Jumatatu, 7 Aprili 2014

JE, INAWEZEKANA MTU KUMNUNUA ROHO MTAKATIFU KWA UWEZO WAKE?


(Metendo 8:14–24 )
“Na Mitume waliokuwako Yesuramu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu wakawaombea wampokee Roho Makatifu kwa maana bado hawajawashukia
hata mmoja wao ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu. Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu. Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya Mitume akataka kuwapa fedha akisema, nipeni na mimi uwezo huu ili kila mtu nitakaye mwekea mikono yangu apokee Roho Mtakatifu. Lakini Petro akamwambia fedha na ipotelee mbali pamoja nawe kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu. Basi, tubia uovu wako huu ukamwombe Bwana ili kama yamkini usamehewe fikira hii ya moyo wako. Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu. Simon akajibu akasema, niombeeni ninyi kwa Bwana yasinifike mambo haya mliosema hata moja.”

Husika na somo kuu katika kifungu hiki, napenda kuleta ujumbe huu iwapo “mtu anaweza kumpokea Roho Mtakatifu ndani yake kwa kupitia juhudi binafsi”. Mitume katika nyakati
hizo za Kanisa la kwanza waliweza kupokea nguvu toka kwa Mungu na kutumwa sehemu kadhaa naye. Yapo matendo ya miujiza kadhaa katika Kitabu cha Matendo, mojawapo likiwa
kushuka kwa Roho Mtakatifu juu ya waumini pale Mitume walipowawekea mikono. Biblia inasema “Mitume walipowawekea mikono wale ambao hawakuwa wamempokea
Roho Mtakatifu ingawa walikwisha mwamini Yesu, walipokea Roho Mtakatifu.”

Sasa basi, ni kwa namna gani walimpokea Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono? Kwa wakati huo maneno ya Mungu bado yalikuwa yakiendelea kuandikwa na hivyo basi kazi ilikuwa bado haijakamilika hivyo Mungu aliwapa Mitume nguvu za pekee kuweza kufanya kazi zake. Alikuwa pamoja na Mitume na kuweza kuleta miujiza mingi na maajabu kupitia kwao. Kilikuwa ni kipindi pekee, wakati Mungu alipofanya maajabu na miujiza ambayo iliweza kuonekana kwa macho ya wanadamu ili kuweza kuwafanya watu waweze kumwamini Yesu Kristo kuwa kweli ni mwana wa Mungu na ndiye mwokozi. Palikuwepo na umuhimu kwa Mungu pamoja na
Mitume kwa nguvu za ajabu kuweza kuonyesha kazi ya Roho Mtakatifu ili kuthibitisha kwamba Yesu Kristo ndiye Mungu na kwamba ndiye Mwana wa Mungu Mwokozi. Ikiwa Roho Mtakatifu asingefanya kazi kupitia miujiza na maajabu kwa nyakati hizo za kanisa la kwanza hakika pasingekuwepo na yeyote awezaye kumwamini Yesu kuwa ni Mwokozi.

Hata hivyo hakuna umuhimu tena kwetu sisi leo hii kumpokea Roho Mtakatifu kupitia miujiza na maajabu ya kuonekana kwa macho ya kawaida kwa sababu Biblia imekamilika. Badala yake sasa, kuwa na Roho Mtakatifu ndani yetu kunategemea imani zetu zaidi. Kwa maneno mengine ni kuamini Injili ya kweli. Mungu ametupatia Roho Mtakatifu awe ndani yetu kwa wale tu watakao kuwa na imani ya Injili ya kweli mbele ya Mungu. Kuwa na Roho Mtakatifu ndani hutokea kwa wale tu wanao amini maneno ya Mungu kama ilivyo timia kwa kuja kwake Yesu hapa ulimwenguni na kwa ubatizo wake na damu yake.

Nyakati hizi wachungaji wengi hufundisha waumini wao kwamba matendo yasiyo ya kawaida yawezayo kuonekana kwa macho ndiyo ishara tosha ya kuwa na Roho Mtakatifu. Hivyo
kuwaongoza waumini kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia hiyo. Huwapotosha watu kwa kuwapa mafundisho ya uongo kama yale ya kunena kwa lugha kuwa ndiyo ishara ya kushukiwa na Roho
Mtakatifu. Wachungaji hawa hujiona kuwa wao ndiyo mitume watendao miujiza na maajabu makuu na hivyo kuvutia washabiki wa kidini ambao hutaka kumjua Mungu kwa hisia zao.

Ushabiki huu umeenea kwa Wakristo walio wengi duniani pote na wengi wao hufuata imani hizo na hatimaye kupatwa na roho za kishetani kwa kupitia njia za nguvu za giza. Hata leo, watu hao waliokumbwa na ushabiki wa aina hii hudhani kuwa nao wataweza kuwafanya wenzao kuweza kumpokea Roho Mtakatifu kupitia kuwekewa mikono.

Hata hivyo kwa jinsi Simoni alivyo potoka, nao huwa kama wachawi wanaonekana katika kifungu hicho. Wameharibiwa kwa kujikonga nafsi zao na tamaa ya mwili lakini matendo yao
yote huleta tafrani katikati ya watu. Aina hii ya mafundisho ya uongo hupindisha njia ya kweli katika kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu mbele ya Mungu.

Hata leo, wengi wa mitume waongo hufanya kazi za ibilisi kupitia mambo yasiyo sahihi ya kidini, wakijifanya kutenda kazi za Roho Mtakatifu. Wakristo walio wa kweli ni lazima
walishike neno la Mungu ambalo ndiyo ufahamu pekee wa kuweza kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani. Wale wote wanaojifanya kuwa ni Wapentekoste, ambao husisitizia mwonekano wa nje kimwili nilazima waache imani hizi potofu wayarejee maneno ya Mungu na kuamini ukweli ambao kwa hakika utawaongoza katika kumpokea Roho Mtakatifu ndani yao.

Simoni alikuwa mchawi maarufu Samaria katika nyakati hizo. Baada ya kuwaona mitume wa Yesu wakisababisha watu kumpokea Roho Mtakatifu, alitamani kumnunua Roho Mtakatifu kwa fedha. Watu wa imani ya aina hii bila shaka huishia kuwa watumwa wa ibilisi wakitumiwa kutenda kazi zake. Simoni alitaka kumpokea Roho Mtakatifu lakini tama zake zilikuwa si nyingine bali ni kujipatia kipato binafsi.

Tunaweza kuona aina hii ya imani siyo yakupelekea kumpokea Roho. Simoni alijaribu kumnunua Roho Mtakatifu kwa fedha kwasababu ya uchoyo ulio tokana na kutamani nguvu za Roho Mtakatifu. Alikemewa vikali na mtumishi wa Mungu Petro. Ingawa ilisemekana kwamba Simoni alikuwa akimwamini Yesu hakuwa ni mtu kamwe aliyekuwa amempokea Roho Mtakatifu kupitia ondoleo la dhambi. Kwa maneno mengine yeye alidhani
ya kwamba angeweza kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yake kwa kutoa mali za kidunia kwa Mungu.

Ingawa muonekano wake wa nje ulionyesha kwamba alikuwa akimwamini Yesu, mawazo yake halisi ndani yalikuwa hayawiani na maneno ya Yesu. Badala yake alijawa na tamaa za kimwili. Petro aliye yagundua mawazo ya Simoni alimkemea kwa kuwa alijaribu kutaka kumpokea Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi ya Mungu kwa fedha. Alimtaadharisha Simoni kwamba angeweza kuangamia na fedha hizo zake.

Nyakati hizi mitume waongo walio tawaliwa na roho za ibilisi hunena kwa kuwalaghai watu kwa kuwafanya kudhani kwamba miujiza na maajabu yote ni kazi za Roho Mtakatifu. Tunaweza kuona mara nyingi watu wakifurahia aina hizi za nguvu na kuomba kwa dhati nao waweze kumpokea Roho Mtakatifu. Hata hivyo mtu imempasa kuwa makini kwamba hapana yeyote utakaye mpokea Roho Mtaktifu ndani yake kupitia maombi yaliyo na tamaa za kidunia.
Je, wapo pia watu wa uamsho wa vipawa (karismatiki) kati yako kwa nafasi yoyote? Imekupasa uwe mwangalifu dhidi ya watu wa aina hii.

Huwafata watu kwa imani hizi za mashamshamu na kishabiki. Husema kwamba wanaweza
kukemea mapepo na hata kuweza kuwafanya watu kumpokea Roho Mtakatifu kupitia kuwawekea mikono. Hata hivyo watu hawa huwa na nguvu ambazo si za Roho Mtakatifu bali ni
nguvu za pepo wachafu. Wale wanaodai kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia ya kuwekewa mikono hujiongoza wao binafsi na wengie katika kumpokea roho chafu.

Kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu huja kwa sisi wote tu, tunaoamini maneno ya maji na Roho (1 Yohana 5:3-7). Ingawa injili ya maji na Roho imeandikwa kwa uwazi katika Biblia, bado watu walio wengi hudhani mioyoni mwao kwamba wataweza jaribu kumfikia Mungu kwa kupitia nguvu za miujiza na kwa hali za kupumbaza, kunena kwa lugha, maono na kukemea pepo. Na ndiyo maana manabii waongo wameweza kuwadanganya watu wengi katika kuamini mazingaombwe ya Kikristo yatokanayo na ibilisi mwovu.


Petro alimkemea Simoni kwa kumwambia, “Fedha yako na ipotee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali. Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili. Basi tubia uovu wako huu ukamwombe Bwana ili kama yamkini usamehewe fikra hii ya moyo wako. Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo na tena u katika kifungo cha uovu.” Yatupasa kujawa na simanzi kwa sababu leo hii wapo watumishi wa aina hii. Wengi wao ni wale wajiitao wenye vipawa au wakarismatiki. Hudai fedha kwa makundi yao. Tuwe mbali sana nao na watu wa imani hizi na tumpokee Roho Mtakatifu ndani yetu kwa Injili ya kweli katika maji na Roho (Mathayo 3:15, 1 Petro 3:21, Yohana 1:29, Yohana 19:21-23).

Maoni 1 :

  1. 1xbet » Free Bet, Bonus, Deposit & Review | Dec 2021
    What is herzamanindir.com/ 1xbet? — งานออนไลน์ 1xbet is a casino that offers a selection of online ventureberg.com/ casino games, such as slots, 1xbet korean roulette, and poker. There are 토토

    JibuFuta