Jumatatu, 3 Machi 2014

MSINGI WA IMANI KATIKA UKRISTO


Somo la pili
Somo hili ni mwendelezo kutoka somo lenye kichwa “MSINGI WA IMANI ULIYOWEKWA NA VIFAA VYA UJENZI WA HEMA TAKATIFU LA KUKUTANIA”.
Sheria ni kivuli cha mambo mazuri yatakayo kuja, Vifaa vya ujenzi vya hema takatifu la kukutania vinatuonyesha sisi kuwa Bwana wetu alikuja hapa duniani katika mwili wa mwanadamu, akazichukuwa dhambi zetu katika mwili wake, kwa ubatizo wake,akabeba adhabu ya dhambi zetu kwa kusulubiwa kwake, akafufuka tena toka kwa wafu, na kwa hiyo amefanyika kuwa mwokozi wetu.
 (Kutoka 25:1-9) “BWANA akanena na Musa, akamwambia: waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu. Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii: dhahabu, na fedha, na shaba; na nyuzi za rangi ya bluu (samawiti), na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani safi, na singa za mbuzi; na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pompoo, na miti ya mshita; na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri; na vito vya shohamu, na vito vingine vya kutiwa kwa ile naivera, na kwa kile kifuko cha kifuani. Nao wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao. Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mtakavyo vifanya.”
MAANA YA KIROHO YA SINGA ZA MBUZI, NGOZI YA KONDOO DUME ILIYOTIWA RANGI NYEKUNDU, NA NGOZI YA POMPOO
Vifaa hivi vilitumika katika kujenga mapaa ya Hema takatifu la kukutania. Paa la kwanza lilifumwa kwa nyuzi za bluu, zambarau, na nyekundu na kitani safi ya kusokotwa ambapo paa la pili la singa za mbuzi lililazwa. Kisha lilifunikwa kwa ngozi ya kondoo dume iliyotiwa rangi nyekundu na mwisho ngozi ya pompoo ililazwa juu yake. Kwa njia hii aina nne tofauti za tabaka la paa zililifunika hema takatifu la kukutania.
Paa la mwisho ambalo lilifunika Hema takatifu la kukutania lilikuwa la ngozi za pompoo. Kwa hiyo kilichoonekana katika uso wa paa la hema takatifu la kukutania lilikuwa ni hizi ngozi nyeusi za pompoo. Pompoo ni mnyama anayepatikana baharini. Kipimo cha ngozi ya pompoo ni kama kipimo cha mtu na pengine ni ndogo zaidi kuliko kipimo cha mtu, na aina hii ya ngozi ilikuwa haipitishi maji. Hii ndiyo sababu ngozi ya pompoo ilitumika kuezekea paa la Hema takatifu la kukutania. Kwa sababu ya hili, hali ya nje ya hema takatifu la kukutania Haikuwa ya kuvutia, na bila shaka halikuwa na mvuto wa kuangalia. Hii ianatueleza sisi kuwa wakati Yesu alipokuwa hapa duniani kwa ajili yetu, kwa hakika alikuja katika hali ya chini kama ilivyo kuwa hali ya nje ya hema takatifu la kukutania, hakukuwa na kitu cha kutamanisha katika mwonekano wake.
Ngozi ya kondoo dume iliyotiwa  rangi nyekundu inatueleza kuwa Yesu Kristo atakuja hapa duniani na atasulibiwa kwa ajili yetu, ilhali singa za mbuzi zinatueleza kuwa atatuokoa kwa kubatizwa kama sadaka yetu ya kuteketezwa na kwa hiyo atazipokea dhambi zetu katika mwili wake kwa kusulubiwa msalabani.
Lakini kwa sababu kuna watu wengi sana katika ulimwengu huu ambao imani yao haina ufahamu wowote kuhusu ubatizo wa Yesu, mara nyingi wamezidharau rangi nne za nyuzi zilizotumika katika hema takatifu la kukutania na badala yake wameyajenga malango yao ya hema takatifu la kukutania kwa nyuzi mbili tu.
Kwa kufanya hivyo wanawadanganya watu wengi, ambao tayari hawana uwelewa wa kutosha kuhusu Mungu na ambao hawajui kabisa neno lake. Hawa wote ni manabii wa uongo. Yesu mwenyewe aliwahi kuwazungumzia watu wa jinsi hii kwa kuwa ni magugu ambayo shetani aliyapanda katikati ya ngano (Mathayo 13:25). Kwa maneno mengine, wamekuwa ni watu ambao wanaeneza uongo kwa kuwacha nyuzi za bluu katika michoro yao ya ua wa Hema takatifu la kukutania. Hii ndiyo sababu watu wengi sana wanabakia ni wenye dhambi hata baada ya kuwa wanamwamini Yesu. Pamoja na imani yao katika Yesu bado wamefungwa katika uharibu kwa sababu ya dhambi zao.
Msingi wetu wa imani lazima uwe imara. Kuna uzuri gani kuishi kipindi kirefu cha maisha ya kidini katika nafsi yako ilhali maisha hayo yapo katika msingi usio wa sheria kiimani? Haijalishi kuwa nyumba zetu ni nzuri kiasi gani, kutakuwa na uzuri gani ikiwa tunajenga nyumba hizi katika msingi dhaifu wa kiimani? Bila kujali jinsi ambavyo umemtumikia Mungu kwa juhudi, ikiwa msingi wako wa imani una dosari, basi utakuwa umejenga nyumba yako katika mchanga; dhoruba itakapokuja na upepo kuvuma, na mafuriko yakaja, yataipiga nyumba yako nayo itaanguka chini mara moja.
Je, ni vipi kuhusu imani ya ambao msingi wao ni imara? Haitaanguka chini kamwe, hata ikitikiswa kiasi gani haitaanguka chini. Mungu alituambia sisi kuwa nyumba iliyojengwa katika mwamba wa kweli uliofumwa kwa nyuzi za bluu, zambarau, nyekundu na kitani safi ya kusokotwa haitaanguka chini kamwe. Na kwa kweli hivi ndivyo ilivyo. Je, imani ya mwamba ni nini? Ni imani inayo amini ukweli wa nyuzi za bluu, zambarau, nyekundu, na kitani safi ya kusokotwa. Imani ya watu waliojenga nyumba za jinsi hiyo za kiimani hazitaanguka kamwe. Na hii ndiyo sababu ni muhimu kwa imani yetu kuwa na msingi imara. Ikiwa hatuamini hata bila ya kufahamu vizuri yale ambayo Bwana amefanya kwa ajili yetu, basi imani ya jinsi hiyo itageuka kuwa imani ya kidini za uongo isiyotakiwa na Mungu.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni