Alhamisi, 27 Machi 2014

JINSI YA KUJAZWA ROHO MTAKATIFU


Moja, wale wanaopenda kupokea Roho mtakatifu ni lazima waamini Injili ya maji na Roho na kupokea ondoleo la dhambi.
Pili, wanahitaji kuwa na imani thabiti juu ya ukweli kuwa, Mungu anatoa Roho mtakatifu kwa wale tu waliopokea ondoleo la dhambi, hata sasa kuanzia enzi za mitume (matendo 2:38).
Tatu, mioyo yao lazima igeuke mbali na dhambi ya kutoamini neno la Biblia na kutokuwa na imani.
Nne, kupokea Roho mtakatifu, Roho zao zinahitaji kufundishwa neno kikamilifu. Wanapaswa kusikiliza kwa uangalifu neno lililobarikiwa la kuzaliwa upya kwa maji na Roho, na wakihitaji zaidi, watapaswa kushirikiana katika vikundi vya Injili pamoja na watumishi wa Mungu na kupokea Roho mtakatifu. Roho mtakatifu atawafanya waliamini Neno la Mungu mioyoni mwao, kuzaliwa upya na kumpokea. Lakini kama wakijaribu kumpokea Roho mtakatifu bila ridhaa yao, ila bila ridhaa kwa kutoa sala za toba na kujaribu kuishi maisha ya utakatifu,
au pia wakimwigiza Roho mtakatifu wakijaribu kumpokea kwa kujinyima, kufunga, au sala za milimani, hapo wataishi kuanguka katika kuchanganyikiwa.
Tunapaswa kukumbuka kwamba Roho wa Mungu haji kwa sababu watu wanataka kumpokea wenyewe, bali huja kwa wale walio tayari kumpokea. Roho mtakatifu haji kwa wale wanaashinda milimani wakiomba, kushiriki mikutano ya karismatiki au wanaotaka vipawa tu, kama unafikiria ulipokea kitu fulani kama karama ya Roho mtakatifu katika mikutano hiyo, au kwa imani yako, basi hapo kuna jambo unapaswa kulitafakari kwanza. Na hii ni kama kuna dhambi au hakuna moyoni mwako. Unapaswa kutambua kuwa ulichokipokea si kutoka kwa Roho mtakatifu bali shetani, na ni lazima ukiondoe. Ni lazima tutambue ni wapi na kwa nini Roho mtakatifu anatenda kazi. Kuna jambo ambalo hatupaswi kulisahau katika kutafuta kupokea Roho mtakatifu. Hii ni kuamini ubatizo wa Yesu (mathayo 3:15) na damu yake msalabani. Roho mtakatifu anajitegemea, ila huja kwa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu kristo na damu yake msalabani na ondoleo la dhambi zao. Roho mtakatifu huja na kutenda kazi ndani ya maisha ya wale wanaoiamini Injili ya maji na Roho kama wokovu wao wa kweli.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni