Ijumaa, 14 Machi 2014

PAZIA LA HEKALU LILILOPASUKA WAKATI YESU ANAKUFA.


( Mathayo 27: 50-53) “Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake. Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka; makabuli yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.”
Patakatifu pa patakatifu palikuwa ni mahali ambapo Mungu aliishi. Na ni kuhani mkuu tu ndiye aliye ruhusiwa kuingia hapo mara moja kwa mwaka, katika ile siku ya Upatanisho hali akiwa amebeba damu ya mbuzi wa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya ondoleo la dhambi la Waisraeli. Kuhani mkuu alifanya hivyo kwa sababu Patakatifu pa patakatifu katika Hema Takatifu la kukutania Palikuwa ni mahali patakatifu sana ambapo hawakuweza kuingia mpaka awe na damu ya mwanasadaka, ambaye kwa huyo mikono iliwekwa juu ya kichwa chake ili kuyatowesha mbali maovu ya wenye dhambi. Kwa msemo tofauti, hata kuhani mkuu hakuweza kuikwepa adhabu ya Mungu hadi baada ya kuwa amepokea ondoleo la dhambi zake kwa kutoa sadaka ya kuteketezwa kabla ya kuingia katika uwepo wa Mungu.
Je, ni lini pazia la Hekalu lilipasuka? Lilipasuka wakatiYesu alipoimwaga damu yake na kufa Msalabani. Kwa nini ilimpasa Yesu kumwaga damu yake Msalabani na kisha kufa? Kwa sababu Yesu mwana wa Mungu kwa kuja kwake hapa duniani katika mwili wa mwanadamu alikuwa ameyachukuwa katika mwili wake maovu yote ya wenye dhambi kwa kubatizwa na Yohana katika mto Yordani. Kwa sababu Yesu alikuwa amezichukuwa katika mwili wake dhambi zote za ulimwengu kwa kupitia ubatizo wake, basi Yesu aliweza kuzimaliza adhabu zote za dhambi ikiwa tu angeliimwaga damu yake na kisha kufa msalabani. Hii ndiyo sababu lile pazia lililokuwa likitenganisha kati ya mahali  patakatifu na Patakatifu pa patakatifu lilipasuka toka juu mpaka chini. Hii inamaanisha kuwa ule ukuta wa dhambi ambao ulimtenganisha Mungu na mwanadamu ulikuwa umeanguka chini mara moja na daima.
Kwa maneno mengine, kupitia ubatizo ambao Yesu aliupokea  na damu yake aliyoimwaga Msalabani, Yesu amezifanya dhambi zote kutoweka. Kwa ubatizo na damu ya Yesu Kristo, Mungu baba amezitowesha mbali dhambi zetu zote mara moja na kwa wote na ameufungua mlango wa Mbinguni, ili kwamba mtu yeyote aweze kuingia Mbinguni kwa kuamini katika ubatizo huu na damu ya Yesu iliyomwaguka.
Wakati Yesu alipokuwa msalabani, giza lilifunika pale alipokuwepo kwa masaa matatu. Baada ya kuwa amezibeba dhambi zote za ulimwengu kwa kupitia ubatizo wake katika mto Yordani, Yesu alisulubiwa na karibu na kifo chake alilia, “Eloi, Eloi, lama sabaktani?” maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” (Mathayo 27:46). Kisha akisema neno lake la mwisho, “Imekwisha!” kisha akafa, na baada ya siku tatu akafufuka kena toka kwa wafu, akabeba ushuhuda kwa siku 40, na kisha akapaa Mbinguni mbele ya macho ya wanafunzi wake na wafuasi wake wengi.
Je, ni kweli kuwa Baba alikuwa amemwacha Yesu?
Kwa sababu Yesu alikuwa amezichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana, Yesu alikuwa ameachwa kwa muda na Baba pale alipokuwa amezibeba adhabu ya dhambi Msalabani. Mungu Baba alipaswa kumuadhibu mtu yeyote ambaye alikuwa na dhambi, na kwa sababu dhambi zote za ulimwengu zilikuwa zimepitishwa kwa Yesu, basi Yesu alipaswa kuraruliwa na kisha kuimwaga damu yake msalabani kama adhabu ya dhambi hizi.
Kwa sababu Yesu ni Mungu mwenyewe katika uwepo wake alikuwa amezichukuwa dhambi zote za wanadamu katika mwili wake kwa kubatizwa, basi dhambi za ulimwengu zilikuwa zimehamishwa katika mwili wake Mtakatifu. Kwa hiyo, alipaswa kuachwa na Mungu Baba kwa kitambo tu, kuteseka hadi kifo Msalabani ili kulipa mshahara wa dhambi zote.
Kama ambavyo unafahamu, baada ya kujengwa kwa Hekalu katika utawala wa mfalume Sulemani, basi nafasi ya Hema Takatifu la Kukutania ilichukuliwa na Hekalu. Lakini msingi wa utaratibu wa Hema Takatifu la kukutania iliendelea kutumika katika Hekalu kama ambavyo ilikuwa ikitumika katika Hema takatifu  la kukutania kabla Hekalu halijajengwa . kwa hiyo, kulikuwa na pazia ambalo lilitenganisha kati ya mahali patakatifu na Patakatifu pa patakatifu katika hekalu. Na wakati ule ule Bwana alipopiga kelele Msalabani, “Eloi, Eloi, Eloi, lama sabaktani?” pazia hili la Hekalu lilipasuka toka juu hadi chini. Ukweli unaozungumziwa na tukio hili ni kuwa kwa sababu Bwana amezioshelea mbali dhambi zetu kwa ubatizo ambao aliopokea na kwa damu ya thamani ambayo aliimwaga Msalabani, basi sasa lango la Mbinguni limefunguliwa ili kwamba wote wanaoamini waweze kuingia. Sasa kwa kuamini katika Injili ya maji na Roho, sisi sote tunaweza kuingia Mbinguni kwa imani.
Ule ukweli kuwa pazia la Hekalu lilipasuka toka juu hadi chini wakati Yesu alipokufa Msalabani unatufundisha sisi ukweli kwamba katika kipindi hiki, wale wote ambao wamesafishwa toka katika dhambi kwa kuamini injili ya maji na Roho na damu wanaweza kuingia Mbinguni. Kulikuwa na ukuta wa dhambi ambao ulikuwa umetutenganisha uliokuwa ukituzuia sisi kuja mbele za Mungu, lakini kwa ubatizo na damu yake, Yesu ameufanya huu ukuta wa dhambi kupotea mara moja na kwa wote. Kule kusema kuwa Muungu alilipasua pazia la Hekalu toka juu hadi chini kunamaanisha kuwa yeyote anayeamini katika ubatizo ambao kwa huo mwana wa Mungu aliyachukuwa katika mwili wake maovu yote ya wenye dhambi na katika damu ya msalaba anaweza kusafishwa dhambi zake kikamilifu na kisha kuingia Mbinguni. Mungu ametuokoa sisi toka katika dhambi kwa namna hii.
Yesu alilipasua pazia la Hekalu toka juu hadi chini kuwa ushuhuda wa kazi hizi za wokovu ambazo alizitimiza. Kwa hiyo (Waebrania 10:19-22) inasema “Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani mwili wake; na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu: na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamira mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi.”
Wakati Yesu alipokufa msalabani, mlango wa kuingilia Patakatifu pa patakatifu ulifunguliwa kwa kuwa pazia lake lilipasuliwa, na huu mlango ulifunguliwa wa Patakatifu pa patakatifu ni neno la Mungu la Injili ambalo limefungua njia mpya na iliyo hai ya kwenda Mbinguni. Hapa, Biblia inatueleza sisi kuwa dhambi zote za mioyo yetu na miili yetu zilitoweshwa mbali kwa kupitia ubatizo wake (maji safi) na damu yake, na kwa hiyo tunaweza kusafishwa kwa uhakika wa imani katika wokovu wake mkamilifu.

Ni lazima kuwepo na “utimilifu wa imani” kama ilivyo andika hapo juu, imani yoyote ambayo inaamini katika mambo mawili tu, kwa mfano damu na Roho Mtakatifu haijakamilika. Kujua kanini nasema hivi soma “Injili ya maji na roho” katika blog hii. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni