Maana yake hatuna dhambi tena baada ya kuokoka, hivyo
hatupaswi kuomba sala za toba za kila siku.
Katika injiri ya Yohana 13 ipo habari ya Yesu kusafisha miguu ya
Petro. Alisafisha miguu ya Petro ili kuonyesha ya kwamba, Petro angetenda
dhambi katika kipindi kijacho na kumweleza ya kuwa alikwisha mkomboa kwa dhambi
hizo pia, Yesu alijua Petro angetenda dhambi tena katika siku zijazo, hivyo
alimimina maji katika karai na kuosha miguu yake.
Petro alijaribu kukataa, lakini
yesu alimwambia “nifanyalo wewe hujui sasa; lakini
utalifahamu baadaye.” Kifungu hiki kina maana kwamba “utatenda dhambi tena baadaye” utanikana
na kutenda dhambi tena baada ya kuosha dhambi zako zote. Utatenda dhambi hata
wakati nitakapo paa kwenda Mbinguni.
Hivyo nasafisha miguu yako ili kumtaadharisha shetani asikutie
majaribuni kwa kuwa nimekwisha zichukuwa dhambi zako hata zile zijazo.
Je, unafikiri alisafisha miguu ya
Petro ili kutueleza kwamba yatupasa kutubu kila siku? Hapana! Ikiwa tulipaswa
kutubu kila siku ili tukombolewe basi ina maana kwamba Yesu isingempasa
kuchukuwa dhambi hizo mara moja na kwa wakati wote wa maisha yetu.
Lakini Yesu alisema alitutakasa
mara moja na kwa wakati wote ikiwa tungehitajika kutubu kila siku, basi
ingekuwa kama vile tumerudi katika kile kipindi cha Agano la kale. Sasa
tungeweza kuwa wenye haki? Nani angeweza kukombolewa kwa ukamilifu? Hata kama
tulimwani Mungu, ni nani angeweza kuishi bila dhambi?
Hivyo, Yesu alibatizwa mara moja
na kujitoa yeye mwenyewe msalabani mara moja ili tuweze kutakaswa mara moja na
wakati wote. Je, unaweza kuelewa hili?
Tumekombolewa kutoka dhambini kwa
kumwamini Yesu aliyezichukuwa dhambi zetu zote,
“ na
kila kuhani kila siku akifanya ibada na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi;
ambazo haziwezi kabisa kuondoa
dhambi. Lakini huyu alipokwisha kutoa kwa ajiri
ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele aliketi mkono wa kuume wa Mungu
tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe
kuwa chini ya miguu yake maana
kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa. Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya
kusema hili ni Agano nitakalo agana nao baada ya siku zile anena Bwana, nitatia
sheria zangu katika nia zao nitaziandika ndipo anenapo. Dhambi zao na uasi wao
sitaukumbuka tena kabisa, basi ondoleo la haya likiwapo, hapana toleo tena kwa
ajiri ya dhambi” (waebrania 10:11-18)
Nini maana ya “basi ondoleo la hayo likiwapo” katika
mstari wa 18 hapo juu? hii ina maana ya kwamba kila dhambi ilifutwa kabisa bila
uchaguzi Mungu alizifuta dhambi zote na kutusamehe.
Nahitimisha kwa kusema kuwa; tuna
okolewa bure kwa neema ya Mungu katika imani, lakini neema hiyo haituruhusu
kutenda dhambi makusudi, kwa sababu ile nguvu ya kuishinda dhambi tumepewa
(Roho Mtakatifu) kwa kuamini katika siri ya Mungu. (kuifahamu siri ya Mungu
soma masomo yaliyopita).
“Tuseme
nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? Hasha! Sisi
tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi? Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo tulibatizwa
katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika
wafu kwa njia ya utukufu wa baba , hivyo
hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima
(Warumi 6:1-4)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni