Jumapili, 23 Februari 2014

MUNGU AMETUPATIA HAKI KWA IMANI KATIKA SHERIA

sheria sehemu ya tano
Mtume Paulo alisema kwamba, Mungu ametupatia haki kwa imani toka mwanzo. Alimpatia Adamu na Hawa, Kaini na Abeli, Sethi na Enoki, Nuhu, Abrahamu, Isaka na mwisho Yakobo na watoto wake kumi na wawili. Hata pasipo sheria, walifanywa kuwa wenye haki mbele za Mungu kupitia haki itokanayo na Imani ya Neno lake; Walibarikiwa na walipata pumziko kupitia imani ya Neno lake.
Muda uliopita wakati uzao wa Yakobo uliishi Misri kama watumwa kwa miaka 400 kwa sababu ya Yusufu. Ndipo Mungu alipowaongoza kutoka kupitia Musa kuelekea Kanaani, pamoja na kuwa watumwa kwa miaka 400, walisahau haki katika Imani.
Ndipo Mungu alipowaongoza kupita kati ya Bahari ya Shamu kwa muujiza na kuwaongoza jangwani walipofika jangwa la dhambi, akawapa sheria katika Mlima Sinai. Aliwapa sheria ambazo zilikuwamo Amri kumi na vipengele 613. Mungu aliahidi “Ndimi Bwana Mungu wako, Mungu wa Abraham, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Musa apande na kuja katika mlima Sinai na nitawapa sheria” Ndipo alipowapa Waisraeli Sheria.
Aliwapa Sheria ili waweze “kutambua dhambi” (Warumi 3:20) Ilikuwa ni kuwafahamisha juu ya anachotaka na asichotaka na kuweka wazi haki yake na utakatifu.Walipokuwa wakiishi kama watumwa kwa kipindi hicho cha miaka 400, walisahau haki ya Mungu katika muda huo hawakuweza kuwa na kiongozi. Yakobo na Yusufu walikuwa viongozi hapo awali. Inaonekana Yusufu alishindwa kuirithisha Imani hiyo kwa watoto wake wa kiume, Manase na Efraimu.
Hivyo, walihitaji kumtafuta Mungu tena na kukutana naye kwa kuwa waliisahau haki yake. Tunapaswa kuweka akilini kwamba Mungu aliwapa haki kwa imani mwanzo na kuwapa sheria baada ya kuisahau Imani. Aliwapa Sheria ili waweze kumrudia.
Kuiokoa Israeli na kuwafanya kuwa wana wake, aliwaambia kwamba iliwalazimu kutahiriwa. Nia ya kuwaita ilikuwa ni kuwafanya watambue kwamba alikuwa kati yao ili kuanzisha Sheria na pili, kufanya watambue walikuwa ni wenye dhambi mbele zake. Mungu alitaka waje mbele zake na kuwa watu wake kwa kukombolewa kwa mfumo wa sadaka ambayo aliyokuwa amewapa. Na aliwafanya kuwa watu wake.
Wana wa Israeli walikombolewa kupitia mfumo wa sadaka wa Sheria kwa kumwamini Masiya ajaye. Lakini mfumo huu ulipitwa na wakati. Na tuangalie hii, ilikuwa ni lini. Katika Luka 10:25 mwanasheria mmoja alitajwa kumjaribu Yesu. Alikuwa ni Mfarisayo. Mafarisayo walikuwa ni wenye kuyashika mafundisho bila kukubali kubadilika kwa kufanya jitihada zao binafsi kuishi kwa kufuata neno la Mungu; Walijaribu kuzilinda sheria za nchi kwanza kwa kuishi kadiri ya maandiko ya sheria. Walikuwa ni “wakereketwa” (kwa lugha ya kisasa) ambao walihamasisha na kufanya ghasia za kuvunja sheria ili kufanikisha malengo ya maono yao juu ya uhuru wa Waisraeli toka kwa Warumi.
Kuna baadhi yao hata nyakati hizi wamo kwenye dini tuzionazo. Huongoza harakati za kijamii kwa usemi kama vile “Okoa wanaogandamizwa duniani!” Huamini Yesu alikuja kuokoa maskini na wanaogandamizwa. Hivyo baada ya kujifunza theologia katika seminari, huchukua nafasi katika mambo ya kisiasa na kujaribu kuwakomboa wanaonyanyaswa katika kila sehemu ya jamii. Ndiyo wenye kushinikiza kwa kusema “Hebu na tuishi kwa sheria na rehema ya sheria takatifu. Tuishi kwa sheria, kwa neno la Mungu” Lakini hawatambui hakika ya ukweli wa Sheria. Hujaribu kuishi kwa sheria iliyoandikwa bila kufahamu na kupata ufunuo wa Mungu juu ya Sheria hiyo.
Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba hapakuwepo na manabii, watumishi wa Mungu katika Israeli kwa kipindi hicho cha miaka 400 kabla ya Kristo. Kwa sababu hii basi, walikuwa ni kundi la kondoo wasio na Mchungaji.
Hawakuwa na sheria wala Kiongozi wa kweli. Mungu hakujidhihirisha mwenyewe kwa hao walio kuwa ni viongozi wa dini zao walio wanafiki. Nchi ilitawaliwa na Dola ya Warumi. Hivyo Yesu aliwaambia watu hawa wa Israeli walio mfuata jangwani kwamba hawatarudishwa kutoka kwake wakiwa na njaa. Alijawa na huruma juu yao waliokama kundi la wanakondoo wasio na Mchungaji kwani wengi wao walikuwa kwenye mateso makubwa.
Wanasheria na wale wengine walio na nafasi za uongozi walikuwa ndiyo wenyewe tu wenye kunufaika. Mafarisayo walikuwa ni kizazi cha “Judaism” na walikuwa ni wenye majivuno sana.
Mwanasheria huyu alimwuliza Yesu katika Luka 10:25“nifanye nini niweze kurithi uzima wa milele?” Alionekana kufikiri kwamba yeye ni bora zaidi kati ya watu wa Israeli. Hivyo mwanasheria huyu (ambaye hajakombolewa) alimwuliza Yesu kwa kusema “nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?”
Mwanasheria huyu anasimama badala yetu leo. Alimwuliza Yesu swali hili, naye akajibu “imeandikwa nini katika Torati? Wasomaje?” Naye akajibu “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote na akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.” Naye akamjibu umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.” Alijaribu kumtia changamoto Yesu bila ya kufahamu yeye alikuwa ni mwenye dhambi, asiyeweza kutenda mema. Hivyo Yesu alivyomwuliza “imeandikwa nini katika Torati, wasomaje?”

“wasomaje” kwa kifungu hiki Yesu anauliza, ni kwa namna gani mimi na wewe tunaijua na kuielewa sheria? Kwa jinsi hii wengi wetu nyakati hizi ndivyo tulivyo. Mwanasheria huyu alifikiri kwamba Mungu alikusudia kuweka sheria ili zifuatwe. Hivyo alijibu kupitia maandiko “mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili zako zote na jirani yako kama nafsi yako.” Sheria haikuwa na kasoro. Alitupa sheria iliyo kamilifu. Alituambia tumpende Bwana kwa moyo na kwa roho na kwa nguvu na akili na kuwapenda majirani zetu kama nafsi zetu. Ni haki tumpende Mungu kwa moyo wetu wote na kwa nguvu zetu zote, lakini hii ni amri takatifu isiyoweza kutimizwa kwa nafsi zetu. “Wasomaje?” Hii ina maana sheria ni kamilifu na sawa lakini je, wewe unaelewa nini juu yake? Mwanasheria alifikiri kwamba Mungu alileta sheria hii ili aweze kuitii. Ingawa Sheria ya Mungu imeletwa kwetu ili tuweze kuziona nafsi zetu na upungufu ndani yake kwa kuukubali udhaifu wetu uliowazi kabisa mbele za Mungu. “Umetenda dhambi, umeua hali nilikuambia usiue. Kwa nini hukunitii” Ndivyo Mungu akuulizavyo. Sheria huweka wazi dhambi za watu ndani ya mioyo yao. Hebu na tufikiri kwa mfano nilipokuwa nikitembea, nikaona tunda zuri na tamu lililoiva katika shamba la mtu. Mungu amenionya kwa sheria” usichume tunda hilo katika shamba. Itaniaibisha mimi ukitenda hilo” “Ndiyo Baba” “Shamba hili ni la ndugu fulani, hivyo usichume” “Ndiyo Baba” Tunaposikia hivyo tusichume, tunahisi msukumo ndani yetu wa kuchuma. Tunapochukua hatua ya kujizuia inashindikana. Na hii ndivyo ilivyo katika dhambi za watu. Mungu ametuonya tusitende dhambi. Aweza kusema hivi kwa kuwa yeye ni mtakatifu, mkamilifu na mwenye uwezo wote.
soma shehemu ya sitaSHERIA NI KWA AJILI YA KUZIFAHAMU DHAMBI"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni