Jumatano, 26 Februari 2014

MAJI, DAMU NA ROHO


(1Yohana 5:4-7) Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko  kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni mwana wa Mungu. Huyu ndiye aliye kuja kwa maji na damu, Yesu Kristo: si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
Yatupasa kuamini kwamba Yesu alichukua dhambi zetu zote kwa ubatizo wake, alihukumiwa na kufa msalabani kwa ajili yetu, na akafufuka siku ya tatu, baada ya kifo chake.
Bila imani hii, ukombozi usingewezekana. Yesu Kristo alikuja kwetu kwa ubatizo, damu na Roho. Alichukuwa dhambi zote za ulimwengu.
Yapo mambo muhimu matatu yenye kushuhudia juu ya wokovu wake hapa duniani, Roho, maji na damu.
Kwanza; ‘Roho mtakatifu’ hushuhudia Yesu ni Mungu na alikuja katika mwili.
Pili ; ‘Maji’ hushuhudia ubatizo wa Yesu katika mto Yordani kwa Yohana Mbatizaji ambaye kupitia kwake dhambi zetu zote alimtwika Yesu. Dhambi zetu alizibeba Yesu alipobatizwa (Mathayo 3:15).
Tatu; ‘Damu’ inasimama kama Yesu kukubali kujitoa kwa hukumu ya dhambi zetu. Alikufa kwa hukumu ya Mungu Baba na alifufuliwa siku ya tatu ili kutupa uhai mpya.
Mungu Baba alimtuma Roho ndani ya mioyo ya wale wote wenye kuamini ubatizo na damu ya mwana wake ili aweze kushuhudia ndani, juu ya ukombozi.
Wale wote waliozaliwa upya wana neno ndani yao lenye kuushinda ulimwengu. Waliokombolewa watamshinda shetani, uongo wa manabii, walaghai, vikwazo au misukosuko ya ulimwengu ambayo haiachi kushambulia. Sababu ya kuwa na nguvu hii ni kwamba, tuna ushuhuda wa yale mambo matatu ndani ya mioyo yetu; maji ya Yesu, Damu yake na Roho.
Haiwezekani kuzaliwa upya au kuushinda ulimwengu ikiwa huna imani katika ukombozi utokanao na ubatizo wa Yesu, damu yake na kuamini Yesu ni Mwana wa mungu na mwokozi. Katika (1Yohana 5:8) inasema “kisha wako watatu washuhudiao duniani, Roho na Maji na Damu na watatu hawa hupatana kwa habari moja.” Wengi bado huzungumzia juu ya damu na Roho tu wakiacha maji ya ubatizo wa Yesu. Ikiwa wataacha habari ya maji, bado wataendelea kudanganywa na shetani. Wanapaswa kuacha upotovu wao na kutubu na kuamini maji ya ubatizo wa Yesu katika kuzaliwa upya.
Hakuna yeyote mwenye kuushinda ulimwengu bila kuamini maji na damu ya Yesu. Nasema tena, hakuna! Yatupasa kupigana kwa kutumia maji na damu ya Yesu kama silaha nzito na kali za kiroho. Neno lake ni upanga wa Roho, Nuru.
Wapo wengi wasioamini ubatizo wa Yesu ulichukua dhambi zetu zote. Wapo wengi wenye kuamini mambo mawili tu. Hivyo, Yesu anapowaeleza “amka na uangaze”, hawawezi kuangaza kwa vyovyote vile. Bado wanazo dhambi mioyoni mwao. Ingawa wanamwamini Yesu, lakini bado watakwenda motoni.
“mfano wa mambo hayo ni ubatizo unaowaokoa ninyi pia siku hizi” (1Petro 3:21). “watu wanane wliokoka kwa maji” (1Petro 3:20).

Ni watu wachache ndiyo waliokoka enzi za Nuhu. Je, walikuwa ni wenye thamani zaidi ya wengine? Hata kidogo! Sisi sote si wenye thamani, bali tumeokolewa kwa njia nyingine kupitia imani katika maji, damu na Roho.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni