Jumatano, 30 Aprili 2014

SHERIA ALIZOTUPATIA MUNGU


Mungu aliweka sheria ulimwenguni kwa sababu zifuatazo;
1. aliwapa wenye dhambi sheria na amri ili waokolewe kwa dhambi zao “ kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria” (Warumi 3:20)
2. Sheria ya pili ni sheria ya imani iokoayo wenye dhambi. “Sheria ya Roho wa uzima” ( Warumi 8:2) inayotoa njia ya wokovu kupitia imani katika Yesu Kristo mwokozi wetu (Warumi 5:1-2).Yesu alishuka ulimwenguni kutimiza hii sheria. Yesu aliweka Sheria ya wokovu ili kuokoa wale wote wenye dhambi ulimwenguni.
Kwa asili kulikuwa na sheria mbili zilizotolewa na Mungu: sheria ya dhambi na mauti na ile sheria ya roho wa uzima. Sheria ya Roho wa uzima ilimwokoa Paulo toka katika sheria ya dhambi na mauti. Hii ilimaanisha kuwa kwa kuamini katika ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani, ambavyo vilichukulia mbali dhambi zake zote, Paulo auliungana na Yesu na kisha akaokolewa toka katika dhambi zake zote. Sisi sote ni lazima tuwe na imani inayotuunganisha na ubatizo wa bwana na kifo chake msalabani. Soma fungu hili; Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo. Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.( wakolosai:2:11-12)
Mungu aliweka sheria ya imani kwa wale tu wenye kuamini wokovu utokanao kwa maji na roho.  Yeye atakaeokolewa na kuwa mwana wa Mungu yampasa kwanza kuamini sheria hii ya imani ambayo Mungu ameitoa. Ndiyo pekee njia ya kuokoka. Kwa haya, ameruhusu njia ya kwenda Mbinguni kwa wale wenye kuamini kuzaliwa kiroho katika kweli tokana na sheria hii.
Vipo vipengele 613 vya sheria ya Mungu vinavyohusu maisha yetu ya kila siku. Lakini iliyo kuu kati ya hii ni amri kumi ambazo yatupasa kuzifuata mbele ya Mungu. Kupitia amri zilizo andikwa na Mungu tutaweza kutambua ni kwa kiasi gani tumeacha utii kwake. (Warumi 3:19-20).
Sababu ya Mungu kutupatia amri zake ilikuwa ni kutufanya tugundue na kuziona dhambi zetu, kamwe hatutoweza kuzishika amri zote, hivyo yatupasa kunyenyekea kwa kukubali ukweli kwamba sisi ni wenye dhambi na Mungu anajua kwamba kamwe hatutoweza kuishi kwa kufuata sheria yake. Hivyo alishuka ulimwenguni kama mwanadamu, alibatizwa na kuhukumiwa msalabani. Kujaribu kuishi kwa kufuata sheria ya Mungu ni dhambi ya kiburi. Hatupaswi kufanya hivyo.
Ku wapi,basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La ! bali kwa sheria ya imani. Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria ( Warumi 3:27-28) Pia soma katika (Warumi 4:1-8)

Kuna sehumu imeandikwa imani bila matendo imekufa lakini soma kwa umakini utaona ya kuwa si matendo ya sheria bali matendo ya imani ndiyo yanayo hitajika. Je mwenye Roho Mtakatifu anaweza kutenda dhambi makusudi kwa sababu tu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria? Hapana, maana mtu huyu amempokea Roho Mtakatifu na matunda ya Roho.

Ijumaa, 18 Aprili 2014

AMINI ILI ROHO MTAKATIFU AKAE NDANI YAKO


(Mathayo 25:1-12)
“Ndipo ufalme wa Mbinguni utakapofanana na wanawali waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana harusi. Watano wao walikuwa wapumbavu na watano wenye busara. Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao na wasitwae na mafuta pamoja nao, bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. Hata bwana harusi alipokawia wote wakasinzia wakalala usingizi. Lakini usiku wa manane pakawa na kelele, haya bwana arusi tokeni mwende kumlaki. Mara wakaondoka wanawali wale wote wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara tupatieni mafutayenu kidogo maana taa zetu zinazimika. Lakini wale wenye busara wakawajibu wakisema hayatatutosha sisi naninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie. Na hao walipokuwa wakienda kununua mafuta bwana harusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana Bwana tufungulie Akajibu akasema, Amin nawaambia siwajui ninyi. Basi kesheni kwa sababu hamwijui siku wala saa.”
Ni watu gani walio mfano wa wanawali walio na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao?
Katika kifungu kilichopita hapo juu tumeona wanawali watano wenye busara na wapumbavu, wanawali wapumbavu waliwaomba wale wenye busara kuwagawia kiasi cha mafuta ya taa lakini wenye busara  wakawajibu wale wapumbavu “hayatatutosha sisi na ninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie”.Hivyo wakati wale walio wapumbavu wakienda nje kununua mafuta hayo, wale wenye busara walikuwa nayo katika taa zao na kuingia katika sherehe za harusi. Sasa basi ni kwanamna gani tunaweza kuyatayarisha mafuta kwa ajili ya Bwana? Kitu pekee tunachoweza kufanya ni kuusubiri msamaha wake wa dhambi katika mioyo yetu.
Katikakati ya watu tunaweza kupata aina mbili za imani. Moja ni imani ya injili ya msamaha wa dhambi. Hii ndiyo inayopelekea kumpokea Roho Mtakatifu. Nyingine ni ile ya kuwa mwaminifu wa kanuni za dini bila kujali mtu kusamehewa au kutosamehewa dhambi.
Kwa wale wote walio waaminifu kwa kanuni za dini, injili hubaki kuwa mzigo kwao kuichukulia. Kama walivyo wanawali wapumbavu waliokwenda nje kununua mafuta pale bwana harusi alipo ingia, wale wote wanaohama toka nyumba moja ya kuabudu kwenda nyingine kwa matumaini ya kumpookea Roho Mtakatifu ndani yao, hawamdanganyi yeyote bali nafsi zao. Watu wa aina hii ni wenye kiburi ambao kwa kweli ndiyo wanao hitaji kuwa na imani ya injili njema katika mioyo yao kabla ya siku ya hukumu. Watuhawa hutamani kuwa na Roho Mtakatifu kwa kumuonyesha Mungu ukereketwa wao.
Tuone ushuhuda wa shemasi mmoja aliyefanya juhudi kubwa katika kumpokea Roho Mtakatifu. Ushuhuda huu kwa hakika utatusaidia sana. “Nilifanya kila niwezalo ili kumpokea Roho Mtakatifu. Nilidhani kwamba, ikiwa nitajitolea nafsi yangu kwa imani yangu kwa uaminifu nitaweza kumpokea Roho Mtakatifu na matokeo yake nilijikuta kuhama kanisa moja hadi jingine, nyumba moja ya sala kwenda nyingine. Watu katika moja wapo ya nyumba hizi za sala walikuwa wakipiga kinanda cha umeme ikiwa ni sehemu ya ibada.Mchungaji aliyekuwa akiongoza mkutano huu aliwaita wale wote waliohitaji kumpokea Roho Mtakatifu moja baada ya mwingine na walipo wekewa mkono wa mchungaji katika mapaji ya nyuso zao, kila mtu baada ya tendo hilo alianza kunena kwa lugha. Mchungaji aliruka huku na kule akishikilia kipaza sauti nakupaza sauti “pokea moto, moto, moto!” na kuweka mkono wake juu vichwa vya watu na kusababisha baadhi yao kupagawa na kuanguka. Mwanzoni nilikuwa na wasiwasi ikiwa tendo hili linamaana ya kumpokea Roho Mtakatifu lakini tayari nilikuwa nimeathirika na mikutano ya aina hii. Licha ya haya yote kamwe sikuweza kupokea Roho Mtakatifu.
Baada ya tukio hili niliamua kwenda milimani nakujaribu kulia na kuomba usiku kucha nikiwa nimeegemea mti. Wakati mwingine nilijaribu kufanya maombi ndani ya pango lakini yote haikusaidia. Baada ya yote haya nilijaribu kufanya maombi usiku kucha kwa siku arobaini lakini kamwe sikuweza kumpokea Roho Mtakatifu. Semina hii ilikuwa ikifanyika kwa juma mara moja na kufululiza majuma saba.
Katika semina hii kulikuwa na mafundisho kuhusu upendo wa Mungu, msalaba na ufufuko wa Yesu, tendo la kuwekewa mikono, tunda la roho na kukua kiroho. Katika muda huo wakati ratiba ya semina ilipokuwa ikikaribia kuisha, mnenaji mkuu katika semina hiyo aliniwekea mikono juu ya kichwa changu na kuanza kuniombea ili niweze kumpokea Roho Mtakatifu huku nikimfuatisha maneno yake kama alivyonielekeza. Nilitulia na kunyanyua viganja vya mikono yangu na kuelekeza juu na kuanza kupiga kelele “la-la-la-la!” kwa kurudia rudia. Mara ghafla nilipokuwa nikipiga kelele “la-la-la-la!” nilianza kunena moja kwa moja lugha ya ajabu. Watu wengi walinipongeza baada ya hapo katika kumpokea Roho Mtakatifu. Lakini nilipokuwa mwenyewe nyumbani nilihofu. Hivyo nikaanza kujitolea kufanya kazi katika semina hiyo. Nilidhani kwamba ilinipasa kujitolea kwa kazi kama hii mapema sana. Hivyo nilisafiri nchi nzima katika kutoa huduma na nilipo wawekea mikono wagonjwa, magonjwa yao yalionekana kupona ingawa baadhi yaliwarudia baadaye.  Na baadaye nikapata maono na nikagundua yakuwa naweza pia kutoa unabii. Chakushangaza unabii wangu mara nyingi ulikuwa wakweli.
Tokea hapo nilialikwa sehemu za kila aina na kulakiwa kwa shangwe. Lakini bado nilikuwa na hofu ndani yangu ndipo nikasikia sauti ikisema “usitange tange toka sehemu moja kwenda nyingine namna hii badala yake nenda ukawasaidie jamaa zako nyumbani katika kupokea wokovu.” Hata hivyo sikuelewa maana halisi ya wokovu. Nilichokuwa nakielewa nikile wengi walichokuwa wakisema kwamba, ikiwa nitaacha kuzitumia karama za Roho Mtakatifu basi atanipokonya. Kwa upande mwingine nilihofu kutumia uwezo wangu lakini sikuweza kujizuia hilo.
Siku moja nilisikia kuwa yupo mwanamke fulani ambaye ni wa dini ya Shama aliyehitaji kumwamini Yesu, hivyo mimi pamoja na rafiki yangu tulikwenda kumtembelea. Hatukumfahamisha juu ya ujio wetu kabla. Lakini mwanamke huyo alikuwa akitusubiria mlangoni nakuanza kutuambia “nilishajua kwamba mnakuja” mara ghafla alianza kutunyunyizia maji na kusema “hakuna tofauti kati ya ushama wa mashariki na ushama wa magharibi”. Alituita sisi kuwa ni “washama wa Yesu” na kutunyoshea kidole akisema “huyu ndugu ni muoga lakini huyu si muoga” Kile ambacho mwanamke huyu alichokua akisema kiligeuka kuwa kama pigo katika kichwa. Nikaanza kuwaza kwamba yote niliyokuwa nikiyatenda hayakuwa tofauti nayale ambayo dini ya shama wakitenda. Hakuna nilichokuwa nimekwisha tenda ili kumleta Roho Mtakatifu ndani yangu kwa sababu bado nilikwa na dhambi moyoni.”
Tokana na ushuhuda huu tunajifunza kwamba, swala la kumpokea Roho Mtakatifu lipo nje ya uwezo wetu. Kwasababu imani ya aina hii haihusiani na injili ya Mungu kwani wale wote wanaoishi katika aina hii ya udini ndiyo wasio kuwa na mafuta katika taa zao.
Taa katika biblia inamaana ya kanisa, na mafuta maana yake Roho Mtakatifu. Biblia inakusudia kwamba wale wote wanao hudhuria kanisani, iwe ni kanisa la Mungu au si la Mungu pasipo kumpokea Roho Mtakatifu, bado ni wapumbavu.
Wapumbavu wote hupandisha mori siku hata siku. Watu hawa hupandisha hisia zao kali na kujitolea kimwili mbele ya Mungu. Ikiwa tungelisema kuwa hisia zetu ziwe za kiwango cha sentimita 20 na hivyo kufanya kila siku 1 kupandisha sentimita 1, basi ingelichukua siku 20 kuweza kufikia kiwango cha juu katika hisia zetu zote. Hisia zao katika imani hupata nguvu mpya kwa kila maombi ya asubuhi, maombi ya usiku kucha, maombi ya kufunga na mikutano ya uamsho na pia katika maisha ya kila siku. Huathirikana tabia hii ya kudumu katika kuenenda kwa hisia.
Hisia zao hupanda katika jina la Yesu. Huudhuria kanisani ili kupandisha hisia zao, lakini mioyo yao bado imechanganyikiwa huku wakitafuta sababu nyingine. Sababu ya hili ni kwamba imani yao imetokana na kile kinachotokana na mwonekano wa nje kimwili na hivyo kuhitaji shinikizo la mara kwa mara ili kusukuma hisia zao ili moto wa hisia usizimike ndani yao. Hata hivyo bado hawato weza kumpokea Roho Mtakatifu kwa aina hii ya imani. Kwa kupandisha hisia hizo kamwe hakutoweza kuwafanya kumpokea Roho Mtakatifu.
Sote imetupasa kuwa tayari na imani sahihi ili kuweza kumpokea Roho Mtakatifu katika uwepo kamili wa Mungu. Na ndipo pekee tutakapo kuwa na haki ya kumpokea Roho Mtakatifu. Ni kwanamna gani basi tunaweza kuwa na imani ambayo inatupa haki ya kuwa na Roho Mtakatifu? Ukweli upo katika injili njema ambayo ilikamilishwa kwa ubatizo wa Yesu Yordani na kumwaga damu yake Msalabani.
Mungu alituita kuwa sisi ni kama “wazao wa watenda mabaya, watoto wanaoharibu” (Isaya 1:4). Lazima tulikubali hili. Kwa asili wanadamu wamezaliwa wakiwa wanadhambi aina 12 (Marko 7:21-23). Wanadamu hawawezi kujizuia kutotenda dhambi tokea wanapozaliwa hadi kufa. Katika Yohana 1:6-7 imeandikwa, “palitokea mtu ametumwa kutoka kwa Mungu jina lake Yohana. Hivyo alikuja kwa ushuhuda ili aishuhudie ile nuru wote wapate kuamini kwa yeye”.Yohana Mbatizaji alimbatiza Yesu na kumtwika dhambi zote za ulimwegu akisema “tazaama mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya dunia” (Yohana 1:29).
Tuliokolewa kwa dhambi zote na kuushukuru ubatizo wa Yesu Kristo. Kama Yohana asingeli mbatiza Yesu Kristo nakutotangaza kwamba alikuwa ndiye mwana kondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu, basi tusingeliweza kumjua Yesu kwamba ndiye aliye beba dhambi zetu zote kuelekea msalabani. Tusingeliweza kuifahamu njia ya kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa hiyo basi tunamshukuru Yohana kwa ushuhuda kwani sasa tunaelewa yakwamba Yesu ndiye aliye beba dhambi zetu zote na hivyo tunaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa imani hiyo.
Kwa imani hii basi tumekuwa wanaharusi tuliotayarishwa kamili kumpokea Yesu Kristo, Bwana harusi. Sisi ni wanawali tulio mwamini Yesu na tumejitayarisha kamili kumpokea Roho Mtakatifu.
Je, unaamini injili ya maji na Roho kwa moyo wako wote? Je, unaanini kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu kwa ubatizo wake kwa Yohana? Biblia inasema “basi imani, chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo” (Warumi 10:17). Nilazima tuamini yakwamba Yesu alibatizwa na Yohana na kufa msalabani ilituweze kumpokea Roho Mtakatifu. Yatupasa kuelawa kwamba kumpokea Roho Mtakatifu kutawezekana ikiwa tutaamini kwamba Yesu alikuja ulimwenguni akiwa kama mwanadamu na kubatizwa na Yohana hivyo alikufa msalabani na kufufuka.
Hata leo hii yapo makundi mawili ya wanaoamini kama ilivyo kwa wanawali kumi katika ile habari ya hapo mwanzo. Sasa basi wewe nawe uko upande upi? Yakupasa ujue ile njia ya kweli ambayo utaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa hakika. Ni kwa imani gani utaweza kumpokea Roho Mtakatifu? Je utaweza kumpokea Roho Mtaktifu kwa kupitia shauku itokanayo na ukereketwa utokanao na dini kama Shama?
Je utaweza kweli kumpokea Roho Mtakatifu katika hali ya kupoteza fahamu? Je utaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini ushabiki wa kidini? Biblia inasema kwamba Yesu alipobatizwa kwa kuzamishwa na kuibuka toka kwenye maji Roho wa Mungu alitua kama hua juu yake. Alibatizwa ili kubeba dhambi zetu zote na hivyo kuweka bayana kwamba atakwenda kusulubiwa ili kulipia mshahara wa makosa yetu yote.
Yesu alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi za ulimwengu na hivyo kwenda msalabani ili tuweze kuokolewa na kupokea kipawa cha Roho Mtaktifu. Jambo hili ni kweli. Yesu alibatizwa na Yohana, akahukumiwa kwa dhambi zetu zote msalabani na kufufuka. Lazima tuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani ili tupate msamaha wa dhambi zetu zote.
Tunaweza kuona toka ubatizo wa Yesu (Mathayo 3:13-15) kwamba, Roho Mtaktifu huja kwa amani kama ashukavyo huwa kwa wale waliotakaswa kwa kuamini ubatizo wa Yesu. Ili kumpokea Roho Mtakatifu ni muhimu kuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani. Roho Mtakatifu huja juu ya mtu katika hali ya utulivu na amani kama vile hua pale mtu huyo anapo amini msamaha wa dhambi. Wale ambao tayari wamekwisha mpokea RohoMtakatifu yawapasa kuelewa kwamba hili limewezekana kutokana na msamaha wa dhambi
kwa imani. Roho Mtakatifu hutua juu ya wale wote wanao amini msamaha wa dhambi kwa mioyo yao yote.
Yesu Kristo alikuja kwa mkate na divai ya uzima wa milele (Mathayo 26:26-28, Yohana 6:53-56) Yesu alipoibuka toka majini baada ya kubatizwa, palitokea sauti mbinguni ikisema “Huyu ni mwanangu mpendwa wangu ninaye pendezwa naye” (Mathayo 3:17).
Nirahisi kuamini katika Mungu kwa Utatu. Mungu ni Baba wa Yesu na Yesu ni Mwana wa Mungu. Roho Mtakatifu pia ni Mungu. Utatu huu ni Mungu mmoja kwetu. Yakupasa kujua kwamba, kamwe hautoweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini msalaba pekee au kujaribu kujitakasa binafsi kwa matendo ya haki. Utaweza kumpokea Roho Mtakatifu pale unapoamini ubatizo wa Yesu na hivyo kumtwika dhambi zote juu yake, na kuamini kusulubiwa kwake ili kutupatanisha kwa dhambi zetu zote.
Hakika hivi ndivyo ilivyo rahasi na wazi ju ukweli huu! Si vigumu kupokea msamaha wa dhambi na Roho Mtakatifu. Mungu huzungumza nasi kwa namna iliyo rahisi. Kiwango cha akili ya mtu wa kawaida ni kati ya 110 na 120 (yaani IQ - intelligence quotient). Injili yaMungu ni rahisi kumtosheleza mtu wa kawaida kuielewa. Hata kwa watoto wa umri kati ya miaka 4 na 5 injili hii njema kamwe haijawa ngumu kueleweka kwao.
Lakini Mungu anapo zungumza nasi juu ya kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani kwa njia iliyo rahisi zaidi, je, tusingeliweza kweli kumwelewa? Mungu husamehe dhambi zetu zote na kutupa Roho Mtakatifu kama zawadi kwa wale wote waaminio injili hii.

Mungu anatuambia kwamba hatutoweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kupitia tendo la kuwekewa mikono au sala ya toba. Roho Mtakatifu haji kwa namna ambavyo tutakapo funga au kujitolea au hata kuomba usiku kucha milimani. Ni aina gani basi ya imani itakayo sababisha kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu? Ni imani ya ukweli wa kwamba Yesu alikuja hapa ulimwenguni alibatizwa ili kubeba dhambi zetu zote, akafa msalabani na alifufuka.

Jumatano, 16 Aprili 2014

UPATANISHO WA DHAMBI KATIKA AGANO LA KALE NA JIPYA


Na mtu awaye yote katika watu wa nchi akifanya dhambi pasipo kukusudia, kwa kufanya neno lolote katika hayo ambayo BWANA alizuiria yasifanywe, naye akapata hatia, akijulishwa hiyo dhambi yake kwa ajiri ya dhambi yake aliyoifanya, ndipo atakapoleta mbuzi mke mkamilifu, awe matoleo yake kwajiri ya dhambi yake aliyoifanya. Naye ataweka mkono wake kichwani mwake hiyo sadaka ya dhambi, na kumchinja sadaka ya dhambi mahali hapo pa sadaka ya kuteketezwa. Kasha kuhani atatwaa katika hiyo damu yake kwa kidole chake, na kuitia katika pembe za madhabahu ya kuteketeza na damu yake yote ataimwaga  chini ya madhabahu (Walawi 4:27-30)
Mwenye dhambi anapotaka kupatanishwa na dhambi alizotenda kwa kila siku ilimpasa kuleta mnyama asiye na doa mbele ya hema takatifu. Ndipo ilimpasa kumwekea mikono juu ya sadaka hiyo ya mnyama  ili kumtwika dhambi zake zote, kumchinja koo na kutoa damu kwa kuhani ili iweze kuletwa mbele ya Mungu. Kitakachofuata ni kumalizia hatua iliyobaki ili ikamilishe msamaha wa wenye dhambi.
Pasipo sheria na amri za Mungu, watu wasingeweza kujua ikiwa kwamba wana dhambi au la. Tunapojichunguza wenyewe kupitia sheria na amri za Mungu tunagundua kwamba tuna dhambi. Dhambi zetu hazikuhukumiwa kwa viwango vyetu, bali ni kwa sheria na amri za Mungu.
Katika Agano la kale, dhambi zilitwikwa juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi kwa kuwekewa mikono. Na baadaye mwenye dhambi hakuwa tena na dhambi ndipo sadaka hiyo ilipopaswa kuchinjwa na kufa badala ya mwenye dhambi. Mpangilio huo wa utoaji wa sadaka ya dhambi ni kivuli cha hukumu na upendo wa Mungu.
“Kisha atayaondoa mafuta yake yote kama vile mafuta yanayoondolewa katika hizo za amani; kisha kuhani atayateketeza juu ya madhabahu iwe harufu ya kupendeza kwa bwana”  (Walawi 4: 31) mafuta katika biblia yana maana ya Roho Mtakatifu. Hivyo, ili tuweze kupatanishwa kwa dhambi zetu zote yatupasa pia kuchukulia ndani ya moyo wetu upatanisho wa dhambi zetu kwa namna ya Mungu aliyo iweka.
Mungu aliwaeleza wana wa Israel kwamba sadaka ya dhambi katika Agano la kale ilipaswa iwe ni mwana kondoo, au mbuzi au ndama dume. Sadaka hiyo ilichaguliwa kwa uwangalifu mkubwa. Sababu ya sadaka kuwa safi ni kwamba ilipaswa kuonyesha Yesu Kristo ambaye angezaliwa kwa uwezo wa Roho mtakatifu na kuwa sadaka ya dhambi kwa wanadamu wote.
Watu wa Agano la kale walizitwika dhambi zao kwa kuweka mikono juu ya mnyama asiye na doa, kuhani alihudumia kwa sadaka hiyo ili kulipizia dhambi. Hii ndiyo namna ambayo Israel walipatanishwa kwa dhambi.

kifungu kingine kinacho zungumzia mambo hayo ni (Walawi16:21). Hivyo tafakari kwa kina na utaona kwamba bila kuwekea mikono juu ya sadaka husika, damu haitakua na maana yoyote katika kuondoa dhambi. Iliwapasa Israel kuamini katika mambo yote ya sadaka ya dhambi.
SABABU GANI YESU ALIBATIZWA YORDANI?
Hebu sasa natuangalie tukio lile Wakati kuhani mkuu wa mbingu alipokutana na kuhani mkuu wa mwisho wa wanadamu. Hapa tunaweza kuona haki ya Mungu kupitia ubatizo ulio leta upatanisho wa dhambi zote za ulimwengu.
Yohana Mbatizaji aliye mbatiza yesu alikuwa mkuu kati ya wote waliozaliwa na mwanamke. Yesu alimshuhudia Yohana Mbatizaji katika (Mathayo 11:11) “amini nawaambieni, hajaondokea mtu katika uwazao wa mwanamke aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji”. Namna ile dhambi za watu zilivyoweza kufutwa wakati kuhani mkuu Haruni alipoweka mikono juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi katika siku ile ya upatanisho, ndivyo hivyo katika Agano jipya dhambi zote za ulimwengu zilivyoweza kufutwa pia pale Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji.
Injiri ya kuzaliwa upya mara ya pili ni injiri iliyokamilisha ondoleo la dhambi zetu zote za zamani, za sasa na zijazo mbeleni. Hivyo injiri ya ukombozi kupitia ubatizo wa Yesu ilikuwa ni injiri ya Mungu iliyopangiliwa ili kutimiza haki yote, ambayo iliokoa wote duniani. Yesu alibatizwa kwa jinsi iliyostahili ili kupatanisha dhambi za ulimwengu.
Nini maana ya’ haki yote’? (Yohana 3: 13-15) Maana yake ni Mungu kusafisha dhambi zote za ulimwengu kwa njia inayostahili. Yesu alibatizwa ili kutakasa dhambi zote za wanadamu “ kwa maana haki ya Mungu anadhihirishwa ndani yake toka imani hadi imani”(Warumi 1:17). Haki ya Mungu imedhihirishwa katika uwamuzi wa kumtuma mwana wake Yesu hapa duniani ili kutakasa dhambi za ulimwengu kupitia ubatizo wake kwa Yohana Mbatizaji na kwa kifo chake msalabani.
Katika Agano jipya, haki ya Mungu imeelezwa kupitia ubatizo wa Yesu na damu yake. Tunakuwa wenye haki kwasababu Yesu Alibeba dhambi zetu zote katika mto Yordani. Tunapoukubali wokovu huu wa Mungu ndani ya mioyo yetu haki ya Mungu inatimizwa kwa uhakika.
Kila kitu katika Agano la kale kina mwenzake katika Agano jipya kwa Agano la kale “tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake imekusanya” (Isaya 34:16)
Kutimia kwa unabii wa wokovu katika Agano la kale kulihitimishwa kwa njia ya ubatizo wa Yesu katika Agano jipya. Hivyo unabii wa Agano la kale hatimaye ulipata mwenzake katika Agano jipya. Vile watu wa Israel walivyopatanishwa kwa dhambi zao mara moja kwa mwaka katika Agano la kale, ndivyo ilivyo sasa dhambi za watu wote ulimwenguni zilivyo twikwa Yesu na kufutiliwa mbali milele katika Agano jipya.
Ikiwa hukubali na kuamini hili moyoni mwako juu ya huu ukweli wa ubatizo wa Yesu na kifo chake pale msalabani kamwe hautoweza kutakaswa dhambi zako hata kama wewe unaishi maisha ya utakatifu kwa kiwango kikubwa. Yesu alikufa msalabani kwasababu alibeba dhambi zako zote kwa ubatizo wake.
(Warumi 8:3-4) maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwasababu ya mwili, Mungu kwa kumtuma mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio na dhambi aliihukumu dhambi katika mwili, ili maagizo ya tirati yatimizwe ndani yetu sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili bali mambo ya roho.
Kwakuwa sisi ni wanadamu tusioweza kamwe kufuata sheria na amri za Mungu kutokana na udhaifu wa miili yetu, Yesu alibeba dhambi zetu zote juu yake. Huu ni ukweli wa ubatizo wake. Ubatizo wa yesu ulitabili kifo chake pale msalabani. Hii ni hekima Halisi ya injiri ya Mungu.
Ikiwa umekuwa ukiamini kifo cha Yesu pekee, sasa nakusihi ugeuke na ukubali kwa moyo wako wote injiri ya wokovu kupitia ubatizo wa Yesu. 

Jumamosi, 12 Aprili 2014

MWANADAMU HUTENDA DHAMBI KATIKA MAISHA YAKE YOTE


Katika 1Yohana1:10 inasema  “tukisema kwamba hatukutenda dhambi twamfanya yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.Hapajatokea yeyote ambaye hajatenda dhambi mbele ya Mungu. Hata biblia inasema “bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani ambaye afanyaye mema asifanye dhambi(Mhubiri 7:20).Watu wote hutenda dhambi mbele ya Mungu.
Ikiwa mtu yeyote atasema kwamba hajatenda dhambi basi ni muongo. Watu hutenda dhambi maishani mwao pote hadi saa ya mwishoni kabla ya kufa, na hii ndiyo maana Yesu alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi hizo zote. Ikiwa hatujawahi kutenda dhambi basi tusingelihitaji kumwamini Mungu kuwa ni mwokozi. Bwana anasema “neno langu si neno lako” kwa wale wenye fikra wakidhani kuwa hawajatenda dhambi.
Ikiwa mtu hana imani katika injili njema ya maji na Roho basi anastahili kuangamia. Ikiwa mtu mwenye haki au mwenye dhambi atasema kwamba hajatenda dhambi mbele za Mungu, basi huyo hatastahili kuiamini injili njema.
Bwana amempa kila mmoja zawadi nzuri ya injili njema. Tulikiri dhambi zetu zote nakutubu ilikupokea msamaha kwa injili njema. Tunaweza kuirudia injili hii ambayo Mungu aliyo tupatia kama msamaha wa dhambi zetu na kuiamini ili kuweza kuwa na usharika wa Roho Mtakatifu. Maana ya kweli ya usharika wa Roho mtakatifu ipo katika injili ya maji na Roho, na pia kwa wale tu walio na injili hii ndiyo watakao weza kuwa na ushirika na Mungu.
Wanadamu walikuwa mbali na Mungu kwa sababu ya dhambi walizorithi kwa Adamu na Hawa. Lakini leo hii sisi tuliokuwa tumerithi mbegu ya uovu tunaweza kutarajia kuwa na usharika na Mungu kwa mara nyingine tena. Ili kuweza kufanikisha hayo yote ni lazima tuwe na imani ya injili ya maji na Roho toka kwa Yesu Kristo, na hivyo kuwa na msamaha wa dhambi ambazo zilituweka mbali na Mungu.
Wale wote wenyekuamini injili njema ndiyo watakao okolewa kutokana na dhambi zote, na hapo basi Mungu atawajaza Roho Mtakatifu. Wenye haki wataweza kuwa na ushirika na Mungu kwa kuwa wamempokea Roho Mtakatifu. Kwa wale wote waliowekwa mbali na Mungu kutokana na dhambi zao lazima wairudie injilinjema ya maji na Roho na kuiamini na hapo ndipo watakapoweza kuanza kuwa na ushirika na Mungu.
Kuwa na Roho Mtakatifu ndani huja kutokana na imani katika injili njema. Lazima tujue kwamba kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu huja pale tunapoamini injili ya maji na Roho tu. Kuiamini injili njema ndiko kunako jenga njia mpya kumuelekea Mungu. Bwana amevunja ukuta wa kati ulio kuwa ukitutenganisha naye kwa sababu ya dhambi zote mbili, yaani dhambi tuzitendazo maishani na ile dhambi ya asili, na hivyo tutaruhusiwa kuwa na ushirika na Mungu kwa kupitia imani yetu katika injili njema ya maji na Roho.
Yatupasa kuanzisha upya ushirika na Roho Mtakatifu kwa mara nyingine tena. Usharika wa kweli na Roho Mtakatifu hufanikishwa kwa kupita kuelewa injili ya maji na Roho na kutii kwa imani. Ushirika wa Roho Mtakatifu huja pale tunapokuwa na imani ya kweli na msamaha wa dhambi ambao unatokana na injili njema. Wale wote ambao wahajapokea msamaha wa dhambi kamwe hatoweza kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu.

Kwa maneno mengine hakuna yeyote atakaye weza kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu pasipo kuiamini injili ya maji na Roho. Ikiwa bado ni vigumu kwako kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu basi ni lazima kwanza ukubali kwamba bado hajaamini injili ya maji na Roho na hivyo dhambi zako hazijasafishwa. Je, unatamani kuwa na uhusiano na Roho Mtakatifu? Sasa basi amini injili iliyokamilishwa kwa ubatizo wa Yesu na damu yake. Ndipo hapo tu utaweza kusamehewa dhambi zako zote na thawabu yako itakuwa ni kumpokea Roho Mtakatifu ndani ya moyo wako. Injili hii njema kwa hakika ndiyo inayotuletea ushirika na Roho Mtakatifu.

Ijumaa, 11 Aprili 2014

ULIMPOKEA ROHO MTAKATIFU ULIPOAMINI?


(Mtendo 19:1–3)
“Ikiwa Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu alifika Efeso, akakutana na Wanafunzi kadhaa wa kadha huko akawauliza Je, mlimpokea Roho Mtakatifu mlipo amini? Wakajibu la, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. Akawauliza basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema kwa ubatizo wa Yohana.”
Aina gani ya Injili Paulo alihubiri? Alihubiri Injili ya ubatizo wa Yesu na damu yake. Matendo 19:1-2 inasema “Ikiwa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo akiisha kupita kati ya nchi za juu akafika Efeso, akakutana na Wanafunzi kadhaa wa kadha huko akawauliza, Je, mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini?”
Hata hivyo watu hawa walikuwa wamekwisha mwamini Yesu huku wakiwa wameweka kando maana ya ubatizo wa Yesu. Hawakujua juu ya Injili njema ambayo hupelekea kumpokea Roho Mtakatifu ndani. Na hii kupelekea Paulo kuuliza “Je, mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” lilikuwa swali geni kwa baadhi ya wafuasi. Watu wengine wangeliweza kuuliza “Je, una mwamini Yesu?” Lakini Paulo aliuliza swali katika njia isiyokuwa ya kawaida ili kwamba waweze kumpokea Roho Mtakatifu, ndani yao kwa kufanya upya imani zao katika Injili njema. Huduma ya Paulo ilikuwa ni kuhubiri Injili njema ya ubatizo wa Yesu kwa Yohana Mbatizaji. 
Hebu tuone ushuhuda wa Mitume katika Injili ya ubatizo. Kwanza Paulo alishuhudia “Hasha sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?” (Warumi 6:2-3). “Maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo” (Wagalatia 3:27).
 Mtume Petro naye pia alishuhudia Injili ya ubatizo wa Yesu katika 1 Petro 3:21–22 akisema “Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unawaokoa ninyi pia siku hizi (siyo kuweka mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamira safi mbele za Mungu) kwa kufufuka kwake Yesu Kristo. Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.”
Mtume Yohana pia alishuhudia hii Injili njema katika 1 Yohana 5:5-9 “Mwenye kuushinda ulimwenguni ni nani isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni mwana wa Mungu? Huyu ndiye aliye kuja kwa maji na damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye kwa sababu Roho ndiye kweli. Kwa maana wako watatu washuhudiao mbinguni Baba na Neno na Roho Mtakatifu na watatu hawa ni umoja. Kisha wako watatu washuhudiao duniani, Roho na maji na damu na watatu hawa hupatana kwa habari moja”.
Yohana Mbatizaji alichukua nafasi muhimu, katika kukamilisha Injili njema. Biblia inazungumzia yafuatayo juu ya Yohana Mbatizaji katika Malaki 3:1-3 na Mathayo 11:10-11.
Yohana Mbatizaji alikuwa mwakilishi wa wanadamu na alikuwa ni nabii Eliya ajaye kama alivyoandikwa katika Agano la Kale. Katika Agano la Kale, sadaka ya dhambi ilichinjwa ili kumwaga damu baada ya kubeba dhambi za mtu kwa tendo la kuwekewa mikono. Katika Agano Jipya, hata hivyo Yesu ndiye aliyesimama kama sadaka ya dhambi kwa kubeba dhambi ya ulimwengu kwa njia ya ubatizo na kifo chake Msalabani kulipa mshahara wa dhambi. Ubatizo wa Yesu kwa Yohana Mbatizaji pale Yordani ndiyo uliokoa wanadamu wote.
Mungu alipanga aina mbili za matukio ili kuweza kuwaokoa wanadamu tokana na dhambi zao na kuweza kutimiza haki yote. Tukio la kwanza lilikuwa ni kumfanya Yesu aje ulimwenguni kupitia mwili wa mwanamwali Bikira Mariam, na kuwezesha abatizwe na kusulubiwa ili kuondoa dhambi za ulimwengu. Tukio la pili ni kuwepo kwa Yohana Mbatizaji duniani kupitia Elizabeti mama yake. Mungu alisababisha matukio haya mawili yatokee ili wanadamu waweze kuokolewa kwa dhambi zao zote. 
Hii ni kazi ambayo Mungu aliipanga katika utatu. Mungu alimtuma Yohana Mbatizaji ulimwenguni miezi sita kabla ya Yesu, ndipo akatumwa Yesu Kristo mwokozi wa wanadamu hapa duniani kuwaweka huru wanadamu tokana na hukumu ya dhambi zao.
Yesu alishuhudia juu ya Yohana Mbatizaji katika Mathayo 11:9 “Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona Nabii? Naam, nawaambia na aliye mkuu zaidi ya Nabii”. Zaidi ya yote, pale Yohana Mbatizaji aliyemtwika dhambi zote za ulimwengu Yesu, alipo mwona tena siku aliyofuata yeye mwenyewe alishuhudia kwa kusema “Tazama! mwana kondoo aichukuaye dhambi ya ulimwengu” (Yohana 1:29).
Biblia ina taarifa nyingi za Yohana, aliye mbatiza Yesu na inatupasa kupekuwa na kutafuta ili kuweza kuwa na ufahamu mzuri juu yake. Yohana Mbatizaji alikuja ulimwenguni kabla ya
Yesu jukumu lake likiwa kutimiza Injili njema ambayo ndiyo mpango wa Mungu. Biblia inasema kwamba Yesu alikubali dhambi zote za ulimwengu juu yake toka kwaYohana, naye Yohana alimtwika dhambi hizo juu yake ili kutimiza mapenzi ya Mungu.
Tunamwita kuwa ni Yohana Mbatizaji kwa sababu alimbatiza Yesu. Ubatizo wa Yesu una maana gani? Neno “ubatizo” linamaanisha “kuoshwa” kwa kuwa dhambi zote zimekwisha kutwikwa juu ya Yesu kwa kupitia ubatizo wake, hivyo basi zimekwisha kuoshwa. Ubatizo wa Yesu una maana sawa na tendo la “kuwekea mikono” ambalo ile sadaka ya dhambi ilipokea katika Agano la Kale. Maana ya kiroho ya tendo la ubatizo ni “kutwika, kuoshwa au kuzikwa”. Ubatizo wa Yesu kwa Yohana ulikuwa ni tendo la ukombozi katika kuondoa dhambi zote za watu wa ulimwengu.
Ubatizo wa Yesu unaumuhimu sawa kama ilivyo tendo la kuwekea mikono, ambapo ni njia ya kutwika dhambi juu ya sadaka ya dhambi katika Agano la Kale. Kwa maneno mengine,
watu wa Israeli walitwika dhambi zao za mwaka mzima juu ya sadaka ya dhambi katika siku ya Upatanisho kwa kupitia tendo la kuwekea mikono ya kuhani mkuu. Sadaka hii katika Agano la Kale ilikuwa na dhambi sawa na ubatizo wa Yesu na kifo chake msalabani.
Mungu aliiteuwa siku ya Upatanisho kuwa ni muda wa kuondoa dhambi za wana wa Israeli. Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba, kuhani mkuu alitwika dhambi za mwaka za watu wake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi kwa kuwekea mikono juu ya sadaka kwa upatanisho wa dhambi za watu. Na huu ndio mpangilio wa utoaji wa sadaka ambao Mungu aliuweka. Ilikuwa ndio njia pekee katika kutwika dhambi za watu juu ya sadaka ya dhambi na alifanya hivyo kwa tendo la kuwekea mikono ambalo ndiyo sheria ya milele Mungu aliyoweka.
“Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli na makosa yao, naam dhambi zao zote, naye
ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu, naye atamwacha mbuzi jangwani” (Walawi 16:21-22).
Katika Agano la Kale, mwenye dhambi aliweka mikono juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi na kutwika dhambi zake juu yake ili aweze kusamehewa. Na siku ya Upatanisho Haruni Kuhani Mkuu akiwa mwakilishi wa Waisrael wote, aliweka mikono yake juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi ili kutwikwa sadaka hiyo dhambi zote za Waisraeli. Ndipo sadaka hiyo huchinjwa baada ya kubeba dhambi hizo.
Tendo hilo linamaana sawa ya kiroho kwa ubatizo (“Baptisma” ni Kigiriki, maana yake “kusafisha kuzikwa kutwikwa”) ambapo Yesu aliupokea toka kwa Yohana katika Agano Jipya. Kama alivyokuwa Kuhani Mkuu katika Agano la Kale alipoweka mikono yake juu ya sadaka ya dhambi ili kutwika dhambi za watu wa Israel, ndivyo hivyo dhambi zote za wanadamu zilitwikwa juu ya Yesu kupitia ubatizo wake na Yohana Mbatizaji. Ndivyo Yesu alivyokufa Msalabani katika kutupatanisha kwa dhambi zetu.
Hii ni Injili njema. Kama ilivyo Haruni kuhani Mkuu alivyotoa sadaka ya Upatanisho kwa niaba ya watu wa Israeli, Yohana Mbatizaji naye aliye uzao wa Kuhani Haruni alichukua jukumu hilo akiwa mwakilishi wa wanadamu juu yake Yesu. Mungu anaeleza mpango huu ulio mzuri wa ajabu kuhusiana na upendo wake katika Biblia kama ifuatavyo katika kitabu cha Zaburi 50:4-5 “Ataziita mbingu zilizo juu na Nchi pia wahukumu watu wake. Nikusanyieni wacha Mungu wangu waliofanya Agano nami kwa dhabihu” Amen, Haleluyah.
Historia ya Kanisa inasema kwamba hapakuwepo na Krismasi kwa karne mbili za mwanzo katika kuanzishwa kwake. Kanisa la Wakristo wa mwanzo pamoja na Mitume wa Yesu
waliadhimisha January 6 kama “Siku ya Ubatizo wa Yesu” tu, uliofanyika katika mto Yordani na Yohana Mbatizaji. Kwa nini waliweka msisitizo zaidi katika hilo, yaani ubatizo wa Yesu katika imani yao? Jibu lake ndilo ufunguo halisi wa Ukristo wadesturi ya Kitume.
Lakini natumaini hamtochanganya ubatizo wa waumini na ule ubatizo wa Yesu. Ubatizo wa waumini kama ilivyo siku hizi una maana tofauti na ule ubatizo wa Yesu alioupokea katika mto Yordani. Hivyo imetupasa sisi sote kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu kwa kuamini ubatizo wa Yesu Kristo ambao alioupokea toka kwa Yohana na pia damu yake Msalabani. Ikiwa mtazamo wa Kanisa la kwanza uliweka kipaumbele juu ya hili kuwa ndilo Sakramenti muhimu, basi hili kwao waliona ndiyo egemeo la imani katika ubatizo wa Yesu na hivyo hata sisi leo hii tuchukulie ubatizo wa Yesu kwa Yohana kuwa ni sehemu isisyo epukika katika wokovu wetu.
Zaidi ya yote ni lazima tuufikie na kuikumbatia imani iliyo sahihi yenye ufahamu kamili ambayo husema kwamba Yesu ilimbidi asulubiwe kutokana na kubatizwa kwake na Yohana. Imetupasa
kuelewa kwamba Roho Mtakatifu huanza kuweka makazi ndani yetu pale tu tunapoamini ubatizo wa Yesu, kufa kwake msalabani na kufufuka kwake ili awe Mwokozi wetu. Ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani vyote vinamaana ya pakee katika Injili njema.
Njia ya tahadhari kwako katika kumpokea Roho Mtakatifu ni kuamini Injili njema ya ubatizo wa Yesu na damu yake. Ubatizo wa Yesu ulitakasa dhambi zote za wanadamu mara moja. Ulikuwa ni ubatizo wa ukombozi uliopelekea kwetu kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa kuwa baadhi ya watu hawajagundua nguvu iliyomo katika ubatizo wa Yesu, basi wao huelewa hili kuwa ni kama sherehe ya kawaida.
Ubatizo wa Yesu hufanya sehemu muhimu katika Injili njema ambayo hutueleza namna ile Yesu alivyobeba dhambi zote za ulimwengu juu yake na hata kuikubali hukumu yake kwa kumwaga damu yake msalabani. Yeyote anayeamini maneno ya Injili hii iliyo njema hufanywa kuwa msharika wa Kanisa ambalo linamilikiwa na Bwana, na kufurahiya baraka ya Roho Mtakatifu.
Roho Mtakatifu ni karama toka kwa Mungu kwa wale wote waliokwisha kusamehewa dhambi zao. Kwa ubatizo wake, Yesu alikuwa “Mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu” kwa namna iliyotosha (Yohana 1:29). Katika Yohana 1:6-7 inasema “Palitokea mtu
ametumwa kutoka kwa Mungu jina lake Yohana. Huyo alikuja kwa ushuhuda ili ashuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye”. Ili kumwamini Yesu kuwa ni mwokozi wetu aliyechukua
dhambi zetu zote ni lazima tuelewe juu ya huduma ya Yohana na ushuhuda kama ilivyo andikwa katika Biblia. Ndipo tutaweza kumwamini Yesu Kristo kama Mwokozi wetu. Ili kuweza kumpokea Roho Mtakatifu pia tunahitajika kuwa na imani madhubuti iliyoshuhudiwa moyoni.
Hivyo kukamilisha Injili ya kweli iliyo njema ni lazima kuamini ubatizo wa Yesu kwa
Yohana na damu yake pale msalabani. Katika Mathayo 11:12 imeandikwa “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa Ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu na wenye nguvu wauteka”. Kifungu hiki husemekana kuwa ndicho kifungu kigumu kueleweka kati ya vifungu kadha katika Biblia. Hata hivyo imetupasa kuwa makini kwa sehemu isemayo “Tangu siku za Yohana Mbatizaji”. Hakika hapa inatangaza kwamba huduma ya Yohana ilikuwa iimeunganika moja kwa moja na huduma ya Yesu kwa wokovu wetu.
Yesu anatuhitaji tuingie katika Ufalme kwa ujasiri wa imani kama ulivyo ujasiri wa mwenye nguvu. Tunatenda dhambi kila leo, sisi ni dhaifu lakini ameruhusu tuweze kuingia katika Ufalme wake kwa imani, kifua mbele bila ya kujali udhaifu wetu. Hivyo kifungu hiki kina maana kwamba watu wataweza kuuteka Ufalme wa mbingu kwa imani katika Injili njema isemayo kwamba Yesu amefuta dhambi zote za ulimwengu kwa kupitia ubatizo wake kwa Yohana na damu yake msalabani. Kwa maneno mengine ina maana kwamba mbingu inawezwa kutekwa kwa imani madhubuti katika Injili hii njema ya ubatizo wa Yesu na damu yake.
Ubatizo wa Yesu ndiyo uliobeba dhambi zote na imani yetu juu yake hatupa uhakika kwamba tutapokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu. Lazima tuhubiri Injili hii kwa majirani zetu, ndugu zetu, wapendwa wetu na kwa yeyote Yule ulimwenguni. Lazima tuwe na imani katika Injili njema ambayo inasema kwamba dhambi zetu zote ulimwenguni zilitwikwa kwake Yesu kupitia ubatizo wake. Kwa kupitia imani yetu ndipo basi tutaweza kupokea tulizo la ukombozi na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani. Kila mtu ataweza kuwa mwana wa Bwana ambamo ndani yake Roho Mtakatifu atakaa, kuwa moja kati ya kaka na dada kwa kuamini Injili njema ya maji na Roho. Ni lazima muwe na imani sawa katika Injili njema kama aliyokuwa nayo Paulo. Namshukuru Bwana kwa kutupa Injili njema na kumsifu yeye. Ameni.

Jumatatu, 7 Aprili 2014

WATU WA VIPAWA HUTENDA KAZI KWA KUWEKEA MIKONO!


Yatupasa kuwa mbali na imani ya aina hii. Baadhi ya watu siku hizi wanaimani potofu kwamba wataweza kumpokea Roho Mtakatifu ikiwa watawekewa mikono na wale waliokwisha kupokea nguvu hizo. Wao hudhani kwamba kwa kuwa maandiko yanasema kuwa watu wengi walimpokea Roho Mtakatifu waliposhuhudia kuwekewa mikono na Mtume, hivyo nao wataweza kufanya namna hiyo pia. Baadhi yao wanajisingizia kwa imani potofu za aina hii, wanadhani kuwa wataweza kuwapa wengine Roho Mtakatifu kwa kupitia kuwawekea mikono juu yao. Yatupasa kuwa makini na kuwepo kwa watu wa aina hii.
Hata hivyo yatupasa kuweka akilini kwamba imani za watu hawa zinautofauti mkubwa na zile za Mitume wakati wa kipindi cha Kanisa la mwanzo. Siku hizi jambo kuu lenye kuleta ubishani mkali katika imani za baadhi ya Wakristo ni kwasababu hawana imani katika Injili ya kweli ya maji na Roho kati yao. Wengi husema kwamba wanamwamini Mungu lakini hawakumweshimu na hivyo badala yake hujidanganya nafsi zao na zawenzao. Hata hivyo wenye dhambi kamwe hawatowezea kudanganya swala la kumpokea Roho Mtakatifu au hata kufanya wengine wadanganyike. Ikiwa mtu fulani atasema kwamba Roho amekuja juu yake yeye mwenye dhambi basi roho huyo hakuwa ni yule Roho Matakatifu kweli, bali badala yake ni roho wa shetani ajifanyaye kuwa Roho wa kweli.
Mitume wakati wa Kanisa la mwanzo walikuwa ni watu waliomjua na kumuamini Yesu Kristo kuwa ndiye mwokozi aliyechukua dhambi zote za wanadamu kupitia ubatizo wake alioupokea kwa Yohana na kifo chake msalabani. Waliweza kupokea Roho Mtakatifu kwa sababu waliamini ukweli juu ya ubatizo wa Yesu na damu yake pale msalabani. Pia walihubiri Injili ya maji na Roho kwa wengine hivyo kuweza kuwasaidia katika kuwaongoza kumpokea Roho Mtakatifu.
Lakini siku hizi Wakristo wengi wamempokea katika imani za kishabiki. Je ni kweli mwenye dhambi katika nyakati hizi ataweza kumpokea Roho Mtakatifu kupitia kuwekewa mikono
toka kwa mhudumu mwingine aliye na dhambi? Hakika hili halifikiriki. Wapo watu wanaosema kwamba ingawa wanadhambi moyoni, wamempokea Roho Mtakatifu ndani yao.
Hata ikiwa mtu anaonekana ni mchungaji mzuri machoni pa kundi lake kamwe hawawezi kumsababisha yeyote kumpokea Roho Mtakatifu  ikiwa yeye mwenyewe anadhambi moyoni.
Hii ndiyo sababu Manabii wengi wa uongo wameweza kuwaongoza watu kuelekea motoni. Yakupasa uelewe ukweli kwamba wale wote wenye kufundisha aina hii ya imani ni manabii wa uongo. Hawa ni watu ambao tayari wameshikiliwa na mapepo. Ikiwa mtu anadhambi moyoni, je, Roho Mtakatifu ataweza kukaa ndani yake? Jibu ni hapana. Jingine, je, itawezekana kwa mtu aliye na dhambi kuweza kusababisha mtu mwingine aweze kupokea Roho Mtakatifu? Kwa mara nyingine jibu ni hapana. Sasa basi nini kinacho sababisha watu wanao semekana kuwa na vipawa (karismatiki) katika nyakati hizi kuweza kufanya miujiza na maajabu katika ukristo huku wakiwa bado wanadhambi moyoni mwanao? Mapepo au roho chafu hufanya hivyo. Roho Mtakatifu kamwe hawezi kuishi ndani ya mwenye dhambi.
Yeye hukaa ndani ya wale tu walio na imani katika Injili ya maji na Roho. Je? wewe nawe unauhakika roho aliye ndani yako ni Roho Mtakatifu? Katika Yohana 3:5 Yesu alisema “Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia ufalme wa Mungu.” Kwa namna hii basi Roho Mtakatifu kuweka makazi ndani kutawezekana kwa wale tu watakao amini injili ya maji na
Roho. Kosa ambalo wakristo wengi wafanyalo nyakati hizi nikwamba, huamini kwamba mtu ataweza pia kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake kwa kuwekewa mikono na mtumishi
mwenye dhambi. Hili nikosa kubwa na la hatari. Nyakati hizi, wakristo wengi na watumishi wao wanaimani na dhamiri zao kwamba, kuwa na Roho Mtakatifu ndani ya mtu huja kwa kupitia kuwekewa mikono.
Uhusiano kati ya ondoleo la dhambi la kweli na tendo la kuwekea mikono.
“Kuwekea mikono” ni namna ambayo mtu huweza kutwikwa au kutoa kitu alicho nacho juu ya kitu kingine. Kwa mfano, ikiwa tutazungumza katika kipaza sauti, sauti hiyo husafiri kupitia waya toka kipaza sauti na kutokea upande wa pili kwa sauti kubwa zaidi katika spika ili kila mtu aweze kusikia. Ndivyo pia katika Agano la kale pale mwenye dhambi alipoweka mikono yake juu kichwa cha mnyama wa sadaka na hivyo kusamehewa. Kwanjia hiyo pia, nguvu ya Mungu
huwekwa juu ya mtu kwa mtu kwa tendo la kuwekewa mikono toka kwa mtumishi wake. Hivyo tendo la kuwekea mikono limechukua maana ya “kuhamisha, kutwika”.
Watu wanaojiita ni wenye vipawa (wanakarismatiki) hawawezi kamwe kusababisha mtu kuweza kuwa na Roho Mtakatifu ndani yake kwa njia ya kuwekea mikono, badala yake kusababisha watu hao kupokea roho chafu. Lazima ukumbuke kwamba mtu aliye na nguvu za roho chafu huamisha roho hizo kwa wengine kupitia tendo la kuwekea mikono. Mtu aliye tawaliwa na mapepo anapoweka mikono juu ya kichwa cha mwingine, pepo lililomo ndani yake huingia ndani ya mtu huyo kwa sababu shetani hutenda kazi kupitia wenye dhambi.
Kwasababu hiyo basi kila mtu imemlazimu kuamini injili ya maji na Roho ikiwa anataka kupokea Roho Mtakatifu ndani yake. Shetani hutawala wale wote walio na dhambi hata ikiwa
wanamwamini Yesu, huku wakiwa wameshindwa kupokea ondoleo la dhambi.
Ikiwa mtu atapokea tendo la kuwekewa mikono toka kwa mtu aliye na mapepo, mapepo hayo yatahamia juu yake mtu huyo, hivyo naye pia moja kwa moja ataweza kufanya miujiza ya uongo. Yatupasa kujua kwamba mapepo huja na kufanya makazi ndani ya mtu kwa kupitia tendo la kuwekewa mikono.
Na kumpokea Roho Mtakatifu ndani huwezakana tu kwa imani katika injili ya maji na Roho.
Tendo la kuwekea mikono ni njia mahususi iliyo wekwa na Mungu katika kutwika kitu juu ya kingine. Lakini shetani husababisha watu wengi kupokea roho chafu kwa kupitia tendo hilo. Ukweli ni kwamba watu wengi nyakati hizi hujaribu kununua nguvu za Roho Mtakatifu kwa fedha na hivyo kufanya tatizo hili kuwa kubwa zaidi.
Wakristo wengi wanaufahamu wa kimakosa juu ya ukweli wa kuwa na Roho Mtakatifu ndani. Tulipouliza kwa namna gani wataweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yao, wengi wa watu
hujibu kwamba inawezekana kwa kupitia sala za toba na kufunga. Hili si kweli kabisa. Je, nikweli Roho Mtakatifu huja juu yako pale unapo fanya maombi maalumu kwa Mungu?
Hapana kuweza kuwa na Roho Mtakatifu ndani yako huja kwa wale tu wanao amini injili ya maji na Roho. Kwa kuwa Mungu ni kweli ameweka sheria kwa ajili ya kuweza kupokea Roho Mtakatifu ndani. Je, Roho Mtakatifu ataweza kuwa ndani ya mtu aliye na dhambi moyoni? Jibu bila shaka hapana. Mtu hawezi kumpokea Roho Mtakatifu kupitia tendo la kuwekewa mikono. Hata ikiwa mtu atahudhuria mikutano ya uamsho na maombi ya uchungu kwa Mungu ili aweze kupokea nguvu ya Roho Mtakatifu, Roho Mtakatifu atabaki kuwa mbali naye. Wenye dhambi hakika hawatoweza kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yao. Wenye dhambi wataweza kupokea kipawa hicho cha Roho Mtakatifu ikiwa tu watapokea ondoleo la dhambi kwa kuamini Injili ya maji na Roho.
Yeyote asiyefahamu injili ya maji na Roho, kamwe hatoweza kumpokea Roho Mtakatifu. Siku hizi injili ya maji na Roho imeenea kwa kasi kupitia vitabu, mikutano ya makanisa, tovuti na hata vitabu vya kielectronikali ulimwenguni pote. Hivyo, yeyote anayetafuta ukweli wa injili, ataweza kuamini hili na kuweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake. Ikiwa bado hujampokea, yakupasa uelewe kwamba ili uweze kumpokea ni lazima uamini injili ya maji na Roho.

JE, INAWEZEKANA MTU KUMNUNUA ROHO MTAKATIFU KWA UWEZO WAKE?


(Metendo 8:14–24 )
“Na Mitume waliokuwako Yesuramu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu wakawaombea wampokee Roho Makatifu kwa maana bado hawajawashukia
hata mmoja wao ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu. Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu. Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya Mitume akataka kuwapa fedha akisema, nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakaye mwekea mikono yangu apokee Roho Mtakatifu. Lakini Petro akamwambia fedha na ipotelee mbali pamoja nawe kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu. Basi, tubia uovu wako huu ukamwombe Bwana ili kama yamkini usamehewe fikira hii ya moyo wako. Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu. Simon akajibu akasema, niombeeni ninyi kwa Bwana yasinifike mambo haya mliosema hata moja.”

Husika na somo kuu katika kifungu hiki, napenda kuleta ujumbe huu iwapo “mtu anaweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake kwa kupitia juhudi binafsi”. Mitume katika nyakati
hizo za Kanisa la kwanza waliweza kupokea nguvu toka kwa Mungu na kutumwa sehemu kadhaa naye. Yapo matendo ya miujiza kadhaa katika Kitabu cha Matendo, mojawapo likiwa
kushuka kwa Roho Mtakatifu juu ya waumini pale Mitume walipowawekea mikono. Biblia inasema “Mitume walipowawekea mikono wale ambao hawakuwa wamempokea
Roho Mtakatifu ingawa walikwisha mwamini Yesu, walipokea Roho Mtakatifu.”

Sasa basi, ni kwa namna gani walimpokea Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono? Kwa wakati huo maneno ya Mungu bado yalikuwa yakiendelea kuandikwa na hivyo basi kazi ilikuwa bado haijakamilika hivyo Mungu aliwapa Mitume nguvu za pekee kuweza kufanya kazi zake. Alikuwa pamoja na Mitume na kuweza kuleta miujiza mingi na maajabu kupitia kwao. Kilikuwa ni kipindi pekee, wakati Mungu alipofanya maajabu na miujiza ambayo iliweza kuonekana kwa macho ya wanadamu ili kuweza kuwafanya watu waweze kumwamini Yesu Kristo kuwa kweli ni mwana wa Mungu na ndiye mwokozi. Palikuwepo na umuhimu kwa Mungu pamoja na
Mitume kwa nguvu za ajabu kuweza kuonyesha kazi ya Roho Mtakatifu ili kuthibitisha kwamba Yesu Kristo ndiye Mungu na kwamba ndiye Mwana wa Mungu Mwokozi. Ikiwa Roho Mtakatifu asingefanya kazi kupitia miujiza na maajabu kwa nyakati hizo za kanisa la kwanza hakika pasingekuwepo na yeyote awezaye kumwamini Yesu kuwa ni Mwokozi.

Hata hivyo hakuna umuhimu tena kwetu sisi leo hii kumpokea Roho Mtakatifu kupitia miujiza na maajabu ya kuonekana kwa macho ya kawaida kwa sababu Biblia imekamilika. Badala yake sasa, kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu kunategemea imani zetu zaidi. Kwa maneno mengine ni kuamini Injili ya kweli. Mungu ametupatia Roho Mtakatifu awe ndani yetu kwa wale tu watakao kuwa na imani ya Injili ya kweli mbele ya Mungu. Kuwa na Roho Mtakatifu ndani hutokea kwa wale tu wanao amini maneno ya Mungu kama ilivyo timia kwa kuja kwake Yesu hapa ulimwenguni na kwa ubatizo wake na damu yake.

Nyakati hizi wachungaji wengi hufundisha waumini wao kwamba matendo yasiyo ya kawaida yawezayo kuonekana kwa macho ndiyo ishara tosha ya kuwa na Roho Mtakatifu. Hivyo
kuwaongoza waumini kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia hiyo. Huwapotosha watu kwa kuwapa mafundisho ya uongo kama yale ya kunena kwa lugha kuwa ndiyo ishara ya kushukiwa na Roho
Mtakatifu. Wachungaji hawa hujiona kuwa wao ndiyo mitume watendao miujiza na maajabu makuu na hivyo kuvutia washabiki wa kidini ambao hutaka kumjua Mungu kwa hisia zao.

Ushabiki huu umeenea kwa Wakristo walio wengi duniani pote na wengi wao hufuata imani hizo na hatimaye kupatwa na roho za kishetani kwa kupitia njia za nguvu za giza. Hata leo, watu hao waliokumbwa na ushabiki wa aina hii hudhani kuwa nao wataweza kuwafanya wenzao kuweza kumpokea Roho Mtakatifu kupitia kuwekewa mikono.

Hata hivyo kwa jinsi Simoni alivyo potoka, nao huwa kama wachawi wanaonekana katika kifungu hicho. Wameharibiwa kwa kujikonga nafsi zao na tamaa ya mwili lakini matendo yao
yote huleta tafrani katikati ya watu. Aina hii ya mafundisho ya uongo hupindisha njia ya kweli katika kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu mbele ya Mungu.

Hata leo, wengi wa mitume waongo hufanya kazi za ibilisi kupitia mambo yasiyo sahihi ya kidini, wakijifanya kutenda kazi za Roho Mtakatifu. Wakristo walio wa kweli ni lazima
walishike neno la Mungu ambalo ndiyo ufahamu pekee wa kuweza kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani. Wale wote wanaojifanya kuwa ni Wapentekoste, ambao husisitizia mwonekano wa nje kimwili nilazima waache imani hizi potofu wayarejee maneno ya Mungu na kuamini ukweli ambao kwa hakika utawaongoza katika kumpokea Roho Mtakatifu ndani yao.

Simoni alikuwa mchawi maarufu Samaria katika nyakati hizo. Baada ya kuwaona mitume wa Yesu wakisababisha watu kumpokea Roho Mtakatifu, alitamani kumnunua Roho Mtakatifu kwa fedha. Watu wa imani ya aina hii bila shaka huishia kuwa watumwa wa ibilisi wakitumiwa kutenda kazi zake. Simoni alitaka kumpokea Roho Mtakatifu lakini tama zake zilikuwa si nyingine bali ni kujipatia kipato binafsi.

Tunaweza kuona aina hii ya imani siyo yakupelekea kumpokea Roho. Simoni alijaribu kumnunua Roho Mtakatifu kwa fedha kwasababu ya uchoyo ulio tokana na kutamani nguvu za Roho Mtakatifu. Alikemewa vikali na mtumishi wa Mungu Petro. Ingawa ilisemekana kwamba Simoni alikuwa akimwamini Yesu hakuwa ni mtu kamwe aliyekuwa amempokea Roho Mtakatifu kupitia ondoleo la dhambi. Kwa maneno mengine yeye alidhani
ya kwamba angeweza kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yake kwa kutoa mali za kidunia kwa Mungu.

Ingawa muonekano wake wa nje ulionyesha kwamba alikuwa akimwamini Yesu, mawazo yake halisi ndani yalikuwa hayawiani na maneno ya Yesu. Badala yake alijawa na tamaa za kimwili. Petro aliye yagundua mawazo ya Simoni alimkemea kwa kuwa alijaribu kutaka kumpokea Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi ya Mungu kwa fedha. Alimtaadharisha Simoni kwamba angeweza kuangamia na fedha hizo zake.

Nyakati hizi mitume waongo walio tawaliwa na roho za ibilisi hunena kwa kuwalaghai watu kwa kuwafanya kudhani kwamba miujiza na maajabu yote ni kazi za Roho Mtakatifu. Tunaweza kuona mara nyingi watu wakifurahia aina hizi za nguvu na kuomba kwa dhati nao waweze kumpokea Roho Mtakatifu. Hata hivyo mtu imempasa kuwa makini kwamba hapana yeyote utakaye mpokea Roho Mtaktifu ndani yake kupitia maombi yaliyo na tamaa za kidunia.
Je, wapo pia watu wa uamsho wa vipawa (karismatiki) kati yako kwa nafasi yoyote? Imekupasa uwe mwangalifu dhidi ya watu wa aina hii.

Huwafata watu kwa imani hizi za mashamshamu na kishabiki. Husema kwamba wanaweza
kukemea mapepo na hata kuweza kuwafanya watu kumpokea Roho Mtakatifu kupitia kuwawekea mikono. Hata hivyo watu hawa huwa na nguvu ambazo si za Roho Mtakatifu bali ni
nguvu za pepo wachafu. Wale wanaodai kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia ya kuwekewa mikono hujiongoza wao binafsi na wengie katika kumpokea roho chafu.

Kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu huja kwa sisi wote tu, tunaoamini maneno ya maji na Roho (1 Yohana 5:3-7). Ingawa injili ya maji na Roho imeandikwa kwa uwazi katika Biblia, bado watu walio wengi hudhani mioyoni mwao kwamba wataweza jaribu kumfikia Mungu kwa kupitia nguvu za miujiza na kwa hali za kupumbaza, kunena kwa lugha, maono na kukemea pepo. Na ndiyo maana manabii waongo wameweza kuwadanganya watu wengi katika kuamini mazingaombwe ya Kikristo yatokanayo na ibilisi mwovu.


Petro alimkemea Simoni kwa kumwambia, “Fedha yako na ipotee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili. Basi tubia uovu wako huu ukamwombe Bwana ili kama yamkini usamehewe fikra hii ya moyo wako. Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo na tena u katika kifungo cha uovu.” Yatupasa kujawa na simanzi kwa sababu leo hii wapo watumishi wa aina hii. Wengi wao ni wale wajiitao wenye vipawa au wakarismatiki. Hudai fedha kwa makundi yao. Tuwe mbali sana nao na watu wa imani hizi na tumpokee Roho Mtakatifu ndani yetu kwa Injili ya kweli katika maji na Roho (Mathayo 3:15, 1 Petro 3:21, Yohana 1:29, Yohana 19:21-23).