Tukiangalia Biblia tunaweza kuona vipawa vya Roho mtakatifu
vinatajwa sehemu tofauti tofauti. Vipawa hivi vinawakilishwa na warumi 12:6-8,
1 wakorintho 12:8-10 na waefeso 4:11. lakini leo hebu tuangalie vipawa tisa
vilivyotajwa katika 1wakorintho 12.
1) Kipawa cha Neno la ufahamu. Huu ni ufahamu wa siri ya
Injili ya maji na Roho iliyofichika kulingana na uvuvio wa Mungu, katika
maandiko ya Biblia yenye nguvu ya Roho mtakatifu. Uwezo wa kueleza na kueneza
Injili hii ya maji na Roho hii kipawa cha Neno la ufahamu.
2) Kipawa cha Neno la Busara. Kipawa cha neno la busara
haina maana ya busara ya kibinadamu kama vile akili na utambuzi. Kipawa hiki
cha kile cha kutatua matatizo mbalimbali yaletwayo na wanadamu katika kueleza
neno la Biblia kwa imani.
3) Kipawa cha Imani. Kipawa cha Imani ni ile hali ya
kuonyesha imani ya matendo katika Neno. Kipawa hiki hutolewa pale tunapolisikia
neno la Mungu na tunapoliamini neno hili kwa imani thabiti. Roho mtakatifu
anafanya kazi ili imani yetu ikue ndani ya mioyo yenu. Kwa kipawa hiki, Mungu
anatuwezesha kuziokoa Roho za watu kutoka katika dhambi zao.
4) Kipawa cha Uponyaji: Badala ya kujaribu kuponya magonjwa
ya mwilini, mitume lazima watambue kuwa Mungu anawataka watambue mapenzi ya
Mungu kupitia madhaifu yao ya mwilini. Anataka wajue ukuu wa Mungu kupitia
magonjwa walio nayo, yeye anaangalia uponyaji wa kiroho zaidi kwanza kuliko
yale ya kimwili. Mungu anatushauri kuwaombea wagonjwa (James 5:14-15) na sala
hizi ni zile ambazo kila mtakatifu anaweza kusema.
5) Kipawa cha kutenda miujiza. Hii ni ile nguvu ya imani
inayoamini na kufuata neno la Mungu miujiza inalenga imani inayoamini neno la
Mungu linalotengua sheria ya asili ya Imani ambazo zinafahamika Imani hiyo ya
mitume inajenga nguvu katika imani zetu na kutuwezesha kuzaa matunda zaidi.
Mungu anawafanya mitume watende kwa imani.
6) Kipawa cha Unabii. Hii ni kuamini neno la Mungu na
kulieneza kwa niaba yake. Tangu Agano la kale hata jipya Mungu ametufunulia
mapenzi yake na mipango. Hivyo manabii wa kweli ndio wanaoweza kuthibitisha
usahihi au makosa ya wengine katika maandiko ya neno la Mungu. Kwa hiyo wale
wasioeneza neno la Mungu lililoandikwa katika maandiko kwa imani za manabii wa
uwongo. Unabii sahihi ni kueneza neno la Mungu kwa imani. Kwa kuwahubiria watu
neno la Mungu mitume na watumishi wa Mungu ni lazima wawawezeshe kumwabudu
Mungu, kufariji na kuhimizana. Yesu kristo ametoa pamoja na mwili wake, kanisa,
kipawa cha imani inayoamini neno la watumishi wa Mungu.
7) Kipawa cha kupambanua Roho. Kupambanua Roho ni kipawa au
uwezo wa kutambua kama watu wamepokea ondoleo la dhambi au tu wamesikia
kinachosemwa. Kwetu sisi tunaoishi nyakati hizi za mwisho, kama hatuna kipawa
hiki, tunadanganywa na shetani (1 Timotheo 4:1) na kipawa hiki, tunaweza
kuwatambua wale wanaotafuta na kufuata vipawa vya Roho mtakatifu, na kuweza
kutofautisha kati ya aliyezaliwa upya na yule ambae hajapokea ondoleo la dhambi
na Roho mtakatifu.
8) Kipawa cha kunena kwa lugha. Inaposemwa kuwa mitume
wanaongea kuwa lugha ina maana wanaongea ukweli juu ya ufalme wa mbinguni.
Mitume wanapomwomba Mungu,, ni rahisi sana kwao kunena kwa lugha, ambayo
inaeleweka na Mungu pekee. Licha ya kujaribu kunena, ni sharti tuweke mkazo
katika kuelewa Neno la Biblia. Ni lazima tutambue kuwa ni bora kuongea maneno
matano tunayoyaelewa na kuwafunza wengine kuliko kunena maneno elfu kumi (1 Wakorintho
14:19).
9) Kipawa cha kutafsiri ndimi. Huu ni uwezo wa kufundisha
mapenzi ya Mungu ili kila mmoja aelewe kuwa kutafsiri neno lililotoka kwa Mungu
kipawa hiki cha kutafsiri lugha kilitolewa na kanisa la kwanza kwa lengo la
kueneza Injili, na sasa kinaweza kuonekana katika huduma ya kutafsiri na
kufafanua mafundisho ya Injili. Kama mtu akiweza kuongea kwa lugha za kienyeji,
hawezi kuhitaji mtafsiri, ila yule anayeweza kuongea lugha nyingi za duniani
anahitaji mtu wa kutafsiri.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni