Jumapili, 6 Aprili 2014

NJIA SAHIHI YA KUMPOKEA ROHO MTAKATIFU – 2


Sehemu ya pili
Roho Mtakatifu aliwashukia Wafuasi wa Yesu ghafla toka Mbinguni!
“Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja”(Matendo 2:1). Wafuasi wa Yesu walikusanyika wakisubiri kutimia kwa ahadi ya Mungu kumtuma Roho Mtakatifu. Ndipo Roho Mtakatifu alipokuja juu yao. “Kukaja ghafla kutoka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kwa kasi ukaijaza nyumba yote waliokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliwakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka” (Matendo 2:2-4).
Roho Mtakatifu alishuka “ghafla kutoka mbinguni” hapo neno “ghafla” maana yake kulifanyika si kwa kupitia mapenzi ya Mwanadamu. Kwa nyongeza tafsiri ya “toka Mbinguni” inaweza kuelezwa mahali Roho Mtakatifu alipotoka, na pia kuondoa mawazo kwamba ujazo wa Roho Mtakatifu ndani ya mtu hutokana na mapenzi yake au juhudi. Tafsiri “Toka mbinguni” inatuonyesha kwamba, kusema Roho Mtakatifu anaweza kupatikana kwa kupitia maombi ni hoja za kitapeli. Kwa maneno mengine, kusema kwamba Roho Mtakatifu alishuka ghafla toka mbinguni maana yake kuwa na Roho Mtakatifu ndani hakutokei kwa kupitia namna za kidunia kama vile kunena kwa lugha au kujitoa nafsi. Wafuasi wa Yesu walinena kwa lugha hapo awali katika kuhubiri Injili njema kwa watu wa mataifa yote.
Sababu ya hili ni kuwa aliwawezesha kuhubiri Injili kwa lugha za kigeni toka ile ya Kiyahudi kwa msaada wake. Watu toka Mataifa yote waliweza kusikia wafuasi hao wakinena kwa lugha zao ingawa wengi wa wafuasi hawa walitokea Galilaya. “Kukawatokea ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu wakaanza kusema kwa lugha nyingine kama Roho alivyowajalia kutamka…” (Matendo 2:3-4). Hapa ni lazima kuwa makini zaidi tunapoona tafsiri, Roho Mtakatifu “kuwakalia kila mmoja wao”. Wafuasi walisubiri kuja kwa Roho Mtakatifu mahali pamoja wakiwa tayari wamekwisha kuamini Injili ya kuzaliwa upya mara ya pili katika maji na Roho.
 Wakristo wengi nyakati hizi huelewa vibaya sehemu hii ya kifungu, wakiamini ya kwamba ujio wa Roho Mtakatifu hutokea kwa sauti kama ya upepo uvumao wanapokuwa kwenye maombi. Hata hivyo hili ni jambo potofu kuhusiana na Roho Mtakatifu litokanalo na upumbavu na kuchanganyikiwa. Je, Roho Mtakatifu hufanya sauti pindi anaposhuka juu ya watu? Hapana, hakika hafanyi.

Kile watu wanachosikia ni sauti ya shetani afanyayo pale anaposhambulia roho za watu. Hufanya sauti hizi pale anapofanya mazingaombwe, sauti za kunongoneza na miujiza ya uongo katika juhudi za kuwaingiza watu katika kuchanganyikiwa kwa kusingizia kuwa ni Roho Mtakatifu. Watu wengi hupokea kwa kudhani mambo haya yote ni ishara na ushuhuda wa kushuka kwa Roho Mtakatifu. Pia hudhani kwamba Roho Mtakatifu huja kwa sauti kama ya “Shwuihhh….” Kama ya upepo mkuu. Wanadanganyika na mapepo. Kuja kwa Roho Mtakatifu kama ilivyoandikwa katika Matendo alikuja kwa kupitia imani katika Injili njema tu.
Imani ya Petro (1 Petro 3:21) ilikuwa ni sahihi kumwezesha kupokea Roho Mtakatifu ndani yake.
Kwa kuweka bayana tukio la kwanza la Pentekoste katika Matendo 2, Mungu anataka kuweka msisitizo wa ukweli kuwa Roho Mtakatifu alishuka juu yao kwa sababu walikuwa tayari wamekwisha amini Injili ya maji na Roho. Lakini watu mara nyingi hudhani Pentekoste ni wakati ule Roho Mtakatifu anaposhuka toka mbinguni kwa ishara zisizo za kawaida na tafrani za makelele. Na ndiyo maana nyakati hizi katika mikutano ya uamsho inaaminika kwamba mtu aweza kupokea Roho Mtakatifu kupitia sala za kurudia rudia, kufunga kula au kuwekewa mikono. Matukio yasiyo ya kawaida kama vile kuwa na mapepo, kuanguka bila fahamu, kukosa fahamu kwa siku kadhaa au kutetemeka bila kujizuia hizi si kazi za Roho Mtakatifu.
Roho Mtakatifu ni nafsi iliyo na utashi kamili na kamwe haidharau utu wa mwanadamu. Roho Mtakatifu hana tabia ya kumdhalilisha mtu kwa sababu yeye ni nafsi ya Mungu aliye na utashi akili na hisia. Huja juu ya watu pale tu wanapoamini maneno ya Injili ya maji na Roho (Matendo 2:38). Petro alishuhudia kwamba Roho Mtakatifu alikuja juu ya wafuasi kama ilivyo tabiriwa na Nabii Joeli. Ilikuwa ni kutimizwa kwa ahadi ya Mungu iliyo sema kwamba Roho Mtakatifu atawashukia wale wote watakao pokea ondoleo la dhambi. Kwa maneno mengine kuwa na Roho Mtakatifu ndani huja kwa wale wanaoamini ukweli kuwa Yesu alibatizwa na Yohana na kusulubiwa ili kuwaokoa wanadamu na dhambi zao. Hotuba ya Petro ukijumuisha na unabii wa Yoeli, hutuonyesha kwamba yatupasa kujua kwanini Yesu alibatizwa, na kwa nini imetulazimu kuamini hili. Kwa kujua ukweli huu ndipo kunako pelekea Wakristo kumpokea Roho Mtakatifu.
Je, unaamini Injili hii njema ambayo Petro anayoshuhudia? (1 Petro 3:21) au bado wewe unaamini upuuzi na mazingaombwe ya imani zisizo na umuhimu kinyume na Injili njema? Je, unajaribu kumpokea Roho Mtakatifu kwa kupitia juhudi zako kwa kuweka kando mpangilio wa Mungu? Hata ikiwa mtu atamwamini Mungu na kufanya maombi ya toba kwa
matumaini ya kutakaswa dhambi zake hakuna njia nyingine ya kuweza kumpokea Roho Mtakatifu zaidi ya kuamini injili ya majina Roho. Je, bado unasubiri kumpata Roho Mtakatifu ndani yako huku ukiwa huna ufahamu wa injili ya maji na Roho? Je, wajua maana halisi ya ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani ambayo hupelekea Roho Mtakatifu kuja ndani ya moyo wako? Ni lazima ujue kwamba Roho Mtakatifu kuweza kuwa ndani yako kunawezakana ikiwa tu unapoamini injili ya maji na Roho. Ukweli wa Roho Mtakatifu kuwa ndani yako unawezekana kwa wote wale watakaoamini Injili ya maji na Roho.
Tunamshukuru Mungu kwa kutupatia Injili yake ya maji na Roho ambayo ndiyo pekee ituwezeshayo kumpokea Roho Mtakatifu ndani yetu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni