Ijumaa, 21 Februari 2014

TOHARA YA MOYO


Lipi lilitangulia, tohara au sheria?
Lipi kati ya moja ya haya Mungu aliwapa Waisraeli kwanza? Tohara. Baada ya ahadi ya ufalme wa Mungu, Mungu alimwambia Abraham na kila mume kati ya wanaume wa nyumba zake kutahiriwa. Mungu alisema kwamba tohara hiyo ni alama ya Agano la Mungu na wao. Hivyo Abraham alitahiriwa govi lake. Wanaume wote katika nyumba yake walifuata tendo hili. Tohara inafanana na imani ambayo tunaiamini.
Tunaokolewa pale tunapoamini kwa moyo. Mungu anasema “tohara ni ya moyo katika roho si katika andiko ambayo sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu” (Warumi 2:29). Yatupasa kuwa na ondoleo la dhambi. Ikiwa hatutakuwa nalo mioyoni mwetu basi ni bure tu. Mwanadamu ana “utu wa ndani” na “utu wa nje” na kila mtu inamlazimu kupokea ondoleo la dhambi ndani ya utu wake.
Wayahudi walikuwa wakitahiliwa sehemu ya mwili (utu wa nje), lakini Paulo aliwaambia “tohara ni ya moyo”. Leo hii Mungu anatuambia nasi kwamba tohara ni ya moyo pale tunapokuwa watoto wake.
Paulo hakuwa akizungumzia tohara ya nje bali tohara na ondoleo la dhambi katika moyo. Hivyo basi aliposema “nini basi ikiwa baadhi yao hawakuamini?”(Warumi 3:3). Alimaanisha kwamba ni nini ikiwa basi baadhi hawatoamini moyoni? Hakuwa akizungumzia juu ya kuamini kwa nje, bali alisema “amini ndani ya moyo.” Yatupasa kujua kile Paulo mtume alichokuwa akimaanisha na ni nini maana ya ondoleo la dhambi moyoni mwetu kupitia neno la Mungu.
“Ni nini basi ikiwa baadhi yao hawakuamini?” maana yake ni kwa vipi basi ikiwa Wayahudi hawakuamini juu ya Yesu Kristo kama mwokozi, je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kutokuwa na maana? Je, ukweli wa Mungu kufuta dhambi zote pamoja na dhambi za kizazi cha Abraham utakuwa ni bure? Kamwe Paulo anasema kwamba hata Wayahudi ambao ni uzao wa Abraham kwa mwili wataweza kuokolewa pale watakapo amini kwamba Yesu Kristo ni mwokozi, mwana wa Mungu aliye beba dhambi zote za dunia kwa njia ya ubatizo na kusulubiwa. Pia anasema kwamba wokovu na neema ya Mungu kupitia Yesu Kristo hautoweza  kamwe kubatilika. (Warumi 3:3-4)
Mungu huchunguza na kuangalia moyoni.Kwa uwazi utu wetu wa ndani umewekwa mbali na hauna uhusiano kabisa na matendo yetu. Wokovu wenyewe hauna uhusiano na matendo yetu (soma katika blog hii “sheria alizotupatia Mungu” utaona kuwa kuna Sheria ya Roho wa uzima na sheria ya dhambi na mauti).

Rejea katika kitabu cha (Warumi 4:1-5) Basi tusemeje juu ya Ibrahim baba yetu kwa jinsi ya mwili? Kwa maana ikiwa Ibrahim alihesabiwa haki kwa ajili ya matendo yake, analo la kujisifia, lakini si mbela za Mungu maana maandiko yasemaje? Ibrahim alimwamini Mungu ikahesabiwa kwake kuwa ni haki. Lakini kwa mtu afanyaye kazi, ujira wake hauhesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni. Lakini kwa mtu asiye fanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiye kuwa mtauwa imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni