sheri sehemu ya pili
Kushindwa kuishi katika mapenzi ya Mungu ni dhambi. Ni sawa
na kutoamini neno lake. Mungu alisema, ni dhambi kuishi kama Wafarisayo ambao
walikataa sheria ya Mungu kwa kukazia zaidi msisitizo wa mafundisho ya desturi
zao. Yesu aliwachukulia kuwa ni wanafiki.
“Ni Mungu yupi unayemwamini? Je, unaniheshimu na kunitukuza?
Unajivunia juu yangu, lakini je unaniheshimu? Mara nyingi watu huangalia umbo
la nje na kupuuzia neno la Mungu ndani ya nafsi zao. Je wajua hilo? Matendo ya
kuvunja sheria chanzo chake yametokana na udhaifu ambao ni maovu. Makosa
tuyafanyayo na upotovu tuutendao kutokana na kutokuwa wakamilifu siyo dhambi kuu
ndani yetu bali ni kuanguka katika usahihi. Mungu ametofautisha kati ya dhambi
na uovu. Wale wote wenye kulidharau neno lake ni wenye dhambi, hata ikiwa
hawana makosa. Ni wenye dhambi zaidi mbele ya Mungu. Na hii ndiyo maana Yesu
aliwakemea Mafarisayo.
Katika nyakati za Agano la Kale, kitabu cha mwanzo hadi
kumbukumbu la Torati ziliwekwa sheria zilizotaja nini cha kutenda na nini cha
kutotenda. Ni maneno ya Mungu Sheria yake. Haitowezekana kwetu kuzitekeleza
katika asilimia mia moja, lakini yatubidi kuzikubali kama ni sheria za Mungu.
Alitupatia hapo mwanzo na yatupasa kuzikubali kuwa ni Maneno ya Mungu.
“Hapo mwanzo palikuwepo na Neno, naye Neno alikuwepo kwa
Mungu, naye Neno alikuwa ni Mungu” Naye alisema “Na uwepo mwanga na ukawepo”
Aliumba vyote. Na baadaye, akaiweka Sheria.
“Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu;” (Yohana 1:14).
Ni kwa namna gani basi Mungu alijidhihirisha kwetu? Alijidhihirisha kwetu
kupitia sheria kwa maana Mungu ni Neno na Roho. Sasa je, Biblia inaitwa nini?
Tunaita Neno la Mungu. Imesemwa hapa “Ninyi mwaiacha amri ya Mungu na kuyashika
mapokeo ya wanadamu” vipo vipengele 613 katika sheria ya Mungu. Fanya hivi na usifanye
vile waheshimu wazazi wako………… nakadhalika. Katika kitabu cha Mambo ya Walawi
imetajwa ni kwa namna gani mwanamume na mwanamke wanapaswa kuenenda na nini
kifanyike endapo mifugo ikitumbukia shimoni………. Hivi ni baadhi ya vipengele 613
katika sheria.
Kwa kuwa haya si maneno ya mwanadamu, tunapaswa kuyatafakari
nyakati zote. Ingawa tutashindwa kutekeleza sheria yote, tunapaswa kwa kiasi
Fulani kuzitambua na kumtii Mungu.
Je, kuna kifungu hata kimoja cha maneno ya Mungu yasiyo
sahihi? Mafarisayo waliziacha sheria za Mungu na kuzifuata taratibu za
mafundisho ya wanadamu dhidi ya sheria ya Mungu. Maneno ya wakuu wao yalichukua
nafasi ya uzito wa juu dhidi ya yale ya Mungu.
Yesu alipokuwa duniani, haya ndiyo aliyoshuhudia, na ndicho
kilicho umiza moyo wake zaidi kwa kuona Neno la Mungu likipuuziwa na wanadamu. Mungu
ametupa vipengele 613 vya sheria ili tuweze kuzitambua dhambi zetu na kutuonyesha
kuwa yeye ni mkweli na mtakatifu kwetu. Kwa kuwa sisi sote ni wenye dhambi
mbele yake, tunapaswa basi kuenenda kwa imani na kumwamini Yesu kuwa ndiye aliyeletwa na Mungu kwa upendo kwetu. Wenye kuweka neno lake
kando na kutoamini watakuwa ni wadhambi. Wenye kushindwa kuenenda katika neno
lake pia ni wadhambi, ingawa kuweka kando neno lake ni hatari zaidi. Wenye
kutenda dhambi hii wataishia motoni. Kutoamini Neno lake ni dhambi iliyo hatari
zaidi mbele za Mungu.
soma sehemu ya tatu"SABABU YA MUNGU KUTUPATIA SHERIA".
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni