(Matendo 4:12) inasema, “Wala hakuna
wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya
mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”
Kwa sababu tunaamini katika ubatizo wa Yesu na damu yake
msalabani, basi sisi tutaingia Mbinguni. Hakuna njia nyingine ya kuingia
Mbinguni bali kwa kuamini katika Injili ya kweli. Ni kwa kuamini tu katika yale
ambayo Yesu amefanya kwa ajili yetu ndipo tunapoweza kuingia Mbinguni, kwa kuwa
Mungu amefanya kazi hizo kwa wale wanaoamini katika Injili ya maji na roho (ipo
katika blog hii).
Hii ndiyo sababu Wakristo hawawezi kuingia Mbinguni kwa
kupitia jitihada zao wenyewe, kwa kujitoa, au majaribio mengine ya kinafiki. Mungu
amedhamiria kuwa ni wale tu ambao wamesafishwa dhambi zao kwa kuamini katika
ubatizo wa Yesu alioupokea na katika damu yake aliyoimwaga ndiyo wanaweza
kuingia Mbinguni. Wale wanaoamini katika ukweli huu ndio wale wanaoamini kwamba
Yesu ni mwana wa Mungu, Mungu mwenyewe, na mwokozi wa milele ambaye amewaokoa
toka katika dhambi kwa kupitia ubatizo wake na damu yake aliyomwaga. Mungu
ameruhusu kusafishwa dhambi kwa watu kama hao
Theolojia haina nafasi yoyote katika kuifahamu Biblia
kiusahihi na kikamilifu. Theologja ni ufahamu wa kibinadamu si wa Roho
mtakatifu. Ndiyo maana kuna lundo la mafundisho ya kikristo na theolojia ambazo ziliinuka katika historia ya ukristo,
watu wengi wameanguka katika mafundisho ya kimafumbo hali wakimwanini Mungu kwa
kutegemea katika uzoefu wao binafsi. Lakini pamoja na tofauti za kitheolojia,
matawi yote ya ukristo yametawaliwa na imani moja kimsingi, ambayo ni kuamini
katika damu ya Yesu tu.
Lakini je, huu ni ukweli? Unapoamini kwa namna hii, je,
dhambi zako zitatoweka kweli? Unafanya dhambi kila siku kwa moyo wako , mawazo,
na matendo. Unaweza basi kuondolewa dhambi zako kwa kuamini katika damu ya Yesu
tu ambayo alimwaga msalabani? Kule kusema kuwa Yesu alizibeba dhambi zetu kwa
kubatizwa na kufa msalabani huo ni ukweli wa kibiblia. Hata hivyo kuna watu
wengi sana ambao wanasema kuwa dhambi zao zimeondolewa kwa kuamini katika damu
ya Yesu tu pale Msalabani na kwa kutoa sala zao za toba kila siku. Je, dhambi
za dhamira zako zilisafishwa mbali kwa kutoa sala za toba za jinsi hiyo? Hii
haiwezekani.
Ikiwa wewe ni mkristo, basi ni lazima ufahamu na kuamini
katika wokovu wa kweli kwamba Yesu alikuja hapa duniani na akazichukuwa dhambi
zetu zote za ulimwengu katika mwili wake kwa kubatizwa na Yohana. Pamoja na
haya, je, bado unaudharau ukweli huu, kiasi kuwa hutaki hata kuufahamu na kisha
kuamini? Ikiwa ndivyo, basi ufahamu kuwa unafanya dhambi ya kumdhihaki Yesu,
dhambi ya kulishusha na kulidharau jina lake, na kwa jinsi hiyo huwezi kusema
kuwa unaamini kweli katika Yesu kuwa ni mwokozi wako. Kwa kuuacha ubatizo wa
Yesu Kristo na kwa kumwamini Yesu kwa namna yoyote unayoipenda, basi kwa kweli
huwezi kuvikwa katika neema ya wokovu, (soma Injili ya maji na roho katika blog
hii utaelewa nachokisema).
Njia ni moja tu ya kuingia Mbinguni (Mathayo
7:13-14) “ingieni
kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana
iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni
mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache” kuna dini nyingi sana duniani ambazo zimefanikiwa
kujikusanyia watu wengi kwa njia mbali mbali, usiangalie wingi wa watu, maana
waionao njia ni wachache. Watu wengi wanapoteza muda kukosoa madhebu ya
wengine, hata wale wasio wakristo mahubiri yao yamekuwa ni ya kukosoa
ukristo. Lakini ndugu unapoteza muda
bure, Biblia si kama vitabu vingine ambavyo unaweza kuvisoma kwa kutumia akili
za kibinadamu, inahitajika hekima ya Mungu, soma fungu hili (1wakorintho
2:10-15) “lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote,
hata mafumbo ya Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu
ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna
ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukupokea roho ya dunia, bali Roho
atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo
twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali
yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni.
Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”
Wale wanao ichambua Biblia kwa kutumia akili zao waache mara
moja, wajisalimishe kwa Yesu, na wasome katika blog hii “Injili ya maji na roho”
ili waweze kupokea Roho mtakatifu. Kuna wengine husoma na kudharau, lakini
kumbuka bila Roho mtakatifu Biblia utaisoma kama kitabu cha hadithi na shetani
atakufunga katika fikira zako. (2 Korintho 4:3-4) “lakini ikiwa Injili yetu imesitirka, imesitirika kwa hao wanaopotea,
ambao ndani yao Mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao, isiwazukie nuru ya
Injili ya utakatifu wake Kristo aliye sura yake Mungu”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni