(Mathayo 25:1-12)
“Ndipo ufalme wa Mbinguni utakapofanana na wanawali waliotwaa taa zao,
wakatoka kwenda kumlaki bwana harusi. Watano wao walikuwa wapumbavu na watano
wenye busara. Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao na wasitwae na mafuta
pamoja nao, bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na
taa zao. Hata bwana harusi alipokawia wote wakasinzia wakalala usingizi. Lakini
usiku wa manane pakawa na kelele, haya bwana arusi tokeni mwende kumlaki. Mara
wakaondoka wanawali wale wote wakazitengeneza taa zao. Wale wapumbavu wakawaambia
wenye busara tupatieni mafutayenu kidogo maana taa zetu zinazimika. Lakini wale
wenye busara wakawajibu wakisema hayatatutosha sisi naninyi shikeni njia muende
kwa wauzao mkajinunulie. Na hao walipokuwa wakienda kununua mafuta bwana harusi
akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana Bwana tufungulie Akajibu
akasema, Amin nawaambia siwajui ninyi. Basi kesheni kwa sababu hamwijui siku
wala saa.”
Ni
watu gani walio mfano wa wanawali walio na uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yao?
Katika kifungu kilichopita hapo juu tumeona wanawali
watano wenye busara na wapumbavu, wanawali wapumbavu waliwaomba wale wenye busara
kuwagawia kiasi cha mafuta ya taa lakini wenye busara wakawajibu wale wapumbavu “hayatatutosha sisi
na ninyi shikeni njia muende kwa wauzao mkajinunulie”.Hivyo wakati wale walio
wapumbavu wakienda nje kununua mafuta hayo, wale wenye busara walikuwa nayo katika
taa zao na kuingia katika sherehe za harusi. Sasa basi ni kwanamna gani tunaweza
kuyatayarisha mafuta kwa ajili ya Bwana? Kitu pekee tunachoweza kufanya ni
kuusubiri msamaha wake wa dhambi katika mioyo yetu.
Katikakati ya watu tunaweza kupata aina mbili za imani.
Moja ni imani ya injili ya msamaha wa dhambi. Hii ndiyo inayopelekea kumpokea
Roho Mtakatifu. Nyingine ni ile ya kuwa mwaminifu wa kanuni za dini bila kujali
mtu kusamehewa au kutosamehewa dhambi.
Kwa wale wote walio waaminifu kwa kanuni za dini, injili
hubaki kuwa mzigo kwao kuichukulia. Kama walivyo wanawali wapumbavu waliokwenda
nje kununua mafuta pale bwana harusi alipo ingia, wale wote wanaohama toka
nyumba moja ya kuabudu kwenda nyingine kwa matumaini ya kumpookea Roho Mtakatifu
ndani yao, hawamdanganyi yeyote bali nafsi zao. Watu wa aina hii ni wenye
kiburi ambao kwa kweli ndiyo wanao hitaji kuwa na imani ya injili njema katika
mioyo yao kabla ya siku ya hukumu. Watuhawa hutamani kuwa na Roho Mtakatifu kwa
kumuonyesha Mungu ukereketwa wao.
Tuone ushuhuda wa shemasi mmoja aliyefanya juhudi
kubwa katika kumpokea Roho Mtakatifu. Ushuhuda huu kwa hakika utatusaidia sana.
“Nilifanya kila niwezalo ili kumpokea Roho Mtakatifu. Nilidhani kwamba, ikiwa
nitajitolea nafsi yangu kwa imani yangu kwa uaminifu nitaweza kumpokea Roho
Mtakatifu na matokeo yake nilijikuta kuhama kanisa moja hadi jingine, nyumba
moja ya sala kwenda nyingine. Watu katika moja wapo ya nyumba hizi za sala
walikuwa wakipiga kinanda cha umeme ikiwa ni sehemu ya ibada.Mchungaji
aliyekuwa akiongoza mkutano huu aliwaita wale wote waliohitaji kumpokea Roho Mtakatifu
moja baada ya mwingine na walipo wekewa mkono wa mchungaji katika mapaji ya
nyuso zao, kila mtu baada ya tendo hilo alianza kunena kwa lugha. Mchungaji
aliruka huku na kule akishikilia kipaza sauti nakupaza sauti “pokea moto, moto,
moto!” na kuweka mkono wake juu vichwa vya watu na kusababisha baadhi yao kupagawa
na kuanguka. Mwanzoni nilikuwa na wasiwasi ikiwa tendo hili linamaana ya
kumpokea Roho Mtakatifu lakini tayari nilikuwa nimeathirika na mikutano ya aina
hii. Licha ya haya yote kamwe sikuweza kupokea Roho Mtakatifu.
Baada ya tukio hili niliamua kwenda milimani
nakujaribu kulia na kuomba usiku kucha nikiwa nimeegemea mti. Wakati mwingine
nilijaribu kufanya maombi ndani ya pango lakini yote haikusaidia. Baada ya yote
haya nilijaribu kufanya maombi usiku kucha kwa siku arobaini lakini kamwe
sikuweza kumpokea Roho Mtakatifu. Semina hii ilikuwa ikifanyika kwa juma mara
moja na kufululiza majuma saba.
Katika semina hii kulikuwa na mafundisho kuhusu
upendo wa Mungu, msalaba na ufufuko wa Yesu, tendo la kuwekewa mikono, tunda la
roho na kukua kiroho. Katika muda huo wakati ratiba ya semina ilipokuwa ikikaribia
kuisha, mnenaji mkuu katika semina hiyo aliniwekea mikono juu ya kichwa changu
na kuanza kuniombea ili niweze kumpokea Roho Mtakatifu huku nikimfuatisha
maneno yake kama alivyonielekeza. Nilitulia na kunyanyua viganja vya mikono
yangu na kuelekeza juu na kuanza kupiga kelele “la-la-la-la!” kwa kurudia
rudia. Mara ghafla nilipokuwa nikipiga kelele “la-la-la-la!” nilianza kunena moja
kwa moja lugha ya ajabu. Watu wengi walinipongeza baada ya hapo katika kumpokea
Roho Mtakatifu. Lakini nilipokuwa mwenyewe nyumbani nilihofu. Hivyo nikaanza kujitolea
kufanya kazi katika semina hiyo. Nilidhani kwamba ilinipasa kujitolea kwa kazi
kama hii mapema sana. Hivyo nilisafiri nchi nzima katika kutoa huduma na nilipo
wawekea mikono wagonjwa, magonjwa yao yalionekana kupona ingawa baadhi
yaliwarudia baadaye. Na baadaye nikapata
maono na nikagundua yakuwa naweza pia kutoa unabii. Chakushangaza unabii wangu
mara nyingi ulikuwa wakweli.
Tokea hapo nilialikwa sehemu za kila aina na
kulakiwa kwa shangwe. Lakini bado nilikuwa na hofu ndani yangu ndipo nikasikia
sauti ikisema “usitange tange toka sehemu moja kwenda nyingine namna hii badala
yake nenda ukawasaidie jamaa zako nyumbani katika kupokea wokovu.” Hata hivyo
sikuelewa maana halisi ya wokovu. Nilichokuwa nakielewa nikile wengi
walichokuwa wakisema kwamba, ikiwa nitaacha kuzitumia karama za Roho Mtakatifu
basi atanipokonya. Kwa upande mwingine nilihofu kutumia uwezo wangu lakini
sikuweza kujizuia hilo.
Siku moja nilisikia kuwa yupo mwanamke fulani ambaye
ni wa dini ya Shama aliyehitaji kumwamini Yesu, hivyo mimi pamoja na rafiki
yangu tulikwenda kumtembelea. Hatukumfahamisha juu ya ujio wetu kabla. Lakini
mwanamke huyo alikuwa akitusubiria mlangoni nakuanza kutuambia “nilishajua
kwamba mnakuja” mara ghafla alianza kutunyunyizia maji na kusema “hakuna
tofauti kati ya ushama wa mashariki na ushama wa magharibi”. Alituita sisi kuwa
ni “washama wa Yesu” na kutunyoshea kidole akisema “huyu ndugu ni muoga lakini
huyu si muoga” Kile ambacho mwanamke huyu alichokua akisema kiligeuka kuwa kama
pigo katika kichwa. Nikaanza kuwaza kwamba yote niliyokuwa nikiyatenda hayakuwa
tofauti nayale ambayo dini ya shama wakitenda. Hakuna nilichokuwa nimekwisha
tenda ili kumleta Roho Mtakatifu ndani yangu kwa sababu bado nilikwa na dhambi
moyoni.”
Tokana na ushuhuda huu tunajifunza kwamba, swala la kumpokea
Roho Mtakatifu lipo nje ya uwezo wetu. Kwasababu imani ya aina hii haihusiani
na injili ya Mungu kwani wale wote wanaoishi katika aina hii ya udini ndiyo
wasio kuwa na mafuta katika taa zao.
Taa katika biblia inamaana ya kanisa, na mafuta
maana yake Roho Mtakatifu. Biblia inakusudia kwamba wale wote wanao hudhuria
kanisani, iwe ni kanisa la Mungu au si la Mungu pasipo kumpokea Roho Mtakatifu,
bado ni wapumbavu.
Wapumbavu wote hupandisha mori siku hata siku. Watu hawa
hupandisha hisia zao kali na kujitolea kimwili mbele ya Mungu. Ikiwa
tungelisema kuwa hisia zetu ziwe za kiwango cha sentimita 20 na hivyo kufanya
kila siku 1 kupandisha sentimita 1, basi ingelichukua siku 20 kuweza kufikia
kiwango cha juu katika hisia zetu zote. Hisia zao katika imani hupata nguvu mpya
kwa kila maombi ya asubuhi, maombi ya usiku kucha, maombi ya kufunga na mikutano
ya uamsho na pia katika maisha ya kila siku. Huathirikana tabia hii ya kudumu katika
kuenenda kwa hisia.
Hisia zao hupanda katika jina la Yesu. Huudhuria
kanisani ili kupandisha hisia zao, lakini mioyo yao bado imechanganyikiwa huku
wakitafuta sababu nyingine. Sababu ya hili ni kwamba imani yao imetokana na
kile kinachotokana na mwonekano wa nje kimwili na hivyo kuhitaji shinikizo la
mara kwa mara ili kusukuma hisia zao ili moto wa hisia usizimike ndani yao.
Hata hivyo bado hawato weza kumpokea Roho Mtakatifu kwa aina hii ya imani. Kwa
kupandisha hisia hizo kamwe hakutoweza kuwafanya kumpokea Roho Mtakatifu.
Sote imetupasa kuwa tayari na imani sahihi ili
kuweza kumpokea Roho Mtakatifu katika uwepo kamili wa Mungu. Na ndipo pekee
tutakapo kuwa na haki ya kumpokea Roho Mtakatifu. Ni kwanamna gani basi
tunaweza kuwa na imani ambayo inatupa haki ya kuwa na Roho Mtakatifu? Ukweli
upo katika injili njema ambayo ilikamilishwa kwa ubatizo wa Yesu Yordani na kumwaga
damu yake Msalabani.
Mungu alituita kuwa sisi ni kama “wazao wa watenda mabaya,
watoto wanaoharibu” (Isaya 1:4). Lazima
tulikubali hili. Kwa asili wanadamu wamezaliwa wakiwa wanadhambi aina 12 (Marko 7:21-23). Wanadamu hawawezi kujizuia kutotenda
dhambi tokea wanapozaliwa hadi kufa. Katika Yohana
1:6-7 imeandikwa, “palitokea mtu ametumwa kutoka kwa Mungu jina lake
Yohana. Hivyo alikuja kwa ushuhuda ili aishuhudie ile nuru wote wapate kuamini
kwa yeye”.Yohana Mbatizaji alimbatiza Yesu na kumtwika dhambi zote za ulimwegu
akisema “tazaama mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya dunia” (Yohana 1:29).
Tuliokolewa kwa dhambi zote na kuushukuru ubatizo wa
Yesu Kristo. Kama Yohana asingeli mbatiza Yesu Kristo nakutotangaza kwamba alikuwa
ndiye mwana kondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu, basi tusingeliweza
kumjua Yesu kwamba ndiye aliye beba dhambi zetu zote kuelekea msalabani.
Tusingeliweza kuifahamu njia ya kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa hiyo basi tunamshukuru
Yohana kwa ushuhuda kwani sasa tunaelewa yakwamba Yesu ndiye aliye beba dhambi
zetu zote na hivyo tunaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa imani hiyo.
Kwa imani hii basi tumekuwa wanaharusi
tuliotayarishwa kamili kumpokea Yesu Kristo, Bwana harusi. Sisi ni wanawali tulio
mwamini Yesu na tumejitayarisha kamili kumpokea Roho Mtakatifu.
Je, unaamini injili ya maji na Roho kwa moyo wako
wote? Je, unaanini kwamba Yesu alizichukua dhambi zetu kwa ubatizo wake kwa
Yohana? Biblia inasema “basi imani, chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja
kwa neno la Kristo” (Warumi 10:17). Nilazima
tuamini yakwamba Yesu alibatizwa na Yohana na kufa msalabani ilituweze kumpokea
Roho Mtakatifu. Yatupasa kuelawa kwamba kumpokea Roho Mtakatifu kutawezekana ikiwa
tutaamini kwamba Yesu alikuja ulimwenguni akiwa kama mwanadamu na kubatizwa na Yohana
hivyo alikufa msalabani na kufufuka.
Hata leo hii yapo makundi mawili ya wanaoamini kama
ilivyo kwa wanawali kumi katika ile habari ya hapo mwanzo. Sasa basi wewe nawe
uko upande upi? Yakupasa ujue ile njia ya kweli ambayo utaweza kumpokea Roho
Mtakatifu kwa hakika. Ni kwa imani gani utaweza kumpokea Roho Mtakatifu? Je utaweza
kumpokea Roho Mtaktifu kwa kupitia shauku itokanayo na ukereketwa utokanao na
dini kama Shama?
Je utaweza kweli kumpokea Roho Mtakatifu katika hali
ya kupoteza fahamu? Je utaweza kumpokea Roho Mtakatifu kwa kuamini ushabiki wa kidini?
Biblia inasema kwamba Yesu alipobatizwa kwa kuzamishwa na kuibuka toka kwenye
maji Roho wa Mungu alitua kama hua juu yake. Alibatizwa ili kubeba dhambi zetu
zote na hivyo kuweka bayana kwamba atakwenda kusulubiwa ili kulipia mshahara wa
makosa yetu yote.
Yesu alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi za ulimwengu
na hivyo kwenda msalabani ili tuweze kuokolewa na kupokea kipawa cha Roho Mtaktifu.
Jambo hili ni kweli. Yesu alibatizwa na Yohana, akahukumiwa kwa dhambi zetu
zote msalabani na kufufuka. Lazima tuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu
yake msalabani ili tupate msamaha wa dhambi zetu zote.
Tunaweza kuona toka ubatizo wa Yesu (Mathayo 3:13-15) kwamba, Roho Mtaktifu huja kwa
amani kama ashukavyo huwa kwa wale waliotakaswa kwa kuamini ubatizo wa Yesu.
Ili kumpokea Roho Mtakatifu ni muhimu kuamini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na
damu yake msalabani. Roho Mtakatifu huja juu ya mtu katika hali ya utulivu na
amani kama vile hua pale mtu huyo anapo amini msamaha wa dhambi. Wale ambao
tayari wamekwisha mpokea RohoMtakatifu yawapasa kuelewa kwamba hili
limewezekana kutokana na msamaha wa dhambi
kwa imani. Roho Mtakatifu hutua juu ya wale wote
wanao amini msamaha wa dhambi kwa mioyo yao yote.
Yesu Kristo alikuja kwa mkate na divai ya uzima wa
milele (Mathayo 26:26-28, Yohana 6:53-56)
Yesu alipoibuka toka majini baada ya kubatizwa, palitokea sauti mbinguni
ikisema “Huyu ni mwanangu mpendwa wangu ninaye pendezwa naye” (Mathayo 3:17).
Nirahisi kuamini katika Mungu kwa Utatu. Mungu ni
Baba wa Yesu na Yesu ni Mwana wa Mungu. Roho Mtakatifu pia ni Mungu. Utatu huu
ni Mungu mmoja kwetu. Yakupasa kujua kwamba, kamwe hautoweza kumpokea Roho
Mtakatifu kwa kuamini msalaba pekee au kujaribu kujitakasa binafsi kwa matendo
ya haki. Utaweza kumpokea Roho Mtakatifu pale unapoamini ubatizo wa Yesu na
hivyo kumtwika dhambi zote juu yake, na kuamini kusulubiwa kwake ili
kutupatanisha kwa dhambi zetu zote.
Hakika hivi ndivyo ilivyo rahasi na wazi ju ukweli
huu! Si vigumu kupokea msamaha wa dhambi na Roho Mtakatifu. Mungu huzungumza
nasi kwa namna iliyo rahisi. Kiwango cha akili ya mtu wa kawaida ni kati ya 110
na 120 (yaani IQ - intelligence quotient). Injili yaMungu ni rahisi
kumtosheleza mtu wa kawaida kuielewa. Hata kwa watoto wa umri kati ya miaka 4
na 5 injili hii njema kamwe haijawa ngumu kueleweka kwao.
Lakini Mungu anapo zungumza nasi juu ya kupokea
uwepo wa Roho Mtakatifu ndani kwa njia iliyo rahisi zaidi, je, tusingeliweza
kweli kumwelewa? Mungu husamehe dhambi zetu zote na kutupa Roho Mtakatifu kama
zawadi kwa wale wote waaminio injili hii.
Mungu anatuambia kwamba hatutoweza kumpokea Roho
Mtakatifu kwa kupitia tendo la kuwekewa mikono au sala ya toba. Roho Mtakatifu
haji kwa namna ambavyo tutakapo funga au kujitolea au hata kuomba usiku kucha
milimani. Ni aina gani basi ya imani itakayo sababisha kumpokea Roho Mtakatifu ndani
yetu? Ni imani ya ukweli wa kwamba Yesu alikuja hapa ulimwenguni alibatizwa ili
kubeba dhambi zetu zote, akafa msalabani na alifufuka.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni