihi.
Ø  Kwetu sisi Mungu ni Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Licha ya ukweli kuwa ukweli huu umetosheleza na kupimwa na maandiko, kuna wengi ambao bado hawatambui hili. Hii ni kwa sababu wale wasiojua Injili ya maji na Roho wanadhania utatu mtakatifu kibinadamu ambayo huwafanya wasielewe. Wale ambao bado hawajazaliwa upya hawawezi kuelewa utatu na Roho mtakatifu ni Mungu mmoja kwetu, kwake ambaye tunaiweka Imani yetu kwa uthabiti.
*      Asili ya Utatu wa Yesu Kristo: 
Yesu Kristo amekuwepo kabla ya uumbaji na amekuwepo kama Mungu kweli na miele. Japokuwa alikuja duniani kama mwandamu, ameendelea kuwa Mungu (Yohana 1:1, 14) kama vile (warumi 9:5) inasomeka “Ambao mababu ni wao, na katika wao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili, ndie aliye juu ya mambo yote, Mungu mwenye kuhimidiwa milele, Amina”. Ukiri wa kanisa la Mungu kuhusu asili ya Yesu Kristo haujatungwa na wanadamu, umepatikana kutoka ufunuo wa Mungu mwenyewe (Mathayo 16:17) zaidi sana ukweli uliomo katika Biblia unaelza asili ya ukuu wa Kristo (Isaya 9:6,Mika 5:2). Katika Agano Jipya, ukuu wa kweli wa Kristo mwokozi umefanuliwa na kuthibitishwa na Kristo mwenyewe. Petro alikiri pia kuwa Yesu “wewe ni Kristo Mwana wa Mungu aliye hai” (Mathayo 16:16, Marko 8:29 na Luka 9:20). Zaidi ya hapo, Paulo alisema “ ambaye, yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu.” (Wafilipi 2:6).Yohana alipokuwa akimtukuza Kristo, naye alikiri. “Nasi twajua ya kuwa mwana wa Mungu amekwishakuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye mwana wa Kweli na uzima wa milele.” (1 Yohana 5:20).
Nabii mkuu alipomuuliza Yesu “tuambie kama wewe ni Kristo Mwana wa Mungu”Yesu akasema “wewe wasema” (Mathayo 26:63-64, na Marko 15:2).Katika matukio mengine Yesu alisema yeye na Mungu ni wa - moja (Yohana 10:30) na kuwa yeye alikuwepo hata kabla ya Abraham (Yohana 8:58). Kristo alielezea nafsi yake kama nabii mkuu wa utukufu ambao yeye alishirikiana na Baba hata kabla ya uumbaji (Yohana 17:5). Pia tunaona, pale Kristo aliposamehe watu dhambi zao au kuponya magonjwa yao na pale alipowahimiza wanafunzi wake kumwamini yeye, haya yote yalifungua njia ya kuufahamu ukuu wa Mungu.
*      Asili Ya Kibinadamu Ya Yesu Kristo:
Agano Jipya pia linaeleza ubinadamu wa Yesu. Mwana wa pekee wa Mungu alizaliwa “kwa mfano wa Mwanadamu” (Wafilipi 2:7-8)  aliitwa “Mwanadamu Yesu Kristo” (1 Timotheo 2:5) licha ya kuwa alikuwa Mungu mwenyewe, alijinyenyekeza na kuwa kama Mwanadamu na Akakaa kwetu (Yohana 1:14). Matokeo yake alibatizwa na Yohana mbatizaji. Akakaa kati ya watu kama mtu, na akashiriki furaha yao na huzuni zao. Pia alikula chakula kile kile kama wanadamu wengine. Yeye alikuwa mtu si tu kwa mwonekanao, bali tabia yake pia. Kama wengine, yeye pia alikuwa wa uzao wa Adamu (Luka 3:38) pia alizaliwa na Mwanamke (Luka 2:6-7) (Mathayo 11:18-25) na (wagalatia 4:4) mojawapo ya mababu zake ni Abrahamu na Daudi (Mathayo 1:1). Licha ya kuwa Yesu mwenyewe hakuwa na dhambi alikuja hapa duniani katika mwili wa nyama ambao Mwanadamu ameudhoofisha kwa dhambi. Kwa maneno mengine Kristo alikuja kwa namna ya mwili wenye dhambi na kwa kubatizwa na Yohana alitimiza haki yote ya Mungu (Yohana 19:30). licha ya kuwa alibeba dhambi zetu mabegani mwake na ubatizo pamoja na mateso aliyopata, hakutofautishwa na wengine (Isaya 53:2-3). Licha ya kuwa Kristo alikuwa na asili yetu hakuthubutu kuingia katika majaribu ya kutenda dhambi kutokana na mwandishi wa kitabu cha Waebrania, Kristo alikuwa kwa namna nyingi akijaribiwa kutenda dhambi kama sisi, lakini bila kutenda dhambi (Waebrania 4:15). Yesu alichukuwa dhambi za dunia kwa kubatizwa na Yohana na hii ndio sababu alisulibishwa kwa ajili ya wenye dhambi. Tukirejea kwa Kristo, Waebrania 7:26 inasema, “kwa maana inatupasa sisi tuwe na Kuhani mkuu wa namna hii aliye mtakatifu, asiye na uovu asiyekuwa na waa lolote, aliyetengwa na wakosaji”.
*      Je, Yesu Alikuwa Mungu?
Ndiyo, Yesu alikuwa Mungu mwenyewe. Yesu ndiye hasa aliyeumba dunia yote kwa neno la kimywa chake. Kwa hakika dunia hii iliumbwa na Mungu Yohana 1:3 inasema “vitu vyote viliumbwa na yeye, na pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa kinaoonekana” Yesu alikuwa Mungu mwenyewe aliyekuja kuwaokoa wakosaji. Yesu aliumba ulimwengu huu kwanza. Pale aliposema “na iwe nuru”, mara ikawa nuru. Aliposema “na liwepo jua”, mara jua likatokeza. Ilikuwa ni amri tu “na iwe” vyote majini, miti, bahari, anga, na hata wanadamu wakatokea. Yesu Kristo aliumba kila kitu hapo
mwanzo (Mwanzo 1:3-15). Alikuwa ndiye Mungu mkuu wa uumbaji. Yote yalifanyika kwake. Na hakuna chochote kilichokuwepo bila yeye. Sasa ni kwa nini alikuja kwa mfano wa Mwanadamu? Alikuja kuokoa, wenye dhambi wote wa dunia hii. Sababu kubwa ya kuja kama Mwanadamu ilikuwa ni kuleta nuru ya kila mwenye dhambi na hatimaye kuwaokoa na dhambi zao. Yohana 1:9-12 inasema “kulikuweko na nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwapo, wala ulimwengu haukumtambua alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea bali waliompokea waliwapa uwezo kufanyika wana wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”. Mungu alikuja kuondoa dhambi za dunia tulizorithi kutoka kwa Adamu, Baba wa wanadamu, na kuondoa giza kutoka duniani. Jina lake yeye ni Yesu Kristo na Yesu Kristo ni mtoto wa Mungu Baba.
*      Utatu wa Mungu
WaKristo wanapaswa kumjua Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kama Mungu mmoja, na kukiri imani kwa nafsi hizo zote? Ndiyo, sababu ni kama ifuatavyo: Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wote walishiriki huduma ya uumbaji na kumkomboa Mwanadamu. Lakini Mungu Baba ni Baba wa Mwana mtakatifu. Mwana alitimiza huduma ya ondoleo la dhambi, kwamba alibatizwa na Yohana, alisulubiwa, ili kumkomboa Mwanadamu kutoka dhambini. Roho Mtakatifu alichukua nafasi ya kubeba ushuhuda wa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu ushuhuda kwa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani kuwa vimetenda kazi ya kutakasa dhambi. Sisi kuwa watu kamili kwa Mungu, tunahitaji kumwamini Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kwa namna hii. Ni kwa sababu Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu waliumba ulimwengu, na sisi tuishio humu, na Mungu Mwana kuwaokoa wenye dhambi, ubatizo uliokamilisha haki ya Mungu na kazi ya kumwaga damu pale msalabani ilihitajika. Kwa kuwa Yesu alibatizwa na Yohana na hapo akachukua dhambi za dunia, alichukua adhabu ambayo sisi tulistahili kuibeba na kufa msalabani badala yetu.

Kwa kufanya hivyo, wenye dhambi hatimaye walipokea ondoleo la dhambi. Ukweli huu uliandaliwa muda mrefu, na ndio msingi hasa wa huduma ya Injili ya maji na Roho. Ni pale tunapoutumia ukweli huu ndipo kazi ya Yesu Kristo ya utakaso inapotimilika kwa ajili yetu, na tunaweza kuokolewa kutoka dhambini kwa kuamini tu. Kama tusingekuwa na ufahamu juu ya Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, hapo tusingeliweza kuujua ulimwengu ulivyoumbwa na nani aliyetupatia uzima, na kusingekuwa na Mungu Mwana, tusingeweza kujua njia ya wokovu, dhambi zetu zingepitishwa wapi? Msingi wa wokovu wetu ungekuwa nini. Na kama kusingekuwa na ushuhuda wa Roho mtakatifu, hapo haijalishi ukubwa na njia ya wokovu iliyoandaliwa, ukweli ungebaki kama alama tu mawinguni usio na lolote la kufanya nasi. Kwa hiyo kila tunapokiri imani ya Mitume , ni lazima tumfikiri Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu aliyetuumba na kutupa uzima na ni lazima tuwe imara katika imani na kuamini kuwa nafsi hizi tatu ni Mungu pamoja.

Jumatano, 19 Machi 2014

FUMBO LA KIROHO KATIKA SANDUKU LA USHUHUDA


(Kutoka 25: 10-22) “Nao na wanifanyie sanduku la mti wa mshita; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu. Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote. Nawe subu vikuku vinne vya dhahabu kwa ajili yake, na kuvitia katika miguu yake minne; vikuku viwili upande mmoja, na vikuku viwili upande wake wa pili. Nawe fanya miti mirefu ya mshita na kuifunika dhahabu. Nawe tia hiyo miti katika vile vikuku vilivyo katika pande mbili za sanduku ili kulichukuwa hilo sanduku. Hiyo miti itakaa katika vile vikuku vya sanduku; haitaondolewa. Kisha tia ndani ya sanduku huo ushuhuda nitakaokupa. Nawe fanya kiti cha rehema cha dhahabu safi; urefu wake utakuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu. Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayo kuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli.”
Sanduku hili lilitengenezwa kwa mti wa mshita na lilifunikwa kwa dhahabu safi. Ndani ya sanduku kulikuwa na mbao mbili za mawe zilizokuwa zimeandikwa Amri kumi na birauli ya dhahabu iliyokuwa na mana, na baadaye iliwekwa ile fimbo ya Haruni iliyochipuka. Je, vitu hivi vitatu vilivyowekwa ndani ya sanduku hili la ushuhuda vinatueleza nini?
Mbao mbili za mawe zilizokuwa zimeandikwa sheria
Mbao mbili za mawe zilizokuwa zimeandikwa Sheria na kuwekwa ndani ya sanduku la ushuhuda zinatueleza sisi kuwa Mungu ndiye mtunga sheria ambaye ametupatia sisi sheria zake. (Warumi 8: 1-2) “ sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti.” Katika kifungu hiki tunaweza kuona kuwa Mungu alianzisha sheria mbili katika mioyo yetu: sheria ya uzima na sheria ya adhabu.
Kwa sheria hizi mbili, Bwana ameleta adhabu na wokovu kwa wanadamu wote. Kwanza kabisa tunaweza kutambua kwa kupitia sheria kwamba sisi tu wenye dhambi ambao bila kukwepa tumepangiwa kuzimu. Hata hivyo, kwa wale ambao wanaifahamu hali yao ya asili kuwa wamepangiwa mabaya, Mungu amewapatia watu wa jinsi hiyo sheria yake ya wokovu, “sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu” Mungu amefanyika kuwa mwokozi wa kweli kwa watu wote kwa kuwapatia sheria hizi mbili.
Maana ya kiroho ya bilauri ya dhahabu
Ile Bilauri ya dhahabu iliyokuwepo katika sanduku la ushuhuda ilikuwa na mana. Wakati watu wa Israeli walipotumia miaka 40 katika jangwa na nyika, Mungu aliwaletea chakula toka Mbinguni na Waisraeli waliishi kwa kutegemea mana hii wakiipika katika hali tofauti. Mana hii ilikuwa ni nyeupe kama vile mbegu za giligilani, na radha yake ilikuwa ni kama maandazi yaliyotengenezwa kwa asali. Hii mana ambayo Mungu alikuwa amewapatia watu wa Israeli iliwawezesha kuishi maisha yao hadi pale walipoingia katika nchi ya kanaani. Kwa hiyo, chakula hiki kiliwekwa kwa ajili ya ukumbusho na hivyo ikawekwa katika bilauri hii.
Hii inatueleza kuwa sisi waamini wa leo tunapaswa pia kula mkate wa uzima, ambao wana wa kiroho wa Mungu ni lazima waule wanapokuwa hapa duniani hadi pale watakapoingia Mbinguni. Lakini kuna nyakati ambapo tunapenda kuupata mkate wa ulimwengu, ambao ni mafundisho ya ulimwengu huu badala ya Neno la Mungu. Pamoja na hayo, kitu ambacho watoto wa Mungu wanapaswa kukiishia na kuishi kwa hicho hadi pale watakapofikia nchi ya kiroho ya kanaani  ni neno la Mungu, ambalo ni mkate wa kiroho wa maisha ya kweli unaotoka Mbinguni.
Mtu hawezi kuchoka kwa kuula mara kwa mara mkate wa maisha ya kweli. Kadri tunavyo upata mkate huu wa kiroho, ndivyo mkate huo unavyofanyika kuwa maisha ya kweli katika nafsi zetu. Lakini ikiwa tunaula mkate wa mafundisho ya ulimwengu badala ya Neno la Mungu, basi hatimaye nafsi zetu zitaishia mautini.
Mungu aliwaamuru watu wa Israeli kuiweka mana iliyotoka Mbinguni katika bilauri ya dhahabu na kuitunza. Kama inavyoonyeshwa katika kutoka 16:33, Mungu alisema, “ twaa kopo, ukatie pishi moja ya hiyo mana ndani yake uiweke mbele ya BWANA, ilindwe ka ajili ya vizazi vyenu.” Ile mana iliyotoka Mbinguni ulikuwa ni mkate wa maisha ya kweli kwa ajili ya nafsi za watu. “ Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali ishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA” (kumbukumbu la torati 8:3)
Mkate wa uzima kwetu sisi ni nani?
Ubatizo ambao Yesu Kristo aliopokea ili kuzichukua dhambi zetu katika mwili wake na kusulubiwa kwake na kuimwaga damu yake hivyo ndivyo vinavyo ufanya mkate wetu wa kweli wa maisha. Kwa kutupatia sisi mwili na damu yake, Yesu Kristo amefanyika kuwa ni mkate wa uzima wa milele. Kama ambavyo Yohana 6: 48-58 inatueleza sisi: “ Mimi ndimi chakula cha uzima. Baba zenu waliila mana jangwani; wakafa,. Hiki ni chakula kishukacho kutoka Mbinguni, kwamba mtu akile wala asife. Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka Mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. ……………………………………………………………… endelea katika Biblia”
Mwili na damu ya Yesu katika Biblia, mwili wa Yesu unatueleza sisi kuwa Yesu Kristo alizichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana katika mto Yordani.  Na damu ya Yesu inatueleza sisi kuwa kwa sababu Yesu alibatizwa, basi alizuchukua dhambi za ulimwengu na akabeba adhabu ya dhambi za ulimwengu na akabeba adhabu ya dhambi hizo kwa kusulubiwa.
Mana katika ile bilauri iliyokuwa imewekwa ndani ya Sanduku la Ushuhuda ilikuwa ni mkate wa uzima kwa Waisraeli walipokuwa nyikani,na katika kipindi cha Agano Jipya, maana yake ya kiroho ina maanisha juu ya mwili wa Yesu Kristo. Ukweli huu unatuonyesha sisi ubatizo ambao kwa huo Yesu Kristo aliyachukuwa makosa na maovu ya wenye dhambi wote na damu ambayo aliimwaga pale msalabani. Kwa kuwa Yesu Kristo alichukuwa dhambi zote za ulimwengu huu katika mwili wake kwa kupitia ubatizo wake na damu yake iliyomwagika vimefanyika kuwa vitu muhimu vya kudumu vinavyowawezesha waaamini kuzaliwa tena upya.
Mwili ambao Yesu aliutoa ili kuyachukua maovu yote ya wenye dhambi kwa kupitia ubatizo wake na damu yake aliyoimwaga msalabani ni mkate wa uzima unaowawezesha wenye dhambi kupokea ondoleo la dhambi. Kwa hiyo ni lazima tutambue sababu ambayo ilimfanya Yesu kusema, “ msipoula mwili wake Mwana wa adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu” (Yohana 6:53).
Maelezo ya ziada; ni kwa kuamini katika ukweli huu halisi ndipo tunapoweza kuula mwili wake na damu yake. Kuoshwa kwa dhambi kulitimizwa pale ambapo dhambi za mwanadamu zilipopitishwa katika mwili wa Yesu kwa kupitia ubatizo ambao aliopokea. Kuinywa damu yake kunamaanisha kuwa Yesu alibatizwa na kuimwaga damu yake msalabani, damu hii aliyoimwaga ilibeba adhabu ya dhambi zetu.
Fimbo ya Haruni iliyochipuka
Miongoni mwa vitu vilivyowekwa ndani ya sanduku la ushuhuda, fimbo ya Haruni iliyochipuka ina maanisha juu ya Yesu Kristo kuwa ni kuhani mkuu wa milele wa ufalme wa mbinguni.  Pia inatueleza sisi kuwa uzima wa milele unaopatikana katika Yesu Kristo. Soma (Hesabu 16:1-2) Basi kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, akatatwaa watu pamoja na dathani na abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi,waliokuwa wana wa Reubeni. Nao pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele za Musa”.
Kifungu hiki kinatueleza sisi kuwa miongoni mwa Walawi, viongozi mashuhuri 250 wa watu walijikusanya na kuinuka dhidi ya Musa. Wakamwambia, “Musa na Haruni mmetufanyia nini kwa kutuongoza sisi toka katika nchi ya Misri? Je, mmetupatia mizabibu? Mmetufanyia nini? Je, hamkutuletea sisi huku nyikani ili hatimaye tufe katika jangwa la mchanga? Je, mwawezaje kujiita ninyi wenyewe kuwa ni watumishi wa Mungu? Je, Mungu anatenda kazi kwa kupitia ninyi tu?” kwa maneno mengine, kulikuwa kumeinuka upinzani na uasi dhidi ya uongozi wa Musa na haruni.
Kwa wakati huo, Mungu akamwambia Kora, Dathani, Oni, na viongozi wengine wa watu waliokuwa wameongoza uasi, “Niletee fimbo kutoka katika kila nyumba ya baba na andika kila jina la nyumba hiyo katika fimbo hiyo. Kisha ziweke hizo fimbo katika Hema takatifu la kukutania. Ziache pale kwa usiku mmoja na kisha uje kuziangalia siku inayofuata.” Kisha Mungu akasema, “Kisha itakuwa, mtu huyo nitakayemchagua, fimbo yake itachipuka; name nitayakomesha kwangu manung’uniko ya wana wa Israeli, wanung’unikayo juu yenu” (hesabu 17:5). Katika aya ya 8, tunaona kuwa “ilefimbo ya Haruni iliyokuwa kwa nyuma ya Lawi ilikuwa imechipuka, imetoa michipukizi, na kuchanua maua; na kuzaa milozi mabivu”.
Kisha katika aya ya 10, tunaona kuwa, “kisha BWANA akamwambia Musa, irudishe fimbo ya Haruni mbele ya ushahidi, ili ituzwe iwe ishara juu ya hawa wana wa maasi; ili uyakomeshe manung’uniko yao waliyoninung’unikia, ili wasife.”  Hivi ndivyo ambavyo fimbo ya Haruni iliyochipuka ilivyo kuja kuwekwa ndani ya sanduku la ushuhuda.
Hii inaonyesha kuwa Haruni wa ukoo wa Lawi alipakwa mafuta kuwa kuhani mkuu wa watu wa Israeli.musa alikuwa ni nabii wa Mungu na Lawi pamoja na ukoo wake wake walikuwa ni makuhani wakuu wa watu wa Israeli. Mungu mwenyewe alikuwa amewakabidhi majukumu ya kuhani mkuu wa kidunia Haruni. Mungu alikuwa amemwonyesha Musa utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa, ambapo watu wa Israeli walileta sadaka ya kuteketezwa na kumtolea Mungu kila walipofanya dhambi, na Mungu alimfanya Haruni kusimamia utoaji wa sadaka hizi kwa mujibu wa kanuni za utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa.




Ijumaa, 14 Machi 2014

KUNA NJIA MOJA TU YA KUINGIA MBINGUNI


(Matendo 4:12) inasema, “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
Kwa sababu tunaamini katika ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani, basi sisi tutaingia Mbinguni. Hakuna njia nyingine ya kuingia Mbinguni bali kwa kuamini katika Injili ya kweli. Ni kwa kuamini tu katika yale ambayo Yesu amefanya kwa ajili yetu ndipo tunapoweza kuingia Mbinguni, kwa kuwa Mungu amefanya kazi hizo kwa wale wanaoamini katika Injili ya maji na roho (ipo katika blog hii).
Hii ndiyo sababu Wakristo hawawezi kuingia Mbinguni kwa kupitia jitihada zao wenyewe, kwa kujitoa, au majaribio mengine ya kinafiki. Mungu amedhamiria kuwa ni wale tu ambao wamesafishwa dhambi zao kwa kuamini katika ubatizo wa Yesu alioupokea na katika damu yake aliyoimwaga ndiyo wanaweza kuingia Mbinguni. Wale wanaoamini katika ukweli huu ndio wale wanaoamini kwamba Yesu ni mwana wa Mungu, Mungu mwenyewe, na mwokozi wa milele ambaye amewaokoa toka katika dhambi kwa kupitia ubatizo wake na damu yake aliyomwaga. Mungu ameruhusu kusafishwa dhambi kwa watu kama hao
Theolojia haina nafasi yoyote katika kuifahamu Biblia kiusahihi na kikamilifu. Theologja ni ufahamu wa kibinadamu si wa Roho mtakatifu. Ndiyo maana kuna lundo la mafundisho ya kikristo na theolojia  ambazo ziliinuka katika historia ya ukristo, watu wengi wameanguka katika mafundisho ya kimafumbo hali wakimwanini Mungu kwa kutegemea katika uzoefu wao binafsi. Lakini pamoja na tofauti za kitheolojia, matawi yote ya ukristo yametawaliwa na imani moja kimsingi, ambayo ni kuamini katika damu ya Yesu tu.
Lakini je, huu ni ukweli? Unapoamini kwa namna hii, je, dhambi zako zitatoweka kweli? Unafanya dhambi kila siku kwa moyo wako , mawazo, na matendo. Unaweza basi kuondolewa dhambi zako kwa kuamini katika damu ya Yesu tu ambayo alimwaga msalabani? Kule kusema kuwa Yesu alizibeba dhambi zetu kwa kubatizwa na kufa msalabani huo ni ukweli wa kibiblia. Hata hivyo kuna watu wengi sana ambao wanasema kuwa dhambi zao zimeondolewa kwa kuamini katika damu ya Yesu tu pale Msalabani na kwa kutoa sala zao za toba kila siku. Je, dhambi za dhamira zako zilisafishwa mbali kwa kutoa sala za toba za jinsi hiyo? Hii haiwezekani.
Ikiwa wewe ni mkristo, basi ni lazima ufahamu na kuamini katika wokovu wa kweli kwamba Yesu alikuja hapa duniani na akazichukuwa dhambi zetu zote za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana. Pamoja na haya, je, bado unaudharau ukweli huu, kiasi kuwa hutaki hata kuufahamu na kisha kuamini? Ikiwa ndivyo, basi ufahamu kuwa unafanya dhambi ya kumdhihaki Yesu, dhambi ya kulishusha na kulidharau jina lake, na kwa jinsi hiyo huwezi kusema kuwa unaamini kweli katika Yesu kuwa ni mwokozi wako. Kwa kuuacha ubatizo wa Yesu Kristo na kwa kumwamini Yesu kwa namna yoyote unayoipenda, basi kwa kweli huwezi kuvikwa katika neema ya wokovu, (soma Injili ya maji na roho katika blog hii utaelewa nachokisema).
Njia ni moja tu ya kuingia Mbinguni (Mathayo 7:13-14) “ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache” kuna dini nyingi sana duniani ambazo zimefanikiwa kujikusanyia watu wengi kwa njia mbali mbali, usiangalie wingi wa watu, maana waionao njia ni wachache. Watu wengi wanapoteza muda kukosoa madhebu ya wengine, hata wale wasio wakristo mahubiri yao yamekuwa ni ya kukosoa ukristo.  Lakini ndugu unapoteza muda bure, Biblia si kama vitabu vingine ambavyo unaweza kuvisoma kwa kutumia akili za kibinadamu, inahitajika hekima ya Mungu, soma fungu hili (1wakorintho 2:10-15) lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukupokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”
Wale wanao ichambua Biblia kwa kutumia akili zao waache mara moja, wajisalimishe kwa Yesu, na wasome katika blog hii “Injili ya maji na roho” ili waweze kupokea Roho mtakatifu. Kuna wengine husoma na kudharau, lakini kumbuka bila Roho mtakatifu Biblia utaisoma kama kitabu cha hadithi na shetani atakufunga katika fikira zako. (2 Korintho 4:3-4) “lakini ikiwa Injili yetu imesitirka, imesitirika kwa hao wanaopotea, ambao ndani yao Mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao, isiwazukie nuru ya Injili ya utakatifu wake Kristo aliye sura yake Mungu”


PAZIA LA HEKALU LILILOPASUKA WAKATI YESU ANAKUFA.


( Mathayo 27: 50-53) “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; makabuli yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.”
Patakatifu pa patakatifu palikuwa ni mahali ambapo Mungu aliishi. Na ni kuhani mkuu tu ndiye aliye ruhusiwa kuingia hapo mara moja kwa mwaka, katika ile siku ya Upatanisho hali akiwa amebeba damu ya mbuzi wa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya ondoleo la dhambi la Waisraeli. Kuhani mkuu alifanya hivyo kwa sababu Patakatifu pa patakatifu katika Hema Takatifu la kukutania Palikuwa ni mahali patakatifu sana ambapo hawakuweza kuingia mpaka awe na damu ya mwanasadaka, ambaye kwa huyo mikono iliwekwa juu ya kichwa chake ili kuyatowesha mbali maovu ya wenye dhambi. Kwa msemo tofauti, hata kuhani mkuu hakuweza kuikwepa adhabu ya Mungu hadi baada ya kuwa amepokea ondoleo la dhambi zake kwa kutoa sadaka ya kuteketezwa kabla ya kuingia katika uwepo wa Mungu.
Je, ni lini pazia la Hekalu lilipasuka? Lilipasuka wakatiYesu alipoimwaga damu yake na kufa Msalabani. Kwa nini ilimpasa Yesu kumwaga damu yake Msalabani na kisha kufa? Kwa sababu Yesu mwana wa Mungu kwa kuja kwake hapa duniani katika mwili wa mwanadamu alikuwa ameyachukuwa katika mwili wake maovu yote ya wenye dhambi kwa kubatizwa na Yohana katika mto Yordani. Kwa sababu Yesu alikuwa amezichukuwa katika mwili wake dhambi zote za ulimwengu kwa kupitia ubatizo wake, basi Yesu aliweza kuzimaliza adhabu zote za dhambi ikiwa tu angeliimwaga damu yake na kisha kufa msalabani. Hii ndiyo sababu lile pazia lililokuwa likitenganisha kati ya mahali  patakatifu na Patakatifu pa patakatifu lilipasuka toka juu mpaka chini. Hii inamaanisha kuwa ule ukuta wa dhambi ambao ulimtenganisha Mungu na mwanadamu ulikuwa umeanguka chini mara moja na daima.
Kwa maneno mengine, kupitia ubatizo ambao Yesu aliupokea  na damu yake aliyoimwaga Msalabani, Yesu amezifanya dhambi zote kutoweka. Kwa ubatizo na damu ya Yesu Kristo, Mungu baba amezitowesha mbali dhambi zetu zote mara moja na kwa wote na ameufungua mlango wa Mbinguni, ili kwamba mtu yeyote aweze kuingia Mbinguni kwa kuamini katika ubatizo huu na damu ya Yesu iliyomwaguka.
Wakati Yesu alipokuwa msalabani, giza lilifunika pale alipokuwepo kwa masaa matatu. Baada ya kuwa amezibeba dhambi zote za ulimwengu kwa kupitia ubatizo wake katika mto Yordani, Yesu alisulubiwa na karibu na kifo chake alilia, “Eloi, Eloi, lama sabaktani?” maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” (Mathayo 27:46). Kisha akisema neno lake la mwisho, “Imekwisha!” kisha akafa, na baada ya siku tatu akafufuka kena toka kwa wafu, akabeba ushuhuda kwa siku 40, na kisha akapaa Mbinguni mbele ya macho ya wanafunzi wake na wafuasi wake wengi.
Je, ni kweli kuwa Baba alikuwa amemwacha Yesu?
Kwa sababu Yesu alikuwa amezichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana, Yesu alikuwa ameachwa kwa muda na Baba pale alipokuwa amezibeba adhabu ya dhambi Msalabani. Mungu Baba alipaswa kumuadhibu mtu yeyote ambaye alikuwa na dhambi, na kwa sababu dhambi zote za ulimwengu zilikuwa zimepitishwa kwa Yesu, basi Yesu alipaswa kuraruliwa na kisha kuimwaga damu yake msalabani kama adhabu ya dhambi hizi.
Kwa sababu Yesu ni Mungu mwenyewe katika uwepo wake alikuwa amezichukuwa dhambi zote za wanadamu katika mwili wake kwa kubatizwa, basi dhambi za ulimwengu zilikuwa zimehamishwa katika mwili wake Mtakatifu. Kwa hiyo, alipaswa kuachwa na Mungu Baba kwa kitambo tu, kuteseka hadi kifo Msalabani ili kulipa mshahara wa dhambi zote.
Kama ambavyo unafahamu, baada ya kujengwa kwa Hekalu katika utawala wa mfalume Sulemani, basi nafasi ya Hema Takatifu la Kukutania ilichukuliwa na Hekalu. Lakini msingi wa utaratibu wa Hema Takatifu la kukutania iliendelea kutumika katika Hekalu kama ambavyo ilikuwa ikitumika katika Hema takatifu  la kukutania kabla Hekalu halijajengwa . kwa hiyo, kulikuwa na pazia ambalo lilitenganisha kati ya mahali patakatifu na Patakatifu pa patakatifu katika hekalu. Na wakati ule ule Bwana alipopiga kelele Msalabani, “Eloi, Eloi, Eloi, lama sabaktani?” pazia hili la Hekalu lilipasuka toka juu hadi chini. Ukweli unaozungumziwa na tukio hili ni kuwa kwa sababu Bwana amezioshelea mbali dhambi zetu kwa ubatizo ambao aliopokea na kwa damu ya thamani ambayo aliimwaga Msalabani, basi sasa lango la Mbinguni limefunguliwa ili kwamba wote wanaoamini waweze kuingia. Sasa kwa kuamini katika Injili ya maji na Roho, sisi sote tunaweza kuingia Mbinguni kwa imani.
Ule ukweli kuwa pazia la Hekalu lilipasuka toka juu hadi chini wakati Yesu alipokufa Msalabani unatufundisha sisi ukweli kwamba katika kipindi hiki, wale wote ambao wamesafishwa toka katika dhambi kwa kuamini injili ya maji na Roho na damu wanaweza kuingia Mbinguni. Kulikuwa na ukuta wa dhambi ambao ulikuwa umetutenganisha uliokuwa ukituzuia sisi kuja mbele za Mungu, lakini kwa ubatizo na damu yake, Yesu ameufanya huu ukuta wa dhambi kupotea mara moja na kwa wote. Kule kusema kuwa Muungu alilipasua pazia la Hekalu toka juu hadi chini kunamaanisha kuwa yeyote anayeamini katika ubatizo ambao kwa huo mwana wa Mungu aliyachukuwa katika mwili wake maovu yote ya wenye dhambi na katika damu ya msalaba anaweza kusafishwa dhambi zake kikamilifu na kisha kuingia Mbinguni. Mungu ametuokoa sisi toka katika dhambi kwa namna hii.
Yesu alilipasua pazia la Hekalu toka juu hadi chini kuwa ushuhuda wa kazi hizi za wokovu ambazo alizitimiza. Kwa hiyo (Waebrania 10:19-22) inasema “Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani mwili wake; na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu: na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamira mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi.”
Wakati Yesu alipokufa msalabani, mlango wa kuingilia Patakatifu pa patakatifu ulifunguliwa kwa kuwa pazia lake lilipasuliwa, na huu mlango ulifunguliwa wa Patakatifu pa patakatifu ni neno la Mungu la Injili ambalo limefungua njia mpya na iliyo hai ya kwenda Mbinguni. Hapa, Biblia inatueleza sisi kuwa dhambi zote za mioyo yetu na miili yetu zilitoweshwa mbali kwa kupitia ubatizo wake (maji safi) na damu yake, na kwa hiyo tunaweza kusafishwa kwa uhakika wa imani katika wokovu wake mkamilifu.

Ni lazima kuwepo na “utimilifu wa imani” kama ilivyo andika hapo juu, imani yoyote ambayo inaamini katika mambo mawili tu, kwa mfano damu na Roho Mtakatifu haijakamilika. Kujua kanini nasema hivi soma “Injili ya maji na roho” katika blog hii. 

Jumatatu, 10 Machi 2014

JENGA MADHABAHU KATIKA MOYO WAKO


Tunaweza kuona katika (kutoka 25:8-9) Nao wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao. Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mtakavyo vifanya.” (waebrania 3:6) “bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba ya Mungu; ambaye nyumba yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na fahari ya taraja letu mpaka mwisho.”  kwamba Mungu alimwita Musa na akammwambia kupajenga mahali pa kuabudia ambapo Mungu ataishi. Mahali ambapo Mungu anaishi au kushinda hapo panaitwa madhabahu. Katika malango na katika mapaa ya madhabahu hii kulikuwa na fumbo lililokuwa limefichika, yaani fumbo la Yesu Kristo. Katika kifungu hiki ambacho Mungu aliwaamuru watu wa Israeli kuijenga madhabahu hii, basi ninaamini kuwa Mungu anatueleza sisi kuijenga madhabahu hii katika mioyo yetu ili kwamba aweze kuishi ndani yetu.
Nini ambacho tunapaswa kukifanya ikiwa tunahitaji Mungu akae ndani yetu? Kwanza kabisa, kwa kweli ni lazima tufahamu jinsi ambavyo Mungu alivyozisafisha dhambi zetu zote kwa kupitia Neno la Injili ya maji na Roho. Na ni lazima tuamini katika ukweli huo. Ili kufanya hivyo, kwanza ni lazima tuziangalie nafsi zetu kimsingi. Tangu kuzaliwa kwetu hatukuwa na chaguo jingine lolote bali kuzaliwa kama wenye dhambi. Inawezekanaje basi kwa Roho wa Mungu mtakatifu kukaa katika mioyo ya watu kama sisi? Ili Roho wa Mungu aweze kukaa katika mioyo ya wenye dhambi ni lazima  basi hawa wenye dhambi wawe na imani inayoamini katika Injili ya kweli. Kwa maneno mengine, Roho mtakatifu anakaa ndani yetu pale tu tunapokuwa tumezioshelea mbali dhambi zetu kwa kufahamu na kuamini katika Injili ya maji na Roho. Kule kusema kuwa Roho mtakatifu anaweza kukaa katika mioyo kumwezesha kwa kuamini katika ukweli wa milele wa maji na Roho.
Madhabahu ambapo Mungu anapenda kukaa
Hata hivyo, watu wengi ambao bado hawajapokea ondoleo la dhambi hawafahamu ukweli huu.  Unafikiri ni kwa nini Mungu alimwamuru Musa kulijenga Hema takatifu la kukutania? Alimwamuru Musa kwa sababu alitaka kukaa katika mioyo yetu. Tatizo ni kuwa watu wengi kutokana na kutojua kwao juu ya ukweli huu (Injili ya maji na Roho), wanatuimia kiasi kikubwa cha fedha kujenga majengo ya makanisa makubwa na ya kushangaza na wanadanganyika kuamini kuwa haya ndiyo mahekalu ambapo Mungu anaishi.
Watu wa jinsi hiyo wapo tayari kutoa fedha yote walioweza kuipata katika kipindi chote cha maisha yao kwa Mungu, kwa sababu wanafikiria kimakosa kuwa makanisa yao yanaweza kufanyika  ni mahekalu ya Mungu mtakatifu ikiwa kama watayajenga majengo ya kifahari na makubwa. Lakini je, ni kweli kuwa Mungu atapendezwa ikiwa tutajenga makanisa makubwa ya kupendeza na kisha tukampatia Mungu?. Je, ni kweli kuwa Mungu atakubaliki ikiwa utafanya jambo kama hili?  Je, kanisa hili litafanyika kuwa madhabahu ambayo inakaliwa na Mungu? Hivyo si kweli kabisa. Haya ni matokeo ya imani isiyofahamu ukweli wa Injili ya maji na Roho na walioangukia katika uongo mkuu.
Madhabahu ambayo Mungu anataka kuishi si jengo kubwa la kanisa bali ni moyo wako ambao umeoshwa dhambi zako. Mungu anapenda kukaa ndani ya mioyo ya wenye haki ambao wamepokea ondoleo la dhambi na waliofanyika watakatifu. Ili kulifanya hili liwezekane tunatakiwa kutoa sala zetu za toba ili tuweze kutakaswa? Hapana, kwa kweli siyo hivyo. Hata hivyo, kuna watu wengi wakristo wa siku hizi wanafikiri na kuamini namna hii.
Ili kulijenga Hema takatifu la kukutania kwa kupitia Musa, Mungu aliwaamuru wana wa Israeli kumtolea sadaka. Kama ilivyoandikwa katika (kutoka 25:3-7). Baada ya kuzipokea sadaka hizi kupitia Musa alijenga madhabahu ya Mungu kwa vifaa hivi kwa kupitia wafanyakazi ambao waliipokea hekima toka kwa Mungu. Kama ambavyo Mungu alimwamuru Musa kulijenga Hema takatifu la kukutania katika Agano la kale, basi katika Agano jipya, Mungu anatutaka sisi pia kujenga madhabahu katika mioyo yetu ili aweze kuishi ndani yetu. Vifaa vya imani ambavyo kwa hivyo tunaweza kuvitumia katika kuijenga madhabahu hii ni Neno la Injili ya maji na Roho. Kwa vifaa vya Injili hii ya maji na Roho ni lazima tuzioshelee mbali dhambi zetu zote na kusafishwa. Kwa kutueleza sisi kujenga madhabahu yake Mungu anatueleza sisi kuweka wazi moyo wako na kisha kuamini katika Injili ya maji na Roho.
Jambo hili sasa linazusha swali jingine juu ya aina ya imani ambayo tunapaswa kuwa nayo ili Mungu aweze kuishi katika mioyo ya wenye dhambi. Jibu ni rahisi na la wazi. Kwa kuwa Mungu mtakatifu aweze kuishi katika mioyo ya wenye dhambi, ni lazima kwanza wenye dhambi hawa wafahamu kile ambacho Injili ya maji na roho inawaeleza, na kisha ni lazima waamini katika ukweli huo. Ndipo mioyo yao inapoweza kusafishwa na kupokea ondoleo la dhambi, na ndipo hapo tu Mungu Mtakatifu anapoweza hatimaye kuishi katika mioyo ya watu wa jinsi hiyo ambao wamepokea ondoleo la dhambi wanapokuwa wameuachilia mbali ugumu wao na wakamini katika  Injili ya maji na roho, ambayo ni majaliwa ya Mungu, basi Mungu anaweza kuja na kukaa katika mioyo yao.
Hii ndiyo sababu 1wakorintho 3: 16-17 inasema, “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.” Mungu ni mtakatifu na asiye na dhmbi. Kwa hiyo, anaeza tu kuja katika mioyo yetu wakati inapokuwa imesafishwa vizuri kwa Neno la Injili ya maji na Roho. Biblia inasema kwa wazi kuwa ni wale tu waliopokea ondoleo la dhambi ndiyo wanaweza kupokea karama ya Roho Mtakatifu (Matendo ya mitume 2:38)
"Injili ya maji na Roho" inapatikana katika blog hii



Jumapili, 9 Machi 2014

BIRIKA LA KUNAWIA


(Kutoka 30:17-21) “BWANA akanena na Musa, na kumwambia, Fanya na birika la shaba, na kitako chake cha shaba, ili kuogea; nawe utaliweka kati ya Hema takatifu la kukutania na madhabahu, nawe utalitia maji. Na Haruni na wanawe wataosha mikono yao na miguu yao humo; hapo waingipo ndani ya hema takatifu la kukutania; watajiosha majini, ili wasife; au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike, kumtengenezea BWANA sadaka ya moto; basi wataosha mikono yao na miguu yao ili kwamba wasife; na neno hili litakuwa amri kwao milele, kwake yeye na kwa wazao wake katika vizazi vyao vyote.”
Birika la kunawia katika Ua wa Hema takatifu la kukutania
Vifaa: ilitengenezwa kwa shaba, ilikuwa imejazwa na maji wakati wote.
Maana ya kiroho: Shaba ina maanisha hukumu ya dhambi zote za mwanadamu, Yesu alizichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana. Kwa hiyo, maana ya birika la kunawia ni kwamba tunaweza kuoshwa dhambi zetu zote kwa kuamini kwamba dhambi hizi zote zilpitishwa kwa Yesu kwa kupitia ubatizo wake.
Makuhani waliohudumu katika Hema takatifu la kukutania pia waliosha mikono yao na miguu yao katika birika la kunawia kabla ya kuingia katika Hema Takatifu la kukutania na kwa hiyo walikiepuka kifo chao. Shaba inamaanisha hukumu ya dhambi, na maji ya kwenye birika la kunawia yanamaanisha ubatizo ambao Yesu aliopokea toka kwa Yohana na ambao kwa huo alizichuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake. Kwa maneno mengine, birika la kunawia linatueleza kuwa Yesu alizipokea dhambi zetu zote zilizopitishwa kwake na akabeba adhabu ya dhambi hizi. Maji katika birika la kunawia yanamaanisha, katika Agano la kale, nyuzi za bluu za hemataktifu la kukutania, na katika Agano jipya, ubatizo ambao Yesu aliopokea toka kwa Yohana (Mathayo 3:15, 1petro 3:21).
Kwa hiyo, birika la kunawia linamaanisha ubatizo wa Yesu, na ni mahali ambapo tunathibitisha imani yetu katika ukweli kuwa Yesu alibeba dhambi zetu zote, zikiwemo dhambi zetu halisi, na akazioshelea mbali zote mara moja kwa kupitia ubatizo alioupokea toka kwa Yohana Mbatizaji.
Watakatifu ambao wameokolewa toka katika dhambi zao kwa imani wamevishwa neema ya Mungu  kwa kuyaamini maji ya kwenye birika la kunawia (ubatizo wa Yesu), Shaba (hukumu ya Mungu kwa dhambi zote), na kwamba Yesu amewakomboa toka katika dhambi zao. Ingawa tuna wingi wa udhaifu na mapungufu kiasi kwamba hatuwezi kujitambua sisi wenyewe kuwa ni wenye haki, kwa hakika tunaweza kudhibitisha kwamba sisi ni wenye haki wakamilifu kwa kuiweka tena na tena imani yetu katika ubatizo wa Yesu (kuzibeba dhambi, maji) na damu yake iliyomwagwa msalabani (adhabu ya dhambi, shaba). Kwa sababu tunaliamini Neno la Mungu ambalo limekwisha kutuokoa sisi sote toka katika dhambi zetu na adhabu ya dhambi hizi, basi tunaweza kufanyika wenye haki wasio na dhambi.
Neno la Mungu tunaloliamini linatueleza sisi kuwa Yesu alizichukuwa dhambi zetu katika mwili wake kwa kupitia ubatizo wake alioupokea toka kwa Yohana, akamwaga damu yake msalabani ili kuibeba adhabu yote ya dhambi badala yetu, na kwa hiyo ametuokoa sisi kikamilifu toka katika dhambi zetu. Mungu aliliweka birika la kunawia katika ua wa Hema Takatifu la kukutania ili kwamba tuweze kudhibitisha kwa imani yetu kuwa sisi ndiyo tuliookolewa kikamilifu toka katika dhambi zetu zote bila kujali hali inavyoweza kuwa.
Matumizi ya birika la kunawia
Birika la kunawia lilitumika katika kuosha uchafu wote wa makuhani walipofanya kazi katika Hema Takatifu la kukutania wakitoa sadaka kwa Mungu. Ilihitajika kuyaosha madoa ambayo makuhani waliyapata katika kuua mwanasadaka wa kuteketezwa, katika kuikinga damu yake, na katika kuikata vipande ili kumtolea Mungu sadaka ambayo itawapatanisha watu wa Israeli na Mungu toka katika dhambi zao. Wakati makuhani walipochafuliwa walipokuwa wakitoa sadaka, iliwapasa kuoshwa kwa maji, na birika la kunawia lilikuwa ni mahali ambapo uchafu huu wote ulisafishwa.
Tunapofanya dhambi, kiroho au kimwili, na kila inapotokea kuwa tumechafuliwa kwa kuzivunja amri za Mungu, ni lazima tuoshelee mbali uchafu wetu wote katika birika hili la kunawia. Ilipotokea kuwa miili ya makuhani imegusa kitu chochote kichafu, walipaswa kwa lazima kuosha sehemu zilizochafuka katika miili yao kwa maji.
Vivyo hivyo, inapotokea kuwa wale wanaoamini katika Mungu wamegusana na kitu chochote kisicho safi na kichafu, maji ya birika la kunawia yanatumika kuoshelea mbali huo uchafu wote. Kwa kifupi, maji ya birika la kunawia yalitolewa ili yatumike katika kuuosha uchafu wa waliozaliwa upya. Kwa hiyo, birika la kunawia lina rehema za Mungu. Maana ya birika la kunawia si kitu cha kuchagua ambacho tunaweza kuchagua kuamini au kutoamini, bali ni kitu cha muhimu na lazima kwa wale wanaomwamini Yesu.
Mungu alitoa vipimo kwa vifaa vingine vyote katika Hema Takatifu la kukutania, akatoa vipimo maluumu jinsi ambavyo vitakuwa na dhiraa kadhaa kwa kimo, urefu, na upana. Lakini hakutoa kipimo cha birika la kunawia. Hii ni tabia ambayo inaapatikana tu katika birika la kunawia. Hii inadhihirisha upendo usiokoma ambao masihi ametupatia sisi, ambao tunatenda dhambi halisi kila siku. Katika upendo huu wa masihi  kunapatikana ubatizo wake, aina ya kuwekewa mikono ambayo inaziosha dhambi zetu zote. Kama ambavyo maji mengi yalitumika wakati makuhani walipokuwa wamechafuka wakati wakitekeleza majukumu yao, ilikuwa ni lazima birika la kunawia lijazwe maji wakati wote. Kwa hiyo, kipimo cha birika la kunawia kilitegemeana na hitaji hili. Kwa sababu birika la kunawia lilitengenezwa kwa shaba, basi kila ilipotokea makuhani wakinawa, walikuwa wanafikiria juu ya hukumu ya dhambi.
(Waebrania 10:22) inasema “tumeoshwa miili kwa maji safi”,  na (tito3:5) “ kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho mtakatifu.” Kama Vifungu hivi vinavyoonyesha, Neno la Agano Jipya pia linatueleza sisi kuhusu kuuosha uchafu kwa maji ya ubatizo.

Ikiwa makuhani waliosha uchafu wao walioupata katika maisha yao kwa maji ya birika la kunawia, sisi wakristo wa leo tuliozaliwa upya, tunaweza kuzioshelea mbali dhambi zetu Halisi zote zilizofanywa katika maisha yetu kwa kuamini ubatizo wa Yesu. Maji ya birika la kunawia la Agano la kale yanatuonyesha sisi kuwa Masihi alikuja hapa duniani na amezisafishaia mbali dhambi zote za ulimwengu kwa ubatizo aliopokea toka kwa Yohana.