Jumamosi, 1 Machi 2014

MSINGI WA IMANI ULIYOWEKWA NA VIFAA VYA UJENZI WA HEMA TAKATIFU LA KUKUTANIA

.
Somo la kwanza
(Kutoka 25:1-9) “BWANA akanena na Musa, akamwambia: waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu. Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii: dhahabu, na fedha, na shaba; na nyuzi za rangi ya bluu (samawiti), na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani safi, na singa za mbuzi; na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pompoo, na miti ya mshita; na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri; na vito vya shohamu, na vito vingine vya kutiwa kwa ile naivera, na kwa kile kifuko cha kifuani. Nao wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao. Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mtakavyo vifanya.”
Baada ya Mungu kumpatia Musa amri kumi na sheria 613, kisha mungu akamwita Musa kwenda mlimani kwa mara nyingine, wakati huu alimwita ili kumwamuru kulijenga Hema takatifu la kukutania.
Kulikuwa na lengo mahususi ambalo kwa hilo Mungu alimwambia kuzileta sadaka hizi. Lengo hilo lilikuwa ni kuijenga hapa duniani nyumba ya Mungu yenye kung’aa, mahali ambapo hapana dhambi na ambapo Mungu atakaa , ili aweze kukutana na watu wa Israeli na kuzifanya dhambi zao kutoweka. Hata hivyo, hii haimaanishi kuwa Mungu aliwaeleza kuleta fedha ili kujenga jumba la kumbukumbu kama yalivyo makanisa ya leo. Manabii wa uongo wa Ukristo wa leo wanatumia kifungu hiki vibaya pale wanapotaka kuyajenga makanisa yao ili kuzitimiza tamaa zao binafsi.
Kwa kweli, sababu iliyomfanya Mungu apokee sadaka hizi ilikuwa ni kwa ajili ya kutukomboa sisi toka katika dhambi zetu na kutuokoa toka katika hukumu yetu. Pia ilikuwa kwa ajili ya Mungu ili aweze kukutana nasi, sisi ambao tulikuwa tukiishi maisha yenye huzuni ya kutisha, ili aweze kuziosha dhambi zetu na kuzifanya zitoweke, na kutufanya sisi kuwa watu wake mwenyewe.
MAANA YA KIROHO YA SADAKA AMBAZO MUNGU ALIAMURU ALETEWE
 Kabla hatujaenda mbali, hebu  tutumie muda kidogo kutafakari juu ya maana ya kiroho ya sadaka hizi ambazo Mungu aliamuru aletewe. Baada ya kutafakari tutaichunguza imani yetu kwa mtazamo wa sadaka hizo.
DHAHABU, FEDHA NA SHABA
Kwanza ni lazima tuchunguze mahali ambapo dhahabu, fedha, na shaba vilitumika. Katika Hema Takatifu la kukutania, dhahabu ilitumika kwa ajili ya mahali patakatifu, Patakatifu pa patakatifu, na vifaa vilivyokuwamo ndani ya hizo sehemu takatifu ikiwemo kinara cha taa, meza ya mkate wa wonyesho, madhabahu ya uvumba, kiti cha rehema, na snduku la ushuhuda.
Dhahabu inamaanisha neema ya wokovu. Inatueleza kuwa ni lazima  tuwe na imani inayoamini katika zawadi ya wokovu iliyotolewa bure na kwa ukamilifu na masihi, na imani ambayo inaamini kuwa Bwana wetu amezichukuwa dhambi zetu zote na kwamba alihukumiwa kwa ajili yetu.
Kwa upande mwingine, shaba, ilitumika katika vitanzi vya nguzo za Hema takatifu la kukutania, katika vigingi vyake, birika la kunawia, na madhahabu ya sadaka ya kuteketezwa. Vifaa au vyombo vyote vya shaba vilifunikwa au vilipigiliwa ardhini. Hii inamaanisha juu ya hukumu ya dhambi za watu, pia shaba inatueleza kuwa tunahukumiwa adhabu na Mungu kwa kushindwa kuitunza na kuifuata Sheria kwa sababu ya dhambi zetu.
Je, ni namna ipi ya kiroho ya dhahabu, fedha, na shaba? Vitu hivi vinaunda misingi ya imani katika kupokea zawadi ya wokovu iliyotolewa na Mungu. Biblia inatueleza kuwa sisi sote ni wenye dhambi ambao hatuwezi kuifuata sheria kikamilifu, na kwamba tunastahili kufa kwa sababu ya dhambi zetu kwa kufanyika sadaka ya kuteketezwa ya dhambi ambayo ilitolewa katika Hema takatifu la kukutania.
Ili kutatua tatizo la dhambi zao, wenye dhambi walileta mnyama asiye na mawaa katika Hema Takatifu la kukutania, na kwa mujibu wa taratibu wa sadaka ya kuteketezwa, walipeleka dhambi zao katika mnyama huyo wa sadaka kwa kuiwekea mikono yao juu ya kichwa chake; kisha sadaka ile ya kuteketezwa ambayo ilizipokea dhambi zao na kumwaga damu yake na kuuawa. Kwa kufanya hivyo, watu wa Israeli ambao walikuwa  wamefungwa kuzimu (shaba), waliweza kupokea ondoleo la dhambi zao (fedha), na walikwepa adhabu ya dhambi zao kwa imani (dhahabu).
NYUZI ZA BLUU (SAMAWITI), ZAMBARAU, NYEKUNDU NA KITANI SAFI YA KUSOKOTWA.
 Hapa kuna vifaa vingine vilivyotumika mara kwa mara; nyuzi za bluu, zambarau, na nyekundu, na kitani safi ya kusokotwa. Nyuzi hizi zilitumika katika lango la ua wa Hema takatifu la kukutania, lango la mahali patakatifu, na katika pazia lilotenganisha kati ya mahali patakatifu na patakatifu pa patakatifu. Nyuzi hizi nne zinatueleza juu ya ukweli kuwa kama ilivyo tabiriwa katika Mwanzo 3:15, kwamba Bwana atakuja kama sehemu ya uzao wa mwanamke, na kuwaokoa wenye dhambi toka katika dhambi zao kwa kubatizwa na kusulibiwa, na kwamba ni mungu mwenyewe ndiye atakaye tuokoa sisi.
Nyuzi nne hazikutumika tu kwa ajili ya malango ya Hema Takatifu la kukutania, bali zilitumika pia katika mavazi ya kuhani mkuu na yalitumika kama kifuniko cha kwanza cha Hema takatifu la kukutania. Hili lilikuwa ni Agano la mungu kwamba Yesu Kristo atakuja hapa duniani na kutuokoa toka katika dhambi zetu kwa kutimiza kazi zake za nyuzi za bluu, zambarau, na nyekundu. Kwa kweli Bwana wetu alitekeleza ahadi hii na kwa hakika ametuokoa toka katika dhambi za ulimwengu.
Sehemu ya msingi katika malango ya Hema takatifu la kukutania ni nyuzi za bluu. Kwanini Yesu Kristo kama masihi alikuja hapa duniani na kufa msalabani? Ni kwasababu Yesu alibatizwa. Nyuzi za bluu zinatuonyesha juu ya ubatizo wa Yesu, nyuzi za zambarau zinatueleza kuwa Yesu ni mfalme (Yohana 19:2-3),na nyuzi nyekundu zinatueleza juu ya kusulubiwa kwake na kumwaga damu yake. Nyuzi hizo zote ni vifaa vya ujenzi, ambavyo ni muhimu sana kutuonyesha jinsi Yesu alivyokuja hapa duniani na kuchua dhambi zetu katika mwili wake.
Watu wengi katika ulimwengu huu wanasisitiza kuwa Yesu ni mwana wa Mungu tu, na kwamba kimsingi yeye ni Mungu mwenyewe. Lakini anatueleza wazi kupitia Hema takatifu la kukutania kwamba mafundisho ya jinsi hiyo hayawezi kuwa ndiyo kweli kamili.
Mtume petro katika 1Petro 3:21, “mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unao waokowa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamira safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.”
Hii inatuonyesha sisi kuwa Yesu aliitimiza ahadi ya wokovu na akaweka msingi wa imani mkamilifu kwa kupokea ubatizo wake, mfano unao tuokoa sisi. Masihi wetu ni nani? Maishi maana yake ni mwokozi, neno hili linatueleza kuwa Yesu alikuja hapa duniani, alibatizwa ili kuzichukuwa  dhambi zetu zote  na dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa njia ya  ubatizo.
Mungu aliwaeleza Waisraeli kulijenga lango la ua wa Hema takatifu la kukutania kwa kufuma nyuzi za bluu, zambarau na nyekundu na kitani safi ya kusokotwa. Na dhumuni la Bwana wetu, ambaye ndiye mfalme wa wfalme na Bwana wa mbingu, kuja hapa duniani katika mwili wa mwanadamu ilikuwa ni kuutimiza ukweli wa nyuzi za bluu, zambarau, na nyekundu na kitani safi ya kusokotwa. Bwana wetu alikuja katika mwili wa mwanadamu na akaupokea ubatizo ambao ungeittimiza haki yote ya Mungu toka kwa Yohana Mbatizaji, ambaye ni mwakilishi wa wanadamu.
Hii inafanana na sadaka ya kuteketezwa ya Agano la kale ambayo ilizipokea dhambi za Waisraeli  ambazo zilipitishwa katika sadaka hiyo kwa kuwekewa mikono na kuhani mkuu katika kichwa chake na kwamba mnyama huyu wa sadaka alihukumiwa kwa dhambi hizo akiwa mbadala kwa dhambi za Waisraeli waliokosa. Kwa maneno mengine, kama ilivyo kuwa kwa sadaka ya kutetezwa ya Agano la kale, Yesu alikuja katika Agano jipya kama sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi za wanadamu, alibatizwa, alisulubiwa, na kwa hiyo alibeba adhabu yote ya dhambi za ulimwengu. Yesu aliutimiza ukweli wa nyuzi za bluu kwa kubatizwa na Yohana kama mwana kondoo wa Mungu wa sadaka. Kwa ubatizo huu Yesu alizichukuwa dhambi za wanadamu katika mwili wake mara moja na kwa wote.
Na nyuzi nyekundu zinamaanisha damu ya Yesu. Sababu iliyomfanya Yesu Kristo akasulubiwa, akamwaga damu yake, na akafa msalabani ni kwa sababu dhambi zetu zote zilikuwa zimepelekwa kwake kupitia ubatizo.  Ni kwa sababu Yesu alizichukuwa dhambi zetu kwa ubatizo wake alioupokea toka kwa Yohana Mbatizaji ndipo alipoweza kufa msalabani, na kwa sababu ya ukweli huu kwamba sadaka ya pale msalabani kwa ajili yetu haikuishia pasipo maana.
Nyuzi za zambarau zinamaanisha kuwa Yesu Kristo ni Mungu na mfalme, lakini kama asingebatizwa na Yohana Mbatizaji ambaye ni mwakilishi wa wanadamu, na kama asingelikuwa amezichukuwa dhambi zetu katika mwili wake (nyuzi za bluu), Haijalishi ni kwa kiwango gani cha mateso na maumivu aliyopata (nyuzi nyekundu), kifo chake kingekuwa hakina maana. Kitani safi ya kusokotwa inatueleza sisi kuwa neno la unabii ambalo Mungu aliliongea katika Agano la kale limetimizwa lote katika Agano jipya.

Soma mwendelezo wa somo hili………………

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni