Ijumaa, 7 Machi 2014

MADHABAHU YA SADAKA YA KUTEKETEZWA.


(Kutoka 27: 1-8) “Nawe fanya madhabahu ya mshita; urefu wake utakuwa ni dhiraa tano; hivyo madhabahu itakuwa mraba; na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu. Nawe fanya pembe nne; hizo pembe zitakuwa za kitu kimoja na madhabahu; nawe utayafunika shaba. Na vyombo vyake vya kuyaondoa majivu yake utavifanya, na majembe yake, na mabakuli yake, na uma zake, na meko yake; vyombo vyake vyote utavifanya vya shaba. Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba; kisha utie pete nne za shaba katika hizo pembe nne za ule wavu. Nawe tia huo wavu chini ya kizigo kiizungukacho madhabahu upande wa chini, ili huo wavu ufikilie katikati ya hiyo madhabahu, miti ya mshita, na kuifunika shaba. Na hiyo miti itatiwa katika pete, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukuwa. Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake; kama ilivyoonyeshwa mlimani, ndiyo watakavyoifanya.”
Tujadili juu ya imani inayodhihirishwa katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa. Wakati watu wa Israeli walipovunja mojawapo ya kanuni 613 za sheria ya Mungu na maagizo yake ambayo walipaswa kuyatii katika maisha yao ya kila siku, na walipozitambua dhambi zao walimtolea Mungu sadaka isiyo na mawaa kwa mujibu wa utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa  uliowekwa na Mungu. Mahali walipozitolea sadaka hizi ni katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa maneno mengine, watu wa Israeli, walipokea ondoleo lao la dhambi kwa kuwekea mikono yao katika kichwa cha mnyama wa sadaka asiye na mawaa, na kwa kukata koo la mnyama na kuikinga damu yake, na kuiweka damu hiyo katika pembe za madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kisha kuimimina ardhini damu iliyosalia, na hatimaye kumchoma mnyama huyo katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
Maana ya kiroho ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa .
Wakati Waisraeli walipoiangalia madhabahu hii ya sadaka ya kuteketezwa, ndipo walipotambua kuwa wao walikuwa wamefungwa katika kifungo cha hukumu (Shaba) na adhabu na kuwa wasingeweza kuikwepa hukumu yao. Na kama ambavyo mnyama wa sadaka ya kuteketezwa alivyouawa, ndipo walipotambua kuwa, hata wao walistahili kufa kwa sababu ya dhambi zao. Pia waliamini kuwa masihi atakuja hapa duniani na atazitowesha dhambi zao kwa kuwadhibiwa na kuuawa kama ilivyokuwa kwa mnyama wa sadaka ya kuteketezwa kwa sababu ya dhambi zao.
Madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa ilikuwa ni kivuli cha Yesu Kristo Mwokozi wetu. Kama ambavyo wanyama wasio na mawaa walivyouawa kwa kuwekewa mikono na kisha kumwaga damu yao, Yesu Kristo  alikuja kwetu kama Mwana wa Mungu na akabeba adhabu ya dhambi zetu zote. Kama ambavyo sadaka ya kuteketezwa ya Agano la kale alivyopokea dhambi zote kwa kuwekewa mikono na kumwaga damu, Yesu alizipokea dhambi zote za ulimwengu zilizopelekwa kwake  kwa kubatizwa na Yohana, na akabeba adhabu ya dhambi hizi kwa kuimwaga damu yake msalabani.
Kwa njia hii, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa inatuonyesha sisi kuwa Yesu Kristo alizichukuwa dhambi zetu akafufuka toka kwa wafu, na kwa hiyo ametuokoa sisi.
Vyombo vyote vya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa vilitengenezwa kwa Shaba
Vyombo vya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa vilivyotumika kuweka na kuondoa majivu vyote vilitengenezwa kwa shaba. Madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa yenyewe ilitengenezwa kwa mti wa mshita na kisha ikafunikwa kwa shaba, na kwa hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote vilitengenezwa kwa Shaba.
Shaba hii ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa ina maana kamili ya kiroho. Shaba inamaanisha hukumu ya dhambi mbele za Mungu. Kwa hiyo, madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa ni mahali panapotuonyesha vizuri kwamba wenye dhambi kwa hakika watahukumiwa kwa dhambi zao. Kwa hakika, Mungu atawaadhibu kwa dhambi zao pasipo kushindwa. Madhabahu hii ya sadaka ya kuteketezwa ni mahali ambapo wnyama wa sadaka ya kuteketezwa walihukumiwa kwa ajili ya wenye dhambi kwa kuteketezwa, madhabahu hii na Vyombo vyake vyote vilitengenezwa kwa shaba; kwa hiyo, vitu hivi vinatueleza sisi kuwa kwa hakika kila dhambi inahusisha hukumu yake.
Madhabahu inatuonyesha sisi kuwa kwa sababu ya dhambi zao, watu wamefungwa kuwadhibiwa na kisha kuuawa, lakini kwa kuwaleta wanyama wao wa kuteketezwa katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kumpatia Mungu, wanaweza kuoshwa dhambi zao, kupokea ondoleo la dhambi, na kisha kuishi tena kwa upya.  Hapa, sadaka zilizoteketezwa katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa vyote vinatueleza kuwa ubatizo wa Yesu Kristo na kule kuimwaga damu yake kumezisamehe dhambi za waamini. Kwa hiyo, imani hii iliyotoa sadaka ya kuteketezwa katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa inaendelezwa katika kipindi cha Agano jipya kama imani katika ubatizo na damu ya Yesu Kristo.
Tunapomwamini Yesu Kristo kuwa ni mwokozi wetu, ni lazima tumpe Mungu imani Yetu inayoamini katika ubatizo na damu ya Yesu kama ondoleo la dhambi zetu zote. Katika Agano la kale, imani hii inahusianishwa na imani inayofungua na kuingia katika lango la ua wa Hema takatifu la kukutania lililokuwa limefumwa kwa nyuzi za bluu,zambarau, na nyekundu, na kitani safi ya kusokotwa.
Sadaka zote ambazo ziliteketezwa katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa ni kivuli cha Yesu Kristo.
Yesu Kristo alifanya nini alipokuja hapa duniani? Tulikuwa wenye dhmbi; tulikuwa tumetenda dhambi kinyume na Mungu na Tulikuwa tumevunja sheria na maagizo yake. Lakini ili kuzitowesha dhambi zetu, Yesu Kristo alibatizwa na Yohana na alichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake, na kwa hiyo akamwaga damu yake msalabani. Bwana wetu alibeba hukumu ya adhabu kwa dhambi zetu zote ili sisi tusiadhibiwe kwa dhambi zetu. Kwa hiyo, ametuokoa toka katika dhambi zetu zote na adhabu.
Pia kuna maana nyingine ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, ambayo ni “kupaa.” Kusema kweli, wewe na mimi tunatenda dhambi kila siku. Kwa hiyo, inatulazimu kutoa sadaka zetu za kuteketezwa kila wakati mbele za Mungu, na kwa sababu ya hali hii, moshi wa adhabu ya dhambi zetu kila siku unapaa kwenda kwa Mungu. Je, kuna siku yoyote ambayo hautendi dhambi bali unaishi kikamilifu? Sadaka ya kuteketezwa ya watu wa Israeli ilitolewa kila siku hadi pale makuhani walipochoka kuzitoa hizi ambazo zilileteleza msamaha wa dhambi za Waisraeli wengi. Kwa sababu watu wa Israeli walivunja sheria na wakafanya dhambi kinyume na Mungu kila siku, vivyo hivyo walipaswa kutoa sadaka zao za kuteketezwa kila siku.
Musa, akiwakilisha taifa la Israeli, alizitamka kanuni 613 za sheria na amri za mungu kwa Waisraeli; “sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika Agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kiliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu. Nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Hayo ndiyo maneno utakayowaambia wana wa Israeli” (kutoka 19:5-6).
Kisha watu wa Israeli wakaahidi, “hayo yote aliyoyasema BWANA tutayashika” (kutoka 19:8). Hivyo watu wa Israeli walitaka kumtambua na kumwamini huyu Mungu aliyemtokea Musa na akaongea nao kwa kupitia Musa kama Mungu wao Halisi, na walitaka Mungu huyu awalinde.  Kwa hiyo, walijitahidi kuzituza amri zote za Mungu ambazo aliwapatia.

Je, Mungu alifahamu mapema kuwa Waisraeli watatenda dhambi? Kwa kweli alifahamu. Hii ndiyo sababu Mungu alimwita Musa katika mlima Sinai, akamwonyesha Hema Takatifu la kukutania katika maono, akamweleza juu ya muundo wake wa kina, na kisha akamfanya Musa kulijenga kama alivyo mwamuru. Pia akaanzisha utaratibu wa sadaka ya kuteketezwa ambao kwa huo sadaka zilipaswa kutolewa katika hili Hema Takatifu la kukutania.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni