Jumapili, 23 Februari 2014

YATUPASA KWANZA KUZIJUA DHAMBI ZETU ILI TUWEZE KUKOMBOLEWA

sheria sehemu ya kwanza

(Marko 7:8-9)“Ninyi mwaiacha amri ya Mungu na kuyashika mapokeo ya wanadamu. Akawaambia, vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu”
(Marko 7:20-23)“Akasema, kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivu, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu; Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”
Kwanza ningependa kufafanua nini maana ya dhambi. Kuna dhambi zilizoelezwa na Mungu na nyingine kuelezewa na mwanadamu. Neno dhambi kwa Kigiriki ‘hamartia’ maana yake ni ‘kukosea katika kulenga shabaha”. Kwa maneno mengine, ni kufanya jambo pasipo usahihi. Ni dhambi kutotii maelekezo ya Mungu. Hebu na tuangalie kwa awali maana ya dhambi kwa mtizamo wa mwanadamu.
Twagundua dhambi zetu kupita dhamira zetu. Ingawa kiwango cha ubinadamu hutofautiana kulingana na jamii anayotoka, hali ya kimawazo, katika mazingira na dhamira.
Hivyo, maana ya dhambi inatofautiana kati ya jamii na jamii. Kitendo cha aina moja chaweza au kisiweze kuchukuliwa kama dhambi endapo kila jamii itakuwa na aina yake ya vipimo. Ndiyo maana Mungu ametupa vipengele vya sheria 613 ili vitumike kama vipimo halisi vya dhambi.
Hatupaswi kamwe kuweka viwango vya dhambi kwa kutumia dhamira iliyowekwa kwa kanuni zetu za kijamii.
Dhambi za dhamira siyo zitokanazo na jinsi ile Mungu anavyoelezea nini maana ya dhambi. Hivyo tusizisikilize dhamira zetu, bali tulinganishe viwango vya dhambi zetu na amri za Mungu.
Kila mmoja ana wazo lake juu ya nini maana ya dhambi. Wengine huchukulia ni udhaifu hali wengine hudhani kwamba ni kutokana na kilema cha tabia.

Matendo ya kistarabu katika jamii moja yanaweza kuchukuliwa kwa jamii nyingine kuwa yasiyo ya kistaarabu na kinyama. Ingawa Biblia inatueleza kwamba dhambi ni kutotii maelekezo ya Mungu. “Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo yenu” (Marko 7:8-9). Muonekano wetu wa nje ni muhimu mbele za Mungu kwa kuwa yeye huangalia kina cha mioyo yetu.
soma sehemu ya pili "KANUNI ZA MTU NI DHAMBI MBELE ZA MUNGU".

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni