Hakika sala ya toba haitoweza kamwe kutakasa dhambi zetu
kwa sababu ukombozi hauwezi kuja kwa kupitia matendo yetu. Bali, ili tuweze
kuwa wenye haki kamili na wakati wote tukiwa tumeoshwa dhambi zetu zote,
yatupasa kuamini katika ubatizo na damu ya Yesu, na kuamini kuwa Yesu ni Mungu.
Ukombozi kamili hupatikana kwa wale tu wenye kuamini kuwa Yesu alibeba dhambi zetu
zote kwa ubatizo wake na kutoa damu yake msalabani kutupa uhai mpya.
Sasa basi, je tutaweza kutakasa dhambi zetu za kila
siku kwa kufanya sala za toba kila mara? Hapana. Dhambi zote tuzitendazo
maishani mwetu kila siku zilikwisha takaswa takribani miaka 2000 iliyopita pale
Yesu alipozibeba kwa ubatizo wake. Hakika tumepata utakaso wa kudumu kwa dhambi
zetu zote kwa ule ubatizo wa Yesu na kwa damu yake pale msalabani. Amekuwa mwanakondoo
wa sadaka kwa ajili yetu wenye kumwamini, kusafishwa dhambi zetu zote, na
kulipia yote kwa ubatizo na kwa damu yake msalabani.
Kwa lugha nyepesi, katika Agano la kale kuhani mkuu
alikuwa akitoa sadaka ya upatanisho wa dhambi kila siku ya kumi ya mwezi wa
saba (Walawi 16: 29-34). Aliye husika
kumbebesha (kumtwika ) mnyama dhambi za Israel ni kuhani mkuu peke yake kwa niaba
ya watu wote. Watu wa Israel hawakuwa na haja ya kila mmoja kuwekea mikono katika
sadaka ya dhambi, bali walitakiwa kuamini kuwa dhambi zao zimesamehewa kupitia
mwakilishi wao. Katika Agano jipya Yohana Mbatizaji amesimama (kama kuhani
mkuu) badala ya watu wote ulimwenguni, hivyo alimtwika Yesu dhambi zetu zote katika
ubatizo, nasi pia tunahitajika kuamini katika yale aliyofanya Yohana Mbatizaji
(kuhani mkuu) na Yesu (mnyama kwa Agano la kale).
TOBA YA KWELI
Sote sisi tumejawa na dhambi. Toba ya kweli ni kukubali
kufuata kweli; kwamba sisi ni wenye dhambi mbele ya Mungu, na hivyo hatuwezi
kujizuia kutenda dhambi maishani mwetu na kwenda jehanamu tutakapokufa. Hivyo
yatupasa kumkubali Yesu kama mwokozi wetu kwa kuamini kwamba alikuja
ulimwenguni kutuokoa sisi wenye dhambi na hivyo alibeba dhambi zetu (kupitia
ubatizo), akafa na alifufuliwa kutuokoa. Toba ya kweli ni kuacha fikra zetu na
kumrudia Mungu (Matendo 2: 38).
Toba ya kweli ni kukiri dhambi zetu na kulirudia neno la
Mungu kukubali wokovu katika maji (ubatizo) na kwa damu kwa moyo wetu wote.
(1Yohana5:6).
Ili tuweze kuokolewa na kusafishwa dhambi zetu zote,
yatupasa kuacha kujaribu kujitakasa kwa kupitia matendo ya sheria, na kukiri
kwamba sisi ni wenye dhambi mbele ya Mungu na sheria yake, sisi basi yatupasa
kukubali kweli ya wokovu wa Yesu, injili ya Maji na Roho, ambayo Yesu
alituachia kwa ubatizo na damu yake.
Tutaokolewa pale tutakapo amini ubatizo wa Yesu uliozichukua
dhambi zetu zote kwake.
Kwa maneno mengine, ubatizo wa Yesu, kusulubiwa kwake, na
ufufuo wake umetimiza haki ya Mungu kwa wokovu wa wenye dhambi. Yesu alikuja
katika mwili, alibatizwa na kusulubiwa ili kutusafisha dhambi zetu zote. Kwa
kuwa na imani iliyo kamili katika yote haya na kuamini kwamba Yesu alifufuka
ili awe mwokozi wa wote wenye kumwamini katika toba ya kweli na imani halisi.
Kila kitu katika Agano la kale kina mwenzake katika
Agano jipya kwa Agano la kale “tafuteni katika
kitabu cha BWANA mkasome hapana katika hao wote atakayekosa kuwapo, hapona
mmoja atakayemkosa mwenzake; kwa maana kinywa change kimeamuru na roho yake
imekusanya” (Isaya 34:16)
Hitimisho; ikiwa utajikuta wewe mwenyewe unamwomba Yesu ili akusamehe dhambi zako za kila siku, basi ni lazima utambue kuwa bado hujazaliwa upya.
Ikiwa kwa namna yoyote ile umekuwa ukijifanya kuwa mtakatifu kwa matendo yako na mwonekano wa mwili wako, ingawa moyo wako una dhambi, basi wewe ni mwanadini mnafiki na ni mtoto wa maangamizi.
Hitimisho; ikiwa utajikuta wewe mwenyewe unamwomba Yesu ili akusamehe dhambi zako za kila siku, basi ni lazima utambue kuwa bado hujazaliwa upya.
Ikiwa kwa namna yoyote ile umekuwa ukijifanya kuwa mtakatifu kwa matendo yako na mwonekano wa mwili wako, ingawa moyo wako una dhambi, basi wewe ni mwanadini mnafiki na ni mtoto wa maangamizi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni