Jumapili, 9 Machi 2014

BIRIKA LA KUNAWIA


(Kutoka 30:17-21) “BWANA akanena na Musa, na kumwambia, Fanya na birika la shaba, na kitako chake cha shaba, ili kuogea; nawe utaliweka kati ya Hema takatifu la kukutania na madhabahu, nawe utalitia maji. Na Haruni na wanawe wataosha mikono yao na miguu yao humo; hapo waingipo ndani ya hema takatifu la kukutania; watajiosha majini, ili wasife; au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike, kumtengenezea BWANA sadaka ya moto; basi wataosha mikono yao na miguu yao ili kwamba wasife; na neno hili litakuwa amri kwao milele, kwake yeye na kwa wazao wake katika vizazi vyao vyote.”
Birika la kunawia katika Ua wa Hema takatifu la kukutania
Vifaa: ilitengenezwa kwa shaba, ilikuwa imejazwa na maji wakati wote.
Maana ya kiroho: Shaba ina maanisha hukumu ya dhambi zote za mwanadamu, Yesu alizichukuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana. Kwa hiyo, maana ya birika la kunawia ni kwamba tunaweza kuoshwa dhambi zetu zote kwa kuamini kwamba dhambi hizi zote zilpitishwa kwa Yesu kwa kupitia ubatizo wake.
Makuhani waliohudumu katika Hema takatifu la kukutania pia waliosha mikono yao na miguu yao katika birika la kunawia kabla ya kuingia katika Hema Takatifu la kukutania na kwa hiyo walikiepuka kifo chao. Shaba inamaanisha hukumu ya dhambi, na maji ya kwenye birika la kunawia yanamaanisha ubatizo ambao Yesu aliopokea toka kwa Yohana na ambao kwa huo alizichuwa dhambi za ulimwengu katika mwili wake. Kwa maneno mengine, birika la kunawia linatueleza kuwa Yesu alizipokea dhambi zetu zote zilizopitishwa kwake na akabeba adhabu ya dhambi hizi. Maji katika birika la kunawia yanamaanisha, katika Agano la kale, nyuzi za bluu za hemataktifu la kukutania, na katika Agano jipya, ubatizo ambao Yesu aliopokea toka kwa Yohana (Mathayo 3:15, 1petro 3:21).
Kwa hiyo, birika la kunawia linamaanisha ubatizo wa Yesu, na ni mahali ambapo tunathibitisha imani yetu katika ukweli kuwa Yesu alibeba dhambi zetu zote, zikiwemo dhambi zetu halisi, na akazioshelea mbali zote mara moja kwa kupitia ubatizo alioupokea toka kwa Yohana Mbatizaji.
Watakatifu ambao wameokolewa toka katika dhambi zao kwa imani wamevishwa neema ya Mungu  kwa kuyaamini maji ya kwenye birika la kunawia (ubatizo wa Yesu), Shaba (hukumu ya Mungu kwa dhambi zote), na kwamba Yesu amewakomboa toka katika dhambi zao. Ingawa tuna wingi wa udhaifu na mapungufu kiasi kwamba hatuwezi kujitambua sisi wenyewe kuwa ni wenye haki, kwa hakika tunaweza kudhibitisha kwamba sisi ni wenye haki wakamilifu kwa kuiweka tena na tena imani yetu katika ubatizo wa Yesu (kuzibeba dhambi, maji) na damu yake iliyomwagwa msalabani (adhabu ya dhambi, shaba). Kwa sababu tunaliamini Neno la Mungu ambalo limekwisha kutuokoa sisi sote toka katika dhambi zetu na adhabu ya dhambi hizi, basi tunaweza kufanyika wenye haki wasio na dhambi.
Neno la Mungu tunaloliamini linatueleza sisi kuwa Yesu alizichukuwa dhambi zetu katika mwili wake kwa kupitia ubatizo wake alioupokea toka kwa Yohana, akamwaga damu yake msalabani ili kuibeba adhabu yote ya dhambi badala yetu, na kwa hiyo ametuokoa sisi kikamilifu toka katika dhambi zetu. Mungu aliliweka birika la kunawia katika ua wa Hema Takatifu la kukutania ili kwamba tuweze kudhibitisha kwa imani yetu kuwa sisi ndiyo tuliookolewa kikamilifu toka katika dhambi zetu zote bila kujali hali inavyoweza kuwa.
Matumizi ya birika la kunawia
Birika la kunawia lilitumika katika kuosha uchafu wote wa makuhani walipofanya kazi katika Hema Takatifu la kukutania wakitoa sadaka kwa Mungu. Ilihitajika kuyaosha madoa ambayo makuhani waliyapata katika kuua mwanasadaka wa kuteketezwa, katika kuikinga damu yake, na katika kuikata vipande ili kumtolea Mungu sadaka ambayo itawapatanisha watu wa Israeli na Mungu toka katika dhambi zao. Wakati makuhani walipochafuliwa walipokuwa wakitoa sadaka, iliwapasa kuoshwa kwa maji, na birika la kunawia lilikuwa ni mahali ambapo uchafu huu wote ulisafishwa.
Tunapofanya dhambi, kiroho au kimwili, na kila inapotokea kuwa tumechafuliwa kwa kuzivunja amri za Mungu, ni lazima tuoshelee mbali uchafu wetu wote katika birika hili la kunawia. Ilipotokea kuwa miili ya makuhani imegusa kitu chochote kichafu, walipaswa kwa lazima kuosha sehemu zilizochafuka katika miili yao kwa maji.
Vivyo hivyo, inapotokea kuwa wale wanaoamini katika Mungu wamegusana na kitu chochote kisicho safi na kichafu, maji ya birika la kunawia yanatumika kuoshelea mbali huo uchafu wote. Kwa kifupi, maji ya birika la kunawia yalitolewa ili yatumike katika kuuosha uchafu wa waliozaliwa upya. Kwa hiyo, birika la kunawia lina rehema za Mungu. Maana ya birika la kunawia si kitu cha kuchagua ambacho tunaweza kuchagua kuamini au kutoamini, bali ni kitu cha muhimu na lazima kwa wale wanaomwamini Yesu.
Mungu alitoa vipimo kwa vifaa vingine vyote katika Hema Takatifu la kukutania, akatoa vipimo maluumu jinsi ambavyo vitakuwa na dhiraa kadhaa kwa kimo, urefu, na upana. Lakini hakutoa kipimo cha birika la kunawia. Hii ni tabia ambayo inaapatikana tu katika birika la kunawia. Hii inadhihirisha upendo usiokoma ambao masihi ametupatia sisi, ambao tunatenda dhambi halisi kila siku. Katika upendo huu wa masihi  kunapatikana ubatizo wake, aina ya kuwekewa mikono ambayo inaziosha dhambi zetu zote. Kama ambavyo maji mengi yalitumika wakati makuhani walipokuwa wamechafuka wakati wakitekeleza majukumu yao, ilikuwa ni lazima birika la kunawia lijazwe maji wakati wote. Kwa hiyo, kipimo cha birika la kunawia kilitegemeana na hitaji hili. Kwa sababu birika la kunawia lilitengenezwa kwa shaba, basi kila ilipotokea makuhani wakinawa, walikuwa wanafikiria juu ya hukumu ya dhambi.
(Waebrania 10:22) inasema “tumeoshwa miili kwa maji safi”,  na (tito3:5) “ kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa mara ya pili na kufanywa upya na Roho mtakatifu.” Kama Vifungu hivi vinavyoonyesha, Neno la Agano Jipya pia linatueleza sisi kuhusu kuuosha uchafu kwa maji ya ubatizo.

Ikiwa makuhani waliosha uchafu wao walioupata katika maisha yao kwa maji ya birika la kunawia, sisi wakristo wa leo tuliozaliwa upya, tunaweza kuzioshelea mbali dhambi zetu Halisi zote zilizofanywa katika maisha yetu kwa kuamini ubatizo wa Yesu. Maji ya birika la kunawia la Agano la kale yanatuonyesha sisi kuwa Masihi alikuja hapa duniani na amezisafishaia mbali dhambi zote za ulimwengu kwa ubatizo aliopokea toka kwa Yohana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni