Ijumaa, 4 Aprili 2014

IMANI KATIKA MSAMAHA WA DHAMBI


Tunaamini kuwa Mungu pekee ndiye anayeweza kuondoa dhambi kwa njia ya Injili ya maji na Roho.( Isaya 1:18) inasema, “haya, njooni, tusemezane, asema Bwana’, dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theruji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”. katika (1 Yohana 1:9) tunasoma  “Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” Hapa ni lazima tutambue kwamba “tukiziungama dhambi zetu” haimaanishi kuwa Mungu hutusamehe dhambi tukitoa sala za toba. Katika 1Yohana 1:9 ina maana, tunapokea ondoleo la dhambi pale tunapokiri kuwa tuna dhambi mbele za Mungu na kuamini kuwa Mungu tayari amekwisha safisha dhambi za dunia kwa njia ya ubatizo alioupokea kutoka kwa Yohana na damu yake msalabani.
Dhambi hapa ni ipi?
Yeyote aliyezaliwa katika uzao wa Adamu ana dhambi. Hivyo hakuna hata mmoja anayeweza kudai kuwa hana dhambi, ile kuwa wandamu, tumezaliwa katika hali ya dhambi, tayari tuna dhambi hata kama hatutendi dhambi. Hii inamaanisha kuwa kila mmoja anahitaji mkombozi anayeweza kumkomboa kutoka dhambini. Wale wanaodai kutokuwa na dhambi na kutokuona umuhimu wa kumwamini Yesu huishia kusimama kinyume na Mungu. Hapo mwanzo, Mungu aliumba dunia na mbingu, alitengeneza bustani ya Edeni na akamruhusu Adamu na Hawa kuishi humo. Katika dunia hiyo ambayo ilikuwa haina dhambi kabisa, mahusiano ya Mungu nao yalikuwa makubwa. Lakini kuwafanya kuwa watoto wake Mungu aliwapa sheria. Sheria hii ilikuwa ni ya kutokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mungu alimwambia, “Siku mtakayokula matunda hayo hakika mtakufa” Na ili kuwapa baraka na uzima wa milele, Mungu aliwaambia kula matunda ya mti wa uzima. Lakini badala ya kula matunda ya mti wa uzima kama Mungu alivyowaagiza, walikula mti wa ujuzi wa mema na mabaya, mti ambao ungewaletea mauti (mwanzo 2:17, 3:22).
Kutumbukia katika majaribu ya shetani, Adam na Hawa waliishia kula matunda yaliyozuiliwa, matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mauti ilikua kama mshahara kwa dhambi hiyo. Ndio sababu (warumi 5:12) inasema “kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” Kwa kifupi ndio sababu wanadamu wanahitaji mwokozi. Watu wengine wanajiamini, kama yule kijana tajiri katika mathayo 19, hujiamini kuwa wameshika amri zote za Mungu tangu utoto, lakini hakuna mwanadamu yeyote aliyezitunza amri zote 613 za Mungu.
 Kwa nini Mungu alitupa sheria ambazo hatuwezi kuzizingatia kabisa? Biblia inasema kuwa kwa sababu ya kuwepo kwa sheria, tumeitambua dhambi (warumi 3:20) Amri kumi ambazo Mungu alitupa zinatuonyesha dhambi. Kwa mfano, mtu anaweza kumchukia mzazi wake, akisema Rohoni mwake “mzee yule ni mjeuri” mtu huyo tayari amekwisha vunja sheria au amri ya tano ya Mungu. Na mtu yeyote akimtamani mwanamke, hata kama asipofanya naye uzizi, tayari amekwishavunja mari ya saba Mungu pia anahesabu tama, uchoyo, wivu, chuki kuua hata kama hatujamuua mtu, kwani matendo haya ndiyo yanayosababisha watu kuuana. Ni nani sasa anayeweza kuzitunza amri za Mungu bila kuzipaka madoa katika ufahamu wa kawaida?
Pia katika (Yakobo 2:10) tunasoma “maana mtu awaye yote, atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika Neno moja, amekosa juu ya yote.” kwa mwanga huu, ni nani atasema hana dhambi mbele ya hii sheria kali ya Mungu?
Katika madhaifu yetu daima tunaanguka dhambini. Kwa nini jambo hili? Ni kwa sababu ile dhambi yetu ya asili, wanadamu kwa asili ni wenye dhambi. Ndio sababu Daudi alitubu kwa kuvunja amri ya saba, kama inavyoonekana katika zaburi 51:5 “Tazama mimi naliumbwa katika hali ya uovu; mama yangu alinichukuwa mimba hatiani.” Daudi kwa maneno mengine alikiri dhambi hiyo ya msingi. Sala za toba zinazotolewa siku hizi za wakristo wa kawaida na ukiri wa Daudi juu ya dhambi ni tofauti sana. Kale walijutia dhambi ile tu mtu aliyoitenda, wakati za siku hizi, kinyume chake mtu hujiona hawezi kujisaidia mwenyewe kwa sababu ya dhambi ya asili. Wale tu wanaotambua dhambi zile za asili na kuamini Injili ya maji na Roho ndio wanaoweza kupata neema ya ondoleo la dhambi kutoka kwa Mungu. Ni jambo lipi jema kwetu kutenda? Je ni kuorodhesha dhambi zetu za kila siku mbele za Mungu na kuomba msamaha. Tukiamini kuwa, kwa kujua na kuamini Injili ya maji na Roho matatizo yetu yanaweza kutatuliwa.
Katika (Yohana 6:53-55) Yesu alisema “hakika nawaambia msipokula mwili wangu na damu yangu hamuwezi kuingia ufalme wa mbinguni. Yeyote aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu, anao uzima wa milele, naye atafufuliwa siku ya mwisho, kwa kuwa mwili wangu ni chakula hakika na damu yangu ni kinywaji” hakika hapa ni lazima tule mwili wa Yesu na kuinywa damu yake, maana yake, ni sharti tuwe na imani ya kuamini Yesu alichukua dhambi za dunia kwa ubatizo aliopokea kutoka kwa Yohana. Maana yake ni kama hatujui ukweli juu ya ubatizo wa Yesu, basi hatuwezi kumpa dhambi zetu, na dhambi zetu haziwezi kusamehewa. Kama kusingekuwa na ubatizo ambao Yesu alipokea kutoka kwa Yohana mbatizaji, mwakilishi wa wanadamu, dhambi zetu kamwe zisingesamehewa (Mathayo 3:15, 11:11-13).
Kusulubiwa kwa Yesu yalikuwa ni matokeo ya ukweli kuwa, kabla ya hili alikuwa amebeba dhambi za wanadamu kwa njia ya ubatizo wa Yohana. Mungu ametuokoa kutoka dhambini kwa kusulubiwa, kuimwaga damu yake ya thamani, na hapo kubeba makosa ya dhambi zetu.
Tunapokiri kumwamini Yesu ni lazima tuamini kuwa, alichukua dhambi zetu zote kwa ubatizo wake. Biblia inasema wazi juu ya ondoleo la dhambi, habari ambayo tunaweza kuifupisha katika pointi mbili kuu.
Kwanza, inatuambia kuwa kwa kubatizwa, Yesu alizikubali dhambi za dunia zilizopitia katika mwili wake. Zaburi 32:1 inasema, “Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake” Neno ‘kusitiriwa’ lina maana kuchukua dhambi na kuzikubali dhambi na 1 Petro 3:21 inasema “mfano wa mambo hayo ni ubatizo unaowaokoa ninyi pia siku hizi (sio kuwekea mbali uchafu wa mwili bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu) kwa kufufuka kwake Yesu kristo” kwa ubatizo aliopokea kutoka kwa Yohana dhambi zote za wanadamu zimeondoshwa moja kwa moja.
 Pili, Biblia inatuambia kuwa Yesu ameondosha dhambi za dunia. Isaya 43:25 inasema, “Mimi, naam mimi ndiye niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako” kuyafuta makosa maana yake ni kuyapoteza kabisa kutoka katika maandishi.
Ina maana, Mungu baba amesafisha dhambi za dunia kwa kuzipitisha kwa mwanae kwa njia ya ubatizo. Kwa wale kati yetu wanaoweza kusema “sina tumaini kwa kuwa nimetenda dhambi nyingi sana” wao pia wanaweza kuwekwa huru mbali na dhambi kwa kulisikia Neno la Injili ya maji na Roho. Shetani anatuambia, “Je hujatenda dhambi nyingi?” Lakini hata kama tungesikia maneno hayo, tukiamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani hapo tunaweza kukombolewa kutoka dhambini. Tukiwa na imani kama hii, shetani hupata woga na kukimbia. Tumshawishi kuwa Bwana amesamehe dhambi kwa njia ya ubatizo na damu yake msalabani. Tukiamini kuwa Yesu amesamehe dhambi kwa njia ya ubatizo na damu yake msalabani ndipo amani ya ajabu huingia maishani mwetu. Hii ndio imani kuu ya ukristo, Imani ya ondoleo la dhambi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni