sehemu ya nne
Hebu na tusome Wagalatia 3:10 na 11“Kwa maana wale wote
walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana: maana imeandikwa, Amelaaniwa
kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati,
ayafanye". Ni dhahiri ya kwamba kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa Imani”kuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika
sheria;
Imesemwa “Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa
katika kitabu cha torati ayafanye “Wale wenye kufikiri kuwa wana mwamini Yesu,
hali wakitaka haki kupitia matendo yao, wamelaaniwa. Wapo wapi wenye kujaribu kuwa
wenye haki? Wapo chini ya laana ya Mungu.
Kwa nini Mungu ametupa Sheria? Ametupa sheria ili tuweze
kuzitambua dhambi zetu (Warumi 3:20). Na pia alitaka tujue kwamba sisi ni wenye
dhambi na mwisho wetu ni jehanamu. Amini ubatizo wa Yesu, Mwana wa Mungu na
uzaliwe upya kwa maji na kwa Roho. Ndipo utakapo okolewa dhambini, kuwa mwenye
haki, kupata uzima wa milele na kwenda mbinguni. Uwe na Imani moyoni mwako.
soma sehemu ya tano "MUNGU AMETUPATIA HAKI KWA IMANI KATIKA SHERIA"
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni