Ijumaa, 4 Aprili 2014

NJIA SAHIHI YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU – 1


Sehemu ya kwanza
Je unafahamu juu ya Injili iwezayo kukupatia Roho Mtakatifu? Ikiwa unataka kumwomba Mungu kumpokea Roho Mtakatifu, ndipo basi kwanza yakupasa kupata ufahamu halisi juu ya hili na kuwa na imani nalo. Sasa basi, nini kilicho muhimu katika kuhitimu kumpokea Roho Mtakatifu? Ni kutakaswa dhambi zako zote kupitia Injili njema ya maji na Roho (inapatikana katika blog hii). Ni pale tu utakapokubali juu ya ufahamu huo, ndipo utatakapompokea Roho Mtakatifu.
Katika jamii ya leo, watu wengi hawaelewi ukweli wa Injili ya maji na Roho, na wanateseka chini ya makosa ya kihisia wanayo pandikizwa na walimu waongo. Watu hao hukusanyika katika kile kinachoitwa mikutano ya uamsho huku wakipiga makofi kwa furaha ya mashamushamu. Mhubiri anapokuwa jukwaani akiimbisha mapambio huku akiwaasa watu kutubu katika Mikutano ya aina hii ambayo mara nyingine huwa katika hali ya mashamushamu, watu hupiga makelele na kuita “Bwana!” na kurudia hata zaidi ya mara tatu wakimwomba Mungu ujazo wa Roho Mtakatifu hadi sauti kukauka.
Wale wote wenye kuhudhuria mikutano kama hii hujifanya kulia wakati wote badala ya kufanya maombi. Hali inapo fikia kilele katika tafrani hii watu hupiga makelele na mayowe hadi kuzimia. Hata hivyo mhubiri aliye jukwaani au madhabauni huweka kipaza sauti karibu kabisa na mdomo wake na kufanya sauti kama upepo upulizao huku akiwaongoza watu katika kina cha mashamshamu ya kidini. Ndipo huaza kuomba kwa kunena kwa lugha huku akiruka ruka na kuanza kuwawekea mikono watu juu ya vichwa vyao. Baadhi yao huanza kunena kwa lugha , na wengine huanguka kwa nguvu ghafla sakafuni na kuzimia.
Watu wengi huvutiwa na mzuka huu wa kidini huku wakitumaini kumpokea Roho Mtakatifu. Huamini kwamba wataweza kumpokea Roho Mtakaatifu kwa kufikia hali ya kiwango cha juu cha mfadhaiko na mzuka wao. Lakini haya yote hutokana na shetani.
Kwa kuchunguza mambo haya namengine ya aina hii tunaweza kuwaona wakristo wanyakati hizi wamepatwa na ugonjwa ambao utaweza kuelezeka kuwa ni “Uamsho wa Wapentekoste” (the pentecostal-Charismatic Movement) au Upentekoste wa kileo (Neo Pentecostalism) ambao umetokana na dini ya Kishama (shamanism). Kwanini basi wanapatwa na ugonjwa huu wa mzuka? Kwa sababu wamekataa ukweli ambao hunena kwamba, imewapasa kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini injili njema ya maji na Roho tu.
Aina hii ya vuguvugu ya uamsho katika dini za nyakati hizi yametapakaa duniani pote na Wakristo walio wengi wamechanganyikiwa kwa sababu hawawezi kujua ni ipi kazi ya Roho Mtakatifu na ile ya mapepo.
Roho Mtakatifu Hufanya kazi kupitia ahadi ya Neno la Mungu
( Matendo 1:4-8 )
“Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohana aliwabatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada siku hizi chache. Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema Je? Bwana wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia si kazi yenu kujua nyakati wala majira Baba aliyo weka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu na katika Uyahudi yote, na Samaria nahata mwisho wa nchi.”
Roho Mtakatifu hukaa ndani ya mioyo ya walio zaliwa upya ambao dhambi zao zote zimesamehewa kwa kuiamini Injili ya maji na Roho. Punde, anapo kuja juu ya mtakatifu, hufanya makazi ndani yake milele na kamwe hatomwacha peke yake kadiri atakapo endelea kuamini Injili. Humpa ushawishi mtakatifu huyo, katika kumwongoza kuelekea mapenzi ya Mungu, kumwongoza katika Biblia, humpatia nguvu ili kushinda majaribu na taabu anazokutana nazo hapa ulimwenguni, na humfanya azae matunda ya Roho kwa wingi. Mungu huutukuza mwili wa mtakatifu ukiwa ni hekalu lake kupitia kuweka makazi ya Roho Mtakatifu (Matendo 2:38-39, Yohana 14:16, 16:8-10, 1 Korintho 3:16, 6:19, Wagalatia 5:22-23).
Wakristo walio wengi hujaribu kumpokea Roho Mtakatifu kwa namna ile alivyo washukia wafuasi wa Yesu katika siku ile ya Pentekoste. Wapo baadhi ya watu wamepata vitita vya fedha kwa kutumia njia hii. Hujidai kwamba Roho Mtakatifu ni kitu fulani kinachoweza kupatikana kupitia juhudi ya mtu binafsi.
Hutamani kuona maono, kutenda miujiza, kuisikia sauti ya Yesu, kunena kwa lugha, kuponya magonjwa na kukemea mapepo. Hata hivyo ndani yao huwa na dhambi mioyoni na wapo katika msukumo wa roho za shetani (Waefeso 2:1-2).
Hata leo hii watu wengi bado wanaendelea kuishi pasipo kujua kwamba wapo chini ya nguvu za roho wa shetani. Hiki ndicho chombo na ulaghai wa shetani anao tumia dhidi ya watu kwa kutumia kila aina ya njia kama vile miujiza na maajabu ambayo hakika ni kiini macho tu. Yesu aliwaagiza wafuasi wake wasitokeYerusalamu, bali waingoje ahadi ya Baba (Matendo1:4). Kupokewa kwa Roho Mtakatifu kunakofunuliwa katika Matendo si kwakupitia “mazoea”, “kujitoa” au “sala za toba” bali kupitia kungojea ahadi ya Baba kumleta Roho Mtakatifu kwao.
Kile tunacho paswa kujifunza kutoka katika ujumbe huu ni kwamba, uwepo wa Roho Mtakatifu ndani ya mtu hautegemei kupitia maombi ya dhati afanyayo. Hii ni karama ya Mungu ambayo itaweza kupatikana pale tu kupitia imani kamili katika Injili njema ya maji na Roho ambayo Baba Mungu na Yesu Kristo aliyowapa wanadamu. Uwepo wa Roho Mtakatifu ndani ya mtu hutokea kupitia imani ya Injili ambayo Yesu kristo ametupatia. Mungu ametupa ukweli wa maji na Roho ili kwamba tuweze kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu (1 Yohana 3:3-5). Neno “ahadi ya Roho Mtakatifu” hutokea mara nyingi katika Agano Jipya. Petro anaongelea katika mahubiri yake (Matendo 2:38-39) juu ya ubatizo wa Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste. “Ni ahadi ya Mungu kutupatia Roho mtakatifu kwa wale walio pokea msamaha wa dhambi kutokana na kuamini injili njema.”
Roho Mtakatifu ni kipawa kilichomo ndani ya wale wote walio pokea msamaha wa dhambi zao na kujumuisha maana ya kutimia kwa ahadi ya Mungu. Roho Mtakatifu katika Agano Jipya si kitu kinachoweza kupatikana kupitia makubaliano kati ya Mungu na watu bali ni ahadi ya zawadi toka kwa Mungu. Hivyo Roho Mtakatifu ndani ya mtu kama ilivyoanishwa katika matendo sio kitu kinachoweza kupatikana kupitia maombi (Matendo 8:19-20).
Roho Mtakatifu huja juu ya wale wote wanaoamini Injili ya maji na Roho ambayo Yesu aliyotupatia. Yesu aliwaahidi Wanafunzi wake kumtuma Roho Mtakatifu ili kwamba waweze kuwa naye ndani yao. “Yohana aliwabatiza kwa maji bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache” (Matendo 1:5). Kwa kuangalia imani za hawa walio katika Biblia ambao walipokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao, tunagundua kwamba haya yalitokea si kwa kupitia juhudi zao bali kwa mapenzi ya Mungu. Uwepo wa Roho Mtakatifu ndani ya wafuasi hao katika Matendo haukutokea kwa msingi wa juhudi za kibinamu au maendeleo ya kiroho. Kuja kwa Roho Mtakatifu punde juu ya wafuasi wa Kristo kama ilivyoandikwa katika Matendo kulitokea kweli.
Hivyo Mitume wake walisubiri kutimia kama vile Yesu alivyosema “siyo siku chache kuanzia sasa”. Hii ndiyo iliyokuwa baraka ya kwanza katika kipindi cha Kanisa la kwanza. Kwa kuchunguza maandiko tunaweza kuona ahadi ya Mungu iliweza kutimia si kwa kupitia kufunga, maombi au kujitolea nafsi bali kupitia imani katika Kristo Yesu. Baada ya Yesu kupaa, waumini walimpokea Roho Mtakatifu kwa wakati mmoja.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni