Jumatano, 26 Februari 2014

MAJI, DAMU NA ROHO


(1Yohana 5:4-7) Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko  kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni mwana wa Mungu. Huyu ndiye aliye kuja kwa maji na damu, Yesu Kristo: si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
Yatupasa kuamini kwamba Yesu alichukua dhambi zetu zote kwa ubatizo wake, alihukumiwa na kufa msalabani kwa ajili yetu, na akafufuka siku ya tatu, baada ya kifo chake.
Bila imani hii, ukombozi usingewezekana. Yesu Kristo alikuja kwetu kwa ubatizo, damu na Roho. Alichukuwa dhambi zote za ulimwengu.
Yapo mambo muhimu matatu yenye kushuhudia juu ya wokovu wake hapa duniani, Roho, maji na damu.
Kwanza; ‘Roho mtakatifu’ hushuhudia Yesu ni Mungu na alikuja katika mwili.
Pili ; ‘Maji’ hushuhudia ubatizo wa Yesu katika mto Yordani kwa Yohana Mbatizaji ambaye kupitia kwake dhambi zetu zote alimtwika Yesu. Dhambi zetu alizibeba Yesu alipobatizwa (Mathayo 3:15).
Tatu; ‘Damu’ inasimama kama Yesu kukubali kujitoa kwa hukumu ya dhambi zetu. Alikufa kwa hukumu ya Mungu Baba na alifufuliwa siku ya tatu ili kutupa uhai mpya.
Mungu Baba alimtuma Roho ndani ya mioyo ya wale wote wenye kuamini ubatizo na damu ya mwana wake ili aweze kushuhudia ndani, juu ya ukombozi.
Wale wote waliozaliwa upya wana neno ndani yao lenye kuushinda ulimwengu. Waliokombolewa watamshinda shetani, uongo wa manabii, walaghai, vikwazo au misukosuko ya ulimwengu ambayo haiachi kushambulia. Sababu ya kuwa na nguvu hii ni kwamba, tuna ushuhuda wa yale mambo matatu ndani ya mioyo yetu; maji ya Yesu, Damu yake na Roho.
Haiwezekani kuzaliwa upya au kuushinda ulimwengu ikiwa huna imani katika ukombozi utokanao na ubatizo wa Yesu, damu yake na kuamini Yesu ni Mwana wa mungu na mwokozi. Katika (1Yohana 5:8) inasema “kisha wako watatu washuhudiao duniani, Roho na Maji na Damu na watatu hawa hupatana kwa habari moja.” Wengi bado huzungumzia juu ya damu na Roho tu wakiacha maji ya ubatizo wa Yesu. Ikiwa wataacha habari ya maji, bado wataendelea kudanganywa na shetani. Wanapaswa kuacha upotovu wao na kutubu na kuamini maji ya ubatizo wa Yesu katika kuzaliwa upya.
Hakuna yeyote mwenye kuushinda ulimwengu bila kuamini maji na damu ya Yesu. Nasema tena, hakuna! Yatupasa kupigana kwa kutumia maji na damu ya Yesu kama silaha nzito na kali za kiroho. Neno lake ni upanga wa Roho, Nuru.
Wapo wengi wasioamini ubatizo wa Yesu ulichukua dhambi zetu zote. Wapo wengi wenye kuamini mambo mawili tu. Hivyo, Yesu anapowaeleza “amka na uangaze”, hawawezi kuangaza kwa vyovyote vile. Bado wanazo dhambi mioyoni mwao. Ingawa wanamwamini Yesu, lakini bado watakwenda motoni.
“mfano wa mambo hayo ni ubatizo unaowaokoa ninyi pia siku hizi” (1Petro 3:21). “watu wanane wliokoka kwa maji” (1Petro 3:20).

Ni watu wachache ndiyo waliokoka enzi za Nuhu. Je, walikuwa ni wenye thamani zaidi ya wengine? Hata kidogo! Sisi sote si wenye thamani, bali tumeokolewa kwa njia nyingine kupitia imani katika maji, damu na Roho.

Jumanne, 25 Februari 2014

KANUNI ZA MTU NI DHAMBI MBELE ZA MUNGU.

sheri sehemu ya pili

Kushindwa kuishi katika mapenzi ya Mungu ni dhambi. Ni sawa na kutoamini neno lake. Mungu alisema, ni dhambi kuishi kama Wafarisayo ambao walikataa sheria ya Mungu kwa kukazia zaidi msisitizo wa mafundisho ya desturi zao. Yesu aliwachukulia kuwa ni wanafiki.
“Ni Mungu yupi unayemwamini? Je, unaniheshimu na kunitukuza? Unajivunia juu yangu, lakini je unaniheshimu? Mara nyingi watu huangalia umbo la nje na kupuuzia neno la Mungu ndani ya nafsi zao. Je wajua hilo? Matendo ya kuvunja sheria chanzo chake yametokana na udhaifu ambao ni maovu. Makosa tuyafanyayo na upotovu tuutendao kutokana na kutokuwa wakamilifu siyo dhambi kuu ndani yetu bali ni kuanguka katika usahihi. Mungu ametofautisha kati ya dhambi na uovu. Wale wote wenye kulidharau neno lake ni wenye dhambi, hata ikiwa hawana makosa. Ni wenye dhambi zaidi mbele ya Mungu. Na hii ndiyo maana Yesu aliwakemea Mafarisayo.
Katika nyakati za Agano la Kale, kitabu cha mwanzo hadi kumbukumbu la Torati ziliwekwa sheria zilizotaja nini cha kutenda na nini cha kutotenda. Ni maneno ya Mungu Sheria yake. Haitowezekana kwetu kuzitekeleza katika asilimia mia moja, lakini yatubidi kuzikubali kama ni sheria za Mungu. Alitupatia hapo mwanzo na yatupasa kuzikubali kuwa ni Maneno ya Mungu.
“Hapo mwanzo palikuwepo na Neno, naye Neno alikuwepo kwa Mungu, naye Neno alikuwa ni Mungu” Naye alisema “Na uwepo mwanga na ukawepo” Aliumba vyote. Na baadaye, akaiweka Sheria.
“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu;” (Yohana 1:14). Ni kwa namna gani basi Mungu alijidhihirisha kwetu? Alijidhihirisha kwetu kupitia sheria kwa maana Mungu ni Neno na Roho. Sasa je, Biblia inaitwa nini? Tunaita Neno la Mungu. Imesemwa hapa “Ninyi mwaiacha amri ya Mungu na kuyashika mapokeo ya wanadamu” vipo vipengele 613 katika sheria ya Mungu. Fanya hivi na usifanye vile waheshimu wazazi wako………… nakadhalika. Katika kitabu cha Mambo ya Walawi imetajwa ni kwa namna gani mwanamume na mwanamke wanapaswa kuenenda na nini kifanyike endapo mifugo ikitumbukia shimoni………. Hivi ni baadhi ya vipengele 613 katika sheria.
Kwa kuwa haya si maneno ya mwanadamu, tunapaswa kuyatafakari nyakati zote. Ingawa tutashindwa kutekeleza sheria yote, tunapaswa kwa kiasi Fulani kuzitambua na kumtii Mungu.
Je, kuna kifungu hata kimoja cha maneno ya Mungu yasiyo sahihi? Mafarisayo waliziacha sheria za Mungu na kuzifuata taratibu za mafundisho ya wanadamu dhidi ya sheria ya Mungu. Maneno ya wakuu wao yalichukua nafasi ya uzito wa juu dhidi ya yale ya Mungu.
Yesu alipokuwa duniani, haya ndiyo aliyoshuhudia, na ndicho kilicho umiza moyo wake zaidi kwa kuona Neno la Mungu likipuuziwa na wanadamu. Mungu ametupa vipengele 613 vya sheria ili tuweze kuzitambua dhambi zetu na kutuonyesha kuwa yeye ni mkweli na mtakatifu kwetu. Kwa kuwa sisi sote ni wenye dhambi mbele yake, tunapaswa basi kuenenda kwa imani na kumwamini Yesu kuwa ndiye aliyeletwa na Mungu kwa upendo kwetu. Wenye kuweka neno lake kando na kutoamini watakuwa ni wadhambi. Wenye kushindwa kuenenda katika neno lake pia ni wadhambi, ingawa kuweka kando neno lake ni hatari zaidi. Wenye kutenda dhambi hii wataishia motoni. Kutoamini Neno lake ni dhambi iliyo hatari zaidi mbele za Mungu.
 soma sehemu ya tatu"SABABU YA MUNGU KUTUPATIA SHERIA".

SABABU YA MUNGU KUTUPATIA SHERIA.

sheria sehemu ya tatu
Sababu ipi Mungu alitupatia Sheria? Ilikuwa ni kutufanya kuzitambua dhambi zetu na kumrudia kwake kwa toba. Alitupatia vipengele 613 vya sheria ili tuweze kuzitambua dhambi zetu na kuweza kukombolewa kupitia Yesu Kristo. Na hii ndiyo maana ya Mungu kutupatia sheria.
Warumi 3:20  inasema  “….. kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya Sheria”.  Hivyo twajua kwamba sababu ya Mungu kutupatia sheria ilikuwa si kutulazimisha kuenenda nayo.
Kwa namna hii sasa, tunapata kujua nini juu ya Sheria? Ni hivi, sisi tu wadhaifu kwa kuitimiza sheria yote na ni wenye dhambi sana. Tunatambua nini juu ya vipengele hivyo 613 vya Sheria? Tunang’amua mapungufu yetu na kushindwa kwetu kuifuata Sheria yake.
Tunatambua yakwamba sisi ni viumbe wa Mungu, tulio dhaifu, na wenye dhambi mbele zake. Ilitupasa sisi sote kutupwa motoni kwa mujibu wa Sheria ya Mungu. Tunapo tambua dhambi zetu na kushindwa kwetu kuishi kwa kuzifuata sheria, sasa, na tufanye nini? Je tunajaribu kuishi kwa ukamilifu wenyewe? Hasha! Yatulazimu kukubali kuwa sisi ni wadhambi, tumwamini Yesu ili tukombolewe kupitia wokovu wake katika Maji na Roho na kumshukuru yeye.
Sababu ya Mungu kutupa sheria ilikuwa ni kutufanya tuzitambue dhambi zetu na kujua adhabu yake juu ya dhambi hizo. Hivyo, itatufanya kuelewa kuwa hakuna njia ya kuokolewa toka motoni pasipo Yesu ikiwa tutamwamini Yesu kuwa ni Mwokozi, tutakombolewa. Mungu alitupa sheria ili ituongoze kuelekea kwa Mwokozi Yesu.
Mungu alizifanya sheria ili kutufanya tuweze kutambua ni kwa namna gani tulivyo wenye dhambi na kuhitaji wokovu wa roho zetu kutoka kwenye dhambi hizo. Alitupa sheria na kumtuma mwana wake wa pekee, Yesu, kutuokoa kwa kuzibeba katika ubatizo wake. Kumwamini Yeye kutatufanya tuokolewe.

Sisi ni wadhambi tusio na tumaini lolote, yatulazimu kumwamini Yesu ili kuwa huru kutoka dhambini, kuwa watoto wa Mungu na kuurudisha utukufu wake. Yatupasa tuelewe, kufikiri na kuamua kupitia neno lake kwa kuwa yeye ni asili ya yote. Yatupasa tuikubali kweli ya wokovu kupitia Neno lake. Hii ni Imani ya Haki na kweli.

soma sehemu ya nne "WENYE KUJARIBU KUKOMBOLEWA KWA KUPITIA MATENDO YAO BADO NI WENYE DHAMBI"

KUPOKEA ROHO MTAKATIFU

Ndugu ninakusihi sana, katika blog hii anza na mafundisho ya awali kama ‘injili ya maji na roho’ ili uweze kumpokea Roho Mtakatifu. Maana bila kumpokea Roho wa Mungu hautoweza kufahamu mafundisho ya ukweli na uwongo. Soma kifungu hichi,  (1wakorintho 2:10-15) lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukupokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”
Roho wa Mungu pekee ndiye atakaye kufundisha neno la Mungu kwa usahihi, njia pekee ya kukuwezesha kupokea Roho mtakatifu ni kuwa na imani sahihi katika ubatizo na damu ya Yesu. Tahadhari, usifikiri ubatizo ninaosema ni ule wa maji mengi, hapana. Maji ni ishara ya nje tu ya kile ulicho amini ndani yako, jiulize, kwanini Yesu alibatizwa na Yohana Mbatizaji?.  (majibu yanapatikana katika masomo yaliyopita).
Wako watu wengi ambao wanajaribu kumpokea Roho mtakatifu kwa kufunga kwa muda mrefu, kujitolea makanisani na mengine mengi, na wengine wakidhani kuwa kila atakaye mwamini Yesu kuwa mwokozi wake basi ataokolewa, lakini ukisoma masomo ya ubatizo utaona kuwa sio sahihi, mfano alikuwapo mtu mmoja aliyeitwa Apolo ambaye Alipoanza kufundisha Efeso kuna mambo hakuyajua kwa usahihi, kama ubatizo wa Yesu, alijua ubatizo wa Yohana tu. Hivyo ilisababisha wale wanafunzi aliowafundisha hawakuweza kumpokea Roho mtakatifu, mpaka pale Paulo alipokuja kuwafundisha kwa usahihi zaidi ndipo wakapokea Roho mtakatifu. (Matendo 19: 24-26) na (Matendo 19:1-6), pia ukisoma habari ya Kornelio (Matendo 10), utaona kuwa Kornelio alikuwa ni mtu wa kujitolea sana, laikini hakuwa na Roho mtakatifu, akapewa maelekezo ya kumwita simioni ili amweleze yampasayo kuyatenda. Ukifika mwisho wa sura hiyo utaona Kornelio kapokea roho mtakatifu kwa sababu ya imani sahihi.
Watu wengi wamekuwa wakidhani kunena kwa lugha, kuombea wagonjwa na kukemea mapepo watakuwa na Roho mtakatifu, lakini nataka nikuambie si kweli. Soma kifungu hiki  ( Luka 10: 20)“lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa Mbinguni."   Ishara hizi ni moja wapo ya mambo yanayoambatana na aliyeokoka, lakini hata mapepo yanaweza hayo yote. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwajina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitaawambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu nyinyi mtendao maovu. (Mathayo 7:22-23). Mfano katika Agano la kale (kutoka 7) unaweza kuona ni jinsi gani Farao alivyowaita wachawi iliwafanye miujiza na waliweza, japo miujiza yao ilikuwa na mipaka.
Watu wengi wanafanya juhudi za kibinadamu  katika kumpokea Roho mtakatifu, lakini hawaijui “haki ya Mungu” ukisoma masomo yaliyopita katika blog hii kuna somo linalo elezea “haki ya Mungu.”  Inabidi uwamini haki ya Mungu ipatikanayo katika ubatizo na damu ya Yesu ili uweze kumpokea Roho mtakatifu.  Pia soma masomo yaliyopita ujue isemwapo “imani bila matendo imekufa”  je ni matendo ya sheria au matendo ya imani? Pia utajua kwamba Mungu alitupatia sheria aina mbili sheria ya” roho wa uzima” na “sheria ya dhambi na mauti” (Warumi 8:1-4). Hivyo mwanadamu ataokolewa kwa sheria ya roho wa uzima na si kwa sheria ya dhambi na mauti. (Warumi 10:2-4) kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawajui haki ya Mungu, kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki.
Kuna wengine husoma na kudharau, lakini kumbuka bila Roho mtakatifu Biblia utaisoma kama kitabu cha hadithi na shetani atakufunga katika fikira zako. (2 Korintho 4:3-4) “lakini ikiwa Injili yetu imesitirka, imesitirika kwa hao wanaopotea, ambao ndani yao Mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao, isiwazukie nuru ya Injili ya utakatifu wake Kristo aliye sura yake Mungu”
(Warumi 8: 8-9) “wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu. Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili’ bali mwaifuata Roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.
Kumbuka mwenye haki hatendi dhambi kwa kukusudia kwa sababu mazingira katika ulimwengu wa Roho yamebadilika, kwamba anaongozwa na Roho wa Mungu, ambaye huingia ndani yake na matunda ya Roho (kama upendo, amani , uvumilivu n.k ).
Agano la kale ni kivuli cha agano jipya,  hivyo kila kitu kina mwenake katika agano jipa kwa agano la kale “tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake imekusanya” (Isaya 34:16)


Jumapili, 23 Februari 2014

SHERIA NI KWA AJILI YA KUZIFAHAMU DHAMBI

sheria sehemu ya sita
Katika Warumi 3:20 tunasoma “ Kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria”. Mwanzo kabisa nilichukulia kifungu hiki kuwa ujumbe binafsi kwa Mtume Paulo na kuamini maneno niliyopendelea. Lakini baada ya machozi yangu kukauka hakika sikuweza kuendelea na maisha yangu ya imani ya kidini. Hivyo niliendelea na dhambi na kufikia hatua ya kugundua nina dhambi ndani ya moyo wangu na kushindwa kuishi kwa sheria. Sikuweza kuvumilia ingawa sikuweza kuachana na sheria kwa kuwa niliamini ilikuwepo ili niweze kuitii. Hatima yake nikawa mwanasheria kama walionyeshwa katika maandiko hapo awali. Ikawa ni vigumu kwangu kuendelea na maisha ya imani.
Nilikua na dhambi nyingi hata kufikia kila ninapo soma sheria naanza kugundua dhambi hizo kila ninapozivunja amri 10 ndani ya moyo wangu. Ikumbukwe kuwa na dhambi moyoni ni sawa kutenda dhambi tu! Sikuweza kufahamu kwamba nilikuwa tayari muumini wa sheria.
Nilipofuata sheria nilifarijika. Lakini nilipoanguka nilikua mnyonge, mwenye hasira na huzuni. Na wakati huo nikawa mwenye kukosa matumini kwa yote. Ingeweza kuwa rahisi ikiwa hapo awali ningefundishwa ukweli juu ya sheria kama vile “Hapana, siyo hivi! Ipo maana nyingine ya sheria nayo ni kama taa kuonyesha dhambi zako kama vile wewe unapenda fedha, kupenda jinsia tofauti na vitu vizuri vya kuonekana.Una vitu unavyovipenda kuliko umpendavyo Mungu. Unapenda sana kufuata mambo ya dunia. Sheria iliwekwa kwako si uifuate bali uweze kugundua nafsi yako kama mwenye dhambi aliye na uovu moyoni”.
Ikiwa mtu yoyote angeweza kunifundisha hivi basi nisingeweza kuteseka kwa muda mrefu namna ile. Hivi ndivyo nilivyo weza kuishi kwa sheria kwa miaka mingi kabla ya kuja kugundua hili. Amri ya nne inasema “Ikumbuke siku ya Sabato na uitakase”. Hii ina maana kwamba tusifanye kazi siku ya jumamosi.Tunafundishwa tusifanye kazi, sio kutembea mwendo wa mbali katika safari kwa siku ya Jumamosi.Nilidhani ilikuwa ni sahihi na niheshima kutembea sehemu nilizo hitaji kuhubiri. Hata hivyo nilitaka kuhubiri sheria. Na nilihisi ilinipasa kutenda yale nihubiriyo. Ikawa ni vigumu na kushindwa. Kama ilivyo hapo mwanzo”wasoma je?” sikuelewa swali hili na kuteseka miaka mingi. mwanasheria hakuelewa vema hili.Alifikiri ya kwamba ikiwa ataheshimu sheria na kuishi kwa uangalifu mkubwa atakuwa amebarikiwa na Mungu.
Lakini Yesu alimwambia “wasomaje?”. Naye akajibu kwa imani itokanayo na sheria. Naye akamjibu “umejibu vema, unaichukua kama ilivyoandikwa. Jaribu kuifuata. Utaishi ikiwa utaweza na utakufa ukishindwa.Mshahara wa dhambi ni mauti.Hakika ukishindwa utakufa” ( kinyume cha kuishi ni kufa,sivyo?). lakini mwanasheria huyu hakugundua hili. Mwanasheria ni mfano wetu sisi leo, mimi na wewe. Nilijifunza theologia (elimu ya dini) kwa miaka mingi. Nilijaribu kila namna, kusoma kila kitu na kutenda kila jambo; kufunga kula, kuwa na maono, kunena kwa lugha……. Nilisoma Biblia kwa miaka mingi kwa kutegemea nitahitimisha jambo fulani mbeleni. Lakini kiroho nilikuwa bado kipofu!
Na ndiyo maana mwenye dhambi huitaji mtu fulani atakayefungua macho yake, na huyu ni Bwana wetu Yesu Kristo. Ndipo mtu hugundua “Ahaa! Hatuna uwezo wa kufuata sheria. Haijalishi ni kwa bidii gani tutaweza kujaribu kuifuata tutaishia kufa tukikosa matumaini. Lakini Yesu alikuja kutuokoa kwa maji na kwa Roho! Haleluya!” Kwa maji na kwa Roho tutaweza kukombolewa. Ni neema, zawadi ya Mungu. Na tumsifu Bwana. Nilikuwa mwenye bahati ya pekee kuhitimu toka kwenye njia ya kukosa matumaini katika sheria, naamini wengi huchukua muda mrefu zaidi katika maisha yao kusoma theologia katika njia panda na bila kugundua ukweli hadi umauti. Wengine huamini kwa mioyo mingi, kizazi hadi kizazi na hawazaliwi upya.
Tunahitimu kutokuwa wadhambi pale tu tunapogundua hatuna uwezo wa aina yeyote binafsi wa kufuata sheria na kusimama mbele ya Yesu kwa kukubali kuisikiliza Injili ya maji na Roho. Tunapokutana na Yesu tunahitimu kutoka kwenye hukumu na jehanamu. Sisi ni wenye wingi wa dhambi, lakini tunafanyizwa haki kwa sababu Yesu ametuokoa katika maji na damu yake. Yesu amesema hatuwezi kuishi katika mapenzi yake. Alimwambia mwanasheria, lakini hakuelewa hili. Hivyo alimpa mfano huu.
 “Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang`anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha wakaenda zao,wakamwacha karibu kufa(Luka 10:30) Yesu alimpa Mwanasheria mfano huu ili kuamsha dhamira yake kwakua huteseka kwa maisha yake yote kama jinsi Mtu yule aliyepigwa na wanyang`anyi karibu kufa.
Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko. Yeriko inawakilisha dunia hii ya sasa, hali Yerusalemu inawakilisha mji wa kidini, mji wa imani uliojawa na majigambo ya sheria. Mfano huu hutuelezea ikiwa tutamwani Kristo kwa njia ya udini tutaangamia.
“ Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko akangukia kati ya wanyang`anyi, wakamvua nguo wakamtia jeraha wakenda zao wakimwacha karibu kufa”. Yerusalemu ulikuwa ni mji mkubwa ukiwa na wakazi wengi. Kulikuwa na Kuhani Mkuu, Jeshi la Makuhani Walawi na wengi wa Wakuu mashuhuri wa dini. Palikuwepo na wengi wenye kuelewa sheria vema. Na walijaribu kuishi kwa sheria, lakini walishindwa na kukimbilia Yeriko wakangukia duniani ( Yeriko ) na kushindwa kuzuia kukutana na wanyang`anyi
Mtu huyu pia alikutana njiani na wanyang`anyi toka Yerusalemu kwenda Yeriko wakamvua nguo. “Kuvuliwa nguo” maana yake kupoteza haki. Ni vigumu kwetu kuishi kwa kufuata sheria, kuishi kwa sheria Mtume Paulo amesema katika Warumi 7:19-20 “Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi, bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilipendalo si mimi nafsi yangu nilitendalo, bali ni ile dhamiri ikaayo ndani yangu”.
Ningetamani kutenda mema na kuishi katika Neno lake Mungu. Lakini ndani ya moyo wa mwanadamu umefurika mawazo mabaya, uasherati,wivi, uuaji, unzizi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu ( Marko 7: 21-23 ).Kwa kuwa haya ndiyo yaliyomo ndani ya mioyo yetu, basi tunafanya yale tusiyopaswa na hatufanyi yale yatupasayo kufanya. Tunaendelea kurudia maovu haya ndani ya mioyo yetu. Hivyo shetani huitaji kukuhamasisha kwa kiasi kidogo tu ili uweze kutenda dhambi.
Alikutana na nani njiani alipokuwa akienda Yeriko? Alikutana na wanyang’anyi. Yeyote yule asiyetambua na kuishi kwa sheria, maisha yake yanafananishwa na mbwa aliyetelekezwa. Hula na kunywa na kwenda haja mahala popote. Mbwa wa aina hii huamka asubuhi nyingine na kwenda haja na kula tena. Huweza hata kula kinyesi chake.
Ndiyo maana mtu huyu hufananishwa na mbwa. Hula na kunywa na kwenda haja lakini huomba toba asubuhi inayofuata na kurudia yale yale kwa mara zote. Ni sawa na mtu aliyekutana na wanyang’anyi akienda Yeriko. Akaachwa akiwa amejeruhiwa karibu ya kifo. Ina maana kwamba kuna dhambi ndani ya moyo. Na hii ndivyo ilivyo kwa mwanadamu.
Watu humwamini Yesu na kujaribu kuishi kwa sheria katika Yerusalemu, jamii ya dini, lakini wanaachwa na dhambi ndani ya mioyo yao. Kile wanachoweza kuonyesha katika maisha yao ya udini ni majeraha ya dhambi. Wale wenye dhambi mioyoni mwao hakika siku za mwisho watakwenda motoni. Wanajua hili, lakini hawajui lakufanya. Je ni kweli hata wewe upo katika mji huo wa dini? Ndiyo. Hata sisi tulikuwepo.
Mwanasheria aliyeshindwa kuielewa sheria ya Mungu angehangaika maishani pote, lakini angeishia motoni kwa majeraha. Ni sisi kati yetu, mimi na wewe. Yesu pekee aokoa. Wapo watu wengi wenye uerevu kati yetu na kila mara kupayuka wanayoyajua. Wote hawa hujifanya kwa kuishi katika sheria ya Mungu na hawapo kweli nafsini mwao. Hawawezi kuita beleshi kuwa ni beleshi, mara zote huzificha nafsi zao kwa nje ili kuonekana waaminifu.
Kati yao ni wenye dhambi kuelekea Yeriko, wale waliopigwa na waovu na kuachwa karibu kufa. Tunapaswa kuelewa vile tusivyo imara, wepesi wa kuumizwa mbele za Mungu. Yatupasa tukiri mbele zake “Bwana, hakika nitaishia motoni ikiwa hutoniokoa. Naomba uniokoe. Nitakufuata popote, ikiwa ni penye kimbunga au dhoruba, ikiwa tu nitaweza kusikia Injili. Ukiniacha peke yangu, nitakwenda motoni. Nakusihi niokoe!”

Wale wenye kugundua kuwa wapo karibu na jehanamu na kujaribu kutenda matendo ya kujitafutia haki wakiwa wanaambatana na Bwana ndiyo pekee watakaookolewa. Hatuwezi kuokolewa kwa juhudi zetu binafsi. Yatupasa kuelewa kwamba, tutafananishwa na mtu yule aliye angukia katika mikono ya wanyang’anyi.
kumbuka
mwenye haki hatendi dhambi makusudi kwa sababu ana Roho wa mungu soma katika blog hii "injili ya maji na roho."

MUNGU AMETUPATIA HAKI KWA IMANI KATIKA SHERIA

sheria sehemu ya tano
Mtume Paulo alisema kwamba, Mungu ametupatia haki kwa imani toka mwanzo. Alimpatia Adamu na Hawa, Kaini na Abeli, Sethi na Enoki, Nuhu, Abrahamu, Isaka na mwisho Yakobo na watoto wake kumi na wawili. Hata pasipo sheria, walifanywa kuwa wenye haki mbele za Mungu kupitia haki itokanayo na Imani ya Neno lake; Walibarikiwa na walipata pumziko kupitia imani ya Neno lake.
Muda uliopita wakati uzao wa Yakobo uliishi Misri kama watumwa kwa miaka 400 kwa sababu ya Yusufu. Ndipo Mungu alipowaongoza kutoka kupitia Musa kuelekea Kanaani, pamoja na kuwa watumwa kwa miaka 400, walisahau haki katika Imani.
Ndipo Mungu alipowaongoza kupita kati ya Bahari ya Shamu kwa muujiza na kuwaongoza jangwani walipofika jangwa la dhambi, akawapa sheria katika Mlima Sinai. Aliwapa sheria ambazo zilikuwamo Amri kumi na vipengele 613. Mungu aliahidi “Ndimi Bwana Mungu wako, Mungu wa Abraham, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Musa apande na kuja katika mlima Sinai na nitawapa sheria” Ndipo alipowapa Waisraeli Sheria.
Aliwapa Sheria ili waweze “kutambua dhambi” (Warumi 3:20) Ilikuwa ni kuwafahamisha juu ya anachotaka na asichotaka na kuweka wazi haki yake na utakatifu.Walipokuwa wakiishi kama watumwa kwa kipindi hicho cha miaka 400, walisahau haki ya Mungu katika muda huo hawakuweza kuwa na kiongozi. Yakobo na Yusufu walikuwa viongozi hapo awali. Inaonekana Yusufu alishindwa kuirithisha Imani hiyo kwa watoto wake wa kiume, Manase na Efraimu.
Hivyo, walihitaji kumtafuta Mungu tena na kukutana naye kwa kuwa waliisahau haki yake. Tunapaswa kuweka akilini kwamba Mungu aliwapa haki kwa imani mwanzo na kuwapa sheria baada ya kuisahau Imani. Aliwapa Sheria ili waweze kumrudia.
Kuiokoa Israeli na kuwafanya kuwa wana wake, aliwaambia kwamba iliwalazimu kutahiriwa. Nia ya kuwaita ilikuwa ni kuwafanya watambue kwamba alikuwa kati yao ili kuanzisha Sheria na pili, kufanya watambue walikuwa ni wenye dhambi mbele zake. Mungu alitaka waje mbele zake na kuwa watu wake kwa kukombolewa kwa mfumo wa sadaka ambayo aliyokuwa amewapa. Na aliwafanya kuwa watu wake.
Wana wa Israeli walikombolewa kupitia mfumo wa sadaka wa Sheria kwa kumwamini Masiya ajaye. Lakini mfumo huu ulipitwa na wakati. Na tuangalie hii, ilikuwa ni lini. Katika Luka 10:25 mwanasheria mmoja alitajwa kumjaribu Yesu. Alikuwa ni Mfarisayo. Mafarisayo walikuwa ni wenye kuyashika mafundisho bila kukubali kubadilika kwa kufanya jitihada zao binafsi kuishi kwa kufuata neno la Mungu; Walijaribu kuzilinda sheria za nchi kwanza kwa kuishi kadiri ya maandiko ya sheria. Walikuwa ni “wakereketwa” (kwa lugha ya kisasa) ambao walihamasisha na kufanya ghasia za kuvunja sheria ili kufanikisha malengo ya maono yao juu ya uhuru wa Waisraeli toka kwa Warumi.
Kuna baadhi yao hata nyakati hizi wamo kwenye dini tuzionazo. Huongoza harakati za kijamii kwa usemi kama vile “Okoa wanaogandamizwa duniani!” Huamini Yesu alikuja kuokoa maskini na wanaogandamizwa. Hivyo baada ya kujifunza theologia katika seminari, huchukua nafasi katika mambo ya kisiasa na kujaribu kuwakomboa wanaonyanyaswa katika kila sehemu ya jamii. Ndiyo wenye kushinikiza kwa kusema “Hebu na tuishi kwa sheria na rehema ya sheria takatifu. Tuishi kwa sheria, kwa neno la Mungu” Lakini hawatambui hakika ya ukweli wa Sheria. Hujaribu kuishi kwa sheria iliyoandikwa bila kufahamu na kupata ufunuo wa Mungu juu ya Sheria hiyo.
Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba hapakuwepo na manabii, watumishi wa Mungu katika Israeli kwa kipindi hicho cha miaka 400 kabla ya Kristo. Kwa sababu hii basi, walikuwa ni kundi la kondoo wasio na Mchungaji.
Hawakuwa na sheria wala Kiongozi wa kweli. Mungu hakujidhihirisha mwenyewe kwa hao walio kuwa ni viongozi wa dini zao walio wanafiki. Nchi ilitawaliwa na Dola ya Warumi. Hivyo Yesu aliwaambia watu hawa wa Israeli walio mfuata jangwani kwamba hawatarudishwa kutoka kwake wakiwa na njaa. Alijawa na huruma juu yao waliokama kundi la wanakondoo wasio na Mchungaji kwani wengi wao walikuwa kwenye mateso makubwa.
Wanasheria na wale wengine walio na nafasi za uongozi walikuwa ndiyo wenyewe tu wenye kunufaika. Mafarisayo walikuwa ni kizazi cha “Judaism” na walikuwa ni wenye majivuno sana.
Mwanasheria huyu alimwuliza Yesu katika Luka 10:25“nifanye nini niweze kurithi uzima wa milele?” Alionekana kufikiri kwamba yeye ni bora zaidi kati ya watu wa Israeli. Hivyo mwanasheria huyu (ambaye hajakombolewa) alimwuliza Yesu kwa kusema “nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?”
Mwanasheria huyu anasimama badala yetu leo. Alimwuliza Yesu swali hili, naye akajibu “imeandikwa nini katika Torati? Wasomaje?” Naye akajibu “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote na akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.” Naye akamjibu umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.” Alijaribu kumtia changamoto Yesu bila ya kufahamu yeye alikuwa ni mwenye dhambi, asiyeweza kutenda mema. Hivyo Yesu alivyomwuliza “imeandikwa nini katika Torati, wasomaje?”

“wasomaje” kwa kifungu hiki Yesu anauliza, ni kwa namna gani mimi na wewe tunaijua na kuielewa sheria? Kwa jinsi hii wengi wetu nyakati hizi ndivyo tulivyo. Mwanasheria huyu alifikiri kwamba Mungu alikusudia kuweka sheria ili zifuatwe. Hivyo alijibu kupitia maandiko “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote na jirani yako kama nafsi yako.” Sheria haikuwa na kasoro. Alitupa sheria iliyo kamilifu. Alituambia tumpende Bwana kwa moyo na kwa roho na kwa nguvu na akili na kuwapenda majirani zetu kama nafsi zetu. Ni haki tumpende Mungu kwa moyo wetu wote na kwa nguvu zetu zote, lakini hii ni amri takatifu isiyoweza kutimizwa kwa nafsi zetu. “Wasomaje?” Hii ina maana sheria ni kamilifu na sawa lakini je, wewe unaelewa nini juu yake? Mwanasheria alifikiri kwamba Mungu alileta sheria hii ili aweze kuitii. Ingawa Sheria ya Mungu imeletwa kwetu ili tuweze kuziona nafsi zetu na upungufu ndani yake kwa kuukubali udhaifu wetu uliowazi kabisa mbele za Mungu. “Umetenda dhambi, umeua hali nilikuambia usiue. Kwa nini hukunitii” Ndivyo Mungu akuulizavyo. Sheria huweka wazi dhambi za watu ndani ya mioyo yao. Hebu na tufikiri kwa mfano nilipokuwa nikitembea, nikaona tunda zuri na tamu lililoiva katika shamba la mtu. Mungu amenionya kwa sheria” usichume tunda hilo katika shamba. Itaniaibisha mimi ukitenda hilo” “Ndiyo Baba” “Shamba hili ni la ndugu fulani, hivyo usichume” “Ndiyo Baba” Tunaposikia hivyo tusichume, tunahisi msukumo ndani yetu wa kuchuma. Tunapochukua hatua ya kujizuia inashindikana. Na hii ndivyo ilivyo katika dhambi za watu. Mungu ametuonya tusitende dhambi. Aweza kusema hivi kwa kuwa yeye ni mtakatifu, mkamilifu na mwenye uwezo wote.
soma shehemu ya sitaSHERIA NI KWA AJILI YA KUZIFAHAMU DHAMBI"

WENYE KUJARIBU KUKOMBOLEWA KWA KUPITIA MATENDO YAO BADO NI WENYE DHAMBI.

sehemu ya nne
Hebu na tusome Wagalatia 3:10 na 11“Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana: maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye". Ni dhahiri ya kwamba kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa Imani”kuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; 
Imesemwa “Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati ayafanye “Wale wenye kufikiri kuwa wana mwamini Yesu, hali wakitaka haki kupitia matendo yao, wamelaaniwa. Wapo wapi wenye kujaribu kuwa wenye haki? Wapo chini ya laana ya Mungu.

Kwa nini Mungu ametupa Sheria? Ametupa sheria ili tuweze kuzitambua dhambi zetu (Warumi 3:20). Na pia alitaka tujue kwamba sisi ni wenye dhambi na mwisho wetu ni jehanamu. Amini ubatizo wa Yesu, Mwana wa Mungu na uzaliwe upya kwa maji na kwa Roho. Ndipo utakapo okolewa dhambini, kuwa mwenye haki, kupata uzima wa milele na kwenda mbinguni. Uwe na Imani moyoni mwako.

soma sehemu ya tano "MUNGU AMETUPATIA HAKI KWA IMANI KATIKA SHERIA"

YATUPASA KWANZA KUZIJUA DHAMBI ZETU ILI TUWEZE KUKOMBOLEWA

sheria sehemu ya kwanza

(Marko 7:8-9)“Ninyi mwaiacha amri ya Mungu na kuyashika mapokeo ya wanadamu. Akawaambia, vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu”
(Marko 7:20-23)“Akasema, kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivu, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu; Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”
Kwanza ningependa kufafanua nini maana ya dhambi. Kuna dhambi zilizoelezwa na Mungu na nyingine kuelezewa na mwanadamu. Neno dhambi kwa Kigiriki ‘hamartia’ maana yake ni ‘kukosea katika kulenga shabaha”. Kwa maneno mengine, ni kufanya jambo pasipo usahihi. Ni dhambi kutotii maelekezo ya Mungu. Hebu na tuangalie kwa awali maana ya dhambi kwa mtizamo wa mwanadamu.
Twagundua dhambi zetu kupita dhamira zetu. Ingawa kiwango cha ubinadamu hutofautiana kulingana na jamii anayotoka, hali ya kimawazo, katika mazingira na dhamira.
Hivyo, maana ya dhambi inatofautiana kati ya jamii na jamii. Kitendo cha aina moja chaweza au kisiweze kuchukuliwa kama dhambi endapo kila jamii itakuwa na aina yake ya vipimo. Ndiyo maana Mungu ametupa vipengele vya sheria 613 ili vitumike kama vipimo halisi vya dhambi.
Hatupaswi kamwe kuweka viwango vya dhambi kwa kutumia dhamira iliyowekwa kwa kanuni zetu za kijamii.
Dhambi za dhamira siyo zitokanazo na jinsi ile Mungu anavyoelezea nini maana ya dhambi. Hivyo tusizisikilize dhamira zetu, bali tulinganishe viwango vya dhambi zetu na amri za Mungu.
Kila mmoja ana wazo lake juu ya nini maana ya dhambi. Wengine huchukulia ni udhaifu hali wengine hudhani kwamba ni kutokana na kilema cha tabia.

Matendo ya kistarabu katika jamii moja yanaweza kuchukuliwa kwa jamii nyingine kuwa yasiyo ya kistaarabu na kinyama. Ingawa Biblia inatueleza kwamba dhambi ni kutotii maelekezo ya Mungu. “Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo yenu” (Marko 7:8-9). Muonekano wetu wa nje ni muhimu mbele za Mungu kwa kuwa yeye huangalia kina cha mioyo yetu.
soma sehemu ya pili "KANUNI ZA MTU NI DHAMBI MBELE ZA MUNGU".

Ijumaa, 21 Februari 2014

TOHARA YA MOYO


Lipi lilitangulia, tohara au sheria?
Lipi kati ya moja ya haya Mungu aliwapa Waisraeli kwanza? Tohara. Baada ya ahadi ya ufalme wa Mungu, Mungu alimwambia Abraham na kila mume kati ya wanaume wa nyumba zake kutahiriwa. Mungu alisema kwamba tohara hiyo ni alama ya Agano la Mungu na wao. Hivyo Abraham alitahiriwa govi lake. Wanaume wote katika nyumba yake walifuata tendo hili. Tohara inafanana na imani ambayo tunaiamini.
Tunaokolewa pale tunapoamini kwa moyo. Mungu anasema “tohara ni ya moyo katika roho si katika andiko ambayo sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu” (Warumi 2:29). Yatupasa kuwa na ondoleo la dhambi. Ikiwa hatutakuwa nalo mioyoni mwetu basi ni bure tu. Mwanadamu ana “utu wa ndani” na “utu wa nje” na kila mtu inamlazimu kupokea ondoleo la dhambi ndani ya utu wake.
Wayahudi walikuwa wakitahiliwa sehemu ya mwili (utu wa nje), lakini Paulo aliwaambia “tohara ni ya moyo”. Leo hii Mungu anatuambia nasi kwamba tohara ni ya moyo pale tunapokuwa watoto wake.
Paulo hakuwa akizungumzia tohara ya nje bali tohara na ondoleo la dhambi katika moyo. Hivyo basi aliposema “nini basi ikiwa baadhi yao hawakuamini?”(Warumi 3:3). Alimaanisha kwamba ni nini ikiwa basi baadhi hawatoamini moyoni? Hakuwa akizungumzia juu ya kuamini kwa nje, bali alisema “amini ndani ya moyo.” Yatupasa kujua kile Paulo mtume alichokuwa akimaanisha na ni nini maana ya ondoleo la dhambi moyoni mwetu kupitia neno la Mungu.
“Ni nini basi ikiwa baadhi yao hawakuamini?” maana yake ni kwa vipi basi ikiwa Wayahudi hawakuamini juu ya Yesu Kristo kama mwokozi, je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kutokuwa na maana? Je, ukweli wa Mungu kufuta dhambi zote pamoja na dhambi za kizazi cha Abraham utakuwa ni bure? Kamwe Paulo anasema kwamba hata Wayahudi ambao ni uzao wa Abraham kwa mwili wataweza kuokolewa pale watakapo amini kwamba Yesu Kristo ni mwokozi, mwana wa Mungu aliye beba dhambi zote za dunia kwa njia ya ubatizo na kusulubiwa. Pia anasema kwamba wokovu na neema ya Mungu kupitia Yesu Kristo hautoweza  kamwe kubatilika. (Warumi 3:3-4)
Mungu huchunguza na kuangalia moyoni.Kwa uwazi utu wetu wa ndani umewekwa mbali na hauna uhusiano kabisa na matendo yetu. Wokovu wenyewe hauna uhusiano na matendo yetu (soma katika blog hii “sheria alizotupatia Mungu” utaona kuwa kuna Sheria ya Roho wa uzima na sheria ya dhambi na mauti).

Rejea katika kitabu cha (Warumi 4:1-5) Basi tusemeje juu ya Ibrahim baba yetu kwa jinsi ya mwili? Kwa maana ikiwa Ibrahim alihesabiwa haki kwa ajili ya matendo yake, analo la kujisifia, lakini si mbela za Mungu maana maandiko yasemaje? Ibrahim alimwamini Mungu ikahesabiwa kwake kuwa ni haki. Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. Lakini kwa mtu asiye fanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiye kuwa mtauwa imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.

KUTEMBEA KATIKA HAKI YA MUNNGU


(Warumi 8:12-16)  “Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa kuwa hamkupokea tena roho ya utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba , yaani Baba. Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na Roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu”
Mtume Paulo, kama mtu aliyepokea wokovu toka kwa Mungu alisema kuwa wale waliozaliwa tena upya hawapaswi kuishi kwa jinsi ya mwili bali kwa jinsi ya Roho. Hasahasa Paulo alisema ikiwa sisi ambao tunayo haki ya Mungu tutaishi kwa jinsi ya mwili basi tutakufa, na kwamba kama tutaishi kwa jinsi ya Roho basi tutaishi. Hivyo ni lazima tuamini katika ukweli huu. Je, inakuwaje basi kwa wale wanaoamini katika haki ya Mungu? Je, wanapaswa kuishi kwa mujibu wa haki ya Mungu au kwa tama ya mwili? Ni lazima  watambue kile kilicho sahihi na kisha waiadabishe miili yao na kujitoa kwa kazi za haki ya Mungu.
“ kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndiyo wana wa Mungu(Warumi 8:14) wale wanaoamini katika haki ya Mungu (kuijua haki ya Mungu soma masomo yaliyopita) wanapokea Roho mtakatifu anawaongoza. Hawa ni “wana wa Mungu” wana Roho Mtakatifu anayekaa ndani yao. Kwa hiyo, wale wasio na Roho Mtakatifu ndani yao basi hao si wa Mungu. Mahali pa kuanzia  kumfuata Mungu ni katika kuamini haki yake. Kufanyika mtoto wa Mungu kunaanza kwa kuamini katika neno la injiri ya maji na Roho. Kwa maneno mengine, kufanyika mtoto wa Mungu kunaanza kwa kuamini katika injiri ya haki yake. Hii ina maanisha kuwa unafanyika kuwa mwana familia ya Mungu kwa kuamini katika haki yake na kwamba Mungu ametoa haki yake ili kukuokoa toka katika dhambi.
Yesu alisema kuwa yeye ambaye hajazaliwa kwa maji na Roho hawezi kufahamu maana ya kuzaliwa tena upya. Imani katika ubatizo wa Yesu alioupokea toka kwa Yohana Mbatizaji na damu yake aliyomwaga msalabani inawawezesha wote wanaoamini katika tendo lake la haki kupokea haki ya Mungu.
Hivyo ndugu ninakusihi, jitahidi sana uijue haki ya Mungu iletayo wokovu, soma katika blog hii somo lililo andikwa “ injili ya maji na Roho”


Alhamisi, 20 Februari 2014

SADAKA YA MATENDO MBELE YA MUNGU


Baadhi ya wakristo hawaamini haki ya Mungu na humsifu Bwana wakiimba “Oh, Mungu chukuwa kilicho changu na ufanye kuwa chako, matendo yangu ya kujitolea mbele yako” kwa njia hii Mungu hana nafasi ya kufanya chochote kwako.
Wanadamu humchosha Mungu kwa kujifanya wao ni wa kujitolea matendo yao zaidi. Mungu amechoshwa na upofu huu wa kujitolea kwa sadaka ya matendo. Wao humsihi Mungu apokee haki zao za kibinadamu ( ukitaka kujua haki ya Mungu soma “injili ya maji na roho” katika blog hii). Hudumu waki mlilia Bwana ‘ O, Mungu! Pokea kujitoa kwetu sadaka” huku wakitenda kazi za kanisa kama vile kufagia, kudeki sakafu, kufanya maombi, na kuimba mapambio. Itatia dosari kwa wakristo wengi. Siku hizi wakristo wengi humsihi Yesu kuyajali matendo yao ya kujitolea kimwili huku hawaijui haki ya Mungu au hata kuiamini. Yatupasa kuacha kujitolea kimwili na kuanza kuikubali na kuielewa haki ya Mungu ambayo ndani yake umo ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Tusome habari ya Kornelio katika kitabu cha Matendo 10, ili ujue namaanisha nini? (Matendo 10:1-6) Palikuwa na mtu kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa kiitalia, mtu mtawa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, kuna nini, Bwana? Akamwambia, sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro.  Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda”
Neno atakuambia yakupasayo kutenda” maana yake yale aliyo kuwa akitenda hayakuwa na msaada wowote kuipata haki ya Mungu (yaani kupata msamaha wa dhambi), ili kuzaliwa upya na kupokea Roho Mtakatifu. Ni sawa na mtu masikini na omba omba kumpa tajiri bilionea kila alichonacho  na kumba akae katika makazi ya kifahari kwa fidia ya kile alichotoa.  Mungu haitaji kwetu kujitia sifa ya haki zetu binafsi. Mungu anahitaji tuwe na imani kwa kuamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Tuendelee na habari hii ya Kornelio katika (Matendo 10:37) Jambo lile ninyi mmelijua, lililoenea katika Uyahudi wote likianzia galilaya, baada ya ubatizo aliouhubiri Yohana.
Baada ya kuambiwa na malaika atume watu Yafa wakamwite Simioni, alipofika alianza kuhubairi habari ya ubatizo. Kwanini Simioni alianzia katika ubatizo?, jibu unalipata katika kifungu hiki (Matendo10: 43) “huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi”  ukisha pokea ondoleo la dhambi nini kinachofuata? (Matendo 10:44) Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waloisikia lile neno”
Tunapokea ondoleo la dhambi ikiwa pale tutakapo amini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani( ufafanuzi wa somo hili soma matoleo yaliyopita).Yesu alibatizwa ili kubeba dhambi zote za dunia na kufa ili ili kuzifuta dhambi hizo mara moja na kwa wakati wote.
Hivyo mtu anapohubiriwa kwa usahihi neno la Mungu anapokea ondoleo la dhambi na kupokea Roho Mtakatifu. Je tusifanye kazi za kujitolea katika makanisa? Hapana. Namaanisha si njia ya kumpokea Roho Mtakatifu (kuzaliwa mara ya pili).
Tuendelee na habari ya Kornelio (Matendo10: 47) Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea roho mtakatifu kama sisi?
Utaona kwamba ubatizo katika maji ni hatuwa ya mwisho, kama ishara ya nje ya kile ulichokiamini ndani yako, Hivyo Roho Mtakatifu huja kabla ya kwenda katika maji ya ubatizo.
Hebu tafakari maandiko haya; (Mathayo 9:13) “lakini nendeni,mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”
(2wakorintho3:12-16) Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi; nasi si kama musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba waisrael wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika; ila fikra zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo; ila hata leo, torati ya musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao. Lakini wakati wowote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.


Jumanne, 18 Februari 2014

YESU KUSAFISHA MIGUU YA PETRO (MAANA YA KIROHO)


Maana yake hatuna dhambi tena baada ya kuokoka, hivyo hatupaswi kuomba sala za toba za kila siku.
Katika injiri ya Yohana 13 ipo habari ya Yesu kusafisha miguu ya Petro. Alisafisha miguu ya Petro ili kuonyesha ya kwamba, Petro angetenda dhambi katika kipindi kijacho na kumweleza ya kuwa alikwisha mkomboa kwa dhambi hizo pia, Yesu alijua Petro angetenda dhambi tena katika siku zijazo, hivyo alimimina maji katika karai na kuosha miguu yake.
Petro alijaribu kukataa, lakini yesu alimwambia “nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye.” Kifungu hiki kina maana kwamba “utatenda dhambi tena baadaye” utanikana na kutenda dhambi tena baada ya kuosha dhambi zako zote. Utatenda dhambi hata wakati nitakapo paa kwenda Mbinguni.  Hivyo nasafisha miguu yako ili kumtaadharisha shetani asikutie majaribuni kwa kuwa nimekwisha zichukuwa dhambi zako hata zile zijazo.
Je, unafikiri alisafisha miguu ya Petro ili kutueleza kwamba yatupasa kutubu kila siku? Hapana! Ikiwa tulipaswa kutubu kila siku ili tukombolewe basi ina maana kwamba Yesu isingempasa kuchukuwa dhambi hizo mara moja na kwa wakati wote wa maisha yetu.
Lakini Yesu alisema alitutakasa mara moja na kwa wakati wote ikiwa tungehitajika kutubu kila siku, basi ingekuwa kama vile tumerudi katika kile kipindi cha Agano la kale. Sasa tungeweza kuwa wenye haki? Nani angeweza kukombolewa kwa ukamilifu? Hata kama tulimwani Mungu, ni nani angeweza kuishi bila dhambi?
Hivyo, Yesu alibatizwa mara moja na kujitoa yeye mwenyewe msalabani mara moja ili tuweze kutakaswa mara moja na wakati wote. Je, unaweza kuelewa hili?
Tumekombolewa kutoka dhambini kwa kumwamini Yesu aliyezichukuwa dhambi zetu zote,
“ na kila kuhani kila siku akifanya ibada na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi. Lakini huyu alipokwisha kutoa kwa ajiri ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele aliketi mkono wa kuume wa Mungu tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe  kuwa chini ya miguu yake maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema hili ni Agano nitakalo agana nao baada ya siku zile anena Bwana, nitatia sheria zangu katika nia zao nitaziandika ndipo anenapo. Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa, basi ondoleo la haya likiwapo, hapana toleo tena kwa ajiri ya dhambi” (waebrania 10:11-18)
Nini maana ya “basi ondoleo la hayo likiwapo” katika mstari wa 18 hapo juu? hii ina maana ya kwamba kila dhambi ilifutwa kabisa bila uchaguzi Mungu alizifuta dhambi zote na kutusamehe.
Nahitimisha kwa kusema kuwa; tuna okolewa bure kwa neema ya Mungu katika imani, lakini neema hiyo haituruhusu kutenda dhambi makusudi, kwa sababu ile nguvu ya kuishinda dhambi tumepewa (Roho Mtakatifu) kwa kuamini katika siri ya Mungu. (kuifahamu siri ya Mungu soma masomo yaliyopita).

“Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa baba , hivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima  (Warumi 6:1-4)

MAANA YA WOKOVU


Wokovu katika ukristo maana yake ni’ ukombozi toka kwenye nguvu au adhabu ya dhambi .’ tunapokea wokovu pale tunapokiri kwamba hatuna uwezo kujizuia kwenda motoni na kumwamini Yesu ametuokoa sisi sote toka katika dhambi zetu zote kwa kupitia kuzaliwa kwake, ubatizo na damu yake msalabani.
Wale wasio na dhambi kwa kuamini wokovu wa Yesu, ubatizo na damu ya Yesu huitwa “walio okoka” waliozaliwa upya wenye haki.

Tunaweza kutumia neno “wokovu”  kwa wale wote walio okolewa tokana na dhambi zao, pamoja na hatia zile za asili na zile za kila siku, kwa kumwamini Yesu. Kama alivyo mtu aliye jongea kwa Mungu, Yule ajongeaye dhambi za ulimwengu atakuwa ameokolewa kwa kumwamini Yesu kama mwokozi, kwa kuamini ubatizo na damu, maneno ya kweli ya kiroho.

INJILI YA KWELI


Injili ya kweli ni ile pekee yenye kutuwezesha kuwa huru kwa dhambi zetu kikamilifu, mara moja na kwa wakati wote pale tunapoamini nguvu ya injili ya Mungu.
Injili ya Mungu ni ile “Yesu Kristo alilipa deni la wadaiwa (wenye dhambi) wasio weza bila shaka kulilipa wenyewe “.
Alikuja hapa ulimwenguni na kubeba dhambi zote kwa ubatizo wake katika mto Yordani na kututakasa daima.
Amelipa mshahara wa dhambi kwa kuchukuwa dhambi zetu zote  kwa ubatizo wake Yordani na kwa kufa msalabani kalvari. Yesu alizifuta dhambi zote za ulimwengu kwa mithili ya nguvu kwa ubatizo na damu yake. Hii ndiyo habari njema (Injili) ya kweli.
Injili ya kweli ni ile Yesu kuja ulimwenguni na kwa ubatizo wake na damu yake msalabani umetuokoa sisi sote wenye kuamini.

Kama ilivyo andikwa katika 1yohana 5:4-6huyu ndiye aliye kuja katika maji na katika damu, yesu Kristo si kwa maji tu, bali katika maji na katika damu’.

Jumapili, 16 Februari 2014

SALA YA TOBA ITAWEZA KUTAKASA DHAMBI ZETU


Hakika sala ya toba haitoweza kamwe kutakasa dhambi zetu kwa sababu ukombozi hauwezi kuja kwa kupitia matendo yetu. Bali, ili tuweze kuwa wenye haki kamili na wakati wote tukiwa tumeoshwa dhambi zetu zote, yatupasa kuamini katika ubatizo na damu ya Yesu, na kuamini kuwa Yesu ni Mungu. Ukombozi kamili hupatikana kwa wale tu wenye kuamini kuwa Yesu alibeba dhambi zetu zote kwa ubatizo wake na kutoa damu yake msalabani kutupa uhai mpya.
Sasa basi, je tutaweza kutakasa dhambi zetu za kila siku kwa kufanya sala za toba kila mara? Hapana. Dhambi zote tuzitendazo maishani mwetu kila siku zilikwisha takaswa takribani miaka 2000 iliyopita pale Yesu alipozibeba kwa ubatizo wake. Hakika tumepata utakaso wa kudumu kwa dhambi zetu zote kwa ule ubatizo wa Yesu na kwa damu yake pale msalabani. Amekuwa mwanakondoo wa sadaka kwa ajili yetu wenye kumwamini, kusafishwa dhambi zetu zote, na kulipia yote kwa ubatizo na kwa damu yake msalabani.
Kwa lugha nyepesi, katika Agano la kale kuhani mkuu alikuwa akitoa sadaka ya upatanisho wa dhambi kila siku ya kumi ya mwezi wa saba (Walawi 16: 29-34). Aliye husika kumbebesha (kumtwika ) mnyama dhambi za Israel ni kuhani mkuu peke yake kwa niaba ya watu wote. Watu wa Israel hawakuwa na haja ya kila mmoja kuwekea mikono katika sadaka ya dhambi, bali walitakiwa kuamini kuwa dhambi zao zimesamehewa kupitia mwakilishi wao. Katika Agano jipya Yohana Mbatizaji amesimama (kama kuhani mkuu) badala ya watu wote ulimwenguni, hivyo alimtwika Yesu dhambi zetu zote katika ubatizo, nasi pia tunahitajika kuamini katika yale aliyofanya Yohana Mbatizaji (kuhani mkuu) na Yesu (mnyama kwa Agano la kale).
TOBA YA KWELI
Sote sisi tumejawa na dhambi. Toba ya kweli ni kukubali kufuata kweli; kwamba sisi ni wenye dhambi mbele ya Mungu, na hivyo hatuwezi kujizuia kutenda dhambi maishani mwetu na kwenda jehanamu tutakapokufa. Hivyo yatupasa kumkubali Yesu kama mwokozi wetu kwa kuamini kwamba alikuja ulimwenguni kutuokoa sisi wenye dhambi na hivyo alibeba dhambi zetu (kupitia ubatizo), akafa na alifufuliwa kutuokoa. Toba ya kweli ni kuacha fikra zetu na kumrudia Mungu (Matendo 2: 38).
Toba ya kweli ni kukiri dhambi zetu na kulirudia neno la Mungu kukubali wokovu katika maji (ubatizo) na kwa damu kwa moyo wetu wote. (1Yohana5:6).
Ili tuweze kuokolewa na kusafishwa dhambi zetu zote, yatupasa kuacha kujaribu kujitakasa kwa kupitia matendo ya sheria, na kukiri kwamba sisi ni wenye dhambi mbele ya Mungu na sheria yake, sisi basi yatupasa kukubali kweli ya wokovu wa Yesu, injili ya Maji na Roho, ambayo Yesu alituachia kwa ubatizo na damu yake.
Tutaokolewa pale tutakapo amini ubatizo wa Yesu uliozichukua dhambi zetu zote kwake.
Kwa maneno mengine, ubatizo wa Yesu, kusulubiwa kwake, na ufufuo wake umetimiza haki ya Mungu kwa wokovu wa wenye dhambi. Yesu alikuja katika mwili, alibatizwa na kusulubiwa ili kutusafisha dhambi zetu zote. Kwa kuwa na imani iliyo kamili katika yote haya na kuamini kwamba Yesu alifufuka ili awe mwokozi wa wote wenye kumwamini katika toba ya kweli na imani halisi.

Kila kitu katika Agano la kale kina mwenzake katika Agano jipya kwa Agano la kale “tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake imekusanya” (Isaya 34:16)
Hitimisho; ikiwa utajikuta wewe mwenyewe unamwomba Yesu ili akusamehe dhambi zako za kila siku, basi ni lazima utambue kuwa bado hujazaliwa upya.
Ikiwa kwa namna yoyote ile umekuwa ukijifanya kuwa mtakatifu kwa matendo yako na mwonekano wa mwili wako, ingawa moyo wako una dhambi, basi wewe ni mwanadini mnafiki na ni mtoto wa maangamizi.