Jumanne, 25 Februari 2014

SABABU YA MUNGU KUTUPATIA SHERIA.

sheria sehemu ya tatu
Sababu ipi Mungu alitupatia Sheria? Ilikuwa ni kutufanya kuzitambua dhambi zetu na kumrudia kwake kwa toba. Alitupatia vipengele 613 vya sheria ili tuweze kuzitambua dhambi zetu na kuweza kukombolewa kupitia Yesu Kristo. Na hii ndiyo maana ya Mungu kutupatia sheria.
Warumi 3:20  inasema  “….. kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya Sheria”.  Hivyo twajua kwamba sababu ya Mungu kutupatia sheria ilikuwa si kutulazimisha kuenenda nayo.
Kwa namna hii sasa, tunapata kujua nini juu ya Sheria? Ni hivi, sisi tu wadhaifu kwa kuitimiza sheria yote na ni wenye dhambi sana. Tunatambua nini juu ya vipengele hivyo 613 vya Sheria? Tunang’amua mapungufu yetu na kushindwa kwetu kuifuata Sheria yake.
Tunatambua yakwamba sisi ni viumbe wa Mungu, tulio dhaifu, na wenye dhambi mbele zake. Ilitupasa sisi sote kutupwa motoni kwa mujibu wa Sheria ya Mungu. Tunapo tambua dhambi zetu na kushindwa kwetu kuishi kwa kuzifuata sheria, sasa, na tufanye nini? Je tunajaribu kuishi kwa ukamilifu wenyewe? Hasha! Yatulazimu kukubali kuwa sisi ni wadhambi, tumwamini Yesu ili tukombolewe kupitia wokovu wake katika Maji na Roho na kumshukuru yeye.
Sababu ya Mungu kutupa sheria ilikuwa ni kutufanya tuzitambue dhambi zetu na kujua adhabu yake juu ya dhambi hizo. Hivyo, itatufanya kuelewa kuwa hakuna njia ya kuokolewa toka motoni pasipo Yesu ikiwa tutamwamini Yesu kuwa ni Mwokozi, tutakombolewa. Mungu alitupa sheria ili ituongoze kuelekea kwa Mwokozi Yesu.
Mungu alizifanya sheria ili kutufanya tuweze kutambua ni kwa namna gani tulivyo wenye dhambi na kuhitaji wokovu wa roho zetu kutoka kwenye dhambi hizo. Alitupa sheria na kumtuma mwana wake wa pekee, Yesu, kutuokoa kwa kuzibeba katika ubatizo wake. Kumwamini Yeye kutatufanya tuokolewe.

Sisi ni wadhambi tusio na tumaini lolote, yatulazimu kumwamini Yesu ili kuwa huru kutoka dhambini, kuwa watoto wa Mungu na kuurudisha utukufu wake. Yatupasa tuelewe, kufikiri na kuamua kupitia neno lake kwa kuwa yeye ni asili ya yote. Yatupasa tuikubali kweli ya wokovu kupitia Neno lake. Hii ni Imani ya Haki na kweli.

soma sehemu ya nne "WENYE KUJARIBU KUKOMBOLEWA KWA KUPITIA MATENDO YAO BADO NI WENYE DHAMBI"

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni