Yatupasa kuwa mbali na imani ya aina hii. Baadhi ya watu siku
hizi wanaimani potofu kwamba wataweza kumpokea Roho Mtakatifu ikiwa watawekewa
mikono na wale waliokwisha kupokea nguvu hizo. Wao hudhani kwamba kwa kuwa
maandiko yanasema kuwa watu wengi walimpokea Roho Mtakatifu waliposhuhudia
kuwekewa mikono na Mtume, hivyo nao wataweza kufanya namna hiyo pia. Baadhi yao
wanajisingizia kwa imani potofu za aina hii, wanadhani kuwa wataweza kuwapa
wengine Roho Mtakatifu kwa kupitia kuwawekea mikono juu yao. Yatupasa kuwa
makini na kuwepo kwa watu wa aina hii.
Hata hivyo yatupasa kuweka akilini kwamba imani za watu hawa
zinautofauti mkubwa na zile za Mitume wakati wa kipindi cha Kanisa la mwanzo.
Siku hizi jambo kuu lenye kuleta ubishani mkali katika imani za baadhi ya
Wakristo ni kwasababu hawana imani katika Injili ya kweli ya maji na Roho kati
yao. Wengi husema kwamba wanamwamini Mungu lakini hawakumweshimu na hivyo
badala yake hujidanganya nafsi zao na zawenzao. Hata hivyo wenye dhambi kamwe
hawatowezea kudanganya swala la kumpokea Roho Mtakatifu au hata kufanya wengine
wadanganyike. Ikiwa mtu fulani atasema kwamba Roho amekuja juu yake yeye mwenye
dhambi basi roho huyo hakuwa ni yule Roho Matakatifu kweli, bali badala yake ni
roho wa shetani ajifanyaye kuwa Roho wa kweli.
Mitume wakati wa Kanisa la mwanzo walikuwa ni watu waliomjua
na kumuamini Yesu Kristo kuwa ndiye mwokozi aliyechukua dhambi zote za wanadamu
kupitia ubatizo wake alioupokea kwa Yohana na kifo chake msalabani. Waliweza kupokea
Roho Mtakatifu kwa sababu waliamini ukweli juu ya ubatizo wa Yesu na damu yake
pale msalabani. Pia walihubiri Injili ya maji na Roho kwa wengine hivyo kuweza
kuwasaidia katika kuwaongoza kumpokea Roho Mtakatifu.
Lakini siku hizi Wakristo wengi wamempokea katika imani za
kishabiki. Je ni kweli mwenye dhambi katika nyakati hizi ataweza kumpokea Roho
Mtakatifu kupitia kuwekewa mikono
toka kwa mhudumu mwingine aliye na dhambi? Hakika hili halifikiriki.
Wapo watu wanaosema kwamba ingawa wanadhambi moyoni, wamempokea Roho Mtakatifu
ndani yao.
Hata ikiwa mtu anaonekana ni mchungaji mzuri machoni pa kundi
lake kamwe hawawezi kumsababisha yeyote kumpokea Roho Mtakatifu ikiwa yeye mwenyewe anadhambi moyoni.
Hii ndiyo sababu Manabii wengi wa uongo wameweza kuwaongoza
watu kuelekea motoni. Yakupasa uelewe ukweli kwamba wale wote wenye kufundisha
aina hii ya imani ni manabii wa uongo. Hawa ni watu ambao tayari wameshikiliwa na
mapepo. Ikiwa mtu anadhambi moyoni, je, Roho Mtakatifu ataweza kukaa ndani
yake? Jibu ni hapana. Jingine, je, itawezekana kwa mtu aliye na dhambi kuweza
kusababisha mtu mwingine aweze kupokea Roho Mtakatifu? Kwa mara nyingine jibu
ni hapana. Sasa basi nini kinacho sababisha watu wanao semekana kuwa na vipawa
(karismatiki) katika nyakati hizi kuweza kufanya miujiza na maajabu katika ukristo
huku wakiwa bado wanadhambi moyoni mwanao? Mapepo au roho chafu hufanya hivyo.
Roho Mtakatifu kamwe hawezi kuishi ndani ya mwenye dhambi.
Yeye hukaa ndani ya wale tu walio na imani katika Injili ya
maji na Roho. Je? wewe nawe unauhakika roho aliye ndani yako ni Roho Mtakatifu?
Katika Yohana 3:5 Yesu alisema “Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia ufalme wa Mungu.” Kwa namna hii basi Roho Mtakatifu kuweka makazi ndani kutawezekana
kwa wale tu watakao amini injili ya maji na
Roho. Kosa ambalo wakristo wengi wafanyalo nyakati hizi nikwamba,
huamini kwamba mtu ataweza pia kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake kwa kuwekewa
mikono na mtumishi
mwenye dhambi. Hili nikosa kubwa na la hatari. Nyakati hizi,
wakristo wengi na watumishi wao wanaimani na dhamiri zao kwamba, kuwa na Roho
Mtakatifu ndani ya mtu huja kwa kupitia kuwekewa mikono.
Uhusiano kati ya
ondoleo la dhambi la kweli na tendo la kuwekea mikono.
“Kuwekea mikono” ni namna ambayo mtu huweza kutwikwa au
kutoa kitu alicho nacho juu ya kitu kingine. Kwa mfano, ikiwa tutazungumza
katika kipaza sauti, sauti hiyo husafiri kupitia waya toka kipaza sauti na
kutokea upande wa pili kwa sauti kubwa zaidi katika spika ili kila mtu aweze
kusikia. Ndivyo pia katika Agano la kale pale mwenye dhambi alipoweka mikono
yake juu kichwa cha mnyama wa sadaka na hivyo kusamehewa. Kwanjia hiyo pia,
nguvu ya Mungu
huwekwa
juu ya mtu kwa mtu kwa tendo la kuwekewa mikono toka kwa mtumishi wake. Hivyo
tendo la kuwekea mikono limechukua maana ya “kuhamisha, kutwika”.
Watu wanaojiita ni wenye vipawa (wanakarismatiki) hawawezi
kamwe kusababisha mtu kuweza kuwa na Roho Mtakatifu ndani yake kwa njia ya kuwekea
mikono, badala yake kusababisha watu hao kupokea roho chafu. Lazima ukumbuke kwamba
mtu aliye na nguvu za roho chafu huamisha roho hizo kwa wengine kupitia tendo
la kuwekea mikono. Mtu aliye tawaliwa na mapepo anapoweka mikono juu ya kichwa
cha mwingine, pepo lililomo ndani yake huingia ndani ya mtu huyo kwa sababu
shetani hutenda kazi kupitia wenye dhambi.
Kwasababu hiyo basi kila mtu imemlazimu kuamini injili ya maji
na Roho ikiwa anataka kupokea Roho Mtakatifu ndani yake. Shetani hutawala wale
wote walio na dhambi hata ikiwa
wanamwamini Yesu, huku wakiwa wameshindwa kupokea ondoleo la
dhambi.
Ikiwa mtu atapokea tendo la kuwekewa mikono toka kwa mtu
aliye na mapepo, mapepo hayo yatahamia juu yake mtu huyo, hivyo naye pia moja
kwa moja ataweza kufanya miujiza ya uongo. Yatupasa kujua kwamba mapepo huja na
kufanya makazi ndani ya mtu kwa kupitia tendo la kuwekewa mikono.
Na kumpokea Roho Mtakatifu ndani huwezakana tu kwa imani katika
injili ya maji na Roho.
Tendo la kuwekea mikono ni njia mahususi iliyo wekwa na Mungu
katika kutwika kitu juu ya kingine. Lakini shetani husababisha watu wengi kupokea
roho chafu kwa kupitia tendo hilo. Ukweli ni kwamba watu wengi nyakati hizi
hujaribu kununua nguvu za Roho Mtakatifu kwa fedha na hivyo kufanya tatizo hili
kuwa kubwa zaidi.
Wakristo wengi wanaufahamu wa kimakosa juu ya ukweli wa kuwa
na Roho Mtakatifu ndani. Tulipouliza kwa namna gani wataweza kumpokea Roho
Mtakatifu ndani yao, wengi wa watu
hujibu kwamba inawezekana kwa kupitia sala za toba na kufunga.
Hili si kweli kabisa. Je, nikweli Roho Mtakatifu huja juu yako pale unapo fanya
maombi maalumu kwa Mungu?
Hapana kuweza kuwa na Roho Mtakatifu ndani yako huja kwa wale
tu wanao amini injili ya maji na Roho. Kwa kuwa Mungu ni kweli ameweka sheria
kwa ajili ya kuweza kupokea Roho Mtakatifu ndani. Je, Roho Mtakatifu ataweza
kuwa ndani ya mtu aliye na dhambi moyoni? Jibu bila shaka hapana. Mtu hawezi kumpokea
Roho Mtakatifu kupitia tendo la kuwekewa mikono. Hata ikiwa mtu atahudhuria mikutano
ya uamsho na maombi ya uchungu kwa Mungu ili aweze kupokea nguvu ya Roho
Mtakatifu, Roho Mtakatifu atabaki kuwa mbali naye. Wenye dhambi hakika
hawatoweza kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu ndani yao. Wenye dhambi wataweza
kupokea kipawa hicho cha Roho Mtakatifu ikiwa tu watapokea ondoleo la dhambi
kwa kuamini Injili ya maji na Roho.
Yeyote asiyefahamu injili ya maji na Roho, kamwe hatoweza
kumpokea Roho Mtakatifu. Siku hizi injili ya maji na Roho imeenea kwa kasi
kupitia vitabu, mikutano ya makanisa, tovuti na hata vitabu vya kielectronikali
ulimwenguni pote. Hivyo, yeyote anayetafuta ukweli wa injili, ataweza kuamini
hili na kuweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake. Ikiwa bado hujampokea,
yakupasa uelewe kwamba ili uweze kumpokea ni lazima uamini injili ya maji na
Roho.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni