Tunaamini
kuwa Mungu pekee ndiye anayeweza kuondoa dhambi kwa njia ya Injili ya maji na
Roho.( Isaya 1:18) inasema, “haya, njooni, tusemezane,
asema Bwana’, dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theruji;
zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”. katika (1 Yohana 1:9) tunasoma “Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na
wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” Hapa
ni lazima tutambue kwamba “tukiziungama dhambi zetu” haimaanishi kuwa Mungu hutusamehe
dhambi tukitoa sala za toba. Katika 1Yohana 1:9
ina maana, tunapokea ondoleo la dhambi pale tunapokiri kuwa tuna dhambi mbele
za Mungu na kuamini kuwa Mungu tayari amekwisha safisha dhambi za dunia kwa
njia ya ubatizo alioupokea kutoka kwa Yohana na damu yake msalabani.
Dhambi hapa ni ipi?
Yeyote
aliyezaliwa katika uzao wa Adamu ana dhambi. Hivyo hakuna hata mmoja anayeweza
kudai kuwa hana dhambi, ile kuwa wandamu, tumezaliwa katika hali ya dhambi,
tayari tuna dhambi hata kama hatutendi dhambi. Hii inamaanisha kuwa kila mmoja anahitaji
mkombozi anayeweza kumkomboa kutoka dhambini. Wale wanaodai kutokuwa na dhambi
na kutokuona umuhimu wa kumwamini Yesu huishia kusimama kinyume na Mungu. Hapo
mwanzo, Mungu aliumba dunia na mbingu, alitengeneza bustani ya Edeni na akamruhusu
Adamu na Hawa kuishi humo. Katika dunia hiyo ambayo ilikuwa haina dhambi
kabisa, mahusiano ya Mungu nao yalikuwa makubwa. Lakini kuwafanya kuwa watoto
wake Mungu aliwapa sheria. Sheria hii ilikuwa ni ya kutokula matunda ya mti wa ujuzi
wa mema na mabaya. Mungu alimwambia, “Siku mtakayokula matunda hayo hakika
mtakufa” Na ili kuwapa baraka na uzima wa milele, Mungu aliwaambia kula matunda
ya mti wa uzima. Lakini badala ya kula matunda ya mti wa uzima kama Mungu alivyowaagiza,
walikula mti wa ujuzi wa mema na mabaya, mti ambao ungewaletea mauti (mwanzo 2:17, 3:22).
Kutumbukia
katika majaribu ya shetani, Adam na Hawa waliishia kula matunda yaliyozuiliwa,
matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Mauti ilikua kama mshahara kwa
dhambi hiyo. Ndio sababu (warumi 5:12) inasema “kwa hiyo,
kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na
hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.” Kwa
kifupi ndio sababu wanadamu wanahitaji mwokozi. Watu wengine wanajiamini, kama
yule kijana tajiri katika mathayo 19, hujiamini
kuwa wameshika amri zote za Mungu tangu utoto, lakini hakuna mwanadamu yeyote aliyezitunza
amri zote 613 za Mungu.
Kwa nini Mungu alitupa sheria ambazo hatuwezi kuzizingatia kabisa? Biblia inasema kuwa kwa sababu ya kuwepo kwa sheria, tumeitambua dhambi (warumi 3:20) Amri kumi ambazo Mungu alitupa zinatuonyesha dhambi. Kwa mfano, mtu anaweza kumchukia mzazi wake, akisema Rohoni mwake “mzee yule ni mjeuri” mtu huyo tayari amekwisha vunja sheria au amri ya tano ya Mungu. Na mtu yeyote akimtamani mwanamke, hata kama asipofanya naye uzizi, tayari amekwishavunja mari ya saba Mungu pia anahesabu tama, uchoyo, wivu, chuki kuua hata kama hatujamuua mtu, kwani matendo haya ndiyo yanayosababisha watu kuuana. Ni nani sasa anayeweza kuzitunza amri za Mungu bila kuzipaka madoa katika ufahamu wa kawaida?
Pia katika (Yakobo 2:10) tunasoma “maana mtu awaye yote, atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika Neno moja, amekosa juu ya yote.” kwa mwanga huu, ni nani atasema hana dhambi mbele ya hii sheria kali ya Mungu?
Katika madhaifu yetu daima tunaanguka dhambini. Kwa nini jambo hili? Ni kwa sababu ile dhambi yetu ya asili, wanadamu kwa asili ni wenye dhambi. Ndio sababu Daudi alitubu kwa kuvunja amri ya saba, kama inavyoonekana katika zaburi 51:5 “Tazama mimi naliumbwa katika hali ya uovu; mama yangu alinichukuwa mimba hatiani.” Daudi kwa maneno mengine alikiri dhambi hiyo ya msingi. Sala za toba zinazotolewa siku hizi za wakristo wa kawaida na ukiri wa Daudi juu ya dhambi ni tofauti sana. Kale walijutia dhambi ile tu mtu aliyoitenda, wakati za siku hizi, kinyume chake mtu hujiona hawezi kujisaidia mwenyewe kwa sababu ya dhambi ya asili. Wale tu wanaotambua dhambi zile za asili na kuamini Injili ya maji na Roho ndio wanaoweza kupata neema ya ondoleo la dhambi kutoka kwa Mungu. Ni jambo lipi jema kwetu kutenda? Je ni kuorodhesha dhambi zetu za kila siku mbele za Mungu na kuomba msamaha. Tukiamini kuwa, kwa kujua na kuamini Injili ya maji na Roho matatizo yetu yanaweza kutatuliwa.
Kwa nini Mungu alitupa sheria ambazo hatuwezi kuzizingatia kabisa? Biblia inasema kuwa kwa sababu ya kuwepo kwa sheria, tumeitambua dhambi (warumi 3:20) Amri kumi ambazo Mungu alitupa zinatuonyesha dhambi. Kwa mfano, mtu anaweza kumchukia mzazi wake, akisema Rohoni mwake “mzee yule ni mjeuri” mtu huyo tayari amekwisha vunja sheria au amri ya tano ya Mungu. Na mtu yeyote akimtamani mwanamke, hata kama asipofanya naye uzizi, tayari amekwishavunja mari ya saba Mungu pia anahesabu tama, uchoyo, wivu, chuki kuua hata kama hatujamuua mtu, kwani matendo haya ndiyo yanayosababisha watu kuuana. Ni nani sasa anayeweza kuzitunza amri za Mungu bila kuzipaka madoa katika ufahamu wa kawaida?
Pia katika (Yakobo 2:10) tunasoma “maana mtu awaye yote, atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika Neno moja, amekosa juu ya yote.” kwa mwanga huu, ni nani atasema hana dhambi mbele ya hii sheria kali ya Mungu?
Katika madhaifu yetu daima tunaanguka dhambini. Kwa nini jambo hili? Ni kwa sababu ile dhambi yetu ya asili, wanadamu kwa asili ni wenye dhambi. Ndio sababu Daudi alitubu kwa kuvunja amri ya saba, kama inavyoonekana katika zaburi 51:5 “Tazama mimi naliumbwa katika hali ya uovu; mama yangu alinichukuwa mimba hatiani.” Daudi kwa maneno mengine alikiri dhambi hiyo ya msingi. Sala za toba zinazotolewa siku hizi za wakristo wa kawaida na ukiri wa Daudi juu ya dhambi ni tofauti sana. Kale walijutia dhambi ile tu mtu aliyoitenda, wakati za siku hizi, kinyume chake mtu hujiona hawezi kujisaidia mwenyewe kwa sababu ya dhambi ya asili. Wale tu wanaotambua dhambi zile za asili na kuamini Injili ya maji na Roho ndio wanaoweza kupata neema ya ondoleo la dhambi kutoka kwa Mungu. Ni jambo lipi jema kwetu kutenda? Je ni kuorodhesha dhambi zetu za kila siku mbele za Mungu na kuomba msamaha. Tukiamini kuwa, kwa kujua na kuamini Injili ya maji na Roho matatizo yetu yanaweza kutatuliwa.
Katika (Yohana 6:53-55)
Yesu alisema “hakika nawaambia msipokula mwili wangu na damu yangu hamuwezi kuingia
ufalme wa mbinguni. Yeyote aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu, anao uzima
wa milele, naye atafufuliwa siku ya mwisho, kwa kuwa mwili wangu ni chakula
hakika na damu yangu ni kinywaji” hakika hapa ni lazima tule mwili wa
Yesu na kuinywa damu yake, maana yake, ni sharti tuwe na imani ya kuamini Yesu
alichukua dhambi za dunia kwa ubatizo aliopokea kutoka kwa Yohana. Maana yake
ni kama hatujui ukweli juu ya ubatizo wa Yesu, basi hatuwezi kumpa dhambi zetu,
na dhambi zetu haziwezi kusamehewa. Kama kusingekuwa na ubatizo ambao Yesu
alipokea kutoka kwa Yohana mbatizaji, mwakilishi wa wanadamu, dhambi zetu kamwe
zisingesamehewa (Mathayo 3:15, 11:11-13).
Kusulubiwa kwa Yesu yalikuwa ni matokeo ya ukweli kuwa, kabla
ya hili alikuwa amebeba dhambi za wanadamu kwa njia ya ubatizo wa Yohana. Mungu
ametuokoa kutoka dhambini kwa kusulubiwa, kuimwaga damu yake ya thamani, na hapo
kubeba makosa ya dhambi zetu.
Tunapokiri kumwamini Yesu ni lazima tuamini kuwa, alichukua
dhambi zetu zote kwa ubatizo wake. Biblia inasema wazi juu ya ondoleo la
dhambi, habari ambayo tunaweza kuifupisha katika pointi mbili kuu.
Kwanza, inatuambia kuwa kwa kubatizwa, Yesu alizikubali dhambi
za dunia zilizopitia katika mwili wake. Zaburi 32:1
inasema, “Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake” Neno ‘kusitiriwa’
lina maana kuchukua dhambi na kuzikubali dhambi na 1
Petro 3:21 inasema “mfano wa mambo hayo ni ubatizo unaowaokoa ninyi pia siku
hizi (sio kuwekea mbali uchafu wa mwili bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu)
kwa
kufufuka kwake Yesu kristo” kwa ubatizo aliopokea kutoka kwa Yohana
dhambi zote za wanadamu zimeondoshwa moja kwa moja.
Pili, Biblia inatuambia
kuwa Yesu ameondosha dhambi za dunia. Isaya 43:25
inasema, “Mimi, naam mimi ndiye niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala
sitazikumbuka dhambi zako” kuyafuta makosa maana yake ni kuyapoteza
kabisa kutoka katika maandishi.
Ina maana, Mungu baba amesafisha dhambi za dunia kwa kuzipitisha
kwa mwanae kwa njia ya ubatizo. Kwa wale kati yetu wanaoweza kusema “sina
tumaini kwa kuwa nimetenda dhambi nyingi sana” wao pia wanaweza kuwekwa huru
mbali na dhambi kwa kulisikia Neno la Injili ya maji na Roho. Shetani
anatuambia, “Je hujatenda dhambi nyingi?” Lakini hata kama tungesikia maneno
hayo, tukiamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani hapo tunaweza kukombolewa
kutoka dhambini. Tukiwa na imani kama hii, shetani hupata woga na kukimbia. Tumshawishi
kuwa Bwana amesamehe dhambi kwa njia ya ubatizo na damu yake msalabani.
Tukiamini kuwa Yesu amesamehe dhambi kwa njia ya ubatizo na damu yake msalabani
ndipo amani ya ajabu huingia maishani mwetu. Hii ndio imani kuu ya ukristo,
Imani ya ondoleo la dhambi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni