Jumanne, 4 Machi 2014

HEMA TAKATIFU LA KUKUTANIA


Somo la tatu
Maana ya kiroho ya
Mti wa mshita, mafuta, na viungo
(Kutoka 25:1-9) “BWANA akanena na Musa, akamwambia: waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu. Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii: dhahabu, na fedha, na shaba; na nyuzi za rangi ya bluu (samawiti), na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani safi, na singa za mbuzi; na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pompoo, na miti ya mshita; na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri; na vito vya shohamu, na vito vingine vya kutiwa kwa ile naivera, na kwa kile kifuko cha kifuani. Nao wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao. Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mtakavyo vifanya.”
Nguzo za hema takatifu la kukutania, madhahabu ya sadaka ya kuteketezwa, na mbao na vifaa vingine vya madhabahu vyote vilitengenezwa  kwa mbao za mti wa mshita. Kwa kawada mti katika Biblia unamaanisha wanadamu (waamuzi 9:8-15, marko 8:24). Pia mti hapa unamaanisha kwetu juu ya asili ya mwanadamu; ile hali ya kuwa mti huu wa mshita ulitumika katika nguzo, katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, na katika hema takatifu la kukutania lenyewe inatueleza kuwa kama ambavyo mizizi ya mti wa mshita mara zote imefunikwa ardhini, basi asili yetu ni ile ambayo haiwezi kujisaidi bali kutenda dhambi wakati wote. Ni lazima watu wote wakiri kuwa hawawezi kujisaidia bali wataendelea kuwa wasio na haki na kutenda dhambi kila mara.
Kwa wakati huo huo, mti wa mshita una maanisha juu ya ubinadamu wa Yesu Kristo. Masihi aliyekuja katika mwili wa binadamu alibeba dhambi zote za ulimwengu, na alihukumiwa kwa haki kwa ajili ya wanadamu. Yeye ni mungu mwenyewe, na kwa hiyo, sanduku la ushuhuda, meza ya wa wonyesho, madhabahu ya uvumba, na mbao za Hema takatifu la kukutania vyote vilitengenezwa kwa mti wa mshita na vikafunikizwa kwa dhahabu safi.
Mafuta kwa ajili ya mwanga na manukato kwa ajili ya mafuta ya kujipaka na kuwekea wakfu na kwa uvumba wa manukato vinamaanisha juu ya imani yetu ambayo tunaitoa kwa Yesu Kristo. Yesu Kristo ni masihi aliyetuokoa mimi na wewe. Maana ya jina “Yesu” ni “yeye atakaye waokoa watu wake toka katika dhambi zao,” na jina “Kristo” lina maana ya “mtiwa mafuta,” hivyo majina haya yanatueleza sisi kuwa Yesu Kristo ni Mungu mwenyewe na kuhahani mkuu wa Mbinguni aliyetuokoa sisi. Ili kuheshimu mapenzi ya Mungu, Bwana wetu alikuja hapa duniani katika mwili wa mwanadamu, alibatizwa, alisulubiwa, msalabani  kwa ajili yetu, na kwa hiyo ametupatia zawadi ya wokovu. Kwa hakika jukumu la kuhani mkuu lililochukuliwa na Yesu aliye tupatia wokovu wetu lilikuwa ndiyo kazi nzuri sana.
Vito vya Shohamu, na Vito vingine vya kuwekwa katika Naivera na katika kile Kifuko cha kifuani cha kuhani mkuu.
Vito kumi na mbili vya aina tofauti vimetajwa hapa ambavyo vitawekwa katika naivera na katika kifuko cha kifuani cha kuhani mkuu. Kuhani mkuu alivaa kwanza gwanda kama kanzu fupi, kisha akavaa joho la bluu, na kisha akavaa naivera juu ya joho. Kisha, kifuko cha kifuani kiliwekwa katika naivera ambayo ilivaliwa wakati wa sherehe maalum ya sadaka ya kuteketezwa, na katika kifuko hiki cha kifuani viliwekwa vito kumi na mbili vya dhamani. Hii inatuonyesha sisi kuwa jukumu la kuhani mkuu lilikuwa ni kuwakumbatia na kuwa jumuisha wa Israeli pamoja na watu wengine wa ulimwengu mzima katika kifua chake, kwenda mbele za Mungu, na kumtolea mungu sadaka zao za kuteketezwa.
Yesu, ambaye ni kuhani mkuu wa milele wa Mbinguni pia aliyakumbatia mataifa yote ya ulimwengu katika kifua chake, akautoa mwili wake mwenyewe ili kuzichukuwa dhambi zetu kwa ubatizo wake na akasulubiwa kwa ajili yetu, na kwa hiyo amewaweka wakfu watu wake kwa Mungu Baba. Vito vya thamani kumi na mbili vilivyowekwa katika kifuko cha kifuani  vina maana ya mataifa yote ya ulimwengu huu, na kuhani mkuu aliye vaa vito hivyo ni alama ya Yesu Kristo ambaye amewaokoa mataifa na kuyakumbatia mataifa yote ya ulimwengu katika kifua chake.
Hivyo, hizi zilikuwa ni sadaka ambazo Mungu wetu aliwaambia Waisraeli kumtolea ili kulijenga hema takatifu la kukutania kwa jili yake. Kuna maana ya kiroho katika ukweli kuwa Mungu aliwaambia Waisraeli kumjengea hema takatifu la kukutania, mahali ambapo Mungu angeishi, kwa sadaka zao. Mara nyingi watu wa Israeli walibakia ni wenye dhambi kwa sababu hawakuweza kuitunza na kuifuata sheria ambayo Mungu aliwapatia. Hii ndiyo sababu Mungu aliwaeleza kupitia Musa kulijenga hema takatifu la kukutania  na kuwapatia utaratibu  wa sadaka ya kuteketezwa, ambayo kwa hiyo ondoleo la dhambi lilitolewa kwa sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa katika Hema takatifu la kukutania. Kwa maneno mengine, Mungu alizifuta dhambi zote za Waisraeli kwa kuzipokea sadaka zao, kwa kutumia sadaka kuijenga nyumba yake, na kwa kuwafanya kumtolea sadaka zao za kuteketezwa katika Hema takatifu la kukutania kwa mujibu wa kanuni za utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa. Hivyo ndivyo ambavyo Mungu angeliweza kuishi katika Hema takatifu la kukutania pamoja na watu wa Israeli.
kumbuka tunapoongelea kulijenga hema takatifu, tunamaanisha vihi sasa wewe ni nyumba (hema) ya Mungu, vifaa vyote vilivyo agizwa na Mungu ni lazima hata sasa vitumike kukujenga kiroho kwa imani.
  


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni