Injili ya kweli ni ile pekee
yenye kutuwezesha kuwa huru kwa dhambi zetu
kikamilifu, mara moja na kwa wakati wote pale tunapoamini nguvu ya injili ya
Mungu.
Injili ya Mungu ni ile “Yesu
Kristo alilipa deni la wadaiwa (wenye dhambi) wasio weza bila shaka kulilipa
wenyewe “.
Alikuja hapa ulimwenguni na
kubeba dhambi zote kwa ubatizo wake katika
mto Yordani na kututakasa daima.
Amelipa mshahara wa dhambi kwa
kuchukuwa dhambi zetu zote kwa ubatizo
wake Yordani na kwa kufa msalabani kalvari. Yesu alizifuta dhambi zote za
ulimwengu kwa mithili ya nguvu kwa ubatizo na damu yake. Hii ndiyo habari njema
(Injili) ya kweli.
Injili ya kweli ni ile Yesu kuja
ulimwenguni na kwa ubatizo wake na damu yake msalabani umetuokoa sisi sote
wenye kuamini.
Kama ilivyo andikwa katika 1yohana 5:4-6 ‘ huyu ndiye
aliye kuja katika maji na katika damu, yesu Kristo si kwa maji tu, bali katika
maji na katika damu’.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni