Alhamisi, 20 Februari 2014

SADAKA YA MATENDO MBELE YA MUNGU


Baadhi ya wakristo hawaamini haki ya Mungu na humsifu Bwana wakiimba “Oh, Mungu chukuwa kilicho changu na ufanye kuwa chako, matendo yangu ya kujitolea mbele yako” kwa njia hii Mungu hana nafasi ya kufanya chochote kwako.
Wanadamu humchosha Mungu kwa kujifanya wao ni wa kujitolea matendo yao zaidi. Mungu amechoshwa na upofu huu wa kujitolea kwa sadaka ya matendo. Wao humsihi Mungu apokee haki zao za kibinadamu ( ukitaka kujua haki ya Mungu soma “injili ya maji na roho” katika blog hii). Hudumu waki mlilia Bwana ‘ O, Mungu! Pokea kujitoa kwetu sadaka” huku wakitenda kazi za kanisa kama vile kufagia, kudeki sakafu, kufanya maombi, na kuimba mapambio. Itatia dosari kwa wakristo wengi. Siku hizi wakristo wengi humsihi Yesu kuyajali matendo yao ya kujitolea kimwili huku hawaijui haki ya Mungu au hata kuiamini. Yatupasa kuacha kujitolea kimwili na kuanza kuikubali na kuielewa haki ya Mungu ambayo ndani yake umo ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Tusome habari ya Kornelio katika kitabu cha Matendo 10, ili ujue namaanisha nini? (Matendo 10:1-6) Palikuwa na mtu kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa kiitalia, mtu mtawa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, kuna nini, Bwana? Akamwambia, sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro.  Yeye ni mgeni wa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi, ambaye nyumba yake iko pwani, atakuambia yakupasayo kutenda”
Neno atakuambia yakupasayo kutenda” maana yake yale aliyo kuwa akitenda hayakuwa na msaada wowote kuipata haki ya Mungu (yaani kupata msamaha wa dhambi), ili kuzaliwa upya na kupokea Roho Mtakatifu. Ni sawa na mtu masikini na omba omba kumpa tajiri bilionea kila alichonacho  na kumba akae katika makazi ya kifahari kwa fidia ya kile alichotoa.  Mungu haitaji kwetu kujitia sifa ya haki zetu binafsi. Mungu anahitaji tuwe na imani kwa kuamini ubatizo wa Yesu na damu yake msalabani.
Tuendelee na habari hii ya Kornelio katika (Matendo 10:37) Jambo lile ninyi mmelijua, lililoenea katika Uyahudi wote likianzia galilaya, baada ya ubatizo aliouhubiri Yohana.
Baada ya kuambiwa na malaika atume watu Yafa wakamwite Simioni, alipofika alianza kuhubairi habari ya ubatizo. Kwanini Simioni alianzia katika ubatizo?, jibu unalipata katika kifungu hiki (Matendo10: 43) “huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi”  ukisha pokea ondoleo la dhambi nini kinachofuata? (Matendo 10:44) Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waloisikia lile neno”
Tunapokea ondoleo la dhambi ikiwa pale tutakapo amini ubatizo wa Yesu kwa Yohana na damu yake msalabani( ufafanuzi wa somo hili soma matoleo yaliyopita).Yesu alibatizwa ili kubeba dhambi zote za dunia na kufa ili ili kuzifuta dhambi hizo mara moja na kwa wakati wote.
Hivyo mtu anapohubiriwa kwa usahihi neno la Mungu anapokea ondoleo la dhambi na kupokea Roho Mtakatifu. Je tusifanye kazi za kujitolea katika makanisa? Hapana. Namaanisha si njia ya kumpokea Roho Mtakatifu (kuzaliwa mara ya pili).
Tuendelee na habari ya Kornelio (Matendo10: 47) Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea roho mtakatifu kama sisi?
Utaona kwamba ubatizo katika maji ni hatuwa ya mwisho, kama ishara ya nje ya kile ulichokiamini ndani yako, Hivyo Roho Mtakatifu huja kabla ya kwenda katika maji ya ubatizo.
Hebu tafakari maandiko haya; (Mathayo 9:13) “lakini nendeni,mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”
(2wakorintho3:12-16) Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi; nasi si kama musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba waisrael wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika; ila fikra zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo; ila hata leo, torati ya musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao. Lakini wakati wowote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni