Jumatano, 26 Machi 2014

UTATU MTAKATIFU


Kuna nafsi tatu za utatu mtakatifu, kwa maneno mengine Mungu ni yule yule.
Tuangalie maandiko yanasema nini kuhusu utatu mtakatifu
*      Agano la kale.
Ø  Kwanza kabisa, katika Agano la kale tunaona kuwa Mungu ni moja: Sikiliza ewe Israel, Bwana Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja”(Kumbukumbu la Torati 6:4).
Ø  Agano la kale pia linaeleza kuhusu nafsi mbalimbali (utatu mtakatifu) “Kisha Mungu akasema, ‘tufanye mtu kwa mafano wetu, kwa sura yetu” (Mwanzo 1:26) “Haya na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao.” (Mwanzo 11:7). Vifungu hivi vinadhihirisha kuwa Mungu yupo katika nafsi nyingi.
*      Agano jipya.
Ø  Nafsi tatu (utatu mtakatifu) unajifunua katika ubatizo wa Yesu Kristo ambao ndio mwanzo wa huduma zake.  “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini, na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake, na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayepenzwa naye” (Mathayo 3:16-17).  Kifungu hicho hapo juu kinaeleza utatu mtakatifu uliofunuliwa katika ubatizo wa Yesu uliofanywa na Yohana Mbatizaji. Katika kifungu hiki tunajua ya kuwa Yesu ni mwana wa Mungu, ambaye Roho Mtakatifu anafanya kazi pamoja nae. Ambaye kwa Mungu ni mwanae mpendwa aliye pendezwa nae. Kupitia ishara hii, utatu mtakatifu wa Mungu unajifunua. Yesu aliweza kukamilisha haki yote ya Mungu kwa sababu alichukua dhambi za mwanadamu kupitia ubatizo alioupata kupitia kwa Yohana mbatizaji. Kwa sababu ya ubatizo ilimpasa Yesu kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na hii ndio “haki ya Mungu”  ambayo baba aliikamilisha kupitia mwanae Yesu. Kwamba Yesu alibeba dhambi zetu kupitia tendo kuu la ubatizo na hiyo ndiyo haki ya Mungu, na ukweli huu umethibitishwa na Baba na Roho mtakatifu. Hivyo Baba, Mwana Roho mtakatifu wamejifunua katika nafsi tofauti, lakini Mungu ni yule yule.
Ø  (Mathayo 28:19) “ basi, enendeni mkawafanye, mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho mtakatifu”. Pia inadhihirisha kwamba Baba, Mwana na Roho mtakatifu kila mmoja ni nafsi inayojitegemea, lakini kwa wakati huo huo wote ni wa moja kwani ni Mungu yule yule mmoja. Tunapomwamini Mungu, twamwamini Mungu mmoja aliyeunganishwa na nafsi tatu. Mungu Baba, Mwana na Roho mtakatifu kama Imani ya Kikristo inavyokiri ni Mungu aliyepo tofauti kabisa na Miungu wengine. Dini zingine zinaamini kuwa Yesu ni nafsi moja kati ya manabii wengi, lakini hii sio sahihi.
Ø  Kwetu sisi Mungu ni Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Licha ya ukweli kuwa ukweli huu umetosheleza na kupimwa na maandiko, kuna wengi ambao bado hawatambui hili. Hii ni kwa sababu wale wasiojua Injili ya maji na Roho wanadhania utatu mtakatifu kibinadamu ambayo huwafanya wasielewe. Wale ambao bado hawajazaliwa upya hawawezi kuelewa utatu na Roho mtakatifu ni Mungu mmoja kwetu, kwake ambaye tunaiweka Imani yetu kwa uthabiti.
*      Asili ya Utatu wa Yesu Kristo: 
Yesu Kristo amekuwepo kabla ya uumbaji na amekuwepo kama Mungu kweli na miele. Japokuwa alikuja duniani kama mwandamu, ameendelea kuwa Mungu (Yohana 1:1, 14) kama vile (warumi 9:5) inasomeka “Ambao mababu ni wao, na katika wao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili, ndie aliye juu ya mambo yote, Mungu mwenye kuhimidiwa milele, Amina”. Ukiri wa kanisa la Mungu kuhusu asili ya Yesu Kristo haujatungwa na wanadamu, umepatikana kutoka ufunuo wa Mungu mwenyewe (Mathayo 16:17) zaidi sana ukweli uliomo katika Biblia unaelza asili ya ukuu wa Kristo (Isaya 9:6,Mika 5:2). Katika Agano Jipya, ukuu wa kweli wa Kristo mwokozi umefanuliwa na kuthibitishwa na Kristo mwenyewe. Petro alikiri pia kuwa Yesu “wewe ni Kristo Mwana wa Mungu aliye hai” (Mathayo 16:16, Marko 8:29 na Luka 9:20). Zaidi ya hapo, Paulo alisema “ ambaye, yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu.” (Wafilipi 2:6).Yohana alipokuwa akimtukuza Kristo, naye alikiri. “Nasi twajua ya kuwa mwana wa Mungu amekwishakuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye mwana wa Kweli na uzima wa milele.” (1 Yohana 5:20).
Nabii mkuu alipomuuliza Yesu “tuambie kama wewe ni Kristo Mwana wa Mungu”Yesu akasema “wewe wasema” (Mathayo 26:63-64, na Marko 15:2).Katika matukio mengine Yesu alisema yeye na Mungu ni wa - moja (Yohana 10:30) na kuwa yeye alikuwepo hata kabla ya Abraham (Yohana 8:58). Kristo alielezea nafsi yake kama nabii mkuu wa utukufu ambao yeye alishirikiana na Baba hata kabla ya uumbaji (Yohana 17:5). Pia tunaona, pale Kristo aliposamehe watu dhambi zao au kuponya magonjwa yao na pale alipowahimiza wanafunzi wake kumwamini yeye, haya yote yalifungua njia ya kuufahamu ukuu wa Mungu.
*      Asili Ya Kibinadamu Ya Yesu Kristo:
Agano Jipya pia linaeleza ubinadamu wa Yesu. Mwana wa pekee wa Mungu alizaliwa “kwa mfano wa Mwanadamu” (Wafilipi 2:7-8)  aliitwa “Mwanadamu Yesu Kristo” (1 Timotheo 2:5) licha ya kuwa alikuwa Mungu mwenyewe, alijinyenyekeza na kuwa kama Mwanadamu na Akakaa kwetu (Yohana 1:14). Matokeo yake alibatizwa na Yohana mbatizaji. Akakaa kati ya watu kama mtu, na akashiriki furaha yao na huzuni zao. Pia alikula chakula kile kile kama wanadamu wengine. Yeye alikuwa mtu si tu kwa mwonekanao, bali tabia yake pia. Kama wengine, yeye pia alikuwa wa uzao wa Adamu (Luka 3:38) pia alizaliwa na Mwanamke (Luka 2:6-7) (Mathayo 11:18-25) na (wagalatia 4:4) mojawapo ya mababu zake ni Abrahamu na Daudi (Mathayo 1:1). Licha ya kuwa Yesu mwenyewe hakuwa na dhambi alikuja hapa duniani katika mwili wa nyama ambao Mwanadamu ameudhoofisha kwa dhambi. Kwa maneno mengine Kristo alikuja kwa namna ya mwili wenye dhambi na kwa kubatizwa na Yohana alitimiza haki yote ya Mungu (Yohana 19:30). licha ya kuwa alibeba dhambi zetu mabegani mwake na ubatizo pamoja na mateso aliyopata, hakutofautishwa na wengine (Isaya 53:2-3). Licha ya kuwa Kristo alikuwa na asili yetu hakuthubutu kuingia katika majaribu ya kutenda dhambi kutokana na mwandishi wa kitabu cha Waebrania, Kristo alikuwa kwa namna nyingi akijaribiwa kutenda dhambi kama sisi, lakini bila kutenda dhambi (Waebrania 4:15). Yesu alichukuwa dhambi za dunia kwa kubatizwa na Yohana na hii ndio sababu alisulibishwa kwa ajili ya wenye dhambi. Tukirejea kwa Kristo, Waebrania 7:26 inasema, “kwa maana inatupasa sisi tuwe na Kuhani mkuu wa namna hii aliye mtakatifu, asiye na uovu asiyekuwa na waa lolote, aliyetengwa na wakosaji”.
*      Je, Yesu Alikuwa Mungu?
Ndiyo, Yesu alikuwa Mungu mwenyewe. Yesu ndiye hasa aliyeumba dunia yote kwa neno la kimywa chake. Kwa hakika dunia hii iliumbwa na Mungu Yohana 1:3 inasema “vitu vyote viliumbwa na yeye, na pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa kinaoonekana” Yesu alikuwa Mungu mwenyewe aliyekuja kuwaokoa wakosaji. Yesu aliumba ulimwengu huu kwanza. Pale aliposema “na iwe nuru”, mara ikawa nuru. Aliposema “na liwepo jua”, mara jua likatokeza. Ilikuwa ni amri tu “na iwe” vyote majini, miti, bahari, anga, na hata wanadamu wakatokea. Yesu Kristo aliumba kila kitu hapo
mwanzo (Mwanzo 1:3-15). Alikuwa ndiye Mungu mkuu wa uumbaji. Yote yalifanyika kwake. Na hakuna chochote kilichokuwepo bila yeye. Sasa ni kwa nini alikuja kwa mfano wa Mwanadamu? Alikuja kuokoa, wenye dhambi wote wa dunia hii. Sababu kubwa ya kuja kama Mwanadamu ilikuwa ni kuleta nuru ya kila mwenye dhambi na hatimaye kuwaokoa na dhambi zao. Yohana 1:9-12 inasema “kulikuweko na nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwapo, wala ulimwengu haukumtambua alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea bali waliompokea waliwapa uwezo kufanyika wana wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”. Mungu alikuja kuondoa dhambi za dunia tulizorithi kutoka kwa Adamu, Baba wa wanadamu, na kuondoa giza kutoka duniani. Jina lake yeye ni Yesu Kristo na Yesu Kristo ni mtoto wa Mungu Baba.
*      Utatu wa Mungu
WaKristo wanapaswa kumjua Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kama Mungu mmoja, na kukiri imani kwa nafsi hizo zote? Ndiyo, sababu ni kama ifuatavyo: Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wote walishiriki huduma ya uumbaji na kumkomboa Mwanadamu. Lakini Mungu Baba ni Baba wa Mwana mtakatifu. Mwana alitimiza huduma ya ondoleo la dhambi, kwamba alibatizwa na Yohana, alisulubiwa, ili kumkomboa Mwanadamu kutoka dhambini. Roho Mtakatifu alichukua nafasi ya kubeba ushuhuda wa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu ushuhuda kwa wale wanaoamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani kuwa vimetenda kazi ya kutakasa dhambi. Sisi kuwa watu kamili kwa Mungu, tunahitaji kumwamini Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kwa namna hii. Ni kwa sababu Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu waliumba ulimwengu, na sisi tuishio humu, na Mungu Mwana kuwaokoa wenye dhambi, ubatizo uliokamilisha haki ya Mungu na kazi ya kumwaga damu pale msalabani ilihitajika. Kwa kuwa Yesu alibatizwa na Yohana na hapo akachukua dhambi za dunia, alichukua adhabu ambayo sisi tulistahili kuibeba na kufa msalabani badala yetu.

Kwa kufanya hivyo, wenye dhambi hatimaye walipokea ondoleo la dhambi. Ukweli huu uliandaliwa muda mrefu, na ndio msingi hasa wa huduma ya Injili ya maji na Roho. Ni pale tunapoutumia ukweli huu ndipo kazi ya Yesu Kristo ya utakaso inapotimilika kwa ajili yetu, na tunaweza kuokolewa kutoka dhambini kwa kuamini tu. Kama tusingekuwa na ufahamu juu ya Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, hapo tusingeliweza kuujua ulimwengu ulivyoumbwa na nani aliyetupatia uzima, na kusingekuwa na Mungu Mwana, tusingeweza kujua njia ya wokovu, dhambi zetu zingepitishwa wapi? Msingi wa wokovu wetu ungekuwa nini. Na kama kusingekuwa na ushuhuda wa Roho mtakatifu, hapo haijalishi ukubwa na njia ya wokovu iliyoandaliwa, ukweli ungebaki kama alama tu mawinguni usio na lolote la kufanya nasi. Kwa hiyo kila tunapokiri imani ya Mitume , ni lazima tumfikiri Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu aliyetuumba na kutupa uzima na ni lazima tuwe imara katika imani na kuamini kuwa nafsi hizi tatu ni Mungu pamoja.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni