Jumatano, 16 Aprili 2014

UPATANISHO WA DHAMBI KATIKA AGANO LA KALE NA JIPYA


Na mtu awaye yote katika watu wa nchi akifanya dhambi pasipo kukusudia, kwa kufanya neno lolote katika hayo ambayo BWANA alizuiria yasifanywe, naye akapata hatia, akijulishwa hiyo dhambi yake kwa ajiri ya dhambi yake aliyoifanya, ndipo atakapoleta mbuzi mke mkamilifu, awe matoleo yake kwajiri ya dhambi yake aliyoifanya. Naye ataweka mkono wake kichwani mwake hiyo sadaka ya dhambi, na kumchinja sadaka ya dhambi mahali hapo pa sadaka ya kuteketezwa. Kasha kuhani atatwaa katika hiyo damu yake kwa kidole chake, na kuitia katika pembe za madhabahu ya kuteketeza na damu yake yote ataimwaga  chini ya madhabahu (Walawi 4:27-30)
Mwenye dhambi anapotaka kupatanishwa na dhambi alizotenda kwa kila siku ilimpasa kuleta mnyama asiye na doa mbele ya hema takatifu. Ndipo ilimpasa kumwekea mikono juu ya sadaka hiyo ya mnyama  ili kumtwika dhambi zake zote, kumchinja koo na kutoa damu kwa kuhani ili iweze kuletwa mbele ya Mungu. Kitakachofuata ni kumalizia hatua iliyobaki ili ikamilishe msamaha wa wenye dhambi.
Pasipo sheria na amri za Mungu, watu wasingeweza kujua ikiwa kwamba wana dhambi au la. Tunapojichunguza wenyewe kupitia sheria na amri za Mungu tunagundua kwamba tuna dhambi. Dhambi zetu hazikuhukumiwa kwa viwango vyetu, bali ni kwa sheria na amri za Mungu.
Katika Agano la kale, dhambi zilitwikwa juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi kwa kuwekewa mikono. Na baadaye mwenye dhambi hakuwa tena na dhambi ndipo sadaka hiyo ilipopaswa kuchinjwa na kufa badala ya mwenye dhambi. Mpangilio huo wa utoaji wa sadaka ya dhambi ni kivuli cha hukumu na upendo wa Mungu.
“Kisha atayaondoa mafuta yake yote kama vile mafuta yanayoondolewa katika hizo za amani; kisha kuhani atayateketeza juu ya madhabahu iwe harufu ya kupendeza kwa bwana”  (Walawi 4: 31) mafuta katika biblia yana maana ya Roho Mtakatifu. Hivyo, ili tuweze kupatanishwa kwa dhambi zetu zote yatupasa pia kuchukulia ndani ya moyo wetu upatanisho wa dhambi zetu kwa namna ya Mungu aliyo iweka.
Mungu aliwaeleza wana wa Israel kwamba sadaka ya dhambi katika Agano la kale ilipaswa iwe ni mwana kondoo, au mbuzi au ndama dume. Sadaka hiyo ilichaguliwa kwa uwangalifu mkubwa. Sababu ya sadaka kuwa safi ni kwamba ilipaswa kuonyesha Yesu Kristo ambaye angezaliwa kwa uwezo wa Roho mtakatifu na kuwa sadaka ya dhambi kwa wanadamu wote.
Watu wa Agano la kale walizitwika dhambi zao kwa kuweka mikono juu ya mnyama asiye na doa, kuhani alihudumia kwa sadaka hiyo ili kulipizia dhambi. Hii ndiyo namna ambayo Israel walipatanishwa kwa dhambi.

kifungu kingine kinacho zungumzia mambo hayo ni (Walawi16:21). Hivyo tafakari kwa kina na utaona kwamba bila kuwekea mikono juu ya sadaka husika, damu haitakua na maana yoyote katika kuondoa dhambi. Iliwapasa Israel kuamini katika mambo yote ya sadaka ya dhambi.
SABABU GANI YESU ALIBATIZWA YORDANI?
Hebu sasa natuangalie tukio lile Wakati kuhani mkuu wa mbingu alipokutana na kuhani mkuu wa mwisho wa wanadamu. Hapa tunaweza kuona haki ya Mungu kupitia ubatizo ulio leta upatanisho wa dhambi zote za ulimwengu.
Yohana Mbatizaji aliye mbatiza yesu alikuwa mkuu kati ya wote waliozaliwa na mwanamke. Yesu alimshuhudia Yohana Mbatizaji katika (Mathayo 11:11) “amini nawaambieni, hajaondokea mtu katika uwazao wa mwanamke aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji”. Namna ile dhambi za watu zilivyoweza kufutwa wakati kuhani mkuu Haruni alipoweka mikono juu ya kichwa cha sadaka ya dhambi katika siku ile ya upatanisho, ndivyo hivyo katika Agano jipya dhambi zote za ulimwengu zilivyoweza kufutwa pia pale Yesu alipobatizwa na Yohana Mbatizaji.
Injiri ya kuzaliwa upya mara ya pili ni injiri iliyokamilisha ondoleo la dhambi zetu zote za zamani, za sasa na zijazo mbeleni. Hivyo injiri ya ukombozi kupitia ubatizo wa Yesu ilikuwa ni injiri ya Mungu iliyopangiliwa ili kutimiza haki yote, ambayo iliokoa wote duniani. Yesu alibatizwa kwa jinsi iliyostahili ili kupatanisha dhambi za ulimwengu.
Nini maana ya’ haki yote’? (Yohana 3: 13-15) Maana yake ni Mungu kusafisha dhambi zote za ulimwengu kwa njia inayostahili. Yesu alibatizwa ili kutakasa dhambi zote za wanadamu “ kwa maana haki ya Mungu anadhihirishwa ndani yake toka imani hadi imani”(Warumi 1:17). Haki ya Mungu imedhihirishwa katika uwamuzi wa kumtuma mwana wake Yesu hapa duniani ili kutakasa dhambi za ulimwengu kupitia ubatizo wake kwa Yohana Mbatizaji na kwa kifo chake msalabani.
Katika Agano jipya, haki ya Mungu imeelezwa kupitia ubatizo wa Yesu na damu yake. Tunakuwa wenye haki kwasababu Yesu Alibeba dhambi zetu zote katika mto Yordani. Tunapoukubali wokovu huu wa Mungu ndani ya mioyo yetu haki ya Mungu inatimizwa kwa uhakika.
Kila kitu katika Agano la kale kina mwenzake katika Agano jipya kwa Agano la kale “tafuteni katika kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake imekusanya” (Isaya 34:16)
Kutimia kwa unabii wa wokovu katika Agano la kale kulihitimishwa kwa njia ya ubatizo wa Yesu katika Agano jipya. Hivyo unabii wa Agano la kale hatimaye ulipata mwenzake katika Agano jipya. Vile watu wa Israel walivyopatanishwa kwa dhambi zao mara moja kwa mwaka katika Agano la kale, ndivyo ilivyo sasa dhambi za watu wote ulimwenguni zilivyo twikwa Yesu na kufutiliwa mbali milele katika Agano jipya.
Ikiwa hukubali na kuamini hili moyoni mwako juu ya huu ukweli wa ubatizo wa Yesu na kifo chake pale msalabani kamwe hautoweza kutakaswa dhambi zako hata kama wewe unaishi maisha ya utakatifu kwa kiwango kikubwa. Yesu alikufa msalabani kwasababu alibeba dhambi zako zote kwa ubatizo wake.
(Warumi 8:3-4) maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwasababu ya mwili, Mungu kwa kumtuma mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio na dhambi aliihukumu dhambi katika mwili, ili maagizo ya tirati yatimizwe ndani yetu sisi tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili bali mambo ya roho.
Kwakuwa sisi ni wanadamu tusioweza kamwe kufuata sheria na amri za Mungu kutokana na udhaifu wa miili yetu, Yesu alibeba dhambi zetu zote juu yake. Huu ni ukweli wa ubatizo wake. Ubatizo wa yesu ulitabili kifo chake pale msalabani. Hii ni hekima Halisi ya injiri ya Mungu.
Ikiwa umekuwa ukiamini kifo cha Yesu pekee, sasa nakusihi ugeuke na ukubali kwa moyo wako wote injiri ya wokovu kupitia ubatizo wa Yesu. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni