Katika 1Yohana1:10 inasema “tukisema kwamba hatukutenda
dhambi twamfanya yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.Hapajatokea
yeyote ambaye hajatenda dhambi mbele ya Mungu. Hata biblia inasema “bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani
ambaye afanyaye mema asifanye dhambi” (Mhubiri
7:20).Watu wote hutenda dhambi mbele ya Mungu.
Ikiwa mtu
yeyote atasema kwamba hajatenda dhambi basi ni muongo. Watu hutenda dhambi
maishani mwao pote hadi saa ya mwishoni kabla ya kufa, na hii ndiyo maana Yesu
alibatizwa na Yohana ili kubeba dhambi hizo zote. Ikiwa hatujawahi kutenda
dhambi basi tusingelihitaji kumwamini Mungu kuwa ni mwokozi. Bwana anasema “neno
langu si neno lako” kwa wale wenye fikra wakidhani kuwa hawajatenda dhambi.
Ikiwa mtu
hana imani katika injili njema ya maji na Roho basi anastahili kuangamia. Ikiwa
mtu mwenye haki au mwenye dhambi atasema kwamba hajatenda dhambi mbele za
Mungu, basi huyo hatastahili kuiamini injili njema.
Bwana
amempa kila mmoja zawadi nzuri ya injili njema. Tulikiri dhambi zetu zote nakutubu
ilikupokea msamaha kwa injili njema. Tunaweza kuirudia injili hii ambayo Mungu
aliyo tupatia kama msamaha wa dhambi zetu na kuiamini ili kuweza kuwa na
usharika wa Roho Mtakatifu. Maana ya kweli ya usharika wa Roho mtakatifu ipo
katika injili ya maji na Roho, na pia kwa wale tu walio na injili hii ndiyo
watakao weza kuwa na ushirika na Mungu.
Wanadamu
walikuwa mbali na Mungu kwa sababu ya dhambi walizorithi kwa Adamu na Hawa.
Lakini leo hii sisi tuliokuwa tumerithi mbegu ya uovu tunaweza kutarajia kuwa
na usharika na Mungu kwa mara nyingine tena. Ili kuweza kufanikisha hayo yote
ni lazima tuwe na imani ya injili ya maji na Roho toka kwa Yesu Kristo, na
hivyo kuwa na msamaha wa dhambi ambazo zilituweka mbali na Mungu.
Wale wote
wenyekuamini injili njema ndiyo watakao okolewa kutokana na dhambi zote, na
hapo basi Mungu atawajaza Roho Mtakatifu. Wenye haki wataweza kuwa na ushirika
na Mungu kwa kuwa wamempokea Roho Mtakatifu. Kwa wale wote waliowekwa mbali na
Mungu kutokana na dhambi zao lazima wairudie injilinjema ya maji na Roho na kuiamini
na hapo ndipo watakapoweza kuanza kuwa na ushirika na Mungu.
Kuwa na
Roho Mtakatifu ndani huja kutokana na imani katika injili njema. Lazima tujue
kwamba kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu huja pale tunapoamini injili ya maji
na Roho tu. Kuiamini injili njema
ndiko kunako jenga njia mpya kumuelekea Mungu. Bwana amevunja ukuta wa kati
ulio kuwa ukitutenganisha naye kwa sababu ya dhambi zote mbili, yaani dhambi
tuzitendazo maishani na ile dhambi ya asili, na hivyo tutaruhusiwa kuwa na
ushirika na Mungu kwa kupitia imani yetu katika injili njema ya maji na Roho.
Yatupasa
kuanzisha upya ushirika na Roho Mtakatifu kwa mara nyingine tena. Usharika wa
kweli na Roho Mtakatifu hufanikishwa kwa kupita kuelewa injili ya maji na Roho na
kutii kwa imani. Ushirika wa Roho Mtakatifu huja pale tunapokuwa na imani ya
kweli na msamaha wa dhambi ambao unatokana na injili njema. Wale wote ambao
wahajapokea msamaha wa dhambi kamwe hatoweza kuwa na ushirika wa Roho
Mtakatifu.
Kwa
maneno mengine hakuna yeyote atakaye weza kuwa na ushirika wa Roho Mtakatifu
pasipo kuiamini injili ya maji na Roho. Ikiwa bado ni vigumu kwako kuwa na
ushirika wa Roho Mtakatifu basi ni lazima kwanza ukubali kwamba bado hajaamini
injili ya maji na Roho na hivyo dhambi zako hazijasafishwa. Je, unatamani kuwa
na uhusiano na Roho Mtakatifu? Sasa basi amini injili iliyokamilishwa kwa
ubatizo wa Yesu na damu yake. Ndipo hapo tu utaweza kusamehewa dhambi zako zote
na thawabu yako itakuwa ni kumpokea Roho Mtakatifu ndani ya moyo wako. Injili
hii njema kwa hakika ndiyo inayotuletea ushirika na Roho Mtakatifu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni