Jumapili, 30 Machi 2014

MANABII WA UONGO


(Yuda 1:11) inasema, “Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya kora.” Ipi sasa ndio njia ya Kaini? Kaini alienda mbali na njia ya Mungu, na Mungu akamwadhibu. Wale waliotekwa na shetani wanafanya kazi ili kupata pesa. Kifungu kinaendelea kusema, “wameikimbilia tamaa katika kosa la Balaam kwa kutafuta faida” Wachungaji waliotekwa na shetani wanahubiri sana ili kupata pesa, wamefungwa na shetani, wanatenda kazi za manabii wa wa uwongo. Manabii hawa wa uwongo hufurahia kupata pesa nyingi zinazotolewa kama sadaka makanisani. Wanatumia nguvu kubwa kuhubiri pale wanapoona waumini wao wanamwaga pesa nyingi makanisani kama sadaka. Na pale waumini wanatoa pesa kidogo, manabii wa uwongo hata hawathubutu kuwabariki. Hivi ndivyo ilivyo kuwa waliomezwa na shetani wanatoa huduma makanisani ili hatimaye wapate pesa.
Ukitoa pesa nyingi, wanakupa hata madaraka makubwa kanisani kama mtumishi ama mzee wa kanisa. Lakini kama wewe sio mtoaji, hawawezi kamwe kukupa hata cheo kanisani. Hawa ambao kifungu hiki cha maneno kinawazungumzia ni wale wapenda pesa tu. Hawa walikuwa akina nani? Biblia inawataaja akina Balaam, Nabii wa Agano la Kale, aliyewaingiza watu wa Israeli katika biashara ya kuwauza ili kupata pesa. Watu kama Balaam wanafanya kazi kwa nguvu za shetani, hao ndio wanaofanya huduma kujichumia pesa. Fungu hilo la maneno hatimaye linatuambia kuwa watu wanaingia kuwa “mateka wa Kora” Watu hawa waliunda vyama vyao na kusimama kinyume na makanisa ya Mungu. Watu wanaopenda pesa wataishia kuwa watu wa kusimama kinyume na Mungu.
(Yuda 1:12) Inasema, “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamupamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawinguyasiyo na maji, yachukuliwayona upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa.” Wale wanaowatazama watu kwa mtazamo wa pesa, ni wataalamu wa kudanganya wengine na kuwaibia waumini wao pesa. Kwa kuwa watumishi wa shetani ni aina ya watumishi wenye njaa ya kujishibisha, wanajijali wao wenyewe, hawafikiri juu ya Roho za wengine. Hata kama watu wanamwamini Yesu, wengi wao wanatawaliwa na hawana amani ndani yao, wana hofu juu ya dhambi zao, na wanaendeshwa na ujinga wa hofu zao. Watumishi wa shetani wanapanda mbegu ya uongo kwa kudanganya wakifuata nguvu ya shetani. Na kila mara wakiongea habari za neno la Mungu, wanachanganya na uongo hata hawana aibu. Kwa hiyo Biblia inawaelezea wao kama “mawimbi yenye nguvu ya baharini, yanayobubujika aibu yao” (Yuda 1:13).
Wakati wa siku za mwisho ukifika, mapepo yataongeza nguvu ya kupotosha watu. Na hivyo hata watumishi watazidisha nguvu. Katika nyakati za mwisho, kabla ya Yesu hajarudi, shetani atafanya kazi kubwa hata ndani ya makanisa katika ulimwengu huu. Mapepo yatapamba moto, unabii utazidi sana. Jambo la muhimu sana hapa ni kwa wale ambao bado hawajazaliwa kwa upya hata kama wanamwamini Yesu, hata kama waiamini Injili ya Maji na Roho iliyotolewa na Bwana, na kupokea ondoleo la dhambi na karama za roho Mtakatifu. Na kwa kuwa na Roho Mtakatifu, ni sharti wawe na uzima wa milele. Lakini wale watumishi wa Mungu waliotekwa na shetani, hutafuta baraka za mwili tu, nguvu ya uponyaji, kuongea kwa ndimi, na kutenda miujiza kama misingi ya matakwa yao na malengo. Ndiyo sababu watu hawa huweka kipaumbele kwa yale shetani anayowaagiza. Katika dunia ya leo, mtu akianza kuongea kwa ndimi katika nyumba zao za ibada, watu wanaomzunguka mtu huyu humsifu na hata kumpigia makofi. Na wale wasioweza kuongea kwa ndimi huwekwa katika chumba kimoja na kufundishwa namna ya kunena kwa lugha ama kuongea kwa ndimi, wakirudia rudia “Lul-lu-lujah, Lul-lu-lujah,
Haleluya.” Wanapojaribu kurudiarudia maneno haya kwa haraka, inafikia hatua wanaongea maneno yasiyoeleweka, maneno ya ajabu ajabu, kama vile umeweka kanda mbovu kwenye redio (Katika kuongea haraka, maneno yanakwama katika ulimi). Inapofikia asilimia 80 ya watu wamepoteza namna ya kuongea vizuri, kwa ndimi zao kukwamisha maneno, ni nani kati yao ataweza kutamka maneno kwa ukamili? Ni kwa sababu wafuasi hao wamewekewa mikono na watu wenye pepo, nao pia hupandwa na roho hiyo. Pepo hufanya makao na kukaa mioyoni mwao. Ni kwa sababu wamejaa pepo, ndiyo maana wanaongea kwa kuongozwa na pepo. Msidanyike na kazi za mapepo, lakini iaminini kuwa Injili ya kweli ya Roho Mtakatifu mioyoni na kati ya wale wanaoamini Injili ya Maji na Roho iliyoandikwa katika Biblia. Hata sasa, kazi potofu za mapepo zinaendelea kati ya wale wanofuata imani za Kikarismatiki.
Lakini Mkitubu Siku Hiyo
(Mathayo 7:22-23) inasema, “Wengi wataniambia siku ile, Bwana Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza? Ndipo nitaawambia dhahiri, sikuwajua ninyi kamwe, ondokeni kwangu ninyi mtendao maovu.” Watu wengi wanaamini kwamba kujifanya nabii kwa jina la Bwana, kutoa pepo, kutenda miujiza, kwa jina la Bwana, ni kazi za Mungu na Roho Mtakatifu, Kuna wakristo katika dunia ya leo wanaodai kutoa pepo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, Manabii wanapoonekana kutenda miujiza, wanasema kwa kujiamini, hiyo ni kazi ya Roho Mtakatifu. Lakini neno linasema, mambo hayo sio kazi ya Roho Mtakatifu. Neno linasema kuwa nguvu hiyo ya kuondoa mapepo, ishara, maajabu na miujiza mbalimbali ni kazi za shetani. Licha ya hayo, watu bado wanaamini kuwa hizo ni kazi za Roho Mtakatifu. Kazi za shetani zilikuja kwa ajili ya wale waliuoandaliwa maangamizi, na watu wale ambao wanafanya ishara na miujiza kamwe hawawezi kuokolewa. Kwa hiyo Biblia inatuonya kuwa “Wapendwa, msiziamini kila roho, bali zijaribuni kuona kama zinatoka kwa Mungu, kwa sababu, manabii wa uongo wamekwenda duniani.” (1 Yohana 4:1).

Maoni 2 :

  1. nataka tu kila somo niwe ninalipata nimejengwa sana na Mungu akubariki. asante

    JibuFuta
  2. Ingiza maoni yako...niwe ninapata kila somo asante

    JibuFuta